Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Shikamoo mzizimkavu.
Nipo Mwanza nielekeze nitume sato wakutosha weekends plz.
 
MziziMkavu usiendlee tena,tayri tumeshafahamu story imeisha.
 
nashkuru nkichlwa kuisoma leo nmeiptia vizuuuurr ngoja nsubir next episode
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-27

ILIPOISHIA:Mzee Andendekisye aliuliza kama vinaweza kupatikana, mganga alimwambia kupatikana vigumu kwa vile vimepelekwa mbali. Pia mwili ule ulitakiwa kuzikwa usiku uleule kwa vile ungelala ungeharibika na kushindwa kuuzika.

“Kwa hiyo tutafanyaje?”
“Mzikeni na mazishi yake yasilale.”

SASA ENDELEA...

IlibidI Atuganile azikwe usiku uleule na watu wachache kwa maelezo ya mganga, baada ya mazishi mzee Andendekisye alipanga usiku uleule asafiri na mkewe kurudi Malawi kwa mganga wake ili akamalizia kazi iliyobakia na kuifyeka familia ya Amangise. Ili kupata nafasi ya kuweza kuondoka usiku ule alitangaza hakuna matanga.
Watu walitawanyikia msibani na yeye na mkewe na baadhi ya majirani zake walirudi nyumbani. Lakini baada ya kufika nyumbani waliwaeleza majirani kuwa hawatalala pale, kwa vile walikuwa wamejiandaa walipanda baiskeli na kuwaacha majirani wakirudi majumbani kwao wakiwa wamepigwa na mshangao juu ya mambo ya jirani yao.
Mmoja alisema huenda anakwenda kuyafanya aliyoahidi makaburini kuufuta ukoo wa Amangise. Wapo waliosema kuwa kifo cha Ambakisye kilitokea baada ya kusafiri na kuuacha mwili wa mwanaye ndani na aliporudi majibu yalipatikana kwa kumuangusha kijana mbichi.
Walijiuliza mwisho wao nini katika vita ile ambayo ilionesha imetawaliwa na uchawi. Wazee wa kijiji walipanga baada ya mazishi ya mtoto wa Amangise waitishe kikao ili kuyaweka mambo yale sawa kwani picha iliyokuwa ikijionesha ilikuwa na mwisho mbaya.
Walipotoka kwa Andendekisye walikwenda kwenye msiba wa Ambakisye ambako nako walikuta mtaalamu akifanya mambo yake na kuzidi kuamini kijiji kinapokwenda kina hatari ya kuharibu jamii iliyowazunguka hasa kutokana na heshima ya wazee wale kijijini pale.
Lakini hawakusema kitu waliungana na majirani wengine kwenye msiba.
Wengi walikuwa na wasiwasi huenda na Amangise naye ataondoka usiku ule, lakini haikuwa hivyo baada ya mtaalamu kufanya mambo yake aliondoka na kuacha watu msibani kama kawaida.
Kwa vile usiku ule wazee wote walikuwepo msibani pale, Amangise alitumia nafasi ile kuzungumza nao kuhusu kinachoendelea kijijini na kauli za jirani yake juu yake na vitisho alivyovitoa kwa familia yake. Baada ya kuwapatia pombe, alisimama na kuzungumza na kufanya wote waelekeze masikio kwake.
“Wazee wenzangu na majirani, nina imani kipindi kifupi kumetokea mshtuko kijijini kwetu cha vifo vya watu watatu kwa mpigo, bibi yetu Tumwambilile, mkwe wangu Atuganile na mwanangu Ambakisye. Kwa kweli vifo vyote hivyo vimetingisha Ibungu na vijiji vya jirani kutokana na mazingira yake.
“Na baada ya vifo hivyo kumetokea vitu vya kushangaza kwenye mazishi ya Atuganile na bibi Tumwambilile. Japo mimi sikuwepo kutokana na msiba wa mwanangu.
Nimesikia maneno mengi ya mzazi mwenzangu Andendekisye juu ya kifo cha mwanaye kuwa mimi ndiye niliyemuua pia ametoa maneno mazito kuwa ndiye mhusika wa kifo cha mwanangu ikiwa kulipa kisasi na pia atahamia kwetu. Nimefikiria mengi kuhusiana na kauli ya kuniua mimi na mke wangu.
“Wazee wenzangu naapa tena mbele yenu katika usiku huu kama mimi nilitia mkono kwenye vifo vyote basi Mungu anihukumu nife sasa hivi. Ni kweli tulikuwa na ugomvi wa chinichini kutokana na mimi kumtafutia mke wa kuoa mwanangu wakati tayari walikuwa na uhusiano na mwanaye.
