Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Magofu hayooooooooooooooooooooooooo!!!!!!!!!!!!!!!

Yanaanza kuonekana, Nyumba ya huyo bibi Tumbwilile haina mtu wa kuishi na yale majoka yake sijui yatakula nini.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-21

ILIPOISHIA:
“Sasa mume wangu tutafanyaje?”
“Labda tumfuate Kigugu nasikia na yeye ni mtaalamu wa mambo haya.”
“Wasi wasi na mwanangu maana sioni dalili zozote za kuwepo mtu hapa.” Mama alisema kwa kukata tamaa.
SASA ENDELEA...

“
Usiseme hivyo jirani.”
Mzee Andendekisye alikwenda kwa mganga Kigugu kumchukua ili aje amtibu mwanaye.
Japo sehemu alipo mganga ilitakiwa baiskeli lakini aliona anachelewa na kuamua kwenda kwa miguu huku akikimbia. Mazingira yale yalimchanganya Ambakisye na kuona heri aondoke na kwenda kuwaeleza familia yake kuwa wamefanikiwa kwa walichokifanya juu ya mpenzi wake.
Alikwenda nyumbani kwao na hasira kwa baba yake na kuapa kufanya kitu ambacho kitakuwa historia kijijini alikuwa tayari kunyongwa kama mpenzi wake atakufa. Alipofika nyumbani kwao hakukuwa na mtu aliamua kuwafuata shamba ili wamueleze jana walizunguza nini na leo yake wamefanya nini. Aliamini kabisa kuwa baba yake ndiye alifanya vile baada ya kifo cha Bupe na kuanza kummaliza bibi Tumwambilile kwa vile ndiyo kimbilio lao.
Alitembea njia nzima huku akilia kwa uchungu na kuichukia familia yake na kujuta kuzaliwa kwenye familia ya viumbe wakatili kama wake.
Mzee Andendeksye pamoja na umri wake mkubwa hakutulia mpaka alipofika nyumbani kwa mganga huku akitweta. Kutokana na kukimbilia umbali mrefu bila kupumzika, aliposimama alianza kusikia vichomi vikali na kizunguzungu. Wasaidizi wa mganga walipojua amechoka kwa vile alikuwa akitweta sana na jasho kumtoka kama maji, walimuacha apumzike kwa muda ili wamuulize.
Kutokana kupatwa na kizunguzungu kikali alianguka chini na kipoteza fahamu, waliingia kazini kumpa huduma ya kurudisha hali yake ya kawaida. Baada ya kupata huduma alipumzika dakika kumi ndipo alipoweza kuzungumza na kuomba kukutana na mganga Kagugu.
Aliingizwa katika chumba cha mganga na kukaa kwenye mkeka.
“Ndiyo mzee wangu unaonekana una jambo zito,” mganga alianza kwa kuuliza.
“Ni kweli hali ya mwanangu ni mbaya sana.”
“Amefanya nini?”
“Ameumwa na nyoka wa mazingara.”
Baada ya kusema vile, mganga alisimama na kutoka nje na kwenda kuangalia jua kwa muda na kurudi ndani.
“Ni kweli kapigwa.”
“Na nani?”
“Hiki ni kisasi.”
“Cha nani?”
“Uchawi umetoka mbali ulivyotumwa ndivyo ulivyorudi.”
“Unamaanisha nini?”
“Aliyepigwa karudisha.”
“Nimeishamjua,” Mzee Andendekisye alijua ni baba Ambakisye ndiye aliyefanya vile baada ya kumpiga mwanaye.
“Sasa mganga utanisaidia nini?”
Mganga alinyanyuka na kutoka tena nje na kuangalia jua kwa muda mrefu kuliko mwanzo na kurudi tena ndani.
Baada ya kukaa kwenye kiti chake alitulia kwa muda na kusema:
“Hamna kitu,” alisema huku akitikisa kichwa kuonesha anakataa.
“Hamna kitu kivipi wakati unasema amepigwa?” mzee Andendekisye alimshangaa mganga.
