Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

I thnk wanaweza ungana na kuipga familia ya bupe kama wakiangaliziwa na kuujua ukweli
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-24

ILIPOISHIA:
Wapo waliosema hizo ndizo dalili za maisha anayokwenda kuishi kwa vile ubaya ndiyo uliomzunguka kuliko mema katika maisha yake. Kwa hiyo picha ya maisha ya kuzimu ilijionesha mapema. Wakiwa wanasubiri vijana wamalizie kuchimba, ghafla walisika sauti ya kushtusha.
“Jamani chini tunapochimba kunatoka maji.”
“Maji?” Watu walishtuka, “ Tena yanatoka kwa wingi kama kumepasua bomba.”
SASA ENDELEA...


“
Makubwa, tokea lini maeneo haya yakawa na chemchem, mbona leo mauzauza kwenye kaburi la bibi?”
“Sasa tutafanyaje tumzike hivyohivyo au tuchimbe lingine?”
“Tukichimba lingine yanaweza kutokea hayahaya.”
“Hapana tuchimbe kaburi lingine hatuwezi kumzika binadamu mwenzetu kwenye maji, bado thamani yake ni kubwa kwetu. Huyu alikuwa bibi wa kijiji nani ambaye alikwenda kwake hakupata msaada japo kuna maneno ya kijinga juu yake. Lakini lazima tumpe heshima yake,” alisema mzee Mwangibile aliyekuwa mzee wa kijiji.
Vijana kwa shingo upande waliingia tena kwenye kazi ya kuchimba kaburi la tatu, muda nao ulikuwa unakatika, kigiza nacho kilianza kuingia. Lakini watu waliendelea kuwepo makaburini mpaka wamzike bibi. Shughuli ya kuchimba iliendelea kwa dakika ishirini kaburi lilikuwa tayari.
Ajabu lilikuwa katika hali ya kawaida tofauti na yaliyotangulia na kumfanya mzee Mwangibile kuuliza.
“Sasa kipo wapi mbona kaburi limeisha vizuri?”
“Mzee usiseme hivyo, subiri tuzike kwanza.”
“Hakuna kitu kitakacho tokea.”
Baada kumaliza kuchimba waliochaguliwa mwanzo waliingia tena kaburini ili kupokea mwili wa bibi Tumwambilile. Wakati wakijiandaa kuupokea mara walishtuka kusikia vitu vikiwatembea miguuni, walipoangalia waliona lundo la siafu ambao walianza kuwapandia miguuni na kufanya watoke huku wakijikung’uta.
Baada ya kutoka ndani ya kaburi waliangalia tena na kukuta siafu wamejazana na kuzidi kuwashtua watu na kujiuliza hali ile inatokana na nini.
Mmoja alitoa wazo waitwe wataalamu wa asili waangalie tatizo ni nini.
Bahati mganga Kagugu alikuwa amefika muda mfupi, alisogea kwenye makaburi yote na kuyatizama kwa muda na kuchukua mchanga uliochimbwa na kuutupia ndani ya kaburi kisha alisema:
“Zikeni kaburi lolote hakuna kitu.”
“Kwa nini unasema hakuna kitu wakati kila kaburi lina mauzauza yake?”
“Nimesema zikeni hakuna kitu chochote, yote yale ni kiini macho tu hakuna nyoka, maji wala siafu.”
Walibeba mwili wa bibi Tumwambilile na kuuzika bila tatizo lolote na kurudi nyumbani wakati giza lilikuwa limeshaingia.
Njiani kila mtu alisema yake huku wengine wakijiuliza kama ni kiini macho kimeonekana kwa ajili gani. Tukio lile lilikuwa gumzo kijijini pale na kushangaza wiki ile kuwa ya mauzauza huku wengine wakijiuliza nini kitatokea kwenye mazishi ya Atuganile na kisha Ambakisye.
Siku ya pili kulikuwa na mazishi ya Atuganile, kama kawaida wanakijiji walikusanyika nyumbani kwa Andendekisye kwa ajili ya mazishi. Wakati watu wakiwa msibani mzee Andendekisye alisema kwa sauti kuwa hataki kumuona Amangise kwenye msiba wa mwanaye na akimuona atamkata mapanga.
Hakuna aliyemsemesha kitu kwa vile waliogopa kuingia kwenye ugomvi usiowahusu.
Muda ulipotimu ilifanyika ibada ya kumsalia maiti iliyoongozwa na Padri Thomas Mayunga iliyochukua zaidi ya saa nzima na zoezi la kuuaga mwili wa marehemu lilianza. Zoezi la kuaga lilipoisha, watu waliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka katika makaburi ya Wakristo.
Walipoufisha mwili makaburini ilifanyika ibada nyingine ya kulibariki kaburi na zoezi la kuteremsha jeneza kaburini lilianza kwa watu kuingiza jeneza kwa kamba. Jeneza baada ya kuteremshwa kaburini na kutolewa kamba, ilifanyika misa ya mwisho kabla ya kuzika.
Padri alifungua kitabu cha sala kusoma ibada ya wafu kisha alichukua udongo na kuutupia kwenye jeneza na kusema:
“Ulitoka mavumbini na mavumbini utarudi.”
Kisha alichukua chetezo chenye uvumba na kupitisha kaburini alipomaliza alichukua maji ya baraka na kuanza kunyunyizia kwenye jeneza (sanduku) huku watu wakiwa wametulia kusikiliza ibada ile.
“Ulibatizwa kwa maji...”
Wakati akinyunyiza maji, ghafla walisikia mtikisiko ndani ya jeneza kama kuna kitu kilicho hai, hali iliyomfanya padri asite kuendelea na ibada na kusababisha watu kusogea kaburini wengine wakiamini Atuganile amefufuka.
Hakuna aliyeweza kuingia kaburini, wote walibakia kimya wakiendelea kusikiliza vurugu zilizokuwa ndani ya jeneza ambazo zilikuwa kubwa.
Wakati watu wakiwa katika wasiwasi, ghafla jeneza lilipasuka na kutokea bonge la mamba likiwa na pande la nyama mdomoni na kufanya watu wote wapige kelele za woga na kutimua mbio. Yule mamba hakushtuka alimalizia kukimeza kipande cha nyama kilichokuwa mdomoni na kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Ndani ya jeneza kulikuwa kumejaa damu lakini mwili wa Atuganile haukuonekana, ilionekana kama yule mamba ndiye aliyemla.
Lakini walijiuliza ameingia muda gani na kuweza kumtafuna kwa muda mfupi wakati wakiaga mwili wa marehemu hawakuona kitu chochote?
Watu wote makaburini walipagawa na kuzidi kuona maajabu kwa wiki nzima toka vifo vyao mpaka mazishi yao. Baada ya muda hali ilitulia huku kila mmoja akiogopa kusogea kaburini kutokana ha hali iliyojitokeza. Wakati wa tukio la kupasuka jeneza, mganga Kagugu alipatwa na mshtuko wa ghafla na kuanguka chini na kupoteza fahamu.
Alirudiwa na fahamu baada ya tukio kutulia alipoombwa kwenda kwenye kaburi akaangalie kumetokea nini, alikataa kwa kuhofia maisha yake. Ilionekana uchawi uliotumika pale ulikuwa mkubwa kuliko uwezo wa nguvu zake za kiganga.
Mzee Andendekisye na mkewe walipagawa na kumshtumu moja kwa moja kwa sauti kuwa Amangise baba wa Ambakisye ndiye aliyefanya vile na kuapa kula naye sahani moja.
Alijikuta akisema kwa sauti na kujisahau kuwa yupo mbele za watu.
“Wewe si umefanya hivi basi moto utakuwakia, nimeanza na mtoto, sasa nafagia ukoo mzima.”

