Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,742
- Thread starter
- #41
HADITHI YA KUSISIMUWA NCHI YA WACHAWI-7
Akatokea mtu mmoja, yeye weusi wake si kama wenzake, alikuwa zaidi. Alikuwa mweusi kama chungu kilichozeeka.
Akiangalia hivi, macho yake yalikuwa kama yanatoa mwanga hafifu huku kichwa kikiwa kipara chote.
Kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha mtu huyo kuwa na rangi hiyo, lakini eti alivaa kanzu nyeupe sana.
Sasa ile rangi nyeusi ya mwili na ile rangi nyeupe ya kanzu, akaonekana kutisha sana, hasa ikizingatiwa kuwa, naye kwenye paji la uso alikuwa na pembe refu lenye kama mita moja.
Alisimama akatuangalia kama vile aliyetaka tunyamaze ili aanze kusema ingawa hakukuwa na watu wanaosema sema, pengine ni kutokana na wasiwasi na hofu iliyokuwepo eneo lile, hasa pale kila mtu mgeni alipojua eneo tulilokuwa si duniani.
Lakini mimi kwa akili zangu nilijua ni duniani, bali ni chini ya dunia. Maana hata ndani ya dunia ni dunia. Nje ya dunia, ingekuwa sayari nyingine, kama vile Uranus, Venus, Mercury au Jupiter.
Basi, ukimya ulitawala, yule mtu akiwa amesimama pembeni ya yule msichana PS, akasema:
Kazi yangu kubwa si kutoa elimu, bali uwezo. Kama ni elimu mtapewa huko huko duniani kila mmoja kwenye eneo lake.
Alipomaliza kusema, akamgeukia yule msichana huku akinyoosha mkono kupokea kitu. Yule msichana akainama, akanyanyua ndoo nyeupe kama kioo cha kujitazamia, akampa, naye akapokea na kuishika mkono mmoja.
Huyu mtu alikuwa mrefu kidogo, kwa sisi wote tuliokuwa ndani, hakuna aliyekuwa mrefu kama yeye, hata yule msichana hakuwa mrefu kama yeye, ingawa na yeye kati yetu hakuna aliyemfikia kwa urefu.
Akiwa ameshika ndoo ya maji, alichovya mkono, akachota maji akayarusha kwetu, yakaja kama maji yayorushwa na mpira wa kumwagilia.
Yalitupata wote na tulilowa sana, lakini wapo waliolowa zaidi na wapo waliolowa kidogo, mimi nililowa zaidi.
Hongera sana kijana wangu, umekuwa mtu mwingine sasa, si kama ulivyokuwa wakati hatujaingia humu ndani, mzee Madume aliniambia huku akiniangalia kwa macho yenye kunipa pongezi.
Kwa hiyo inakuwaje? Nilimuuliza.
Kuanzia sasa, wewe ni jasiri, una nguvu za ajabu na una uwezo wa ajabu.
Nitajuaje? Nilimuuliza.
Tukifika duniani utajua tu.
Mara sauti ya yule mtu ikatukatisha:
Kuanzia sasa, kila neno kutoka kwenye vinywa vyenu litakuwa na maana, kila mtakachotenda kwa kutegemea nguvu hii pia kitafanyika.
Alipomaliza kusema hivyo aligeuka na kurudi. Kama nilivyosema, ukumbi ulikuwa mkubwa kama viwanja vya mpira, kwa hiyo mpaka anaondoka tulimkazia macho hadi anapotea zake.
Pale alibaki yule msichana, lakini naye baada ya yule mzee kupotea, aligeuka na kutoka ndani ya ule ukumbi tukisubiri amri nyingine ya juu.
Mara alitokea yule mwanamke ambaye naye ni wa ajabu aliyetupokea na kutuingiza mle. Akasimama mbele ya watu wote na kupaza sauti akisema:
Hiki ni kipindi cha wageni kupotezana, sasa kila aliyekuja na mwenzake amshike mkono, mnatoka nje kabisa, huko kila mmoja anakutana na maelekezo mengine.
Alipomaliza kusema, akageuka na kuondoka zake.
Kwa haraka sana nilichojifunza mimi ni kwamba, utawala wa kule ulikuwa kama wa duniani, kwa maana kwamba, kulikuwa na protokali. Kila mtu alitambua jukumu lake ni lipi na linaanza kufanya kazi wakati gani.
