Haitoshi! - Chenge jiuzulu na Ubunge!

Nyani ngabu
Hapana sijakubaliana na wewe,wasukuma hawakumtuma kuiba hiyo ni aibu yake na familia yake ambayo inaogelea kwenye ukwasi wakati wananchi waliomchagua wanakufa kwa ufukara.
 
Sitaki kusikia hiki chama ccm,chama cha majambazi,wezi,mafisadi,wenye roho mbaya na wasio kuwa na akili timamu.
 
yote yametokea,bungeni ataenda kufanya nini!!! lowassa,msabaha,karamagi,mramba,chenge,mwanasheri mkuu mwanyika wote wasiingie bungeni wala wasiwajibika kwa taifa letu.... wametulia pesa zetu
 
Halafu mimi siamini kabisa kama Kikwete naye yuko safi ingawa ushahidi sina. Lakini kama yuko clueless kabisa na ufisadi unaondelea basi na yeye hastahili kuwa raisi. Ajiuzulu mara moja! Kama anajua kuhusu huo ufisadi na yeye kwa namna moja au nyingine anahusika nao halafu anaendelea kuwateua mafisadi ktk nyadhifa kubwa serikalini basi judgement yake ni mbovu na hilo pekee linatosha kwa yeye kubwaga manyanga chini. We just can't have a head of state whose judgement is grossly flawed. Let's have same standards for everyone.


Nyani ,

Nakubalina na wewe asilimia mia , Kikwete naye sio msafi kama vyombo vya habari vinavyotaka kuonyesha. Kikwete kwa njia moja au nyingine amehusika na kuiua Tanesco kwa kuingia mkataba na IPTL wakati yeye akiwa waziri wa nishati na madini . Watu hawataki kabisa kulizungumzia hili kwani wanaogopa ukweli . Pia kwenye suala la Rada yeye akiwa waziri wa mambo ya nje alilitetea ununuzi wa radar na alisema yafuatayo:

People say we do not need this system, what are they waiting for? When two jumbo jets crash over Tanzania, will people accept the need for us to have a radar system? This problem is real not fiction.

Source: http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/1723673.stm

Pia JK alisema yafuatayo katika kumtete Mkapa na ununuzi wa radar

President Jakaya Kikwete has declared that he sees no need for his predecessor, Benjamin Mkapa, to explain how the 40 billion/- radar now at the centre of heated debate inside and outside Tanzania was purchased.
What do you want (retired President Benjamin) Mkapa to explain.


Source : http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2007/02/23/84983.html

Kwa hiyo nadhani watu hawataki kusoma alama zilizoko ubaoni...
 
Nyani ,

Nakubalina na wewe asilimia mia , Kikwete naye sio msafi kama vyombo vya habari vinavyotaka kuonyesha. Kikwete kwa njia moja au nyingine amehusika na kuiua Tanesco kwa kuingia mkataba na IPTL wakati yeye akiwa waziri wa nishati na madini . Watu hawataki kabisa kulizungumzia hili kwani wanaogopa ukweli . Pia kwenye suala la Rada yeye akiwa waziri wa mambo ya nje alilitetea ununuzi wa radar na alisema yafuatayo:

People say we do not need this system, what are they waiting for? When two jumbo jets crash over Tanzania, will people accept the need for us to have a radar system? This problem is real not fiction.

Source: http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/1723673.stm

Pia JK alisema yafuatayo katika kumtete Mkapa na ununuzi wa radar

President Jakaya Kikwete has declared that he sees no need for his predecessor, Benjamin Mkapa, to explain how the 40 billion/- radar now at the centre of heated debate inside and outside Tanzania was purchased.
What do you want (retired President Benjamin) Mkapa to explain.


Source : http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2007/02/23/84983.html

Kwa hiyo nadhani watu hawataki kusoma alama zilizoko ubaoni...

Rufiji ahsante kwa hizo link,

Mimi nilipata tabu sana kumuelewa Andrew Chenge na statement yake ya "vijisenti", nikajiuliza hivi Chenge anapata wapi kiburi cha kujibu hivi.

Sasa ninaweza ku-connect the dots, kiburi hiki kimeanzia mbali, tangu kwa Mkapa na mpaka sasa kwa kikwete viongozi wamejenga utamaduni wa kiburi, ndiyo maana Mramba kasema "hata mkila majani" Chenge kasema "vijisenti" ukiangalia quotes za Kikwete hapo juu zote zimejaa ubabe wa "mnataka nini?" tu.