Itaendelea Kesho............
 
Hatobaki hata panya kwenye hizo nyumba mbili!
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-25

ILIPOISHIA:
Alirudiwa na fahamu baada ya tukio kutulia, alipoombwa kwenda kwenye kaburi akaangalie kumetokea nini alikataa kwa kuhofia maisha yake. Ilionekana uchawi uliotumika pale ulikuwa mkubwa kuliko uwezo wa nguvu zake za kiganga.
Mzee Andendekisye na mkewe walipagawa na kumshtumu moja kwa moja kwa sauti kuwa Amangise baba wa Ambakisye ndiye aliyefanya vile na kuapa kula naye sahani moja. Alijikuta akisema kwa sauti na kujisahau yupo mbele za watu.
“Wewe si umefanya hivi basi moto utakuwakia, nimeanza na mtoto sasa nafagia ukoo mzima.”
SASA ENDELEA...


Kauli ile ilifanya watu wote makaburini wagune na kuanza kunong’ona chinichini kuonesha kumbe yeye ndiye muhusika wa kifo cha Ambakisye mpenzi wa mwanaye. Walijiuliza alifanya vile ili iweje na kujiuliza kama aliyefanya yake makaburini ni Amangise amefanya kwa faida gani. Wapo waliojiuliza anajiamini nini kusema hadharani yeye ndiye kamuua Ambakisye.
Kwa vile ndani ya kaburi hakukuwa na kitu zaidi ya jeneza lililoloa damu walishindwa kuzika. Baadhi ya watu waliamua kutoka makaburini kukiwa na sintofahamu huku mzee Andendekisye na mkewe wakisema hawatoki makaburini mpaka wamuone mtoto wao.
Wazee wa kijiji ilibidi waitane pembeni ili kutatua tatizo lile, mmoja alitoa wazo wamfuate mtaalamu kijiji cha Mbako kabla giza halijaingia ili wajue hatima ya mwili wa Atuganile ni nini kwani ilikuwa wiki ya miujiza. Walitumwa vijana na baiskeli kwenda kijiji cha Mbako kumfuata mtaalam.
Kukiwa na sintofahamu baadhi ya watu waliotoka makaburini mtu wa karibu na Amangise walikwenda kumwambia maneno aliyosema Andendekisye makaburini baada ya tukio la kushangaza na kutisha katika kaburi la Atuganile. Baada ya kumsikiliza alisema kwa masikitiko.
“Hivi mimi nimuue Atuganile ili iweje?”
“Basi mwenzako anatamba kamuanza mtoto, sasa anahamishia majeshi kwenu na atahakikisha unaufagia ukoo mzima.”
“Unasema watu wote msibani wamesikia?”
“Ndiyo, yaani namshangaa sana jamaa yule kujisifia kwamba kamuua Ambakisye kwa vile wewe ulimuua mwanaye na pia wewe ndiye uliyetuma mamba kumla mwanaye makaburini.”
“Kwa kweli Mungu ndiye anayejua kama mimi ndiye niliyetia mkono kumuua Atuganile atanihukumu. Ni kweli mwanangu nilimtafutia mchumba baada ya siku moja kwenda Kilasilo na kumuona mtoto wa Ambokile, Bupe.
“Kwa kweli binti wa Ambokile alinivutia kwa heshima aliyonionesha na kupenda awe mkwe wangu. Nilizungumza na wazazi wake wakanikubalia na kuanza mipango ya kuoa mara moja. Ni kweli nilikuwa najua mwanangu ana uhusiano na mtoto wa Andendekisye lakini hakuna hata siku moja mwanangu alinieleza kuwa anataka kumuoa.
“Tumeona watoto wangapi wanaanzisha uhusiano na baadaye kila mtu kufanya mambo yake. Kama mzazi niliamini nilitakiwa kumtafutia mwanangu mke bora hasa kwa historia ya familia yake na yeye mwenyewe. Bupe alikuwa binti ambaye kila mmoja anamsifia kama mzazi unataka nini kama una mtoto wa kiume si kumtafutia amuoe.”
‘Ni kweli.”
“Basi nilianza maandalizi na kupeleka posa kisha nilimbeba mwanangu kwenda Kilasilo kuonana na mchumba wake. Ni kweli mwanangu alishtuka kusikia nimemtafuta mwanamke mwingine wakati ana mpenzi wake. Nilimweleza sikuwa na lawama kwa vile sikuona malengo yao.
