Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

ILIPOISHIA:
Walianza kutangulia mabinti
ambao nao walikuwa katika
kampuni hiyo. Baada ya kupita
wote ikafika kipindi akatokea
Cecy katika vazi la kitenge
chenye kilemba kirefu na
kufanya ukumbi ulipuke
mayowe.
Alipita kwa mavazi zaidi ya
kumi ya ubunifu na kuacha
historia kwenye onesho hilo.
SHUKA NAYO SASA . ..
“Mage huyu si yule msichana
aliyeingia na Colin siku ya Send
Off yako?” Brenda aliuliza
baada ya kumfananisha Cecy .
“Ndiye yeye.”
“Mage tuache utani msichana
huyu mzuri tena ana uzuri wa
asili,” Brenda alimsifia Cecy.
“Hana lolote uzuri upo wapi?”
Mage aliponda .
”Wivu huo, kwenye ukweli
uongo hujitenga , yule msichana
mzuri.”
“Brenda tutakorofishana
tumekuja kuangalia mavazi au
kuja kumsifia mtu, kwanza
mavazi aliyovaa ya kishamba
nani sasa hivi anavaa mavazi ya
kanga na kitenge. Angejua wala
hakupendeza lolote, ’ Mage
alimbeza Cecy.
“Mageee! Siamini kama una
nafasi katika moyo wa Colin ,
kitu kama hiki hata mimi
nikimuona yupo mpenzi wangu
lazima nipate presha, ” Brenda
alizidi kumuumiza roho shoga
yake.
“Brenda naona umetumwa kuja
kuniumiza roho, kosa langu kuja
na wewe pamoja?” Mage alikuja
juu.
“Lakini Mage kwani nikimsifia
yule mwanamke kuna ubaya
gani ikiwa wewe ni mchumba
wa mtu na Colin si mtu wako ?”
“Unajuaje kama nitarudiana na
Colin. ”
“Mrudiane kivipi ikiwa wewe
utaolewa na Hans na Colin
anaweza kumuoa huyo
msichana.”
Wakiwa katikati ya onesho hilo,
Colin ambaye alifahamika kama
mkurugenzi wa kampuni ile ya
urembo na mavazi , alifuatwa na
watu wenye majarida ya
urembo kumtaka Cecy kwa ajili
ya kuyapamba majarida yao kwa
sura yake kwa mkataba mnono.
Pia makampuni mengine ya
Afrika ya Kusini na Ufaransa
ambao walikuwa wageni
waalikwa walivutiwa na Cecy
kisha kuomba kufanya naye kazi
kwa mkataba mnono .
Nyota ya Cecy ilizidi kung ’aa,
Colin aliwakubalia lakini
walitakiwa waonane kesho kwa
ajili ya mazungumzo zaidi ,
walikubaliana.
Siku ile pia ilikuwa maalumu
kwa Colin . Wakati burudani
ikiendelea, MC alisimamisha
kwa muda ili mkurugenzi aseme
neno.
Colin alichukua kipaza sauti na
kuwasalimia wageni wote kisha
alisema:
“Ndugu zangu kwanza
nashukuru kwa muitikio katika
onesho la leo ambalo limekuwa
na mafanikio makubwa tofauti
na nilivyofikiria . Mpaka sasa
tumepata naombi ya kumtaka
Malkia Cecy kupamba majarida
na pia kwenda kufanya
maonesho Afrika Kusini,
Marekani na Ufaransa ,” kauli ile
ilifanya ukumbi ulipuke kwa
mayowe.
“Lakini hilo silo lililonifanya
nimnyang’anye kipaza sauti MC ,
nia yangu nilikuwa nimeweka
ahadi moyoni mwangu siku ya
leo nifanye kitu gani. Naomba
nimwite malkia wa usiku wa leo
Cecilia hapa mbele. ”
Cecy alitoka chumba maalumu
akiwa na gauni refu jekundu
lililokuwa likiburuza kwa nyuma ,
lililokuwa limempendeza sana
kama bi harusi .
