Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

mwisho wa ubaya ni aibu mage ananikera sijui nimfanyaje
Amefanya nini? watu kama hao wapo duniani ili kuhakikisha maisha yanaenda, bila kuwepo changamoto kama hizi uwezo wetu wa kufukir ungekuwa mdogo na misimamo isingekuwepo
 
Amefanya nini? watu kama hao wapo duniani ili kuhakikisha maisha yanaenda, bila kuwepo changamoto kama hizi uwezo wetu wa kufukir ungekuwa mdogo na misimamo isingekuwepo

wew huoni anachofanya???? yani nashindwa kumuelewa
 
Najaribu kumuona Mage anavyochachawa na taarifa ya ndoa ya Cecy na Collins
 
ILIPOISHIA:
Wazo la kuua aliliweka kando kwa muda kwa kuamini lile lingekuwa la mwisho kabisa baada ya mipango ya awali kufeli. Aliamini anaweza kutumia njia nyingi kuhakikisha Cecy aolewi na Colin.
SASA ENDELEA...



Mpango ulikuwa kummwagia tindikali au kutuma vijana kumbaka na picha zake kusambazwa kitu ambacho aliamini Colin na familia yake wasingekivumilia lazima angempiga chini Cecy.


Mpango wake alipanga kuufanya kabla ya Colin na mpenzi wake kurudi kutoka Afrika ya Kusini. Alijua ndoa ingechukua muda ili kusubiri afya ya Cecy iimarike naye angetumia nafasi ile kumtia doa Cecy na yeye kuichukua nafasi aliyokuwa akiitafuta usiku na mchana kama wokovu baada ya mwenyewe kuichezea shilingi kwenye tundu la choo.


Aliapa kutumia kiasi chochote cha fedha kuhakikisha anampoteza Cecy na kulimiliki penzi la Colin. Walijipanga kutafuta watu ambao angewalipa kiasi cha pesa watakachokubaliana ili wamfanyie kazi yake kwa uhakika bila mtu yeyote kujua kitu.


Wakati akiwaza hayo taarifa ya kuitwa Afrika ya Kusini iliwafikia wazazi wa Colin na Cecy kuwa wanatakiwa mara moja. Japokuwa hawakujua wanaitiwa nini, walikubaliana kuondoka kwenda kuwasikiliza watoto wao wana lipi.


Baada ya siku nne, Colin na Cecy waliwapokea uwanja wa ndege wa Port Elizabeth na kuwapeleka katika Hoteli ya The Beach waliyofikia wao.


Wote walifarijika kukuta afya ya Cecy imeimarika haraka na nuru yake ya awali ikianza kuonekana kwa mbali. Ilikuwa furaha kwa familia kukutana wote wakiwa katika hali ya furaha. Usiku wa siku ile baada ya chakula walikaa pamoja kwa ajili ya mazungumzo.


Mzungumzaji mkuu alikuwa Cecy ambaye ndiye aliyemuomba Colin aseme yeye.
"Wazazi wetu najua mmeshtuka na wito wetu wa ghafla, lakini wito huu una maana kubwa katika maisha yetu watoto wenu. Wito huu ni kwa ajili ya kuja kusimamia harusi ya watoto wenu."
"Watoto wetu kina nani?" mama Colin aliuliza.


"Ya mimi na mume wangu Colin ambayo tumepanga kuifunga wiki ijayo."
"He! Mbona haraka sana kwa nini mnataka kufungia huku?" aliuliza mama Cecy.
"Mama kuna kitu kilinijia haraka akilini mwangu ambacho nilikiamini kabisa na nilipomwambia mwenzangu ambaye alikubaliana na nilichokiona na kukubaliana kufunga ndoa huku."
"Kitu gani?" mama Colin aliendelea kuuliza.