“Kweli ile ilileta mpasuko mkubwa, nakumbuka majuzi mwanangu alikuja na kunieleza tukae chini kumaliza tofauti zetu na kama nisingemsikiliza angeondoka nyumbani. Japokuwa nilikuwa na hasira kwa kitu alichomfanyia mwanangu za kumuua nguvu za kiume ili asioe.
“Nilikubali na kuwa tayari kumrudisha mwanangu Ambakisye kwa mpenzi wake Atuganile, nilikubali kukutana na familia ya Andendekisye ili tumalize tofauti zetu ili wanetu waoane.”
“Samahani mzee mwenzetu, ulisema ulimtafutia mwanao mke Kilasilo, kwa hiyo angeoa wanawake wawili?” mzee mmoja aliuliza baada ya kushindwa kumuelewa.
“Nilisahau kuwaeleza habari za mchumba wa mwanangu wa Kilasilo, wakati tunajiandaa kupanga tarehe ya harusi alitoweka katika mazingira ya kutatanisha baada ya kuchukuliwa na mamba wa kimuujiza.
“Alipatikana baada ya siku mbili akiwa amekufa, hapo niliona ni muda muafaka wa kumsikiliza mwanangu. Lakini upande wa pili bado walikuwa na hasira na sisi. Baada ya kukubaliana na mwanangu tukae chini tumalize tatizo, siwezi kuelezea jinsi nilivyopata mshtuko baada ya kuelezwa kuwa Atuganile amefariki.
“Lakini niliumizwa nilipoelezewa kuwa mimi ndiye niliyemuua Atuganile pamoja na bibi Tumwambilile. Kwa kweli iliniuma sana hasa kutokana na hatua niliyofikia na mwanangu. Siku iliyofuata kulikuwa na mazishi ya mchumba wa mwanangu Kilasilo ambapo ilitubidi twende tukazike ili tuwahi mazishi ya Atuganile na bibi jioni.
“Lakini tukiwa njiani mwanangu alianza kulalamika kichwa na kufanya tusimame, baada ya hapo aliendelea kulalamika kichwa huku akikishika na kusema kinataka kupasuka. Ghafla alianguka chini na kuanza kuzungumza kwa shida na kuniambia anakufa.
“Ila aliniomba kama atakufa basi nisilipe kisasi, nina imani alijua aliyefanya vile ni Andendekisye kwa vile mwanzo alimuua nguvu za kiume. Ghafla sauti ilipotea na kuanza kutokwa damu puani, mdomoni, masikioni, machoni na kufariki mikononi mwangu,” alipofika hapo sauti ilibadilika na kuzungumza kwa huzuni na kufuta machozi ya uchungu na kuondoa kamasi nyembamba.
“Wazee wenzangu kwa kweli nimeumizwa sana tena sana na kifo cha mwanangu halafu kuna mtu anajisifu ndiye kamuua, kwa kosa gani au uhakika gani kama mimi nimemuua mwanaye. Nami kusema ukweli wa Mungu nilichokipanga kukifanya kwa Andendekisye wala nisingemvukia boda kutafuta wachawi ningekwenda kumchinja kama kuku nyumbani kwake kwa mkono.
“Lakini niliheshimu usia wa marehemu mwanangu, nimeamua kumuachia Mungu najua majibu yake yatapatikana hapahapa duniani. Najua wapo wengi wana maswali juu ya mtaalamu aliyekuja hapa. Lazima niseme ukweli mwenzangu katangaza vita na tayari kanichukulia jicho langu, lazima na mimi nijihami lakini si kwa kulipa kisasi bali kujikinga na mashambulizi ya adui yangu.”
“Mi nafikiri suala hili tunatakiwa kulizungumza kwa kuwakutanisha ili tumalize uadui kwa vile hali inayokuja mbele ni mbaya sana,“ alisema mzee John.
“Ni kweli, suala hili hatutakiwi kulifumbia macho kwa vile wote watu wetu hatuwezi kuona mnaumizana tunawatazama,” mwingine alichangia.
“Amangise upo tayari kukutana na mwenzako tuyazungumze?”
“Nipo tayari hata usiku huu ili kesho tukiamka tuanze upya japo kaniulia mwanangu.”
“Mzee Mwakyoma unaweza kwenda kwa Andendekisye kuzungumza naye ili tulizungumze?”
“Nipo tayari, lakini baada ya mazishi Andendekisye na mkewe wameondoka nyumbani kwao na hawakutueleza wanakwenda wapi lakini amesema hakuna matanga na kutufanya wote tuliokuwa msibani kuondoka.”