Kwa hiyo mkiona viongozi wanaua watu, wengine wanatukana watu bila woga, msifikiri ni mambo random tu yanatokea, wakikaa kwenye vikao vyao wanafurahi wanavyowanyoosha watanzania.

Kikwete mwenyewe alisema katika a Freudian slip alivyokuja US, watu walimuuliza kuhusu kuchangia maendeleo Tanzania akasema "mtakuja kututafuta ubaya tu na vihela vyenu". I do not wonder where Chenge got the visenti comment, it is very probable that the comment is part of this despicable culture.
 
Kumbe aende wapi wakati huko ndiko makao makuu ya wenye matendo hayo. Hivi kuna watu wanaamini kwamba ufisadi wa Chenge ndio umejulikana leo na kuna watu wanaamini kwamba JK alikuwa hamjui Chenge vizuri wakati anamteua? Kwa nini hatujiulizi ilikuwaje JK akamteua Chenge kwenye baraza lake la mawaziri na akamteua tena? Tujiulize tena kwa nini Chenge ni mjumbe wa Kamati ya Maadili ya CCM? Kikubwa zaidi, tujiulize kwa nini Chenge anapendwa sana na wana CCM wenzake hadi akaongoza kwenye kura za ujumbe wa Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ya chama chao? Where am I going: we are still making the same mistake to think that ufisadi is only a problem of few crooks in CCM like Chenge. To me, ufisadi is simply a CCM phenomenon. To hate ufisadi but love CCM is simply wanting to eat the cake and have it at the same time and is a display of hypocrisy of the highest order, which is increasingly becoming part of us watanzania. We have only two choices: to hate ufisadi and its root causes and mobilise all necessary forces to wipe it out or hate ufisadi but continue patting its breeding ground (CCM)and continue whining!

Kitila umeyasema yote siwezi kuongeza neno. CCM = MAFISADI=CCM. Aliye msafi na ambaye ameunyooshea kidole ufisadi anyooshe mkono. Wote ni aidha mafisadi au wanawashangilia na kuwaficha mafisadi.
 
Ni kweli yawezekana kuwa kujiuzulu Uwaziri kumepokelewa kwa furaha na wengi (mimi mmoja wao). Yawezekana kwa kufanya hivyo uchunguzi utakuwa huru (sidhani alikuwa anazuia uchunguzi anyway); yawezekana kujiuzulu kwake kumekuwa ni kitulizo cha kelele dhidi ya ufisadi; Yawezekana kujiuzulu kwake kumeonesha ufisadi wa viongozi wa serikali ya JK na hivyo kumuondoa kumeonesha jitihada za kusafisha serikali hiyo;

Hata hivyo, hadi hivi sasa CCM haijalipa gharama yoyote ya viongozi wake kuhusishwa na ufisadi na hakuna wakati hadi hivi sasa ambao wao kama CCM wamechukua hatua za viongozi wa serikali waliofanya vitendo vya ufisadi wakiwa ni wanachama wake.

Ni kwa sababu hiyo basi naamini kujiuzulu kwa Chenge toka serikalini hakutoshi bali lazima kufuatiwe na kujiuzulu toka Ubunge. Kwanini?

a. Kiasi cha fedha anachodaiwa kukutwa nacho kingeweza kuleta mabadiliko makubwa kwa watu wa Jimbo lake lakini aliwaficha wapiga kura wake.
b. Kwa kukiita kiasi hicho "vijisenti" kwa kisingizio cha "usukuma wake" ni tusi kwa wasukuma wengine ambao hawajui maana ya "vijisenti" hasa baada ya yeye mwenyewe kuelezea kuwa "kila mtu ana kiwango chake".
c. Mwakilishi wa wananchi anapotajwa na kuhusishwa na kitendo cha matumizi mabaya ya nafasi yake, nafasi ambayo imetokana na kuchaguliwa na wananchi hao, basi anapojiuzulu nafasi yake basi hana budi kuachia kiti chake ili ampishe mtu mwingine kushika nafasi hiyo.