“Kwa sasa sina msaada wowote kwa vile waliopiga wamemaliza kazi.”
“Unamaanisha nini?”
“Mtoto wako hana uhai.”
“Nimekusikia lakini sijakuelewa.”
“Nimeangalia jua na kukutana na kiza cha kutisha, ukiona jua kali lakini limetandwa na kiza kizito inaonesha hakuna kitu.”
“Mganga mbona unanizungusha hivyo, hicho kiza umekiona peke yako?”
“Ndiyo maana umekuja hapa ungekuwa na uwezo wa kuona wala usingesumbuka kuja hapa.”
“Basi naomba unifahamishe hakuna kitu gani?”
“Mwanao amefariki.”
“Etiii?” mzee Andendekisye alisema macho yamemtoka pima.
“Ukweli ndiyo huo yule nyoka aliyetumwa ndiye aliyemmaliza, inaonesha amekufa kipindi, hesabu zinaonesha saa moja iliyopita.”
“A..a..sante,” alisema huku akinyanyuka na kutoka nje bila kuaga na kurudi nyumbani akilia kama mtoto mdogo.
Alipofika nyumbani mkewe alikuwa bado ameupakata mwili wa mwanaye, alipoingia eneo la nyumbani kwake aliangua kilio na kumfanya mke wake ampokee kwa kilio.
“Mume wangu unalia nini?” alimuuliza kwa sauti ya kilio.
“Amangise kaniulia mwanangu...Amangise kaniulia mwanangu.”
“U..u...na..maanishaaa Atu amefariki?”
“Ndiyo mke wangu, Amangise kaniweza kuchukua jicho langu.”
Taarifa ile iliwashtua watu wengi na kufanya vilio vitawale kwa majirani hasa mashoga wa Atuganile. Walimchukua na kumpeleka kwenye hospitali ya wilaya ambako vipimo vilithibitisha Atuganile amefariki dunia.
Mwili alihifadhiwa kwenye chumba cha maiti na kuanza matayarisho ya msiba na taarifa zile kusambaa kila kona ya mji wa Ibungu.
Wakati huo Ambakisye bila kujua nini kinaendelea nyuma alikwenda hadi shamba walipokuwa wakilima wazazi wake. Alipofika aliangua kilio kitu kilichowashtua wazazi wake na kuhoji kulikoni hali ile kutokea.
“We Amba kuna nini?”
“Jamani wazazi wangu mmenifanyia ukatili gani?”
“Ukatili! Wa nini tena?” walishtuka wote.
“Jana tumezungumza nini na leo mmenifanyia nini?”
“Amba mbona hatukuelewi una maanisha nini?” wote waliacha kulima na kumsogelea mtoto wao aliyekuwa akilia.
“Baba umemfanya nini Atuganile?” alimuuliza baba yake.
“Mimiiii!” baba mtu alishtuka.
“Wazazi wangu kwa nini mmenigeuka, kwani umenitendea unyama huu?”
“Unyama upi huo mwanangu?”
“Mpaka mmetimiza azma yenu ya kumuumiza mpenzi wangu.”
“Kwani amefanya nini?”
“Mnajua mnajua wazazi wangu... niliwaeleza jana kuwa kama vita yenu kwa nini msipigane wenyewe kuliko kutugeuza ngao katika mapigano yenu.”
“Hebu tufafanulie Atuganile amefanya nini?” mama yake alimuuliza.


Itaendelea Kesho.........
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-22

"Wazazi wangu kwa nini mmenigeuka, kwa nini mmenitendea unyama huu?"
"Unyama upi huo mwanangu?"
"Mpaka mmetimiza azima yenu ya kumuumiza mpenzi wangu."
"Kwani amefanya nini?"
"Mnajua, mnajua wazazi wangu... niliwaeleza jana kuwa kama vita yenu kwa nini msipigane wenyewe kuliko kutugeuza ngao katika mapigano yenu."
"Hebu tufafanulie Atuganile amefanya nini?" mama yake alimuuliza.
SASA ENDELEA...