“Ndugu zangu, wazazi wangu
na wageni waalikwa katika
onesho hili la kwanza la
kimataifa. Leo ndiyo
namtambulisha kwenu wakili wa
moyo wangu, binti mrembo
Cecy kuwa ndiye mke wangu
mtarajiwa,” ukumbi ulilipuka
tena kwa mayowe.
Colin aliendelea kwa kujipapasa
na kutoa mkebe mdogo na
kusema:
“Cecy mpenzi fumba macho ,”
Cecy alifanya vile .
Colin alitoka pete ya tanzanite
iliyochanganywa na almasi na
kukishika kidole cha Cecy na
kumvisha na kufanya ukumbi
wote kulipuka kwa mayowe kila
mtu akisema kapo nzuri
imepatikana.
Lile lilikuwa pigo mujarabu kwa
Mage aliyekuwa na ndoto za
kurudi kwa Colin kama Hans
atafungwa.
Mapigo ya moyo yalianza
kumwenda mbio na jasho
kumtoka kwa wingi ,
kizunguzungu kikali kilimshika
na kiza kinene kilitanda mbele
yake na kumfanya adondoke
alipokuwa amekaa .
Alichukuliwa haraka kwenda
kupewa huduma ya kwanza kwa
vile pale ukumbini kulikuwa na
kila kitu.
Shughuli ilendelea kwa MC
kulitangaza vazi jipya la
wachumba siku ya kuvishana
pete lililompendeza vilivyo
Cecy. Baada ya maonesho yale,
Colin alijiandaa kuingia
mkataba mnono wa Cecy na
hayo makampuni.
Cecy aliingia mkataba wa
mamilioni ya fedha wa miaka
miwili kwa makampuni mawili
ya majarida makubwa Marekani
moja la Vibe na Ebony kwa ajili
ya kupamba ukurasa wa mbele
pia aliingia mkataba mnono wa
kampuni ya maonesho ya
mavazi ya Ufaransa ambayo
yalibadili maisha ya Cecy toka
umaskini wa kutupwa mpaka
msichana bilionea .
Baada ya kuingia mkataba
mnono uliomtaka aanze kazi
hiyo mwezi mmoja baadaye kwa
ajili ya mazoezi ya mwezi
mmoja na kujifunza lugha vizuri
kabla ya kuianza kazi hiyo mara
moja, Cecy aliomba
kuzungumza kwanza na familia
yake pamoja na mpenzi wake
Colin ili ajue ataanza lini kazi
yake, walikubaliana kumpa siku
mbili za kutoa jibu ili
wakiondoka wajipange vipi.
Ilikuwa tofauti na mapokeo ya
Cecy baada ya kulala maskini
na kuamka tajiri mkubwa.
Ndoto yake ilikuwa kuolewa na
Colin na si kufanya kazi ya
mabilioni, alijiuliza kukaa miaka
mwili nje ya nchi lazima Colin
atatafuta mwanamke mwingine
na yeye kupoteza kitu muhimu
maishani zaidi ya fedha
atakazolipwa katika kazi yake.
Kwake alichokitafuta kilikuwa
kuwa karibu na Colin na
kufanikiwa kuwa naye karibu na
kubakia kitu kimoja ndoa
ambayo aliiota siku zote. Baada
ya kuachana na wenye
makampuni toka nchi za nje ,
Cecy alionekana mtu mwenye
mawazo tofauti na kitu
alichokipata cha kugeuka
bilionea kwa kufanya onesho
lake moja na kuonekana .
Baada ya kufika nyumbani
ilibidi amuulize:
“Vipi mpenzi wangu mbona
kama hauna furaha wakati leo
umeuaga umaskini ?”
“Mi kwangu naona kama ndiyo
unataka kuniongezea umaskini ,”
Cecy alijibu kinyonge .
“Vipi?”
“Hivi nikiwa huko tutakuwa
pamoja?”
“Hapana ila tutaonana mara
chache kwa vile utakuwa bize
na kazi yako ya kuizunguka
dunia kufanya maonesho. ”
“Huoni kama nitakuwa
nimepata fedha zisizo na faida
kwangu.”