Bw. Chenge amewaangusha wapiga kura wake, na amekiletea aibu kubwa chama chake. Kati ya wote walioatajwa katika tuhuma za ufisadi ni yeye pekee ambaye tunajua angalau kiasi gani che fedha kimefichwa huko Jersey. Kwa sababu hiyo basi Chenge siyo tu ajiuzulu Uwaziri kama alivyofanya bali pia ajiuzulu Ubunge wake na Uwakilishi wake ili mwana CCM au mtu mwingine aweze kuwawakilisha wananchi wa Bariadi Magharibi.

JIUZULU UBUNGE BW. CHENGE, UMEKUWA AIBU YA TAIFA LETU!

Asante kwa hoja yako. Lakini ni kipengele gani katika katiba yetu kinadai kwamba waziri akijiuzulu uwaziri ni lazima ajiuzulu na ubunge alionao?. Nadhani ingekuwa ni hekima kutoa ombi kwamba kama uwezekano basi kipengele hicho kiwekwe ndani ya katiba yetu.
 
Asante kwa hoja yako. Lakini ni kipengele gani katika katiba yetu kinadai kwamba waziri akijiuzulu uwaziri ni lazima ajiuzulu na ubunge alionao?. Nadhani ingekuwa ni hekima kutoa ombi kwamba kama uwezekano basi kipengele hicho kiwekwe ndani ya katiba yetu.
Naona tunakubaliana tuu!Wana jf sasa tuelekeze nguvu kwenye katiba mupya!
 
Naona tunakubaliana tuu!Wana jf sasa tuelekeze nguvu kwenye katiba mupya!

Sawa kabisa bwasheee. Haya yote ya ufisadi kwa sasa hatuwezi kufanya kitu chochote zaidi ya kupiga kelele tu hapa. Tugombanie katiba mpya kwanza.
 
Sawa kabisa bwasheee. Haya yote ya ufisadi kwa sasa hatuwezi kufanya kitu chochote zaidi ya kupiga kelele tu hapa. Tugombanie katiba mpya kwanza.
No MTAMBO..Tunapiga miguu yote..katiba mpya sambamba na uwajibishwaji pamoja na urudishwaji na seizings!hapa jf hakuna cha bwashee wala nani!hizo ni lugha mbovu za vichochoroni..i really dont think i understand!kwi kwi kwi!
 
Katika moja ya mambo ambayo JF inaweza kujivunia ni kwamba Serikali ya JK inajua wazi NGUVU ya JF na inafuata kwa njia moja au nyingine kile tunachopendekeza humu ndani ya Baraza.

Kuna mwanachama mmoja hapa kapendekeza kuwa tutumie pressure kuwang'oa Lowassa na wenzake kwenye Ubunge. Mie naungana naye kwa asilimia 500, these guys know JF FULL PRESSURE. Hivyo nawashauri wana JF wenzangu tutumie hii JF-FP kuhakikisha mafisadi hawa waachie ubunge wao ili watu waadilifu waweze kupata nafasi ya kuwatumikia wananchi wao. Inaweza kuwa ngumu kidogo kutokana na SISIEMU kuogopa kuachia hayo majimbo kwa sasa ukitilia maanani kuwa wananchi sasa wana Uchungu kutokana na UPUPU unaofanya na hicho chama. Lakini ninaamini tukiungana na tukatumia hii nguvu tuliyonayo hapa, wataona aibu wenyewe.
naungana na wewe, hebu sema tufanye mkakati gani? Ujumbe unatakiwa uwafikie walengwa na je unawafikia au tutumie njia gani kuhakikisha unafika. Watu wengine huwa wanatumia petition sisi tunatumia nini?
 
MWANAKIJIJI asante sana kwa mada yako chokozi, ina mameno mazito yenye busara. Kwangu mimi nakubaliana nawe kuwa baada ya kujiuzuru UWAZIRI, aende zake kwa kuachia UBUNGE na vyeo lukuki alivyo navyo kwenye CCM, na akienda kwa wapiga kura wake Bariadi wakampe wakati mgumu ajue Tanzania ya leo si ya mwaka 1960. Ninatamani sana kumuhimiza mgosi MAKAMBA kusoma hiyo mada ili aweze kukishauri chama chake kichukue hatua madhubuti kujisafisha mbele ya Watanzania na hatimaye kiondokane na ufisadi.