"Nilifuatilia hatua zote za harusi za mpenzi wangu ambazo huvurugika mwishoni, mfano wa kwanza muda mfupi kabla ya kumuoa Mage lilitokea tatizo lililomjeruhi moyo mpenzi wangu. Mfano wa pili muda mfupi kabla ya ndoa yetu likatokea la kutokea, hivyo imeonesha kuna tatizo.


"Nilichokiwaza mimi ni kuhusiana na matukio yote hivyo naamini huku tutafunga ndoa isiyo na starehe ambayo itakuwa na baraka ya wazazi wa pande zote. Kwa hiyo wazazi wetu tunaomba mkubali ombi letu ili tukirudi Tanzani tuwe tayari mke na mume. Kuhusu sherehe tutaifanya tukijipanga."
"Mmh! Colin we ulikuwa unasemaje?" mama Colin alimuuliza mwanaye.


"Mimi namuunga mkono mpenzi wangu amekuwa na jicho la tatu ambalo wote tulikuwa hatuna."
"Mipango ya harusi mmeshaandikisha kanisani?""Tumeshakamilisha kila kitu mlikuwa mkisubiriwa ninyi tu."
"Basi hakuna tatizo kwa vile jambo ni la heri tutakuwa pamoja, sijui dada unasemaje?" mama Colin alimuuliza mama Cecy.


"Hata mimi naungana na wewe."
Wazazi hawakuwa na pingamizi lolote walikubaliana kusimamia ndoa ya watoto wao ili wakirudi nyumbani Tanzania wajipange kwa sherehe.
***
Baada ya taratibu zote kufuatwa, Colin na Cecy walifunga ndoa katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Augustine jijini Port Elizabeth Afrika ya Kusini. Ndoa iliyokuwa na watu wachache lakini ilikuwa ni furaha isiyo kifani moyoni mwa Cecy pale alikupoulizwa kama anakubali kuwa mke halali wa Colin katika shida na raha pia Colin kukubali kuwa Cecy ni mkewe katika shida na raha na kifo ndicho kitakachowatenganisha.


Baada ya kufunga ndoa waliondoka na kurudi kwenye hoteli waliyofikia na jioni ya siku ile ilifanyika sherehe ndogo katika ufukwe wa Hoteli ya The Beach na baadhi ya jamaa zao walikuwa katika mji wa Port Elizabeth.


Japo ilikuwa sherehe ndogo iliyoanzia ufukweni na kuishia kwenye ukumbi wa hoteli ile, ilikuwa sherehe yenye kufana kila aliyekuwepo alifurahia sherehe ile ambayo watu walikunywa na kusaza.
Baada ya sherehe, maharusi waliingia ndani ya chumba cha VIP ambacho walikichukua mahususi kwa ajili ya fungate.


Siku ya tatu mama Colin na Cecy walirudi Tanzania na kuwaacha watoto wao wakila fungate. Wakiwa ndani ya ndege kila mtu alimshukuru Mungu kwa kutenda jambo ambalo lililoonekana kwa akili ya kibinadamu limeshindikana."Yaani unajua dada mpaka muda huu siamini kama nimeweza kuiona harusi ya Cecy na Colin," alisema mama Cecy.


"Si wewe yaani mpaka sasa naamini Mungu akiamua kutenda hutenda jambo."
"Kwangu naona kama muujiza siamini... siamini kama kuna siku nitamuona mwanangu akitabasamu lazima nimshukuru Mungu asante Mungu kwa kila unitendealo."
"Kweli nimeamini Colin na Cecy wanapendana mapenzi ya dhati."
"Kwa nini unasema hivyo?"