Itaendelea wiki ijay
 
Sasa mkuu unavotufanyia sio fair... yaani tumesubir siku zote leo unasema itaendelea wik ijayo... duh kuwa na huruma bas
 
Hii hadithi haina mwenyewe sasa wote hawataki kuiendeleza! Daudi1 hata wewe umeingia mitini?
 
Last edited by a moderator:
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA :
“Mi kwangu naona kama ndiyo
unataka kuniongezea
umaskini,” Cecy alijibu
kinyonge.
“Vipi?”
“Hivi nikiwa huko tutakuwa
pamoja?”
“Hapana ila tutaonana mara
chache kwa vile utakuwa bize
na kazi yako ya kuizunguka
dunia kufanya maonesho .”
“Huoni kama nitakuwa
nimepata fedha zisizo na faida
kwangu.”
SHUKA NAYO SASA . ..
“Kivipi?”
“Colin wewe ni kila kitu
kwangu, niliapa kuwa mbali na
wewe ni pale mmoja wetu
akichukuliwa na umauti na si
vinginevyo. ”
“Hilo tu, nitakuwa naonana na
wewe kila mara wala usihofu .”
“Colin nina wasiwasi nikiwa
mbali kuna vipanga watu
watakunyakuwa na mimi
kuichukia dunia, kukupata
nimetoka jasho la damu.
Furaha yangu ni kuwa karibu
yako na si kuingiza mamilioni
ya fedha. ”
“Najua mpenzi unanipenda
lakini hili dili ni zaidi ya
mapenzi kwa vile
litayabadilisha maisha yako
sasa hivi una uwezo wa kujenga
gharofa Masaki au Kunduchi. ”
“Colin mimi huko siendi na
hizo hela zao sizitaki . ”
“Usifanye hivyo , ukilipoteza
utakuja kujuta maisha yako
yote.”
“Moyo wangu naujua hauna
shida ya mabilioni ya fedha bali
upendo toka kwako, pia naona
umekwenda kinyume na
makubaliano yetu. ”
“Kivipi mpenzi?”
“Ulisema unataka kunifungulia
kampuni ili niwe nafanya
maonesho na si kwenda kufanya
kazi nje ya nchi. ”
“Mpenzi, yaani dili ulilolipata ,
fedha utakayoipata kwa miaka
yote hiyo unaweza kukaa bila
kufanya kazi na kuishi maisha
ya juu .”
“Sina maana hiyo, uliniahidi
baada ya kumaliza masomo
unanioa sasa ahadi yetu ipo
wapi? Au ndiyo unanitoa
kijanja urudiane na Mage
baada ya mpenzi wake
kufungwa?” Cecy alilia wivu .
“Ahadi yetu ipo palepale, we
fanya kazi mwaka mmoja kisha
tunafunga ndoa ndipo nitajua
nitafanya nini. ”
“Cecy mpenzi hujui tu kiasi
gani cha fedha utakacholipwa ,
ni wasichana wachache duniani
wenye bahati hii . Tukitaka
tufanye harusi itachukua muda
wakati mwezi ujao unatakiwa
Afrika Kusini kwa mazoezi ya
wiki mbili kabla ya kwenda
Ufaransa.
Kutokana na makubaliano, picha
za Jarida la Ebony watatumia za
kwenye onesho na zile
walizokupiga siku ile. Malipo
yako ya kwanza yataingia mwezi
ujao ya dola elfu mia mbili
arobaini (Sh 408 ,000 ,000 ) kwa
mwaka.
Baada ya mwaka malipo
yataongezeka na kuwa dola elfu
mia tatu ( Sh 510 , 000 ,000 ). Pia
utapata bonasi ya asilimia tano
kutokana na mauzo, huoni kwa
miaka miwili utakuwa mbali
mpenzi wangu kwa kutengeneza
dola elfu mia tano arobaini ( Sh
918 ,000 ,000 )?
Bado kampuni ya maonesho
itakulipa dola elfu mia tatu ( Sh.
510 ,000 ,000 ) kwa mwaka na
bonasi kila onesho la nchi
kubwa barani Ulaya na Amerika.
Unataka nini tena mpenzi
wangu, kipindi hiki, hebu ndoa
iweke pembeni tupige pesa .”