“Kibaya zaidi wakati huo Atuganile alikuwa na ujauzito ambao baadaye kwa bahati mbaya ulitoka. Hapo ndipo wenzetu wakasema tumeutoa na kuanzisha vita ya kishirikina iliyopelekea kumuua mwanangu bila kosa,” mzee Amangise alijitetea kwa uongo wenye ukweli kidogo.
“Sasa ndugu yangu akumulikae mchana usiku anakuchoma, kama ulikuwa hujui basi kamuanza mwanao sasa mnafuata wenyewe. Kwa hiyo liwahi neno kabla halijadondoka chini.”
“Itabidi niondoke baada ya mazishi ya mwanangu ili niwawahi kabla hajaniwahi.”
“Wewe Amangise, uzembe wako ndiyo uliofanya umpoteze mwanao. Mwenzio kajipanga wewe unafanya mchezo. Sasa tegemea kumpoteza mkeo kisha wewe mwenyewe,” Amangise alipewa tahadhari.
“Sasa nitafanyaje wakati unajua siwezi kutoka kabla ya mazishi ya mwanangu, unafikiri watu si wataamini maneno ya Andendekisye kuwa mimi mwanga na pengine mkewe au yeye afe jamii itanielewa vipi ikiwa tayari kanipaka kinyesi masikioni kwa watu kuwa nimemuua mwanaye.”
“Kwani unataka kwenda wapi?”
“Kalonga.”
“Huko si Malawi?”
“Ndiyo kuna rafiki yangu mtaalam wa mambo haya.”
“Unajua ninyi ndiyo mnaofanya kuonekane Tanzania hakuna watu wa kuweza kuwadhibiti watu kama hawa mpaka Malawi, kila mtu utamsikia amevuka mipaka wakati humuhumu ndani kuna watu wakali kuliko hao mnaowafungia safari.”
“Wengi watu wa hapa wanatibu hawawezi kulipua mabomu.”
“Kweli umechanganyikiwa, nani alimrudisha mtoto wa Mwakasege.”
“Ooh! Nilimsahau yule kijana.”
“Basi yule kijana kazi yake ni kulinda na kutega bomu mtu akitaka kukufanyia kitu kibaya linamlipukia.”
“Mi sitaki la kujilinda tu bali kulipa kisasi kwa kifo cha mwanangu kwa vile sihusiki chochote kwenye kifo cha mtu.”
“Hiyo vita lazima akirudisha linakupata, siku zote kilio cha kuonewa husikilizwa kuliko kujilinda mwenyewe.”
“Jirani moyo haunipi kujikinga tu kwani nitakuwa nimemuogopa wakati kaniulia mwanangu bila kosa.”
“Nataka kukueleza kitu dawa ya huyo kijana ni zaidi ya kuloga, kwa vile ameahidi kufyeka familia yako. Ukishajizindika akija kukumaliza anajimaliza mwenyewe hata watu wakienda kwa waganga kuangalia atakuwa amejimaliza mwenyewe.”
“Una uhakika moto utamuwakia?”
“Nina imani jamaa nilivyo mjua lazima usiku wa leo atasafiri kwa vile kabla ya mazishi ya mwanaye alisafiri na inaonekana majibu ni kifo cha mwanao.”
“Basi nipeleke.”
“Nitakupeleka, yaani jamaa sijui anajiamini nini kwa kusema kuwa kamuua Ambakisye?” jirani wa Amangise alisema kwa masikitiko.
“Anajivunia uchawi wake, aliua nguvu za kiume za mwanangu eti kwa vile anataka kuoa mwanamke mwingine tofauti na mwanaye.”
“Wewee!” jirani alishtuka.
“Yaani nimemvumilia vya kutosha sasa too much.”
“Sikiliza jirani usimfanye lolote wewe twende huko jibu utaniambia.”
“Nitafanya hivyo japo nilitaka tupambane kwa uchawi tuone nani zaidi.”
Majira ya saa mbili usiku Amangise aliondoka msibani na kuwaacha watu wakiombeleza na kupanda baiskeli kuelekea kijiji cha jirani ambako alikuwepo mganga kijana ambaye hakuwa mwenyeji wa mkoa ule. Walikwenda kwa saa moja mpaka kwenye kijiji hicho.
Bahati nzuri walikuta mganga amerudi jioni ya siku ile toka Mbeya mjini alipokwenda kufanya kazi zake. Walipofika aliwapokea na kuwasikiliza shida zao. Jirani wa Amangise ndiye alikuwa mzungumzaji mkuu na kueleza kilichowapeleka pale.Mganga alikuwa kijana mdogo sana, baada ya kuangalia rada zake alitikisa kichwa na kusema:


Itaendelea Kesho....
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-25

ILIPOISHIA:
Alirudiwa na fahamu baada ya tukio kutulia, alipoombwa kwenda kwenye kaburi akaangalie kumetokea nini alikataa kwa kuhofia maisha yake. Ilionekana uchawi uliotumika pale ulikuwa mkubwa kuliko uwezo wa nguvu zake za kiganga.

Mzee Andendekisye na mkewe walipagawa na kumshtumu moja kwa moja kwa sauti kuwa Amangise baba wa Ambakisye ndiye aliyefanya vile na kuapa kula naye sahani moja. Alijikuta akisema kwa sauti na kujisahau yupo mbele za watu.
“Wewe si umefanya hivi basi moto utakuwakia, nimeanza na mtoto sasa nafagia ukoo mzima.”
SASA ENDELEA...


Kauli ile ilifanya watu wote makaburini wagune na kuanza kunong’ona chinichini kuonesha kumbe yeye ndiye muhusika wa kifo cha Ambakisye mpenzi wa mwanaye. Walijiuliza alifanya vile ili iweje na kujiuliza kama aliyefanya yake makaburini ni Amangise amefanya kwa faida gani. Wapo waliojiuliza anajiamini nini kusema hadharani yeye ndiye kamuua Ambakisye.

