Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,742
- Thread starter
- #61
HADITHI YA KUSISIMUWA NCHI YAWACHAWI-12
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
Niliuweka pale na kushuka ambapo nilipokelewa na watu wawili lakini weupe, waliovaa kama mimi, yaani nguo nyeusi (kaniki) ya kukata lubega nao walikuwa wamejichafua mwili mzima kwa masizi. Chini walikuwa pekupeku.
Kutoka? Mmoja wao akiwa ameshika vikadi vingi vilivyoandikwa mambo mbalimbali ambayo haikuwa rahisi kusoma kwa hatua za mbali ikizingatiwa kwamba, ilikuwa usiku.
Tanzania, nilijibu nikiwaangalia kwa umakini wa hali ya juu.
Ooo, Taifa Kuu TZN, alisema yule mwenye vikadi huku akinipa kikadi chenye kamba na kuniambia nivae shingoni na ile sehemu yenye maandishi iwe mbele wazi, nikafanya hivyo.
Nilichukuliwa hadi nje ya uwanja ambako kulikuwa na giza nene na la ajabu.
ENDELEA MWENYEWE
Tembea kuelekea mbele hatua kumi na tano utakutana na ukumbi wa mikutano, aliniambia yule mtu.
Nilitii agizo lile kwa kutembea huku nikihesabu hatua moja baada ya nyingine, moja baada ya nyingine mpaka nilipofika hatua kumi na nne, ikiwa imebaki moja, ghafla nilijikuta nimetokea kwenye eneo lenye taa nyingi na majumba mbalimbali. Ni mji kabisa, kwani watu mbalimbali ambao hawafanani sana na binadamu walikuwa wakipitapita kila mmoja na hamsini zake.
Nilipokanyaga hatua ya kumi na tano, nikajikuta nimezungukwa na watu wengi wenye kufanana na wale walionipokea na wale waliokuwa wakiendelea na hamsini zao.
Basi, walinichangamkia sana huku wakiniuliza habari za nitokako.
Niliwajibu ni nzuri sana, mmoja wao akanishika mkono wa kushoto huku akiniambia nakaribishwa kuingia kwenye jumba la mikutano la nchi ya Mpingaji huku akisema sijachelewa sana kwani nusu ya wajumbe kutoka pande zote za dunia wameshafika, nusu bado.
Lakini ratiba ya mkutano inasema wakishafika robo tatu ya wajumbe wote, kikao kinafunguliwa, aliniambia yule mtu, au naweza kusema kiumbe kwani ni kama mtu lakini si kwa kufanana na sisi binadamu.
Nje ya jumba la mikutano kulikuwa na watu wa sampuli ile ile wakipiga ngoma na wengine kucheza kwa furaha.
Nje ya jumba, mlangoni kwa juu palikuwa na tambara kubwa jeusi, maandishi meupe yanayosomeka; Mkutano Mkuu wa Dunia wa Kujadili Mambo Mbalimbali. Karibuni nchi ya Mpingaji.
Pembeni ya tambala na maandishi kulikuwa na picha ya kichwa cha mtu, alionekana hadi usawa wa shingo tu. Masikio marefu mfano hakuna, naweza kusema yalipita kichwa kama ya Sungura. Macho ya pembe tatu, makubwa na mbaya au cha kutisha zaidi alikuwa na pembe moja kwenye paji la uso, midomo mirefu kama mdomo wa kibuyu. Tafsiri ya haraka ungeweza kusema ni mnyama na si binadamu.
Nilikazia macho zaidi chini ya ile picha kwani kulikuwa na maandishi. Nikasoma yakiwa yameandikwa; Mkuu wa Nchi ya Wachawi.
Mheshimiwa karibu sana, tuingie ndani, mtu mmoja miongoni mwa watu wale wa ajabu aliniambia akinielekeza kwa mkono mlango mkuu.
Niliingia ndani ya ukumbi ambapo nyuma ya mlango tu nilikutana na watu watano walionipokea na kunisindikiza sehemu ya kukaa.
Macho yangu yalistaajabu sana kuona ukumbi umepambwa kama inavyokuwa kwa kumbi za ninazozifahamu mimi. Kifupi ulipambwa kama kumbi za sherehe mbalimbali, ikiwemo harusi.
Ndaki ya ukumbi kulikuwa na meza kubwa moja na pana na kuna watu mchanganyiko walikaa kasoro viti vitatu vya katikati.
Ninaposema watu mchanganyiko walikaa maana yangu ni kuwa, kulikuwa na binadamu wa kawaida kama mimi. Pia kulikuwa na watu wa kule ambao kama nilivyosema, hawakuwa wamefanana na binadamu sisi.