Asante OGAH kwa uchambuzi wako kuhusu huyu CHENGE kukejeli WASUKUMA inasikitisha sana. Licha ya kwamba Kiswahili kimeanzia na kinaongewa sana Pwani, si kweli kwamba Wasukuma hawajui gramar ya Kiswahili kiasi hicho ati waanze kubwabwaja VIJISETI badala ya senti, VIJITOTO badala ya watoto, VIJIMAMBO badala ya mambo. Huyu mtu alipoongea VIJISENTI alikuwa anajua anaongea nini kwani alipoulizwa kwa nini bilioni anaiita VIJISENTI alijibu na kusema KILA MTU ANA VIWANGO VYAKE. Siju kama ni kweli alikuwa amesha-panick tayari au ni ile jeuri ya pesa / ubilionare ndiyo ilimpa nguvu ya kutamka hayo. Ninavyowafahamu Wasukuma ni kuwa wakiongea kitu kwa msisitizo wanatanguliza MA na hivyo angesema MASENTI tungemuelewa. Nawasilisha
Huyo Makamba ndio usimtaje kabisa, nadhani inabidi akariri maneno "no comments" kuliko majibu aliyowapa waandishi wa habari kwamba ccm inashughulikia mambo mengine sio Chenge(ufisadi) na uwaziri ulikuwa kazi yake(Chenge) na watoto wake? Huyo alikuwa mkuu wa mkoa na ni katibu mkuu wa ccm. kama Chenge asingekuwa mbunge wa ccm asingekuwa waziri na asingejua ujumbe wa NEC ni nini? kwa kuwa ni mmoja wao, ni shughuli yao pia . Kama walikuwa hawajalijua hilo basi tuwasaidie. Unajua hawa viongozi wa Tanzania wanafikiri kuwa wako juu ya kila mtu na wana haki ya kumtendea na kumjibu mtu yeyote kama watakavyo.
 
Na yule aliyesema hata ikibidi watu kula nyasi ili ndege ya raisi inunuliwe, naye hakuwatukana Watanzania? Lipi ni tusi kubwa...kusema dola milion moja ni visenti au kumwambia mtu kula nyasi (sina nukuu kamili)? Hivi huyo waziri alijiuzulu wadhifa wake serikalini na ubunge aliokuwa nao?

Halafu mimi siamini kabisa kama Kikwete naye yuko safi ingawa ushahidi sina. Lakini kama yuko clueless kabisa na ufisadi unaondelea basi na yeye hastahili kuwa raisi. Ajiuzulu mara moja! Kama anajua kuhusu huo ufisadi na yeye kwa namna moja au nyingine anahusika nao halafu anaendelea kuwateua mafisadi ktk nyadhifa kubwa serikalini basi judgement yake ni mbovu na hilo pekee linatosha kwa yeye kubwaga manyanga chini. We just can't have a head of state whose judgement is grossly flawed. Let's have same standards for everyone.

POINT!!!!!
 
tatizo ni la CCM ya leo, tumeingiliwa na Mafia ambao kazi yao ni Ufisadi tu, nothing else. Ufisadi ulikuwepo before but not to these levels whereby these guys feel untouchable. It is a gang of select people that needs to be weeded out. kusema CCM nzima ni wafisadi isnt true


Unajua mwanahabari tatizo liko wapi, CCM kilikuwa chama cha wakulima na wafanyakazi wa Tanzania, vijana, wazazi, wanawake - yaani watanzania wote, ijapo tulilazimishwa uanachama wakati ule.

lakini hapo katikati kimegeuka. kinakumbatia matajiri, wafanyabiashara, tena bila kuchagua wala kuchuja. kilikumbatia hata rushwa - kwa kuiita TAKRIMA. sasa hapo kikaacha kuwa chama cha walio wengi kikawa cha matajiri. na hawa CCM iliwakubali nadhani sababu mojawapo ni kwamba baada ya kuruhusu na kurasimisha rushwa, unahitaji watu wenye uwezo wa kuitoa ndio wawe wagombea. sasa CCM imekubwa ikijivunia ushindi wa kishindo, katika mazingira kama haya. CCM imeacha kutetea wakulima na kilimo, kinakumbatia MAFISADI ambao wanaweza kugharimia uchaguzi, na hivyo inabidi wapewe nafasi warejeshe gharama walizotumia.