"Mwanzo niliamini labda Cecy anampenda mwanangu kwa ajili ya utajiri wake lakini alinionesha hamuhitaji kwa ajili ya mali zake bali mapenzi ya dhati, pia Colin alinihakikishia hataoa mwanamke mwingine zaidi ya Cecy na alikuwa radhi kuioa maiti na Cecy kama angekufa."
"Ni jambo la kushukuru

Nb: kuna kipande cha toleo liliopita nimekirudia ili kupata mtiririko mzuri, na jahazi karibu la tia nanga ndo maana spidi imepungua, Je Mage akisikia kuwa ndoa tayari atafanya maamuzi gani? ataomba kuwa mchepuko? au ataomba ardhi imfunike tuendelee kufautilia mdogo mdogo
 
ILIPOISHIA:
"Mwanzo niliamini labda Cecy anampenda mwanangu kwa ajili ya utajiri wake lakini alinionesha hamuhitaji kwa ajili ya mali zake bali mapenzi ya dhati, pia Colin alinihakikishia hataoa mwanamke mwingine zaidi ya Cecy na alikuwa radhi kuioa maiti ya Cecy kama angekufa."
ENDELEA...


"Ni jambo la kushukuru watoto wetu kupendana ni mwanzo wa kutengeneza familia yenye upendo."
Wazazi wakiwa wanabadilisha mawazo ndani ya ndege jijini Port Elizabeth ndani ya chumba cha VIP katika Hoteli ya The Beach, Cecy alikuwa akimuangalia Colin kwa muda mrefu na kuanza kutokwa na machozi kitu kilichomshtua Colin na kuhoji.

"Vipi mpenzi wangu mbona unalia?"
Cecy hakujibu machozi yaliendelea kumtoka kama maji na kuzidi kumweka mumewe kwenye wakati mgumu.

"Mke wangu kuna nini tena? Leo ni siku ya furaha baada ya kufika nusu ya safari yetu kutokana na mitihani mingi. Badala ya kufurahi mke wangu unalia, kipi kimekusibu mpenzi wangu au kama kuna nilichokukosea nipo radhi kwa adhabu yoyote," Colin alisema huku akijisogeza mbele ya Cecy kumpigia magoti.

Kabla hajapiga magoti Cecy alikurupuka alipokuwa amekaa na kumuwahi mpenzi wake na kumvamia na kuwafanya wote waanguke mweleka.

"Colin machozi haya si maumivu bali furaha iliyopitiza nashindwa, nashindwa kuvumilia mume wangu. Siamini kama ndoto niliyoota mchana imekuwa kweli, leo hii mimi ni mke wa Colin, asante Mungu asante kwa kila jambo sitaacha kukushukuru usiku na mchana siku zote za pumzi zangu."
"Cecy mpenzi wangu nilikupenda toka siku ya kwanza nilipokuona lakini nilikuta chaguo lingine la mama yangu. Lakini amini uliingia moyoni mwangu toka siku ya kwanza jicho langu lilipokuona. Naamini kabisa jicho la mwanzo lilikuwa sahihi kuliko mtu niliyechaguliwa.

"Umekuwa kiumbe wa ajabu ambaye siwezi kumfananisha na kiumbe wa kawaida, umeweza kunipigania japo katika hali yako ya umaskini, lakini ulikuwa radhi ukose kitu chochote chini ya jua ili unipate mimi. Nakuahidi lile jicho lililokuona mara ya kwanza na kukufungulia mlango moyoni mwangu ndilo hilohilo linalokuona ua zuri lililochanua mbele yangu.
"Wewe ni mwanamke niliyepewa zawadi na Mungu, nimeamini bundi hawezi kukaa kundi moja na njiwa."

"Unamaanisha nini?"
"Mage hakuwa njiwa katika safari ya maisha yangu, naamini mbeleni lazima angenitenda, Mungu alilijua hilo ndiyo maana alikuleta wewe wakili wa moyo wangu bila wewe nina wasiwasi ningekuwa nimeshakufa kwa vile aliuhukumu moyo wangu kifo, lakini umeweza kuutoa moyo wangu kwenye adhabu nzito niliyopewa na Mage sijui usingekuwepo ingekuwaje."

"Colin niliyafuatilia maisha yako kila hatua ni moyo wa upendo ulinisukuma, niliamini kabisa wewe ndiye mume wangu. Nilikupenda sitachoka kukupenda kwa vile kila siku unakuwa kiumbe kipya moyoni mwangu."

"Hata mimi mke wangu."
Walikumbatiana kwa furaha kuifurahia fungate yao iliyokuwa na raha ya aina yake baada ya safari ndefu yenye misukosuko.

****

Nchini Tanzania taarifa za mama Colin kwenda Afrika Kusini zilimshtua sana Mage, alijikuta akiwaza huenda Cecy amezidiwa na hivyo amekwenda kuangalia hali yake inavyoendelea. Aliomba kama ni hivyo basi akute Cecy amezidiwa na kufariki dunia, lakini bado alibakia na akiba ya mpango wake wa kumfanyia kitu kibaya Cecy kama atakuwa hai ili kuhakikisha ndoa haifungwi.

Aliwaandaa watu kwa ajili ya kufanya utekaji na kumfanyia vitendo vichafu, walikubaliana kuifanya kazi baada ya Cecy kurudi nchini kutoka Afrika ya Kusini. Vijana walimuahidi kumfanyia kazi vizuri kwa vile walikuwa na uzoefu wa kazi zile. Aliwaahidi kuwaongeza mara mbili ya malipo waliyokubaliana kama watafanikisha kazi ile.

"Sister mbona utakubali kazi yetu, hata ungetaka kichwa chake tungekuletea," alijisifia Wakora.
"Sasa damu yenye virusi tutaipata wapi?"
"Hilo dogo mbona kuna mshkaji wetu mmoja ameumia tutachukua damu yake kidogo na kumdunga mtu wako."

"Nawaamini msiniangushe."
"Hatujawahi kuharibu kazi hata siku moja, hata kama kuna kazi nyingine we tupe tukufanyie tena tutakupunguzia kwa vile wewe mtu wetu."
"Picha nimewapa?"

"Ndiyo sister, tumemcheki vizuri mbona huyu amekwisha."
Baada ya mipango yake kwenda sawa Mage alijipanga kuhakikisha Colin hamuoi Cecy, alipanga baada ya tukio hilo la kumteka Cecy na kumdunga damu yenye virusi atumie laini mpya ya simu na kumtumia picha za Cecy akibakwa na ujumbe kuwa ameathirika.

Baada ya kuwaza yote yale alitabasamu na kuamini kila kitu kipo vizuri anachosubiri utekelezaji tu. Akiwa amejipumzisha alipata taarifa toka kwa mama yake kuwa mama Colin amerudi toka Afrika ya Kusini.

"He! Mbona hajakaa sana, karudi na Colin?"
"Hapana karudi peke yake."
"Mbona karudi peke yake kwani alikwenda kufanya nini?"
"Kwa kweli sikumuuliza."

Mage hakutaka kuuliza swali lingine alinyanyuka na kutoka kuelekea kwa mama Colin kutaka kujua sababu ya safari yake ya Afrika ya Kusini na kwa sababu gani hakurudi na Colin. Alitoka hadi kwenye gari na kuchukua aina ya Toyota Harrier na kuelekea kwa mama Colin, aliendesha kwa kasi ili kuwahi kupata taarifa.

Alipofika alipaki gari kwenye maegesho, kwa shauku ya kuyajua ya Afrika ya Kusini hakufunga hata mlango wa gari. Alitembea mwendo wa haraka hadi kwenye mlango wa kuingia ndani.

*Baada ya mafuriko ya Escro kupita tuendelee na uhondo, tukutane wiki ijayo, Mage ataendelea na mpango wake baada ya kujua ukweli au atabadili mpango tuendelee kuwemo*
 
ILIPOISHIA:
Mage hakutaka kuuliza swali lingine alinyanyuka na kutoka kuelekea kwa mama Colin kutaka kujua sababu ya safari yake ya Afrika ya Kusini na kwa sababu gani hakurudi na Colin. Alitoka hadi kwenye gari na kuchukua aina ya Toyota Harrier na kuelekea kwa mama Colin, aliendesha kwa kasi ili kuwahi kupata taarifa.
SASA ENDELEA...