Wale walionipokea walinielekeza hadi kwenye kiti kimoja kule mbele, lakini si kati ya vile viti vitatu vya katikati. Nilikaa kwenye kiti ambacho mbele yake kulikuwa na kibao kilichoandikwa; MWAKILISHI TAIFA LA TZ.
Nilipokaa tu, nikapewa maelekezo ya kutumia waya nyembamba headphone kwenye masikio endapo nitataka, lakini naweza nisitumie pia.
Mimi nilisema situmii, kwani sikupewa ufafanuzi zaidi wa madhara ya kutumia au faida zake.
Wageni waliendelea kuingia, wakati fulani waliingia kwa mpigo kama saba, wakapewa viti vya kukaa.
Lakini ikumbukwe pia kulikuwa na viti vilivyopangwa mbele ya meza kuu. Watu wengine walikuwa wanakwenda kukaa huko, wengine wakiwa na kamera, wengine na mabegi tu wengine mafaili na kalamu.
Nusu saa baadaye ukumbi wote ulikuwa umejaa, sauti ikasikika ikisema:
Sasa tunaomba utulivu kwani wakati wowote Mkuu atatokea ili kuanza kikao chetu.
Hii ilikuwa sauti isiyotoka kokote, yaani ilisikika tu, lakini msemaji hakuonekana licha ya kwamba alikuwa mwanamke kulingana na sauti.
Ukimya ulitawala, kilichokuwa kikisikika ni watu kukohoa au makaratasi kukaa vizuri, pengine na watu waliokuwa wakidondosha vitu mbalimbali.
Mara, mlango mmoja kulia kwa meza niliyokaa ulifunguliwa.
Ghafla ulitangulia mwanga mkali, halafu mlio wa viatu vya ngozi vilivyoashiria kuwa, visigino vyake vilikuwa, ama vya chuma au vya kitu kigumu sana kwani mlio ulisikika kwa sauti na pia kwa wingi kuonesha kuwa, hakuwa na mtu mmoja.
Mara, watu watatu walitokea, wawili wakiwa pembeni kwa yule mmoja ambaye ni wazi alikuwa ndiye Mkuu wa nchi ile ya Wachawi.
Mkono mmoja alishika kitu kama chupa au labda almasi kwani ilikuwa ikiwaka sana, mkono mwingine wa kushoto alishika chupa kubwa mfano wa zile za pombe kali kama za whisky.
Je, nini kitaendelea? Kesho usikonde........
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
Niliuweka pale na kushuka ambapo nilipokelewa na watu wawili lakini weupe, waliovaa kama mimi, yaani nguo nyeusi (kaniki) ya kukata lubega nao walikuwa wamejichafua mwili mzima kwa masizi. Chini walikuwa pekupeku.
Kutoka? Mmoja wao akiwa ameshika vikadi vingi vilivyoandikwa mambo mbalimbali ambayo haikuwa rahisi kusoma kwa hatua za mbali ikizingatiwa kwamba, ilikuwa usiku.
Tanzania, nilijibu nikiwaangalia kwa umakini wa hali ya juu.
Ooo, Taifa Kuu TZN, alisema yule mwenye vikadi huku akinipa kikadi chenye kamba na kuniambia nivae shingoni na ile sehemu yenye maandishi iwe mbele wazi, nikafanya hivyo.
Nilichukuliwa hadi nje ya uwanja ambako kulikuwa na giza nene na la ajabu.
ENDELEA MWENYEWE
Tembea kuelekea mbele hatua kumi na tano utakutana na ukumbi wa mikutano, aliniambia yule mtu.
Nilitii agizo lile kwa kutembea huku nikihesabu hatua moja baada ya nyingine, moja baada ya nyingine mpaka nilipofika hatua kumi na nne, ikiwa imebaki moja, ghafla nilijikuta nimetokea kwenye eneo lenye taa nyingi na majumba mbalimbali. Ni mji kabisa, kwani watu mbalimbali ambao hawafanani sana na binadamu walikuwa wakipitapita kila mmoja na hamsini zake.
Nilipokanyaga hatua ya kumi na tano, nikajikuta nimezungukwa na watu wengi wenye kufanana na wale walionipokea na wale waliokuwa wakiendelea na hamsini zao.
Basi, walinichangamkia sana huku wakiniuliza habari za nitokako.
Niliwajibu ni nzuri sana, mmoja wao akanishika mkono wa kushoto huku akiniambia nakaribishwa kuingia kwenye jumba la mikutano la nchi ya Mpingaji huku akisema sijachelewa sana kwani nusu ya wajumbe kutoka pande zote za dunia wameshafika, nusu bado.