“Colin nakuona kama
unampigia mbuzi gitaa,
nakueleza kwa mara ya mwisho,
pesa inaweza kununua kitu
chochote chini ya jua lakini si
furaha ya moyo wa mtu , dawa
ya mtu ni mtu si kitu. ”
“Mmh ! Sasa wewe ulikuwa
unatakaje?”
“Kwanza tuoane kisha tutajua
kama kwenda au kufanyia kazi
hapa lakini si kukaa mbali na
wewe .”
Ulikuwa mtihani mzito kwa
Colin kutokana na msimamno
wa mpenzi na kuliona kama dili
lile litapeperuka kwani
walikuwa wapo nchini
wakisubiriwa kauli yao kwamba
ataanza lini kufanya kazi. Lakini
kwa Cecy alikuwa haelewi kitu .
Jioni ya siku ile Colin alikutana
na mama Cecy na kumuelezea
hatua waliyofikia na uamuzi wa
Cecy.
“Mama nilikuwa naomba
umweleze mwenzangu akubali
kwanza kwenda kufanya kazi,
ndoa itafuata baadaye .”
“Mmh ! Nitajaribu kumweleza ,
nina imani atanielewa .”
“Yaani nitashukuru sana,
sijawahi kuona mwanamke
mwenye msimamo kama Cecy .”
Kwa vile Cecy alikuwa
amekwenda kuoga aliporudi
alikaa pembeni ya mama yake
na kumuacha Colin aliyekuwa
amekaa kochi la peke yake.
Baada ya ukimya mfupi mama
Cecy aliuvunja ukimya ule .
“Cecy mama. ”
“Abee mama .”
“Nina imani leo Mungu
atuangazia maisha yetu ?”
“Ni kweli mama, lakini maisha
hayatakuwa na furaha bila
kutimiza ndoto yangu .”
“Najua una hamu ya kutimiza
ndoto yako , lakini kilichotokea
ni muhimu kwa wakati huu
ndoa yako ipo palepale .”
“Hilo nalijua , siku zote fimbo ya
mbali haiuwi nyoka, kama
nitaanza kazi naweza kukaa
hata miezi mitatu bila kumuona
Colin na wakati penzi langu
limenitoa jasho la damu.
Naweza kupata fedha lakini
nikapata jeraha lisilopona
mpaka nakufa na pengine
likawa ndiyo sababu ya kifo
changu.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mama kama unavyojua
mchumba wa Mage yupo ndani
na kesi yake ni nzito , kwa
habari za juujuu kweli
anahusika katika vifo vya mkewe
na mwanaye ili arudiane na
Mage . Kwa hiyo uwezekano wa
kutoka ni mdogo , huoni muda
huo nikiwa mbali na Colin
penzi linaweza kuzaliwa upya
na nafasi yangu kupotea.
“Kama nilijitoa kwa ajili ya
Colin ifike wakati nimkose hizo
fedha zitakuwa na faida gani
kwangu. Nipo tayari kupoteza
hata fedha zilizojaa bahari
lakini si kumpoteza Colin , moyo
wangu ndiyo unaojua thamani
yake si yeyote.
Mama hujui kiasi gani niliumia
niliposikia Colin akioa lakini
machozi yangu hayakwenda
bure, Mungu alisikia kilio
changu na kunirudishia mpenzi
wangu mikononi mwangu na
kuamini haki ya mtu huwa
haipotei bali hucheleweshwa .”
“Sasa kama unafahamu hivyo
kwa nini una wasiwasi na
Mage ?”
“Mama, Golden chance never
came twise .”
“Hapo umeniacha feri una
maanisha nini?”
“Kwangu hii ni nafasi ya
dhahabu kamwe haijirudii mara
mbili. ”
“Cecy nakuahidi wewe ndiye
mwanamke wa maisha yangu ,
nilivyofahamu thamani yako
ndani ya moyo wangu upengo
wangu uliongezeka mara dufu.
Itaendelea wiki ijayo .
 
Aya mkuu... tutaenda ivoivo ingawa ni mwendo wa kudorora sana ila naamini tutafika ty...