Alipofika alipaki gari kwenye maegesho, kwa shauku ya kuyajua ya Afrika Kusini hakufunga hata mlango wa gari. Alitembea mwendo wa haraka hadi mlango wa kuingia ndani. Alibisha hodi na kukaribishwa na mama Colin aliyekuwa amekaa na mama Cecy wakiangalia mkanda wa video huku wakinywa vinywaji.
"Karibu ma mkwe," mama Colin alisema.
"A..a..sa.."


Alishindwa kumalizia sentesi ambayo ilikatikia njiani baada ya jicho lake kutua kwenye kioo cha runinga alichokiona mbele yake.
Alimuona Cecy katika vazi la harusi akiwa na Colin katika suti ya gharama, alikaza macho kama yanataka kudondoka.


"Maa..a..ma."
"Vipi mkwe?"
"Huyu si Colin?" alisema huku akinyoosha kidole.
"Ndiyo."
"Na..na..huyu si Cecy?"
"Ndiyo."
"Hii si..si..harusi?"
"Ndiyo."


"Wameoana lini?"
"Leo ni siku ya nne toka waoane na sisi tumerudi jana usiku kutoka huko."
"Mmh! Si kweli, haya ni maigizo tu ili kuniumiza roho."
"Kukuumiza roho ili iweje? Na picha zao hizi hapa."


Mage alizichukua albamu akiwa haamini anachoambiwa, aliifungua na kuanza kuangalia picha mojamoja huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio. Kila ukurasa alioufunua uliupasua moyo wake alijikuta machozi yamefunika macho na kushindwa kuona picha.


Alihisi mapigo ya moyo yakiongeza kasi pumzi zikamjaa na kutoka kwa shida, kiza kizito kilitanda mbele yake kilichoendelea hakukijua. Mage alianguka kama mzigo akiwa amepoteza fahamu, kitendo kile kiliwashtua sana. Walijikuta wakitaharuki ilibidi wamchukue na kumkimbiza hospitali kisha kumjulisha mama yake.


Kwa vile huduma ile haikuwepo alitakiwa kupelekwa Afrika Kusini haraka kwani walisema ugonjwa ule ikiwa atapata matibabu ya haraka anaweza kupona.
***
Mage alisafiri na mama yake mpaka Afrika Kusini katika Hospitali ya Milpark iliyopo katika Jiji la Johannesburg. Alipokelewa na kuanzishiwa matibabu mara moja, madaktari walifanikiwa kufanya upasuaji uliochukua saa tatu kuondoa damu zilizovuja baada ya mshipa kupasuka.


Baada ya upasuaji kwenda vizuri alirudishwa kwenye chumba maalumu chini ya uangalizi ya madaktari bingwa. Taarifa za Mage kuumwa zilimfikia Colin aliyekuwa katika mji wa Port Elizabeth.
"Mpenzi nasikia Mage anaumwa ameletwa hospitali ya Milpark, Johannesburg," Colin alimwambia Cecy aliyekuwa akicheza game kwenye Ipad.


"Maskini mke mwenzangu nini kimemsibu?"
"Nasikia kapata mshtuko baada ya kuona video na picha zetu za harusi."
"Maskini, Mage alikuwa kama fisi aliyeamini siku moja mwanadamu atadondosha mkono."
"Namshangaa kutaka kufa wakati anajua mimi ni wa nani."
"Wa Cecy."


"Najiuliza bila Cecy, Colin leo ningekuwa wapi?"
"Anajua Mungu si sisi wanadamu ambao hupokea matokeo."
"Asante mpenzi wangu kwa kuyaokoa maisha yangu, huwezi kuamini baada ya kuachwa ghafla na Mage nilijawa na mawazo mengi na kujiona nina mapungufu."


