Haji Manara kaacha ndara (ndala) mbele ya John Heche

Haji Manara kaacha ndara (ndala) mbele ya John Heche

huyo hua hajielezi gentleman,
ni mzuri zaidi kwenye kuropoka nonsense ambazo hata wanachadema wenyewe huona anaropoka nonsense tu

Kwa style yako nakushauri usije kutana Nate hasa ukiwa public au mbele ya kamera. Kwa sababu atakuabisha. Heche ni Mzuri akikutana na watu Aina yako.

Unamuona Emanuel Nchimbi? Yeye pia anahuo utulivu. Hana papara. Na Kila akiongea anaongea kwa uhakiki
 
Kwanza wale ukiwaita uwahoji,media ujipange sana maana mnaweza pata msala 😄

Ova

Tena ukitaka uone Moto na uwezo wake jifanye unampelekea za uso kama unataka kumshinda. Hapo lazima bodi ya ithibati sijui wahariri like barua hicho chombo
 
Aiseeh!

Haji Manara ni muongeaji mzuri Sana. Na mwenye uwezo mkubwa hasa akikutana na watu wajingawajinga, wenye uelewa Mdogo.

Umaarufu na nguvu yake kuu ya kuongea ipo kwenye udhaifu wa wanaomsikiliza na anaokutana nao head by head. Wengi amewatoa nishai kwa sababu zifuatazo;

1. Haji Manara ni muongeaji mno mwenye uswahili ndani yake
Kwenye uongeaji wake hutumia mbinu ya maneno ya shombo na vikejeli vya hapa na pale Jambo ambalo huwafanya opponents wake kupoteza mhimili kwani wanakuwa too emotional au wanapoteza kujiamini.

2. Pili, Manara hutumia mbinu ya Victims na kujifanya mhanga ila yeye akikushambulia anakuja full. Hii inawafanya anaopambana nao wawe wamefungwa mikono. Kwani hawajiachii moja kwa moja.

3. Haji Manara hutumia mbinu ya kujifanya mtoto mjini na mtu mwenye connection ndefu. Hii huwatisha opponents wake wengi.
Kwani wengi huogopa watoto wa mjini.

Katika mechi ambazo Haji Manara kazicheza amepoteza Mechi Mbili tuu.
Mechi ya Kwanza ni Ile Aliyocheza na Jerry Muro. Ambapo Jerry yeye alifunguka na kurusha missile huku akikataa kufungwa mikono.
Hapa Manara aliacha Ndala( ndara) akaishia kulalamika na mashabiki na waamuzi waliingilia kati wakimtetea.

Jana Haji kama kawaida Yake akiwa na uzoefu Mkubwa wa mapambano ya kupepeta mdomo, kupangua hoja, kujenga hoja, kushusha vimondo na kejeli za hapa na pale.
Akiwa na uhakika na KAZI yake.

Manara hakuamini alipojikuta katika Hali ngumu dhidi ya Opponent wake John Heche.

John Heche alikuwa akiyajibu maswali na hoja za Manara kwa namna ambayo Manara mwenye hakuitarajia licha ya mbinu alizotumia Manara kama kawaida yake kumjaza Na kumpandisha Heche Sukari.
Lakini Heche alikuwa Mtulivu mwenye kujua nini anatakiwa kufanya kwa watu wa karba ya Manara.

Hatimaye Manara alijikuta akiacha ndara na akiondoka na ONYO kuwa HUKU USIJE yaani kwa vijana wa Chadema ni kumfuata Mamba kwenye kina kirefu.

Siri kuu ya kupambana na Vijana wa Chadema unapokuwa nao kwenye mahojiano;

1. Epuka Uchawa.
2. Ongea Ukweli.
Kwa sababu ukiongea ukweli automatic utaonekana uko smart.

3. Kama kuna sehemu serikali inakosea usikatae sema ni kweli. Lakini elezea namna serikali inavyohangaika kupambana na kukosea kwake huku nawe ukitoa maoni ya jinsi ya kurekebisha.

4. Tafuta Makosa ya Chadema yataje ili kumfanya opponent wako atumie muda mwingi kujitetea katika Makosa. Kumbuka kujitetea katika Makosa ndio Uchawa wenyewe.
Hata hivyo Opponent wako pia anaweza kuku neutralise hoja yako kwa kukubali Makosa ili asitumie muda mwingi kujitetea.

Huku usije utaacha ndala athee!
Manara alikuwa anahoji kama uvccm ila sio kama journalist
 
Kwa style yako nakushauri usije kutana Nate hasa ukiwa public au mbele ya kamera. Kwa sababu atakuabisha. Heche ni Mzuri akikutana na watu Aina yako.

Unamuona Emanuel Nchimbi? Yeye pia anahuo utulivu. Hana papara. Na Kila akiongea anaongea kwa uhakiki
:pedroP:ni rafiki yangu sana gentleman,

kwamba Dr.Nchimbi hana papara, na ana aina ya utulivu mithili ya heche?:pedroP:

mbona hao watu ni tofauti kama chmvi na sukari gentleman? hakuna kabisa wanachofanana hata kimoja.
 
:pedroP:ni rafiki yangu sana gentleman,

kwamba Dr.Nchimbi hana papara, na ana aina ya utulivu mithili ya heche?:pedroP:

mbona hao watu ni tofauti kama chmvi na sukari gentleman? hakuna kabisa wanachofanana hata kimoja.

Gentlemen
Fuata ushauri wangu😃😃
 
Sawa tutakuandalia interview akufanyie j.lokole basi 😄

Ova
Gentleman,
ni kupoteza muda au kupata hasara eti mnajadiliana na huyo mropokaji aliepoteza uelekeoa wa maisha
 
Sasa watu wenye kariba ya Lucas mwashamba kweli mkawakutanishe na Heche na watoke salama? Lazima apigwe spana. Uchawa na akili havikai pamoja..!!
maskini heche mropokaji,
kumbe anaonekani ni kichwa sana kwa mamluki wake, dah!
 
daima siachagi ushauri wa maana jukwaani hasa kutoka kwa wadau wa heshima wa JF,
lakini eti unishauri kuhusu mropokaji heche? :pedroP:

naona kama unanitukana kisayansi gentleman, jamaa ana mihemko ya kikurya ya kindezi sana aise

😂😂 Mkuu Mimi na kisayansi wapi na wapi Mzee.
Matusi ya kisayansi nimewaachia nyie Wazee wa Archimedes ngule.

Ila zingatia sana
 
Back
Top Bottom