Atuganile ameumwa na nyoka kisha kamuingia tumboni."
"Mungu wangu! Unasema kweli?" mama yake alishtuka.
"Mama unaweza kuwa hujui lakini baba anajua kila kitu," Ambakisye alimshutumu baba yake.
"Ambakisye nakuapia kwa jina la Mungu kuwa sihusiki na kitu chochote kuhusu mpenzi wako, tuliongea jana yalitosha kukuelewa na kuwa radhi umuoe Atuganile."
"Hapana, baba aliapa kutenda na ametenda," Ambakisye aliendelea kumshutumu baba yake.
"Najua huwezi kuamini lakini nakuapia kuwa sijatenda, nenda popote hutakuta ukweli mimi baba yako nimeshiriki."
"Mmh! Sasa yupo kwenye hali gani?" mama yake aliyekuwa bado kapigwa na bumbuwazi aliuliza.
"Mama nikiambiwa Atu amekufa siwezi kushangaa."
"Baba Amba hebu kuwa muwazi ni kweli Atu umemtenda?"
"Siwezi kumtenda mke wangu, kama nilivyo usafi moyo jana, japokuwa nilikuwa na hasira, lakini niliuapia moyo wangu kutoshiriki kwenye jambo lolote la kumchukiza Mungu na hivi nilikuwa mbioni kuokoka.
Kusema nilishiriki kweli moyo unaniuma sana, Mungu ndiye anayejua nani katenda pia namuomba kwa kila aliyetenda amhukumu na hukumu yake asichukue muda mrefu kabla jua halijazama basi awe ametoweka katika sura ya dunia," mzee Amangakisye alisema kwa uchungu mkubwa.
"Sasa nani katenda unyama ule?" Ambakisye aliuliza.
"Mwanangu dunia hii kuna maadui wengi tunaweza kufikiri sisi ndiyo tulikuwa tunagombana tu kumbe kuna adui wa pembeni aliyeingiza mkono wake."
"Hivi nimekimbia kwao baada ya mzee Andendekisye na mkewe kukushutumu kuwa umemuua mtoto wao."
"Wamethibitishaje?"
"Mimi nitajuaje, waliniambia kuwa wewe umemuua na kuapa kama umekula mbuzi wao lazima utalipa ng'ombe. Huoni hapo ile kauli ya kubakia magofu itatimia ninaamini lazima wataanza na mimi," Ambakisye alijitetea baada ya kuona akitoka mpenzi wake atakayefuata ni yeye.
"Najua lazima watajua ni sisi kwa vile nao walikuwa wanataka kushindana na sisi."
"Sasa mume wangu tuwahi kumsaidia mtoto kwani bila hivyo kuna baya linaweza kumpata."
"Hilo ndilo linalonila akili, inatakiwa kesho nisafiri naye kwa ajili ya kumkinga."
"Fanya hivyo mume wangu."
Zoezi la kulima halikuendelea tena na waliamua kurudi nyumbani, wakiwa njiani walikutana na taarifa ya kifo cha Atuganile. Habari zile zilimshtua sana Ambakisye ambaye alianguka chini na kupoteza fahamu. Wazazi wake waliingia kazi ya kumsaidia kumpa huduma ya kwanza hata alipoamka hakuwa na uwezo wa kutembea, alisaidiwa na baba yake kupelekwa nyumbani.
Ambakisye alikuwa na maumivu makali moyoni kwa kumpoteza kipenzi chake, mwanamke wa ndoto yake. Alitembea njia nzima akilia kwa sauti huku wazazi wake wakimbembeleza mpaka walipofika nyumbani. Taarifa zilizagaa kijijini kuwa mzee Amangise ndiye aliyemloga Atuganile ili asiolewe na mwanaye.
Mzee Amangise aliamini hakuna atakayeamini kuwa yeye hausiki na kifo cha Atuganile, kutokana na taarifa ile kusambaa, alijua lazima kuna bomu zito litatua nyumbani kwake hasa kwa kuanza kwa mwanaye, Ambakisye.
Alipanga kesho yake alfajiri aondoke ili kuvuka boda kwenda Malawi kwa ajili ya kujilinda ikiwezekana wawahi kabla hawajawahiwa. Safari yao walipanga kuondoka kabla hakujakucha ili mpaka saa nne wawe wamevuka boda na kufika kwa mtaalamu.