 
WAKILI WA MOYO

ILIPOISHIA:
“Sasa kama unafahamu hivyo kwa nini una
wasiwasi na Mage ?”
“Mama , Golden chance never came
twise. ”
“Hapo umeniacha feri una maanisha nini ?”
“Kwangu hii ni nafasi ya dhahabu kamwe
haijirudii mara mbili. ”
SASA ENDELEA .. .
“ Cecy nakuahidi wewe ndiye mwanamke wa
maisha yangu , nilivyofahamu thamani yako
ndani ya moyo wangu upendo wangu
uliongezeka mara dufu. Cecy wewe ndiye
wakili wa moyo wangu uliyenitetea wakati
wa matatizo hakuahidi sitamfungulia
mwanamke mwingine moyo wangu
nilipokufungia moyoni mwangu ufunguo
niliutupa baharini, ” Colin alimuhakikishia
mapenzi yake ya dhati kwake .
“ Colin ufunguo kuutupa baharini ni usemi tu
lakini mnasahau ufunguo unaweza kumezwa
na samaki na kuurudisha watu wakauokota
na kuufunguo moyo wako na mimi ukanitoa
moyoni mwako . Colin unanipenda ?” Cecy
alimuuliza Colin huku amemkazia macho .
“ Zaidi ya sana na kama kuna kauli nyingine
zaidi ya hiyo ungeijua ningeisema mbele
yako .”
“ Naomba unioe .”
“ Nitakuoa kwa vile wewe ndiye mwanamke
wa maisha yangu .”
“ Si kwa wakati mnaotaka ninyi bali kabla ya
kuanza kazi yangu nataka nikisimama
sehemu nijulikane kama Mrs Colin na si
Miss Cecy . ”
“ Muda tuliopewa ni mdogo sana wa
maandalizi ya harusi , hivyo ungekwenda
kufanya kwanza kazi kisha ukirudi
tutafunga ndoa utakuta maandalizi tayari
ukifika tunafunga ndoa na kuondoka. ”
“ Kwani kazi si naanza mwezi unaokuja huu
muda hatuwezi kufunga ndoa?”
“ Cecy wewe sasa si Cecy muuza ndizi bali
wa kimataifa kwani wiki ijayo sura yako
inaruka dunia nzima kwenye Jariba la Ebony
harusi yako haitakiwi kuwa ya kulipua bali
iendane na wewe mwenyewe .”
“ Mimi Cecy hata niwe vipi bado nitabakia
Cecy muuza ndizi, kwa hiyo kama mna nia
nifanye kazi, tufunge ndoa ya kawaida ila
sherehe nikirudi zaidi ya hapo kazi yenyewe
siitaki na msiniambie kitu kinachohusu hiyo
kazi. Fedha inatafutwa kwa njia yoyote lakini
upendo kwa kweli ni adimu kama maji
jangwani.
“ Naweza kumsifu Mage kwa kuvunja
uchumba wetu si kwanza nimepata nafasi
bali amezieleza hisia zake za kweli toka
moyoni kwake kuwa kuna mtu aliyekuwa
akipenda kwa dhati . Kosa walilofanya kuua
viumbe wasio na hatia lakini walikuwa wapo
sahihi kabisa . Kama mliona Mage yupo
radhi kulaaniwa na dunia kwa ajili ya
mapenzi basi na mimi nipo tayari kufa
masikini kwa ajili ya mapenzi, ” Cecy alisema
kwa sauti kavu isiyo na mzaha hata kidogo.
“ Mmh ! Mwanangu Colin mpaka hapo mimi
sina neno siku zote mwenye kujua maumivu
ya moyo ni mhusika , wengine ni washauri
na mwisho wa siku ana uamuzi wa kukubali
au kukataa anabakia nao mwenyewe na
mwenzio amekataa , ” mama Cecy hakuwa
na la kuongeza baada ya kauli ya mwanaye.
“ Mama nimesikia yote nitayafanyia kazi,
najua kabisa Cecy ananipenda na
ameteseka juu yangu .