Basi, tulianza kutoka nje na kila aliyekuwa na mwenzake alimshika mkono, mimi mzee Madume alinishika mkono. Tukaongozana hadi nje kabisa ambako tulikuta watu, wanawake kama yule aliyetuamuru kutoka nje, lakini wakiwa wengi sana. Kila mmoja alikuwa na ubao mweupe, maandishi mekundu yakisomeka mahali mtu alipotokea.
Sisi wetu yule pale, aliniambia mzee Madume baada ya kusoma ubao wa mtu yule ambao uliandikwa Wavuvi Mwanza.
Tulimfuata yule mwanamke, naye alipotuona akasimama ghafla, kisha akageuka kutupa mgongo huku akisema:
Nifuateni.
Tulimfuata kwa nyuma hadi nje ya geti kubwa la jengo hilo, akatuonesha njia akisema:
Hii njia inafika mlikotoka, ifuateni moja kwa moja. Tahadhari, msikate kulia wala kushoto, alisema akisimama pembeni ili kutupa nafasi sisi ya kuanza safari.
Tulitembea umbali wa mita kama mia moja hivi, njia ilikuwa ya kupita kwa miguu tu na si gari, halafu udongo wake kama mchanga wa pwani mweupe.
Tukiwa tunazidi kwenda, tulifika eneo fulani mbele yetu tuliona ukomo wa njia. Kwa maana kwamba, endapo tungeendelea kwenda tungetumbukia, mzee Madume akasimama na kusema:
Tatizo la huku bwana ni hili. Kila ukija kunakuwa na ugeni wa jinsi ya kuingia na jinsi ya kutoka, sijawahi kuja nikatoka kwa mtindo huu wa kukutana na gema kama hili, sasa mbona njia hapa imefika mwisho na yule alituambia moja kwa moja, tumekosea wapi?
Mimi sikumjibu kitu zaidi ya kukaa kimya, maana kama ni kujua yeye mwenzangu ndiye alikuwa mwenyeji zaidi.
Nimesema nyoosheni, sasa mnasita nini, nyoosheni, sauti ile iliyotupokea ilisema huku ilikotokea hakujulikani.
Mzee Madume alinishika mkono, akanivuta, tukanyoosha hadi kwenye mwisho wa njia ambapo ni gema kubwa na kwa chini kulikuwa kunaonekana mawingu ya bluu. Yaani ilikuwa kama vile sisi tupo juu ya dunia.
Sasa rukeni hapo mrudi kwenu, sauti ilisema.
Je, nini kitaendelea? Kesho tena
Akatokea mtu mmoja, yeye weusi wake si kama wenzake, alikuwa zaidi. Alikuwa mweusi kama chungu kilichozeeka.
Akiangalia hivi, macho yake yalikuwa kama yanatoa mwanga hafifu huku kichwa kikiwa kipara chote.
Kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha mtu huyo kuwa na rangi hiyo, lakini eti alivaa kanzu nyeupe sana.
Sasa ile rangi nyeusi ya mwili na ile rangi nyeupe ya kanzu, akaonekana kutisha sana, hasa ikizingatiwa kuwa, naye kwenye paji la uso alikuwa na pembe refu lenye kama mita moja.
Alisimama akatuangalia kama vile aliyetaka tunyamaze ili aanze kusema ingawa hakukuwa na watu wanaosema sema, pengine ni kutokana na wasiwasi na hofu iliyokuwepo eneo lile, hasa pale kila mtu mgeni alipojua eneo tulilokuwa si duniani.
Lakini mimi kwa akili zangu nilijua ni duniani, bali ni chini ya dunia. Maana hata ndani ya dunia ni dunia. Nje ya dunia, ingekuwa sayari nyingine, kama vile Uranus, Venus, Mercury au Jupiter.
Basi, ukimya ulitawala, yule mtu akiwa amesimama pembeni ya yule msichana PS, akasema:
Kazi yangu kubwa si kutoa elimu, bali uwezo. Kama ni elimu mtapewa huko huko duniani kila mmoja kwenye eneo lake.
Alipomaliza kusema, akamgeukia yule msichana huku akinyoosha mkono kupokea kitu. Yule msichana akainama, akanyanyua ndoo nyeupe kama kioo cha kujitazamia, akampa, naye akapokea na kuishika mkono mmoja.
Huyu mtu alikuwa mrefu kidogo, kwa sisi wote tuliokuwa ndani, hakuna aliyekuwa mrefu kama yeye, hata yule msichana hakuwa mrefu kama yeye, ingawa na yeye kati yetu hakuna aliyemfikia kwa urefu.
Akiwa ameshika ndoo ya maji, alichovya mkono, akachota maji akayarusha kwetu, yakaja kama maji yayorushwa na mpira wa kumwagilia.