"Asante niseme mimi uliyoyapa majibu maswali yangu kama kuna siku maji yatapanda mlima."
"Nina imani huu ni muda muafaka wa ku-renew mkataba wako na makapuni yote ya mavazi ya majarida. Waliniuliza afya yako nikawaambia hujambo kabisa hivyo wameomba tupange siku ya wao kuja ili uendelee na kazi yako."


"Mpenzi moyoni mwangu nimepanga kwanza nikae na mume wangu kwa mwaka mzima ndipo nifanye kazi nyingine.""Cecy si tumeshafunga ndoa wasiwasi wako nini?"
"Sijaifaidi raha ya ndoa kazi ipo tu, kama wameweza kunisubiri muda wote waendelee kusubiri."
"Makubaliano ya awali ni kwamba tutakuwa tupo pamoja katika kazi zako zote kwa vile mimi ndiye meneja wako."


"Mmh! Kama hivyo sawa."
"Mmh! Bado tu una wasiwasi wa kuibiwa?" Colin alimtania.
"Si umesikia mtu kataka kufa baada ya kusikia umeoa, vipi niwe mbali nawe? Nikisikia upo na Mage ningekufa mimi."
***
Baada ya kuwajulisha siku ya kuonana na Kampuni ya Ebony walifika katika Hoteli ya The Beach na kuingia mkataba mpya wa miaka miwili. Pia kampuni ya maonesho ya mavazi na urembo nayo iliingia mkataba mpya na makubaliano ya kuanza kazi baada ya miezi mitatu.


Mage naye alitoka hospitali akiwa na afya njema, mama yake alipotaka kujua sababu ya mshtuko ule, alimweleza ukweli kuwa baada ya kuona harusi ya Colin na Cecy alipata mshtuko wa ajabu kilichoendelea hakujua mpaka alipozindukia Hospitali ya Muhimbili akiwa amepooza upande mmoja.
"Unasema nani kaoa? Sijakuelewa vizuri," mama Mage alishtuka kusikia Colin kaoa.
"Colin, mama."


"Kama ni kweli basi mwanangu achana na mawazo ya Colin, Mungu atakupa mume wa kweli."
"Mama hata mimi nimejifikiria hivyo lakini Colin nilimpenda sana."


"Si kweli, ulimpenda Hans, Colin anapendwa na Cecy kwa hiyo waache na ndoa yao."
"Ndiyo mama, japo nilikuwa na nia mbaya kwa Cecy, lakini kuanzia sasa sitashughulika na Colin wala Cecy nami nasubiri ndoa yangu."


"Hilo ndilo neno la kijasiri mwanangu."
Baada ya Cecy kumaliza mapumziko alianza kazi rasmi, mwaka mmoja baadaye alishika ujauzito na kusubiri muda wa kujifungua. Mage naye alipata mchumba na mambo yalikwenda kama yalivyopangwa.


Siku ya harusi akiwa anajiandaa kwenda kanisani anapata habari zilizomshtua moyo na kufanya apoteze fahamu kuwa mpenzi wake Hans yupo huru baada ya kushinda rufaa yake.


*****************************************MWISHO***********************************


Baada ya kuwa safari ndefu hatimaye chombo kinatia nanga, mambo ya kujifunza kutokana na simulizi hii yako mengi ngoja nianishe machache tu, 1. mapenzi ya kweli hayaangalii hali ya mtu awe na pesa asiwe na pesa, 2. tuthamini hisia za mtu anayekupenda, 3.usimfanyie unyama mwenzio hasa wa kimapenzi aliyoyafanya Mage kwa coliny ndo yaliyomtesa mpaka mwisho. Mwisho wa yote mpende akupendae asiye kupenda chapa lapa
 
Back
Top Bottom