Sasa kama wanaCCM wenyewe wameruhusu hili, basi chama chote kimeoza. Naam, Mwanahabari, CCM kinahitaji ukombozi, wana CCM wenyewe walio wengi, wakirejeshe chama chao kwa wafanyakazi na wakulima. hii washirikiane na wapiganaji. wakiendelea kupiga makofi tu, hawana haki ya kudai CCM kina chembe ya usafi
 
Sasa usishangae watu wa Bariadi wakaandamana kumuunga mkono mbunge wao kama walivyofanya watu wa Monduli.

Unajua ambacho nimejifunza kutokana na mkutano wa juzi pale London ni kwamba pengine sisi hapa JF tunaona mambo kwa jicho tofauti sana na watanzania wengine. Yaani pale ilikuwa kama vile mambo Tanzania ni shwari kabisa; tena habari za akina Chenge hazikuonekana kama ni issue. Na kuna afisa moja wa serikali mkubwa sana alinifuata akaniambia hivi nyie mnaona mtu kuwa na $1m ni issue kweli, hiyo mbona ni pesa kidogo sana? So the question is, are we (JF) out of touch with the rest of Tanzanians?

Hiyo ndiyo kete ambayo bado serikali ya CCM inaitegemea sana, kwamba watanzania walio wengi huko vijijini bado ni mbumbumbu, bado wataendelea kuipigia kura CCM. Hii ndio challenge kubwa ambayo wapambanaji, vyama vya upinzani, na wengine wote wanaoitakia mema Tanzania, ikiwemo JF, (pamoja na CCM ORIGINAL) inabidi kukabiliana nayo.

Lakini kuna dalili njema. Mfano kufuatia sakata la Zitto kusimamishwa ubunge, na ziara za viongozi wa vyama vya upinzani huko vijijini, mwamko uliooneshwa na watu, wa kuonesha upinzani wa wazi kwa sera za serikali ya CCM, unaonesha kwamba kuna hali ya watu kufuatilia kwa karibu. kazi kubwa imefanywa na CCM katika kumomonyoa goodwill yake yenyewe kwa wananchi. Hali ngumu ya maisha ikijumlishwa na kashfa hizi mfululizo, inatoa mwanya kwa walio wengi kutambua hali halisi ikoje. hii ni dalili nzuri na one must build on that.

Lakini challenge iko pale pale, watu walio wengi wanafikiwa namna gani?

kitu kingine kinasumbua watu ni umaskini. Chenge akirusha rundo la noti hewani, wengi watasahau kashfa zake na kuanza kugombea hizo noti, and he can afford to throw around quite a bit of it. lakini kuelimisha watu, kuanzisha mijadala ngazi ya chini, ndio challenge kubwa, maana unahitaji angalau basi hao maskini wawe MASKINI JEURI.
 
Na yule aliyesema hata ikibidi watu kula nyasi ili ndege ya raisi inunuliwe, naye hakuwatukana Watanzania? Lipi ni tusi kubwa...kusema dola milion moja ni visenti au kumwambia mtu kula nyasi (sina nukuu kamili)? Hivi huyo waziri alijiuzulu wadhifa wake serikalini na ubunge aliokuwa nao?

Kelele zilipigwa sana kuhusu huyu jamaa, hasa na vyombo vya habari rasmi. uzuri ni kwamba sasa hivi kuna mabadiliko makubwa na watu wengi wana njia nyingi za kuwasilisha ujumbe. siku hizi hata Sitta hawezi kudharau "taarifa za kwenye Internet". kuna vyombo huru zaidi sasa na pia mazingira ya sasa ni tofauti kidogo.

sasa hili sijui nisemeje maana inaonekana, frankly, kama vile Kikwete is softer kuliko Mkapa? Mkapa alikuwa anasema tena kwa ukali: no salary rise! "hatulipi ng'o" semi zake ingawa zilijibiwa kwa kiasi fulani, ni kama ali-discourage watu kumwandama hasa. na pengine watanzania wengi ni waoga? Kikwete anafuatilia taarifa za vyombo vya habari na anarespond somehow. hii inafanya watu wawe bolder. hata system nyingi katika serikali zimekuwa bolder kuliko zamani. Pengine pia kuna mchango wa hizo factor zingine - sina hakika hapo
 
Kama kawaida yao, baada ya kujiuzulu atakwenda jimboni mwake kujitetea jinsi 'alivyoonewa' na baada ya hapo atatumia 'vijisenti' vyake kujisafisha kupitia vyombo vy habari vya Bongo.

Huyooo anakwenda 'kujisafisha' baada ya hapo tutaambiwa eti watu wa mkoa wa shinyanga wanapigwa vita!

Mwanasiasa anayetuhumiwa kwa ufisadi aanza ziara ya kujisafisha nyumani kwao
Na Mwandishi Wetu, Mwanza

BAADA ya kukumbwa na tuhuma nzito za ufisadi, Andrew Chenge, sasa ameamua kwenda jimboni kwake Bariadi Magharibi, kujisafisha kwa wapigakura wake.

Mtindo kama huo ulitumiwa pia na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ambaye baada ya kujiuzulu katika mkutano wa 10 wa Bunge la Februari alikwenda jimboni kwake Monduli ambapo alipokewa na watu na magari mengi, kitendo ambacho kilitafsiriwa kuwa alikuwa anajisafisha kutokana na kashfa ya Richmond.

Ziara hiyo ya Chenge kwenda jimboni ni ya kwanza tangu aanze kuchunguzwa na makachero wa Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza ya Serious Fraud Office (SFO).

Uamuzi huo wa Chenge pia kufanya ziara jimboni kwake umekuja ikiwa ni wiki moja baada ya kuzushiwa kifo.

Habari zilizopatikana kutoka jijini hapa zilisema Chenge alitarajiwa kuwasili Bariadi jana usiku akitokea Mwanza.

Taarifa hizo ziliongeza kwamba, Chenge ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu baada ya kukutwa na Sh1.2 bilioni katika akaunti yake katika kisiwani Jersey, zinazohusishwa na biashara ya kifisadi ya rada, pia atawaeleza wananchi wake sababu za kujiuzulu kwake.

"Tumemwandalia mapokezi makubwa, kwanza ni kwa ajili ya kuja kuwathibitishia wapigakura wake kuwa yuko hai, kutokana na uzushi kuwa amefariki dunia," kilisema chanzo hicho na kuongeza:

"Lakini pia kuwaeleza wapigakura wake watapenda kujua sababu ya yeye kujiuzulu kwake, maana yamekuwa yakisemwa mambo mengi,� alieleza msemaji mmoja kutoka Bariadi ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Habari zaidi zilieleza kwamba, Chenge atakwenda katika jimbo hilo ambako baadhi ya watu wanaojiita wafuasi wake wamemwandalia mapokezi makubwa ya kumsafisha na tuhuma za ufisadi zinazomkabili.

Hata hivyo, pamoja na kuandaliwa maandamano hayo, huenda yakageuka mwiba mchungu kwake kwa kuzomewa kwani eneo hilo ni ngome ya chama cha upinzani cha United Democratic (UDP).

Mara baada ya Chenge kujiuzulu, wananchi wa jimbo hilo waliandaa maandamano ya kumpongeza kuachia ngazi kwake. Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kuwa, Chenge bado anakabiliwa na wakati mgumu kuweza kujisafisha, kutokana na tuhuma za ufisadi zinazomkabili kuwa kubwa.

Chenge mbali ya kukabiliwa na tuhuma za kujipatia mabilioni hayo ya pesa kwa njia ya rada, pia anatuhumiwa kuiingiza nchi katika mikataba mibovu.

Miongoni mwa mikataba mibovu inayohujumu uchumi wa nchi hadi leo, ambayo Chenge alishiriki ama kutia saini au kushauri akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ni pamoja na Kampuni ya Uzalishaji Umeme ya IPTL, mabilioni ya Kampuni ya Tangold na mengineyo.

Chenge pia katika ziara hiyo atakabiliwa na wakati mgumu kutokana na uamuzi wake wa kuziita Sh bilioni 1.2 alizoficha Jersey kuwa ni 'vijisenti', wakati jimboni kwake, baadhi ya wapigakura hawana huduma za maji safi na salama, uhaba wa huduma bora za kijamii kama afya na elimu.

Hadi sasa uchunguzi dhidi ya tuhuma za Chenge kuhusiana na Sh1.2 bilioni zinazohusishwa na rada, umebaki wiki mbili kukamilika.

Lengo la makachero wa SFO ni kuona kama fedha hizo zinahusiana na kutoa kashfa ya ununuzi wa rada inayodaiwa kununuliwa kwa bei kubwa zaidi ya uwezo na ubora wake.

SOURCE: Mwananchi
 
Back
Top Bottom