Kwa vile ndani ya kaburi hakukuwa na kitu zaidi ya jeneza lililoloa damu walishindwa kuzika. Baadhi ya watu waliamua kutoka makaburini kukiwa na sintofahamu huku mzee Andendekisye na mkewe wakisema hawatoki makaburini mpaka wamuone mtoto wao.
Wazee wa kijiji ilibidi waitane pembeni ili kutatua tatizo lile, mmoja alitoa wazo wamfuate mtaalamu kijiji cha Mbako kabla giza halijaingia ili wajue hatima ya mwili wa Atuganile ni nini kwani ilikuwa wiki ya miujiza. Walitumwa vijana na baiskeli kwenda kijiji cha Mbako kumfuata mtaalam.
Kukiwa na sintofahamu baadhi ya watu waliotoka makaburini mtu wa karibu na Amangise walikwenda kumwambia maneno aliyosema Andendekisye makaburini baada ya tukio la kushangaza na kutisha katika kaburi la Atuganile. Baada ya kumsikiliza alisema kwa masikitiko.
“Hivi mimi nimuue Atuganile ili iweje?”
“Basi mwenzako anatamba kamuanza mtoto, sasa anahamishia majeshi kwenu na atahakikisha unaufagia ukoo mzima.”

“Unasema watu wote msibani wamesikia?”
“Ndiyo, yaani namshangaa sana jamaa yule kujisifia kwamba kamuua Ambakisye kwa vile wewe ulimuua mwanaye na pia wewe ndiye uliyetuma mamba kumla mwanaye makaburini.”
“Kwa kweli Mungu ndiye anayejua kama mimi ndiye niliyetia mkono kumuua Atuganile atanihukumu. Ni kweli mwanangu nilimtafutia mchumba baada ya siku moja kwenda Kilasilo na kumuona mtoto wa Ambokile, Bupe.

“Kwa kweli binti wa Ambokile alinivutia kwa heshima aliyonionesha na kupenda awe mkwe wangu. Nilizungumza na wazazi wake wakanikubalia na kuanza mipango ya kuoa mara moja. Ni kweli nilikuwa najua mwanangu ana uhusiano na mtoto wa Andendekisye lakini hakuna hata siku moja mwanangu alinieleza kuwa anataka kumuoa.
“Tumeona watoto wangapi wanaanzisha uhusiano na baadaye kila mtu kufanya mambo yake. Kama mzazi niliamini nilitakiwa kumtafutia mwanangu mke bora hasa kwa historia ya familia yake na yeye mwenyewe. Bupe alikuwa binti ambaye kila mmoja anamsifia kama mzazi unataka nini kama una mtoto wa kiume si kumtafutia amuoe.”
‘Ni kweli.”

“Basi nilianza maandalizi na kupeleka posa kisha nilimbeba mwanangu kwenda Kilasilo kuonana na mchumba wake. Ni kweli mwanangu alishtuka kusikia nimemtafuta mwanamke mwingine wakati ana mpenzi wake. Nilimweleza sikuwa na lawama kwa vile sikuona malengo yao.
“Kibaya zaidi wakati huo Atuganile alikuwa na ujauzito ambao baadaye kwa bahati mbaya ulitoka. Hapo ndipo wenzetu wakasema tumeutoa na kuanzisha vita ya kishirikina iliyopelekea kumuua mwanangu bila kosa,” mzee Amangise alijitetea kwa uongo wenye ukweli kidogo.
“Sasa ndugu yangu akumulikae mchana usiku anakuchoma, kama ulikuwa hujui basi kamuanza mwanao sasa mnafuata wenyewe. Kwa hiyo liwahi neno kabla halijadondoka chini.”
“Itabidi niondoke baada ya mazishi ya mwanangu ili niwawahi kabla hajaniwahi.”

“Wewe Amangise, uzembe wako ndiyo uliofanya umpoteze mwanao. Mwenzio kajipanga wewe unafanya mchezo. Sasa tegemea kumpoteza mkeo kisha wewe mwenyewe,” Amangise alipewa tahadhari.
“Sasa nitafanyaje wakati unajua siwezi kutoka kabla ya mazishi ya mwanangu, unafikiri watu si wataamini maneno ya Andendekisye kuwa mimi mwanga na pengine mkewe au yeye afe jamii itanielewa vipi ikiwa tayari kanipaka kinyesi masikioni kwa watu kuwa nimemuua mwanaye.”
“Kwani unataka kwenda wapi?”
“Kalonga.”

