Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

"Hukutakiwa kununua pilipili" huyu Maza naye mtata kama kinyonga anaelekea kufuta maslahi yake kwa mwanaye kuoa msomi na tajiri na sasa anaanza kuwekeza kwenye afya ya mwanaye.
Khantwe na muuza ubuyu kuja kipande ii.
DAUDI 1 asante kumsogeza wakili.
 
Last edited by a moderator:
"Hukutakiwa kununua pilipili" huyu Maza naye mtata kama kinyonga anaelekea kufuta maslahi yake kwa mwanaye kuoa msomi na tajiri na sasa anaanza kuwekeza kwenye afya ya mwanaye.
Khantwe na muuza ubuyu kuja kipande ii.
DAUDI 1 asante kumsogeza wakili.
Kwenye upendo wa kweli pesa wala usomi havina nafasi, Asante
 
"Hukutakiwa kununua pilipili" huyu Maza naye mtata kama kinyonga anaelekea kufuta maslahi yake kwa mwanaye kuoa msomi na tajiri na sasa anaanza kuwekeza kwenye afya ya mwanaye.
Khantwe na muuza ubuyu kuja kipande ii.
DAUDI 1 asante kumsogeza wakili.

Nimesoma wii....huyu mama naona taratibu anaanza kuukubali ukweli
 
Last edited by a moderator:
duuuuuhhh.....hadithi tamu ila huwa mnatuacha njiapanda kama ya akina Bitungu imeishia wapi??
 
ILIPOISHIA
Muda mwingi walitumia kukaa wawili chumbani kila asubuhi na jioni walifanya mazoezi madogomadogo katika Gym iliyokuwa katika hoteli waliyofikia na majira ya saa moja walitembeatembea pembezoni mwa ufukwe.
SASA ENDELEA..
.

Lilikuwa penzi lililozaliwa upya kwa wapendanao baada ya kupoteana kwa kipindi kirefu.
Baada ya wiki mbili, Cecy naye, kimwili kilianza kurudi wakiwa wamejipumzisha chumbani kwao, Cecy alimuuliza mpenzi wake ambaye aliamini alikuwa na ufahamu tofauti na yeye alikuwa nusu mfu.
“Colin nina imani wakati naumwa ulikuwa karibu na Mage.”

“Si kweli, huwezi kuamini toka ile ajali sina ukaribu na mtu, nilikuwa sitoki ndani hata simu kuanzia siku ile situmii. Najua Cecy huniamini lakini nakuhakikishia niliapa mbele ya mama yangu na mama Mage walipokuja kuniona hospitali kuwa sitaoa mwanamke mwingine kama wewe ungekufa.

“Niliwaeleza kama utakufa nitatimiza ahadi niliyokuahidi kwa kufunga ndoa na maiti yako na nisingeoa tena mpaka nakufa.”“He! Kwa nini ufanye hivyo, ningekufa mimi si ingekuwa nafasi ya mwingine. Heri tungekuwa tumezaa ungekuwa na sababu ya kufanya hivyo.”

“Cecy kuoa mwanamke mwingine wakati ajali nimesababisha mimi ningekuwa nimeshiriki kwenye kifo chako. Wewe ndiye wakili wa moyo wangu umenitetea wakati wote wa matatizo yangu. Bila wewe kitendo alichonifanyia Mage ningeweza kuwa chizi.”

“Asante kwa kunipenda kwa kipindi chote cha mateso yangu, Colin nimeamini wewe ni mume wa maisha yangu naomba Mungu adumishe penzi letu ufe nikuzike nife unizike.”
“Asante mpenzi wangu nitakupenda siku zote za maisha yangu.”
“Hata mimi. Colin...” Cecy alimwita mpenzi wake akimtazama usoni.
“Naam.”

“Siku ya kuondoka ulikataa kubeba simu sasa tutawasiliana vipi na nyumbani?”
“Nimeapa sitatumia tena simu katika maisha yangu kwani ndiyo sababu ya kutaka kuyachukua maisha yetu. Pia wazazi nimewajulisha tupo hoteli gani wakitutaka watupata tukiwataka tutawapata kwa njia ya simu ya hotelini.”

“Colin, naweza kusema wivu wangu wa kijinga umetufikisha hapa, sikutakiwa kukosa imani kiasi kile cha kutaka kila kitu katika simu yako nikione. Naweza kusema nilijitakia mwenyewe. Nimejifunza kitu sikutakiwa kukubana kiasi kile kwa vile mapenzi ya kweli yako moyoni na wala si kwenye simu.

“Colin nilikupenda kupitiliza na kujikuta nakuwa kichaa wa mapenzi kwa ajili yako, lakini umenidhihirishia kwa vitendo kuwa unanipenda mapenzi ya dhati kwa vile hukuyumba wakati wa matatizo yangu. Angekuwa mwanaume mwingine angekwishakuwa na mchumba mwingine au ameshafunga ndoa.

“Colin mpenzi wangu nakuomba kuanzia leo hii tumia simu, mimi si limbukeni tena wa simu. Upendo na uaminifu wako ameufanya moyo wangu uwe huru na kukuamini kwa asilimia mia. Colin najivunia kuwa na mwanaume kama wewe nimekutafuta kwa udi na uvumba japo mama yako alifanya utani kuniita mkwe lakini niliamini nami nina haki ya kuwa na mwanaume nimtakaye aliye katika hali yoyote.

“Asante Colin kugeuza mazoea ya maskini hana haki ya kupenda, nipende Colin nikupende, Colin unajua wewe ndiye mwanaume wangu wa mwanzo na wa mwisho. Nakupenda Colin zaidi ya kupenda.”

“Cecy najua thamani yako moyoni mwangu ni zaidi ya madini yote unayoyajua na usiyoyajua. Niliapa moyoni mwangu sitakupoteza mtetezi wa moyo wangu. Cecy mpenzi wewe ni zaidi ya mwanamke, ni malaika wangu.”

“Asante mpenzi, ila hujanihakikishia utatumia simu?”
“Cecy, nilitaka kuacha kutumia simu kwa ajili yako, lakini kwa vile umeniruhusu nitatumia.”
“Colin.”
“Naam.”

“Nina ombi moja naomba ukikubalie kwani toka nimefika hapa kuna kitu kimekuwa kikinisumbua jibu lako ni faraja ya moyo wangu.”“Cecy malkia wangu, sema chochote nitakitekeleza.”
“Kuna kitu nimejifunza kwako kila unapotaka kufunga ndoa kunatokea matatizo umeshalingudua hilo?”
“Dah! Kweli kabisa mpenzi hilo jambo hutokea.”

“Sasa nitataka tufanye kitu tofauti katika safari yetu hii.”
“Kitu gani?”“Tufunge ndoa kabisa hukuhuku, tukirudi tuwe mke na mume.”
“Mmh! Lakini ndoa yenye baraka lazima wazazi wawepo.”

“Wazazi tutawaita huku tukirudi Tanzania tunafanya sherehe tu.”
“Sawa hakuna tatizo.”Walikumbatiana kwa furaha walizima taa ya mwanga mkali na kuwasha ya mwanga hafifu kila mmoja aliyasikia mapigo ya moyo wa mwenzake.
***
Mage alionekana kuchanganyikiwa kutokana na taarifa za kupona kwa Cecy, mwanamke aliyejua ni wa kufa siku yoyote. Kilichomchanganya zaidi ni kugeuka kwa mama Colin kusimama upande wa Cecy wakati mwanzo alimpa moyo wa kumpata mwanaye.

Akiwa bado hajajua atafanya nini alipata taarifa iliyomkata maini ya Colin kwenda Afrika Kusini na mchumba wake kwa ajili ya mapumziko ya muda mrefu. Lakini hakutaka kukata tamaa aliamini njia ya kumpata Colin ni kumuua Cecy au kumtia kilema ambacho kitamfanya asiolewe na Colin.

Wazo la kuua aliliweka kando kwa muda kwa kuamini lile lingekuwa la mwisho kabisa baada ya mipango ya awali kufeli. Aliamini anaweza kutumia njia nyingi kuhakikisha Cecy aolewi na Colin.

Mpango ulikuwa kummwagia tindikali au kutuma vijana kumbaka na picha zake kusambazwa kitu ambacho aliamini Colin na familia yake wasingekivumilia lazima angempiga chini Cecy.
Mpango wake alipanga kuupanga kabla ya Colin na mpenzi wake kurudi kutoka Afrika Kusini.

Alijua ndoa ingechukua muda ili kusubiri afya ya Cecy iimalike naye angetumia nafasi ile kumtia doa Cecy na yeye kuichukua nafasi aliyokuwa akiitafuta usiku na mchana kama wokovu baada ya mwenyewe kuichezea shilingi kwenye tundu la choo.

Aliapa kutumia kiasi chochote cha fedha kuhakikisha anampoteza Cecy na kulimiliki penzi la Colin. Walijipanga kutafuta watu ambao angewalipa kiasi cha pesa watakachokubaliana ili wamfanyie kazi yake kwa uhakika bila mtu yeyote kugunuda kitu.

Wakati akiwaza hayo taarifa ya kuitwa Afrika Kusini iliwafikiwa wazazi wa Colin na Cecy kuwa wanatakiwa mara moja. Japokuwa hawakujua wanaitiwa nini, walikubaliana kuondoka kwenda kuwasikiliza watoto wao wana lipi. Baada ya siku nne Colin na Cecy waliwapokea Uwanja wa Ndege wa Port Elizabeth na kuwapeleka katika Hoteli ya The Beach waliyofikia wao.

Wote walifarijika kukuta afya ya Cecy imeimalika haraka na nuru yake ya awali ikianza kuonekana kwa mbali. Ilikuwa furaha kwa familia kukutana wote wakiwa katika hali ya furaha. Usiku wa siku ile baada ya chakula walikaa pamoja kwa ajili ya mazungumzo.

Mzungumzaji mkuu alikuwa Cecy ambaye ndiye aliyemuomba Colin aseme yeye.
“Wazazi wetu najua mmeshtuka na wito wetu wa ghafla, lakini wito huu una maana kubwa katika maisha yetu watoto wenu. Wito huu ni kwa ajili ya kuja kusimamia harusi ya watoto wenu.”
“Watoto wetu kina nani?” mama Colin aliuliza.

“Ya mimi na mume wangu Colin ambayo tumepanga kufunga ndoa wiki ijayo.”
“He! Mbona haraka sana kwa nini mnataka kufungia huku?” aliuliza mama Cecy.
“Mama kuna kitu kiliniijia haraka akilini mwangu ambacho nilikiamini kabisa na nilipomwambia mwenzangu ambaye alikubaliana na nilichokiona ni kukubaliana kufunga ndoa huku.”
“Kitu gani?” mama Colin aliendelea kuuliza.

“Nilifuatilia hatua zote za harusi za mpenzi wangu ambazo huvurugika mwishoni, mfano wa kwanza muda mfupi kabla ya kumuoa Mage lilitokea tatizo lililomjeruhi moyo mpenzi wangu. Mfano wa pili muda mfupi kabla ya ndoa yetu likatokea la kutokea, hivyo imeonesha kuna tatizo.

“Nilichokiwaza mimi ni kuhusiana matukio yote hivyo naamini huku tutafunga ndoa isiyo na starehe ambayo itakuwa na baraka ya wazazi wa pande zote. Kwa hiyo wazazi wetu tunaomba mkubali ombi letu ili tukirudi Tanzania tuwe tayari mke na mume. Kuhusu sherehe tutaifanya tukijipanga.”
“Mmh! Colin we ulikuwa unasemaje?” mama Colin alimuuliza mwanaye.

“Namuunga mkono mpenzi wangu amekuwa na jicho la tatu ambalo wote tulikuwa hatuna.”
“Mipango ya harusi mmeshaandikisha kanisani?”
“Tumeshakamilisha kila kitu na tulikuwa tukiwasubiri ninyi tu.”
“Basi hakuna tatizo kwa vile jambo ni la heri tutakuwa pamoja, sijui dada unasemaje?” mama Colin alimuuliza mama Cecy.

“Hata mimi naungana na wewe.”
Wazazi hawakuwa na pingamizi lolote walikubaliana kusimamia ndoa ya watoto wao ili wakirudi nyumbani Tanzania wajipange kwa sherehe.
Je ndoa itafanikiwa? na mage mpango wake utafanikiwa? tukutane hapa hapa jumamosi ijayo
*Kumbuka haki ya mtu haipotei bali hucheleweshwa na mwisho wa ubaya ni aibu*
 
"Hukutakiwa kununua pilipili" huyu Maza naye mtata kama kinyonga anaelekea kufuta maslahi yake kwa mwanaye kuoa msomi na tajiri na sasa anaanza kuwekeza kwenye afya ya mwanaye.
Khantwe na muuza ubuyu kuja kipande ii.
DAUDI 1 asante kumsogeza wakili.
Wakili yuko mahakamani unasubiriwa wewe
 
Back
Top Bottom