Itaendelea kesho...............
 
"hakuna matanga na kutufanya wote tuliokuwa msibani kuondoka"
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-28

ILIPOISHIA
“Nipo tayari, lakini baada ya mazishi Andendekisye na mkewe wameondoka nyumbani kwao na hawakutueleza wanakwenda wapi lakini amesema hakuna matanga na kutufanya wote tuliokuwa msibani kuondoka.”
SASA ENDELEA...


“Mmh! Sasa atakuwa amekwenda wapi usiku huu baada ya mazishi?”
“Labda ndiyo amekwenda kuufuta ukoo wangu,” Amangise alisema.
“Basi tumsubiri arudi tuyazungumze.”
“Mtazungumza na nani kama amesafiri na akirudi atakuta mimi na mke wangu tumegeuka mizoga.”
“Kivipi?”
“Si aliondoka baada ya kifo cha mwanaye na aliporudi kakuta mwanangu kawa mzoga.”
“Huenda alisema kwa hasira tu, sidhani kama kuondoka kwake kaenda kufanya hivyo.”
“Mmh! Sawa, kama hakwenda uko atatukuta tutayazungumza nipo tayari hata aletwe mtaalam aseme ukweli wa vifo vyote na kama mimi nahusika nipo tayari kufa. Lakini kama amekwenda na mengine msiache kunizika na mke wangu nina imani tutakufa wote.”
“Amangise nina imani Mungu atawalinda.”
“Ndugu zangu kuyasema haya usiku huu nilitaka kuliweka jambo hili wazi mbele yenu hata kama atakuja leo nitalisema haya mbele yake bila kuacha hata moja,” Amangise alisisitiza kauli yake.
“Tumekusikia mzee mwenzetu, kila kitu tutakifanyia kazi nina imani amani itarudi mioyoni mwenu.”
“Kwangu nimekubali kumpoteza mwanangu tena kwa uhakika wa mdomo wake, lakini ajue amenionea kifo cha mwanaye sihusiki lolote. “
“Tumekuelewa.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda baada ya chakula cha usiku, walikubaliana kuzike kesho yake saa saba mchana. Wapo waliolala msibani na wengine alirudi majumbani ili kujipanga kwa mazishi ya siku ya pili.
***
Andendekise na mkewe waliondoka usiku ule na kufika mpakani saa tano na nusu za usiku. Kama kawaida aliweka sehemu baikeli yake na kuvuka upande wa pili wa nchi ya Malawi ambako alipanda gari mpaka Matipa kwa mtaalamu wake. Alikuta hajalala kwa vile usiku ule alikuwa na kazi ya mteja mmoja naye kutoka Tanzania.
Alipofika alibidi asubiri mpaka saa kumi za usiku ndipo walipokutana na mganga ambaye kwanza alitaka kupata jibu la kazi aliyoifanya.
“Vipi za huko?”
“Mmh! Ni matatizo makubwa.”
Alimuhadithia kilichotokea makaburini siku ya kumzika mwanaye.
“Kama ningejua tungeondoka pamoja, hao washenzi ningewafanya kitu kibaya ambacho hakijawahi kuonekana duniani kote. Ila nitawakomesha waliofanya hivyo, nataka kila mtu akuone kama moto, hakuna wa kukusogelea wala kukugusa.”
“Nitafurahi sana.”
“Vipi kazi yangu?”