Wakati wao wakiwaza hivyo mzee Andendekisye alipanga kutozika haraka mpaka asafiri kwenda kupata ukweli kama kweli mwanaye amekufa basi alipue bomu hukohuko ili akirudi kumzika mwanaye na jirani yake naye anamzika wa kwake.
Yeye alipanga kuondoka usiku uleule akatafute kitu cha kumtia adabu mzee Amangise baada ya kuamini ndiye mhusika mkuu.
***
Kijijini Kilasilo siku ya pili mzee Ambokile alimtuma kijana mmoja kwenda kijiji cha Ibungu kusikia kuna taarifa gani. Kijana aliyetumwa alipanda baiskeli mpaka kijiji cha Ibungu na kukuta taarifa za msiba wa watu wawili mmoja msichana na bibi wa kijiji ambao wote walikufa katika mazingira ya kutatanisha.
Baada ya kuzipata taarifa zile alirudi Kilasilo kurudisha taarifa ya Ibungu, habari zile zilimfurahisha sana mzee Ambokile na mkewe kwa kuamini aliyemuua mwanaye naye kamfuata, watakutana kwa Mungu na kumueleza kwa nini walimuua bila kosa.
Wakati mzee Ambokile akifurahia kulipa kisasi, mzee Amangise alikuwa anajiandaa na safari ya kwenda Malawi kumuwahi adui yake.
Usiku wa siku ile jirani yake aliondoka kuvuka boda kwenda kutafuta tatizo la mwanaye ili awahi kurudi siku ya pili yake jioni ili siku ya tatu kama amekufa kweli wafanye mazishi.
***
Mzee Andendekisye alivuka boda saa sita usiku na kupanda land rover old model mpaka mji wa Matipa jirani na msitu mkubwa wa Matipa. Alifika saa nane za usiku. Usiku uleule alikutana na mtaalamu wake Maemba. Baada ya kumweleza tatizo lililomkuta na kutaka kupata ukweli.
"Kwanza pole, najua umesafiri umbali mrefu kutaka kujua binti yako ana matatizo gani?"
"Ni kweli."
"Ukweli ulioelezwa kwenu ndiyo huohuo."
"Upi?"
"Juu ya mwanao."
"Ni kweli amekufa au kiini macho?"
"Ni kweli amekufa."
"Sasa nataka kwanza huyu kijana aitwaye Ambakisye Amangise jua la leo jioni asilione."
"Hakuna tatizo."
"Baada ya kumkata kijana huyo kisha familia yake aondoke mmojammoja."
"Kazi hiyo ndogo."
Baada ya kukubaliana mganga alisema kazi ile inafanyika usiku uleule na yeye alitakiwa kurudi kuendelea na mazishi lakini kesho yake mpaka jua linazama ataipata taarifa ya kifo cha mtu.
Mganga aliingia kazini kuandaa kombora litakalo msambaratisha Ambakisye ambaye alfajiri ya siku ile angekuwa akivuka boda naye kwenda kufanya mambo yake.
Baada ya mganga kukamilisha kazi yake iliyochukua saa tatu, mpaka anamalizia kulikuwa kumekucha.
Waliagana na mzee Andendekisye aliyetakiwa kurudi kule baada ya mazishi kwani aliamini adui yake naye lazima atahangaika japokuwa Maemba aliamini kwa kinga ndogo aliyompa itamuwezesha kurudi salama baada ya mazishi ya binti yake.
Mzee Andendekisye aliondoka Matipa alfajiri na kufika mpakani saa moja asubuhi alivuka na kwenda kuchukua baiskeli yake alipoiacha na kurudi kijijini kwake kuendelea na maandalizi ya mazishi ya mwanaye kipenzi. Wakati akirudi jirani yake Amangise alikuwa safarini kuelekea kwa jamaa yake ambaye alisoma na kuingia kwenye utaalamu wa miti shamba Ligula.
Walitoka vizuri na mwanaye kwa kupakiana kwenye baiskeli na kuelekea boda ili wavuke kwenda Karonga ili wakamzime mzee Andendekisye kabla hajawazima. Kama kawaida Ambakisye ndiye alikuwa akimuendesha baba yake.


Itaendelea Kesho.........
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-23

ILIPOISHIA:
Mzee Andendekisye aliondoka Matipa alifajiri na kufika mpakani saa moja asubuhi alivuka na kwenda kuchukua baiskeli yake alipoicha na kurudi kijijini kwake kuendelea na maandalizi ya mazishi ya mwanaye kipenzi. Wakati akirudi jirani yake Amangise alikuwa safarini kuelekea kwa jamaa yake ambaye alisoma na kuingia kwenye utaalamu wa miti shamba.
Walitoka vizuri na mwanaye kwa kupakiana kwenye baiskeli na kuelekea boda ili wavuke kwenda Karonga ili wakamzime mzee Andendekisye. Kama kawaida Ambakisye ndiye alikuwa akimuendesha baba yake.
SASA ENDELEA...


Baada ya mwendo wa saa mbili Ambakisye alisimamisha baiskeli na kufanya baba yake kumuuliza.
“Vipi umechoka nikusaidie.”
“Hapana baba kichwa kimenishika ghafla.”
“Mmh! Mbona unanitisha,”
Mara Ambakisye alishika kichwa na kuanza kupiga kelele za maumivu.
“Baba kichwa, nakufa mimi kichwa kinapasuka kinapasuka….Mungu wangu nakufa..baba nakufa kichwa kinapasuka,” Ambakisye alisema huku ameshikilia kichwa kama kinataka kutoka.
“Ni nini mwanangu?” baba yake alishtuka.“Baba nina wasiwasi na familia ya kina Atuganile wamelipa kisasi, kama ni wao naamini siponi,” Ambakisye alisema kwa shida.
“Hapana utapona tu mwanangu, mbona mimi sijafanya lolote kwa kifo cha mpenzi wako kisasi hicho kitokane na nini? Wacha niendeshe mimi nikuwahishe kwa mganga,”
“Baba…niagie kwa mama nakufa bila kumuaga,” Ambakisye alisema kwa sauti ya kukata tamaa.
“Huwezi kufa mwanangu,” mzee Amangise alisema huku akimshika mwanaye aliyetaka kuanguka na kumdaka na na kumkalisha kwenye miguu yake.
“Ba..ba..ba..” Ambakisye alimwita baba yake kwa shida kwa sauti ya chini.
“Na..na..am mwanangu,” baba yake aliitikia huku hofu kubwa ikiwa imemtawala.
“U..u..naona ubishi wako?”
“Mbona mwanangu nilikubaliana na wewe.”
“Alichelewa tayari cheche imeisha unguza msitu na moto hakuna wa kuuzima.”
“La..la..kini..”
“ Ba..ba, suluhu ya hili ka..ka..ma ..Mu..mungu watanichukua usilipe kisasi, ukilipa patabakia ma..ma..ma..go..fu..”
Ambakisye hakumalizia, ghafla alibadilika na damu zilianza kumtoa mdomoni, puani, masikioni na machoni huku macho yakiongezeka ukubwa. Taratibu alifumba macho na kutulia.
“Amba..Ambakisye…Ambaaaa,” alimtikisa kwa nguvu lakini hakukuwa na jibu lolote. Alimshika mapigo ya moyo yalikuwa yametulia, mzee mzima aliangua kilio kumlilia mwanaye ambaye alijua amechelewa kumpeleka kwenye kinga .
Wapita njia walishtuka kumkuta mtu wanayemfahamu kampakatia mtu huku akilia.
“Vipi mzee Amangise?”
“Jamani mwanangu,” alijibu kwa sauti ya kilio.
“Ha! Ni Ambakisye! Amefanya nini?” walishtuka kumuona ni mtu wanayemjua katika hali ile.
“Jamani mwanangu ameniacha ghafla.”
“Mungu wangu, alikuwa akiumwa?”
“Wala, tulikuwa na safari ya kuelekea Kilasilo lakini ghafla kichwa kimemuuma hata dakika kumi hazikuchukua amefariki dunia.”
Mzee Amangise aliangua kilio kama mzazi wa kike akimlilia mwanaye, walimsaidia kuurudisha mwili wa Ambakisye kijijini. Watu wote njiani walishtuka kuwaona walivyobebwa Ambakisye kwenye baiskeli huku baba yake akilia kilio cha chini chini.
“Jamani kuna nini?”
“Nimemkuta mzee Amangise akilia huku amemkumbatia mwanaye kwa kweli mpaka sasa hatujajua nini kimemsibu.”
“Eti mzee wangu kuna nini?”
“Wa..wa…,” alishindwa kuzungumza kwani doge la uchungu lilimkaba kooni.
Walimsaidia kuufikisha mwili wa Ambakisye ambaye hakuwa na uhai wakati huo, ujaji ule ulimshtua mama Ambakisye aliyekuwa akifanya usafi uani. Alitulia akiwa amepigwa na butwaa na kujikuta vitu alivyoshikilia mkononi vikimdondoka na kuanguka chini.
Aliyekuwa ameshikiliwa kwenye baiskeli alikuwa mwanaye Ambakisye, walipofika waliuteremsha mwili wa mwanaye na kuingiza ndani.
“Kafanya nini?” mama Ambakisye aliuliza huku akisogea alipokuwa mumewe ameinama huku akilia kilio cha sauti ya chini.
“Vipi mume wangu Amba kafanya nini?” alimuuliza kwa sauti ya juu.
“Wametuwahi.”
“Wametuwahi nini mume wangu?”
“Inaonekana walitangulia kabla hatajafika.”
“Una maanisha Amba anaumwa?”
“Ha..ha..p..”
“Hapana nini mume wangu, kwani kafanya nini?” mama Ambakisye alimuuliza mumewe akiwa amemkwida shati na kumtikisa kwa nguvu.
“A..a..me..ku..ku..u.”
Kauli ile ilimfanya mama Ambakisye amuachie mumewe taratibu na kuteremka chini na kujitupa kama mzigo akiwa amepoteza fahamu baada ya kupata mshtuko kutokana na taarifa ile. Wakati huo wajirani walikuwa wamefika kutokana na kelele za mama Ambakisye kabla ya kupoteza fahamu.
“Jamani kuna nini?”
“Ambakisye amefariki ghafla,” alijibu mmoja wa watu walioleta mwili wa Ambakisye.
“Wewee!” msichana mmoja alishtuka na kuweka mikono kichwani.
“Kweli Ambakisye hatunaye.”
“Mungu wangu mambo gani haya, mpenzi wake si amefariki juzi tu,” mwanamke mmoja alisema huku ameshika mdomo.
Kina mama walimpa huduma ya kwanza mwanamke mwenzao huku wazee wa eneo lile wakimchukua mzee Amangise na kukaa naye pembeni kutaka kujua tatizo, pia wafanye nini baada ya kutokea kitu kama kile kwa ghafla.
“Vipi mzee mwenzetu kulikoni?”
Aliwaelezea hali iliyomtokea Ambakisye ghafla, aliongeza uongo walikuwa wakienda kuhani kwa mchumba wa mwanaye aliyefariki katika mazingira ya kutatanisha.
“Sasa hii itakuwa nini, juzi mtoto wa Andendekisye, Atuganile na bibi Tumwambilile wamefariki katika mazingira hayahaya .


Itaendelea Kesho....
 
Back
Top Bottom