Lakini ratiba ya mkutano inasema wakishafika robo tatu ya wajumbe wote, kikao kinafunguliwa, aliniambia yule mtu, au naweza kusema kiumbe kwani ni kama mtu lakini si kwa kufanana na sisi binadamu.
Nje ya jumba la mikutano kulikuwa na watu wa sampuli ile ile wakipiga ngoma na wengine kucheza kwa furaha.
Nje ya jumba, mlangoni kwa juu palikuwa na tambara kubwa jeusi, maandishi meupe yanayosomeka; Mkutano Mkuu wa Dunia wa Kujadili Mambo Mbalimbali. Karibuni nchi ya Mpingaji.
Pembeni ya tambala na maandishi kulikuwa na picha ya kichwa cha mtu, alionekana hadi usawa wa shingo tu. Masikio marefu mfano hakuna, naweza kusema yalipita kichwa kama ya Sungura. Macho ya pembe tatu, makubwa na mbaya au cha kutisha zaidi alikuwa na pembe moja kwenye paji la uso, midomo mirefu kama mdomo wa kibuyu. Tafsiri ya haraka ungeweza kusema ni mnyama na si binadamu.
Nilikazia macho zaidi chini ya ile picha kwani kulikuwa na maandishi. Nikasoma yakiwa yameandikwa; Mkuu wa Nchi ya Wachawi.
Mheshimiwa karibu sana, tuingie ndani, mtu mmoja miongoni mwa watu wale wa ajabu aliniambia akinielekeza kwa mkono mlango mkuu.
Niliingia ndani ya ukumbi ambapo nyuma ya mlango tu nilikutana na watu watano walionipokea na kunisindikiza sehemu ya kukaa.
Macho yangu yalistaajabu sana kuona ukumbi umepambwa kama inavyokuwa kwa kumbi za ninazozifahamu mimi. Kifupi ulipambwa kama kumbi za sherehe mbalimbali, ikiwemo harusi.
Ndaki ya ukumbi kulikuwa na meza kubwa moja na pana na kuna watu mchanganyiko walikaa kasoro viti vitatu vya katikati.
Ninaposema watu mchanganyiko walikaa maana yangu ni kuwa, kulikuwa na binadamu wa kawaida kama mimi. Pia kulikuwa na watu wa kule ambao kama nilivyosema, hawakuwa wamefanana na binadamu sisi.
Wale walionipokea walinielekeza hadi kwenye kiti kimoja kule mbele, lakini si kati ya vile viti vitatu vya katikati. Nilikaa kwenye kiti ambacho mbele yake kulikuwa na kibao kilichoandikwa; MWAKILISHI TAIFA LA TZ.
Nilipokaa tu, nikapewa maelekezo ya kutumia waya nyembamba headphone kwenye masikio endapo nitataka, lakini naweza nisitumie pia.
Mimi nilisema situmii, kwani sikupewa ufafanuzi zaidi wa madhara ya kutumia au faida zake.
Wageni waliendelea kuingia, wakati fulani waliingia kwa mpigo kama saba, wakapewa viti vya kukaa.
Lakini ikumbukwe pia kulikuwa na viti vilivyopangwa mbele ya meza kuu. Watu wengine walikuwa wanakwenda kukaa huko, wengine wakiwa na kamera, wengine na mabegi tu wengine mafaili na kalamu.
Nusu saa baadaye ukumbi wote ulikuwa umejaa, sauti ikasikika ikisema:
Sasa tunaomba utulivu kwani wakati wowote Mkuu atatokea ili kuanza kikao chetu.
Hii ilikuwa sauti isiyotoka kokote, yaani ilisikika tu, lakini msemaji hakuonekana licha ya kwamba alikuwa mwanamke kulingana na sauti.
Ukimya ulitawala, kilichokuwa kikisikika ni watu kukohoa au makaratasi kukaa vizuri, pengine na watu waliokuwa wakidondosha vitu mbalimbali.
Mara, mlango mmoja kulia kwa meza niliyokaa ulifunguliwa.
Ghafla ulitangulia mwanga mkali, halafu mlio wa viatu vya ngozi vilivyoashiria kuwa, visigino vyake vilikuwa, ama vya chuma au vya kitu kigumu sana kwani mlio ulisikika kwa sauti na pia kwa wingi kuonesha kuwa, hakuwa na mtu mmoja.
Mara, watu watatu walitokea, wawili wakiwa pembeni kwa yule mmoja ambaye ni wazi alikuwa ndiye Mkuu wa nchi ile ya Wachawi.
Mkono mmoja alishika kitu kama chupa au labda almasi kwani ilikuwa ikiwaka sana, mkono mwingine wa kushoto alishika chupa kubwa mfano wa zile za pombe kali kama za whisky.
Je, nini kitaendelea? Kesho usikonde........