“Imekwenda kama ulivyosema, mtu kaanguka.”
“Umeamini mimi si mtu wa maneno bali vitendo?”
“Nimekuamini unatisha ila utatisha zaidi kama utammaliza na yule jamaa.”
“Hakuna tatizo kwangu hiyo kazi ndogo sawa na kunusa na kutoa chafya.”
“Fanya mambo, nataka nikirudi kesho nikute matuta mawili.”
“Hilo limefanikiwa omba jingine.”
“Kama vyote ulivyonifanyia nina imani hiki ni muhimu kuliko vyote.”
“Kipo, nilitee beseni na maji nusu na kisu kikubwa,” mganga alimwita msaidizi wake.
Baada ya muda Kipo alileta beseni lenye maji nusu na kisu cha kuchinjia mbuzi na kuviweka pembeni ya mganga aliyekuwa akichukua dawa kwenye vikopo huku akisema:
“Kipo weka hapo nataka kuwaonesha Watanzania kwamba sisi ndiyo wajukuu wa wachawi tuliorithisha sio wao wa kununua.”
Aliliweka beseni katikati ya Andendekisye na mkewe na kuwauliza:
“Ndani ya beseni hili mnaona nini?”
“Hamna kitu,” walijibu pamoja.
“Mmh! Jamani hata maji hamyaoni?”
“Maji tumeyaona tulidhania kitu kingine.”
“Zaidi ya maji kuna nini?”
“Hakuna kitu.”
“Angalieni vizuri.”
“Hakuna kitu.”
Baada ya kusema vile mganga alichukua kitambaa chekundu na kufunika juu ya beseni kisha alimimina dawa ya maji juu ya kitambaa na kusema maneno ya Kinyasa na kuchukua dawa ya unga na kunyunyiza juu ya kitambaa na kuuliza.
“Mbaya wako anaitwa nani?”
“Andendekise.”
“Na mkewe?”
“Tuntufye.”
Baada ya kutajiwa majina yale aliyarudia huku akinyunyiza dawa ya unga juu ya kitambaa. Alichukua kibuyu kidogo na kukizungusha kwenye beseni huku akiendelea kusema maneno yake. Baada ya muda walisikia ndani ya beseni kama kuna vitu vinacheza. Mganga aliacha kuzungusha kibuyu na kusema:
“Nina imani mambo yamekwenda vizuri mnaweza kufunua.”
“Afunue nani?” Andendekise aliuliza.
“Wewe mwanaume ambaye ndiye utakayeifanya kazi hii.”
Andendekisye alifunua kitambaa na kushtuka baada ya kuona watu wakiwa ndani ya beseni kama sinema.
“Umeona nini?”
“Watu wawili.”
“Unawafahamu?”
“Ndiyo.”
“Nani na nani?”
“Amangise na mkewe.”
“Ni wenyewe?”
“Ndiyo.”
“Hebu shemeji angalia.”
Mke wa Andendekiye alichungulia na kusema:
“Ni wenyewe.”
“Sasa tunafanya kazi moja.”
“Ipi?”
“Iliyowaleta. Hapa ni pigo moja, hakikisha unachoma kwenye moyo.”
“Sawa.”
“Uchawi huu haukopeshi, ukichomoa kisu na mtu kule ameondoka.”

Je, nini kitaendelea? Tukutane jumamosi jioni...
 
Mimi bado sijajua itaushaje nieleze please

miss ngatara
Inaelekea darasani ulikuwa mzembe,au mpiga chabo.
Hapo jiongeze utajuwa tuu,usitafuniwe kila kitu.
Je unakumbuka
666 Nyayo ya kuzimu iliishia wapi?
Basi ndo ivo,unaji tune unajua whre is it ended.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom