Umuhimu wa digirii ni ofisini kwako tuu. Na tena ubahatike uwe na ofisi dizaini ya zenye viyoyozi za walioajiriwa, lakini kama ni zile zetu tuliojiajiri penda usipende utakujajifunza mbinu kwa waso digirii vingenevyo unapotezwa kwenye gemu. Uliza digirii wenzio. Digirii sio mali kama mnavodhani. Si tunaona watu na madigirii yao wanavyoingizwa mjini na madalali hapa? Wanaume na madigirii yao wanaingizwa kingi wanarudi hapa na hadithi za mawakili sijui polisi sijui takataka gani bado inakula kwao, ngumbaru wanapeta! Hapo nimezungumzia wanaume, sa unategemea mwanamke anayejivunia digirii kitampata nini kama si majanga tu? Mwanamke ka una digirii katambe nazo huko kwenye makongamano upigiwe makofi, lakini huku pande za kitaa ni manundu tu kwa kwenda mbele, yakikuuma sana pitia supermarket nunua wine ukanywee nyumbani ulewe ikuondoke haya ya kumpigia dereva toyo.