Yalitupata wote na tulilowa sana, lakini wapo waliolowa zaidi na wapo waliolowa kidogo, mimi nililowa zaidi.
Hongera sana kijana wangu, umekuwa mtu mwingine sasa, si kama ulivyokuwa wakati hatujaingia humu ndani, mzee Madume aliniambia huku akiniangalia kwa macho yenye kunipa pongezi.
Kwa hiyo inakuwaje? Nilimuuliza.
Kuanzia sasa, wewe ni jasiri, una nguvu za ajabu na una uwezo wa ajabu.
Nitajuaje? Nilimuuliza.
Tukifika duniani utajua tu.
Mara sauti ya yule mtu ikatukatisha:
Kuanzia sasa, kila neno kutoka kwenye vinywa vyenu litakuwa na maana, kila mtakachotenda kwa kutegemea nguvu hii pia kitafanyika.
Alipomaliza kusema hivyo aligeuka na kurudi. Kama nilivyosema, ukumbi ulikuwa mkubwa kama viwanja vya mpira, kwa hiyo mpaka anaondoka tulimkazia macho hadi anapotea zake.
Pale alibaki yule msichana, lakini naye baada ya yule mzee kupotea, aligeuka na kutoka ndani ya ule ukumbi tukisubiri amri nyingine ya juu.
Mara alitokea yule mwanamke ambaye naye ni wa ajabu aliyetupokea na kutuingiza mle. Akasimama mbele ya watu wote na kupaza sauti akisema:
Hiki ni kipindi cha wageni kupotezana, sasa kila aliyekuja na mwenzake amshike mkono, mnatoka nje kabisa, huko kila mmoja anakutana na maelekezo mengine.
Alipomaliza kusema, akageuka na kuondoka zake.
Kwa haraka sana nilichojifunza mimi ni kwamba, utawala wa kule ulikuwa kama wa duniani, kwa maana kwamba, kulikuwa na protokali. Kila mtu alitambua jukumu lake ni lipi na linaanza kufanya kazi wakati gani.
Basi, tulianza kutoka nje na kila aliyekuwa na mwenzake alimshika mkono, mimi mzee Madume alinishika mkono. Tukaongozana hadi nje kabisa ambako tulikuta watu, wanawake kama yule aliyetuamuru kutoka nje, lakini wakiwa wengi sana. Kila mmoja alikuwa na ubao mweupe, maandishi mekundu yakisomeka mahali mtu alipotokea.
Sisi wetu yule pale, aliniambia mzee Madume baada ya kusoma ubao wa mtu yule ambao uliandikwa Wavuvi Mwanza.
Tulimfuata yule mwanamke, naye alipotuona akasimama ghafla, kisha akageuka kutupa mgongo huku akisema:
Nifuateni.
Tulimfuata kwa nyuma hadi nje ya geti kubwa la jengo hilo, akatuonesha njia akisema:
Hii njia inafika mlikotoka, ifuateni moja kwa moja. Tahadhari, msikate kulia wala kushoto, alisema akisimama pembeni ili kutupa nafasi sisi ya kuanza safari.
Tulitembea umbali wa mita kama mia moja hivi, njia ilikuwa ya kupita kwa miguu tu na si gari, halafu udongo wake kama mchanga wa pwani mweupe.
Tukiwa tunazidi kwenda, tulifika eneo fulani mbele yetu tuliona ukomo wa njia. Kwa maana kwamba, endapo tungeendelea kwenda tungetumbukia, mzee Madume akasimama na kusema:
Tatizo la huku bwana ni hili. Kila ukija kunakuwa na ugeni wa jinsi ya kuingia na jinsi ya kutoka, sijawahi kuja nikatoka kwa mtindo huu wa kukutana na gema kama hili, sasa mbona njia hapa imefika mwisho na yule alituambia moja kwa moja, tumekosea wapi?
Mimi sikumjibu kitu zaidi ya kukaa kimya, maana kama ni kujua yeye mwenzangu ndiye alikuwa mwenyeji zaidi.
Nimesema nyoosheni, sasa mnasita nini, nyoosheni, sauti ile iliyotupokea ilisema huku ilikotokea hakujulikani.
Mzee Madume alinishika mkono, akanivuta, tukanyoosha hadi kwenye mwisho wa njia ambapo ni gema kubwa na kwa chini kulikuwa kunaonekana mawingu ya bluu. Yaani ilikuwa kama vile sisi tupo juu ya dunia.
Sasa rukeni hapo mrudi kwenu, sauti ilisema.
Je, nini kitaendelea? Kesho tena