Nimemuhakikishia yeye ndiye chaguo la
moyo wangu na mwanamke wa maisha
yangu kwa vile moyo wake imeingia
wasiwasi basi nitafanya anavyotaka mpenzi
wangu ili aamini mbegu yake ya upendo
imemea kwangu na kuzaa matunda. ”
“ Hilo ndilo neno nililokuwa nikilisubiri usiku
na mchana , najua hukupenda maamuzi
yangu lakini utaamini siku moja kwa nini
nimeharakisha harusi .” Baada ya
makubaliano ya kufunga ndoa kabla ya
kwenda kuanza kazi, Colin alikwenda kwa
mama yake kumweleza taarifa ya Cecy
kupata mkataba mnono na kutakiwa
kwenda kufanya kazi nje na
alivyong ’ ang’ ania kuolewa kuliko kufanya
kazi. Alipofika nyumbani alimkuta mama
yake amekaa sebuleni , alimsalimia na kukaa
pembeni yake .
“ Vipi baba, una jambo ?” mama yake
alimuuliza kwa vile alimfahamu vizuri
mwanaye.
“ Ndiyo mama .”
“ Ehe , ” mama yake aliweka vitu vyake chini
na kugeuka amsikilize vizuri mwanaye kwa
vile kila kukicha alikuwa na jaka moyo . Hasa
baada ya ndoa ya mwanaye na Mage
kuvunjika katika hatua za mwisho.
Colin alimweleza mkataba alioingia Cecy na
makampuni yote ambayo yalimuacha mama
yake kinywa wazi kufikia hatua ya kusema .
“ Yaani Cecy muuza ndizi alipwe mamilio ya
fedha kwa kazi ya kupamba jarida na
kuonesha mavazi huoni atakutana na watu
wengi wenye fedha na wewe kukuacha ?
Kwa nini umemtafutia kazi kama hiyo wakati
shida yako ilikuwa awe mkeo kwa vile
hatuna shida katika maisha yetu.”
“ Mama, yote hayo tisa kuna kitu Cecy
kanichanganya sana yaani mpaka kichwa
kinaniuma, ” Colin alisema kwa sauti ya
unyonge.
“ Kitu gani? Nilijua lazima uhusiano wenu
utaingia dosari pesa atakazolipwa ni nyingi
sana hasa akizingatiwa alikuwa hohehahe , ”
mama Colin alichangia bila kujua anataka
kuambiwa nini .
“ Sivyo unavyofikiria mama , Cecy anataka
ndoa kabla ya kwenda kuanza kazi.”
“ He! Si umesema mwezi ujao anatakiwa
kuondoka?”
“ Ndiyo, lakini yeye amesema bila ndoa na
kazi hataki. ”
“ Mbona sikuelewi, hataki kazi kwa ajili ya
ndoa?”
“ Ndiyo mama , anataka akiondoka hapa awe
tayari mke wangu .”
“ Kwa nini anafanya haraka hivyo, kwa nini
asiende kwanza kisha arudi kufunga ndoa
wakati huo maandalizi yatakuwa
yamekamiliksa anaolewa na kuondoka .”
“ Amekataa, amesema nikimlazimisha
kwenda na kazi yenyewe hataki. ”
“ Kweli elimu ni muhimu . Yaani anataka
kuyakataa mamilioni kwa ajili ya ndoa tu?”
Mama Colin alishangaa .
“ Mama Cecy ni tofauti na wanawake wengi ,
mimi kwake ni kila kitu hasikii wala haoni
anasema anaweza kuondoka huku nyuma
Hans akafungwa hivyo naweza kurudiana na
Mage na yeye kupoteza alichokitafuta muda
mrefu.”
Itaendelea Jumamosi wiki ijayo .
Yupo radhi kuendelea kuuza ndizi lakini si
kunikosa mimi. ”
“ Mmh ! Kazi ipo , sasa utafanyaje ?”
“ Nilikuwa naomba ushauri wako japo
nilimkubalia kufunga naye ndoa kabla ya
kuanza kazi.”
“ Ninafikiri wazo lako zuri , japokuwa
sikupenda harusi ya aina hiyo, lakini kwa
Svile naujua msimamo wa yule msichana
sina budi kukubaliana nawe. Sijawahi kuona
mwanamke msimamo mkali kama yule
binti. Anajiamini katika kitu anachokitafuta
hasa akiwa na haki nacho .”
Itaendelea wiki ijayo Jumamosi .
 
ILIPOISHIA :
“Ninafikiri wazo lako zuri, japokuwa sikupenda
harusi ya aina hiyo, lakini kwa vile naujua
msimamo wa yule msichana sina budi
kukubaliana nawe . Sijawahi kuona mwanamke
msimamo mkali kama yule binti. Anajiamini
katika kitu anachokitafuta hasa akiwa na haki
nacho.”
SASA ENDELEA .. .
Walikubaliana kufanya maandalizi ya harusi
kwa kuandaa vikao vya wiki tatu, wiki ya nne
inakuwa harusi .
***
Baada ya upelelezi wa kesi ya Hans ya
kupanga njama za kifo cha mkewe na
mwanaye kukamilika , ilisomwa hukumu katika
mahakama kuu . Siku hiyo walijaa watu
mahakamani kutaka kusikiliza nini
kitakachoamuliwa juu ya tuhuma za Hans
kumuua mkewe .
Baada ya jaji kukaa kwenye kiti chake na watu
wote kukaa chini, alitulia kupanga karatasi
zake vizuri kisha alikohoa kidogo kuwafanya
watu wote wakae tayari kumsikiliza wakiwemo
Mage , mama yake shoga yake Brenda , familia
nzima ya Hans pia alikuwepo mama Colin, Colin
na mchumba wake Cecy .
Watu wote walitulia kumsikiliza jaji huku mioyo
ikiwadunda wakiomba itokee muujiza
utakaobadili damu kuwa maji meupe . Kwa sauti
yenye kusikika alisema:
“Nina imani wote mliopo hapa mnajua tupo
hapa kwa sababu gani, leo ndiyo siku
tunayohitimisha kesi inayomkabili Hans
Simgao ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji
iliyochukua takribani mwezi mzima na leo
ndiyo siku ya hukumu.
“Kama kawaida kesi hii ilianza kusikilizwa
mahakama ya hakimu mkazi ambayo haikuwa
na uwezo wa kuhukumu na kuamuliwa kuletwa
huku mahakama kuu kwenye uwezo wa
kusikiliza na kutoa hukumu ya kesi yoyote
nzito kama hii.
“Baada ya hukumu hii, kama mtuhumiwa
hataridhika, bado ana nafasi ya kwenda mbele
zaidi kwenye mahakama ya rufaa.
“Baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote za
mashtaka na utetezi na mahakama kuridhika
utetezi wa pande zote.
“Kutokana na maelezo upande mashtaka
unaosema kuwa mtuhumiwa aliwatuma watu
kumuua mkewe ili arudiane na mpenzi wake
wa zamani ambaye wakati huo alikuwa kwenye
maandalizi ya kuolewa na mwanaume
mwingine, baada ya mashahidi wote
waliopanda kizimbani akiwemo mchumba wa
marehemu kutoa ushahidi wao ambao
ulifanyiwa kazi na hatimaye kujiridhisha na
ushahidi upande wa mashtaka ambao unamtia
hatiani moja kwa moja mtuhumiwa, kwa hiyo
mahakana inamuhukumu Hans Simgao kifungo
cha maisha gerezani na kazi ngumu .
“Narudia tena kusema kuwa kama
hamjaridhika na hukumu hii mna nafasi ya
kukata rufaa mahakama ya rufaa ,” jaji
alimaliza kusoma hukumu yake.
Jaji baada ya kutoa hukumu ile iliamsha vilio
mahakamani huku mama mzazi na Mage
akianguka chini na kupoteza fahamu . Ilibidi
kundi la huduma ya kwanza lifanye kazi yake
ya ziada kutoa huduma ya kwanza kutokana na
watu wengi walipoteza fahamu baada ya
hukumu nzito iliyompoteza Hans uraiani .