“Huko si Malawi?”
“Ndiyo kuna rafiki yangu mtaalam wa mambo haya.”
“Unajua ninyi ndiyo mnaofanya kuonekane Tanzania hakuna watu wa kuweza kuwadhibiti watu kama hawa mpaka Malawi, kila mtu utamsikia amevuka mipaka wakati humuhumu ndani kuna watu wakali kuliko hao mnaowafungia safari.”

“Wengi watu wa hapa wanatibu hawawezi kulipua mabomu.”
“Kweli umechanganyikiwa, nani alimrudisha mtoto wa Mwakasege.”
“Ooh! Nilimsahau yule kijana.”

“Basi yule kijana kazi yake ni kulinda na kutega bomu mtu akitaka kukufanyia kitu kibaya linamlipukia.”
“Mi sitaki la kujilinda tu bali kulipa kisasi kwa kifo cha mwanangu kwa vile sihusiki chochote kwenye kifo cha mtu.”

“Hiyo vita lazima akirudisha linakupata, siku zote kilio cha kuonewa husikilizwa kuliko kujilinda mwenyewe.”
“Jirani moyo haunipi kujikinga tu kwani nitakuwa nimemuogopa wakati kaniulia mwanangu bila kosa.”
“Nataka kukueleza kitu dawa ya huyo kijana ni zaidi ya kuloga, kwa vile ameahidi kufyeka familia yako. Ukishajizindika akija kukumaliza anajimaliza mwenyewe hata watu wakienda kwa waganga kuangalia atakuwa amejimaliza mwenyewe.”

“Una uhakika moto utamuwakia?”
“Nina imani jamaa nilivyo mjua lazima usiku wa leo atasafiri kwa vile kabla ya mazishi ya mwanaye alisafiri na inaonekana majibu ni kifo cha mwanao.”
“Basi nipeleke.”

“Nitakupeleka, yaani jamaa sijui anajiamini nini kwa kusema kuwa kamuua Ambakisye?” jirani wa Amangise alisema kwa masikitiko.
“Anajivunia uchawi wake, aliua nguvu za kiume za mwanangu eti kwa vile anataka kuoa mwanamke mwingine tofauti na mwanaye.”
“Wewee!” jirani alishtuka.

“Yaani nimemvumilia vya kutosha sasa too much.”
“Sikiliza jirani usimfanye lolote wewe twende huko jibu utaniambia.”
“Nitafanya hivyo japo nilitaka tupambane kwa uchawi tuone nani zaidi.”
Majira ya saa mbili usiku Amangise aliondoka msibani na kuwaacha watu wakiombeleza na kupanda baiskeli kuelekea kijiji cha jirani ambako alikuwepo mganga kijana ambaye hakuwa mwenyeji wa mkoa ule. Walikwenda kwa saa moja mpaka kwenye kijiji hicho.

Bahati nzuri walikuta mganga amerudi jioni ya siku ile toka Mbeya mjini alipokwenda kufanya kazi zake. Walipofika aliwapokea na kuwasikiliza shida zao. Jirani wa Amangise ndiye alikuwa mzungumzaji mkuu na kueleza kilichowapeleka pale.Mganga alikuwa kijana mdogo sana, baada ya kuangalia rada zake alitikisa kichwa na kusema:
Itaendelea Kesho....
Mzizi mkavu najiunga bando ya bb kwa ajili ya hii story,weka hata part mbili kwa siku plssssssssssssssssssss
 
Very interesting


Sina cha kusema zaid ya kukupa hongera maana sijui ulikuwa unafikiria nini
Binadamu bwana ni very complex. Mtu unaweza ukawa unazungumza naye na ukimwangalia ni wa kawaida sana lakini akiyaandika ayawazayo utashangaa sana! Mwingine unaweza kumwogopa ukimwona kwa mbali unaogopa kama umeona kiumbe cha ajabu sana! Sasa hapa unaweza kukuta MziziMkavu ana kichwa kidogoooo kisichoendana hata na mwili lakini chenye very 'sophisticated brain!' Shikamoo MziziMkavu!!!
 
Last edited by a moderator:
Binadamu bwana ni very complex. Mtu unaweza ukawa unazungumza naye na ukimwangalia ni wa kawaida sana lakini akiyaandika ayawazayo utashangaa sana! Mwingine unaweza kumwogopa ukimwona kwa mbali unaogopa kama umeona kiumbe cha ajabu sana! Sasa hapa unaweza kukuta MziziMkavu ana kichwa kidogoooo kisichoendana hata na mwili lakini chenye very 'sophisticated brain!' Shikamoo MziziMkavu!!!

Ni kweli kabisa usemayo
 
Last edited by a moderator:
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-24

Walipoufisha mwili makaburini ilifanyika ibada nyingine ya kulibariki kaburi na zoezi la kuteremsha jeneza kaburini lilianza kwa watu kuingiza jeneza kwa kamba. Jeneza baada ya kuteremshwa kaburini na kutolewa kamba, ilifanyika misa ya mwisho kabla ya kuzika.
Padri alifungua kitabu cha sala kusoma ibada ya wafu kisha alichukua udongo na kuutupia kwenye jeneza na kusema:
[/FONT][/COLOR]
"Ulitoka mavumbini na mavumbini utarudi."
Kisha alichukua chetezo chenye uvumba na kupitisha kaburini alipomaliza alichukua maji ya baraka na kuanza kunyunyizia kwenye jeneza (sanduku) huku watu wakiwa wametulia kusikiliza ibada ile.
"Ulibatizwa kwa maji..."


Sasa uchawi n Ibada ya Padri wapi na wapi.

Kuchanganya dini na ushirikina.

Huyu Padri kafuata nini hapo!!!!

MmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmHhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-26

ILIPOISHIA:
Mganga alikuwa kijana mdogo sana, baada ya kuangalia ‘rada' zake alitikisa kichwa na kusema:
SASA ENDELEA...


"Hii ni vita kubwa tena kubwa sana ambayo msipotumia busara hakuna atakayebaki, uchawi unaotumika ni mkubwa sana bila sababu ya msingi. Vijana wenu mmewaua bila sababu na kama mngewasikiliza, yote haya yasingetokea. Adui yako anaamini wewe ndiye mhusika kwa vile kuna kitu ulimtendea mwanaye kabla. Lakini kifo cha mwanaye mhusika ni mwingine kabisa.
"Kifo cha mpenzi wa mwanao na yule bibi ni lipizo toka kule ulipotaka kuoa ambao hawakukubali kumpoteza mtoto wao ambaye unajua kifo chake kilivyokuwa, walihangaika na kujua aliyemuua ni nani walipomjua na walirudishia majibu."
"Unataka kuniambia aliyemuua mchumba wa mwanangu ni bibi Tumwambilile na Atuganile?" Amangise aliuliza kwa mshangao.
"Ndiyo waliohusika lakini sababu kubwa ni wewe, kwani alifanya vile ili aolewe na mwanao, msaada mkubwa alifanya yule bibi aliyekuwa mzoefu wa kazi ile."
"Mmh!" Amangise na jirani yake waliguna kusikia taarifa ile.
"Baada ya kufanikiwa kumuua yule binti, mazingira ya kifo chake yalifanya familia ihangaike na kuvuka mipaka. Baada ya kumjua mbaya wao, nao walirudisha mashambulizi. Kombora lililotumwa liliwafikia wakusudiwa tu, lakini mzazi wa mchumba wako alitumia hasira bila kuchunguza na kumuua mwanao bila kosa lolote. Bado dhamira yake ni mbaya sana kwako kuhakikisha anaifuta familia yako na usiku huu ana safari ya mbali ambayo akirudi anataka akute matanga kama alivyofanya kwa mwanao."
"Duh!" Amangise na jirani yake walishika midomo.
"Kuna kitu kimoja kimetokea leo makaburini cha mamba kutokea ndani ya jeneza na jana siafu, maji na nyoka kwenye kaburi la bibi Tumwambilile, vitu vile vinamaanisha nini?" Jirani wa Amangise aliuliza.
"Ule ni uchawi uliotumika kumuua yule binti aliyetaka kuolewa na mwanao, yale ni majibu ya uchawi wao."
"Mbona kuna mganga alisema wazike hakuna kitu, wakati mwanzo katika kaburi la kwanza tuliona nyoka, la pili tuliona maji na la tatu siafu?"
"Alisema tu lakini kwa tabia za yule bibi za kichawi vyote mlivyoviona ndivyo alivyozikwa navyo. Kaburi lake amezikwa na maji, nyoka na siafu si rahisi kwa macho ya kawaida kuona."
"Mmh!" waliguna tena kwa pamoja.
"Na tukio la leo la mamba ni kweli mamba alitokea lakini hakumla mtu kama mlivyoona, ila amechukua baadhi ya viungo kama sehemu za siri na ulimi tu."
"Mungu wangu!" walisema huku wakishika vichwa.
"Hilo ndilo kosa alilolifanya mwenzako, baada ya kifo cha mwanaye japo alijua wewe ni adui yake angefanya uchunguzi kabla ya kuchukua uamuzi mzito wa kutoa roho ya mwanao."
"Sasa mzee wangu tulikuwa tunataka msaada wako," alisema jirani.
"Msaada gani? Kama vita mi siwezi kwa vile nitachukuliwa muda wa kupigana na watu nisio na ugomvi nao. Siku zote vita ya kisasi haina mshindi, kila atakayepigwa atataka kurudisha."
"Sasa wewe utatusaidia vipi?"
"Msaada wangu mkubwa ni kumlinda mzee na mkewe ili baya lolote watakalotupiwa lisiwapate na kila mwenye dhamira mbaya basi imrudie mwenyewe." "Hata huo msaada mkubwa sana kwani jirani yangu amenisihi nisilipe kisasi hata marehemu mwanangu alinieleza kitu hicho kabla ya kufa," alisema Amangise.
"Ni kweli, kwa vile adui yako anajiamini sana kishirikina, wewe jikinge, majibu utakuja kuniambia."
"Sawa."
"Sasa unatakiwa upatiwe kinga na mkeo kwa vile mbaya wenu inaonekana yupo safarini, dhamira yake akirudi asikie matanga kama alivyosikia kwenye msiba wa mwanao."
"Sasa utatusaidiaje nasi tupo msibani hatuwezi kuondoka wote?" Amangise aliuliza.
"Hakuna tatizo, nitakwenda kuifanyia kazi yangu hapohapo kwenu."
"Pia vipi kuhusu mazishi, hakutakuwa na mauzauza kama yaliyotangulia?" jirani wa Amangise aliuliza.
"Hayawezi kuwepo kwa vile marehemu hakujihusisha na uchawi kama wenzake, atazikwa kawaida tu."
Walimchukua mganga mpaka Ibungu na kumpeleka msibani kama watu wengine, kwa vile kulikuwa na hali ya sintofahamu ilijitokeza. Mganga aliomba kufanya kazi yake kutokana na mambo yanayotokea pale kijijini ili kuweka mambo sawa. Alipewa nafasi na kufanya mambo yake sehemu yote kisha aliwafanyia zindiko Amangise na mkewe na kuondoka usiku uleule.
***
Upande wa pili, Mganga toka Mbako alifika Ibungu saa moja na nusu usiku na kwenda makaburini huku baadhi ya watu wenye mioyo migumu wakielekea eneo la makaburini. Mganga alipofika eneo la makaburini alifanya dawa zake na kumwagia kaburini huku akizungumza anayoyajua kisha aliuliza.
"Kuna la ziada?"
"Shida yetu kujua hali iliyojitokeza kama tulivyokueleza," mzee mmoja alimweleza mganga.
"Nimemaliza kazi mliyoniletea, vipi mnaweza kuzika usiku huu au kesho?"
"Kuzika nini?" mzee Andendekisye aliuliza.
"Mwili wa binti yako umo kwenye jeneza kama kawaida ila hauna baadhi ya viungo."
"Huo mwili upo wapi?"
"Ndani ya kaburi, kama kuna watu wenye nguvu waingie ndani kulitoa jeneza nje."
Vijana walikuwepo pale waliogopa kuingia ndani ya kaburi, lakini mganga alitangulia kuingia ndani ya kaburi. Vijana baada ya kumuona mganga ameingia nao waliingia ndani na kushangaa kukuta jeneza lipo kama lilivyowekwa kaburini halikuwa limepasuka.
Walilibeba jeneza kulitoa nje, wakati wanalibeba jeneza lilikuwa na uzito wa mtu kuwemo ndani lakini kwa chini kulikuwa na damu iliyokuwa ikidondoka kutoka ndani ya jeneza. Walilitoa nje ya kaburi na kuliweka pembeni na kusubiri kauli ya mganga yaliyekuwa amesimama pembeni na usinga wake.
Aliomba jeneza lifunguliwe, vijana walilifungua na kuutoa mwili wa Atuganile na kuulaza chini.
Walielezwa wauchunguze kama kweli ni yeye, walitazama kila kona na kukubali ni wenyewe lakini sehemu za siri na mdomoni kulikuwa na damu. Mganga aliwaeleza mwili wa marehemu umetolewa viongo sehemu za siri na ulimi vilikuwa vimechukuliwa.
Mzee Andendekisye aliuliza kama vinaweza kupatikana, mganga alimwambia kupatikana vigumu kwa vile vimepelekwa mbali. Pia mwili ule ulitakiwa kuzikwa usiku uleule kwa vile ungelala ungeharibika na kushindwa kuuzika.
"Kwa hiyo tutafanyaje?"
"Mzikeni na mazishi yake yasilale."

Itaendelea Kesho.......
 
Back
Top Bottom