Baba yake hakukubaliana na hukumu ile na
kuapa kukata rufaa kuhakikisha mwanaye
anaachiwa huku kwa vile makosa yalionekana
ya kutengeneza lakini aliamini mwanaye
hawezi kumuua mkewe kwa ajili ya
mwanamke. Wakili aliyewekwa kutetea kesi ile
aliomba nakala ya hukumu ili waweze kukata
rufaa.
***
Mage alizinduka na kujikuta amelala kwenye
kitanda cha hospitali akiongezewa maji,
pembeni alikuwa mama yake na shoga yake
Brenda. Alipowaona aliangua kilio upya huku
akisema:
“Mama mkosi gani nimekosa Bara na Pwani ,
hivi nitaweka wapi uso wangu mbele ya jamii
wakijua mimi ndiye niliyesababisha kifo cha
mke wa Hans huku wengine wakiniona mimi
ndiye sababu ya Hans kufungwa maisha .”
“Mage aliyoyafanya Hans hukumtuma , kafanya
kwa matakwa yake siamini kama
angekushirikisha ungekubalia afanye unyama
kama ule. Ni heri angempa talaka kuliko
alichokifanya ,” alisema Brenda .
“Brenda naamini nuksi ndiyo nyota yangu,
haiwezekani Hans afungwe maisha Colin naye
awe na mpenzi . Nina imani sina faida ya
kuendelea kuishi. ”
“Mage unataka kufanya nini ?” Brenda
alishtuka.
“Mwanangu hayo ni mawazo gani, Hans
kufungwa si mwisho wa maisha bado una
nafasi ya kuitafuta furaha,” mama yake alimtia
moyo .
“Sasa mama hiyo furaha nitaipata wapi ikiwa
hata niliyemweka kama ‘ spare tyre’ ana
mwanamke mwingine ambaye ni mzuri kuliko
mimi.”
“Mage yote umeyataka mwenyewe
ungenisikiliza sasa hivi ungekuwa kwa
mumeo .”
“Mama sikubali nitalipigania penzi la Colin kwa
gharama yoyote.”
“Sasa Mage unataka kuchanganyikiwa, juzi tu
Colin kamtangaza mchumba wake mbele za
watu tena mtu maarufu , utaanzia wapi ?”
Brenda alimuuliza.
“Kama mnataka niendelee kuishi naomba hili
ninalotaka kuamua mniachie mimi, zaidi ya
hapo mtaokota mzoga wangu,” Mage alitoa
vitisho.
“Lakini Mage wanaume wameisha ? Mbona
kuna wavulana wazuri kuliko huyo Colin na
Hans?” Brenda alimuuliza.
“Ni kweli wapo wanaume wazuri lakini si kila
mbegu humea kwenye udongo wowote.
Mapenzi yangu kwa Hans na Colin ni kama
mtende kwenye jangwa , si rahisi mti mwingine
kumea sehemu ile, basi ndivyo mapenzi ya
Hans na Colin walikuwa kama mapacha ndani
ya moyo wangu .”
“Basi ndivyo hivyo mtaka pupa hadiriki kula
tamu. ”
“Jamani nimewaeleza naomba mniache ni
uamuzi wangu mtu atakayeingilia uamuzi
wangu ajue ndiye atakayehusika na kifo
changu. ”
“Mmh ! Fanya mchezo utakwenda kufunga ndoa
na Hans gerezani ,” mama Mage alitoa taadhali
kwa mwanaye aliyetaka kuingilia mapenzi ya
watu.
***
Kufungwa kwa Hans kuliongeza umakini kwa
Cecy kuhakikisha kila kona aliyokuwepo Colin
na yeye yupo huku moyo wake ukimpa
tahadhari ya yeye kuwa mbali na Colin lazima
kuna kitu kitatendeka. Wazo lake lilikuwa
kuachana na kazi ya kufanya maonesho ya
mavazi ili kumlinda mumewe na Mage
msichana aliyebakia kama changu ambaye
anaweza kuvamia mume wa mtu bila aibu .
Baada ya kutoka gym wakati wa kurudi
nyumbani, Cecy alionekana mtu mwenye
mawazo mengi kitu kilichomfanya apoteze
uchangamfu wake wa kawaida .
Je nini kiliendelea , fuatilia wiki ijayo.
 
Back
Top Bottom