Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

bucho wacha fujo zako bana
Ukiitoa niambie aise nije fasta maana aise ni nzuri balaa
 
Last edited by a moderator:
Wakili wa moyo 43


ILIPOISHIA:


Colin alipewa kiti ili amsubiri Cecy aliyekwenda ndani kubadili nguo, alitoka amejifunga upande wa khanga na kutoka kuelekea bafuni kuoga. SASA ENDELEA…

Colin alimsindikiza kwa macho baada ya kupata nafasi ya kuliona umbile la Cecy katika vazi la khanga,rangi adimu

isiyochanganywa madawa ya ngozi. Aliamini chaguo la kwanza la mama yake lilikuwa sahihi,alijua ni wakati wa mama yake kuamini chaguo la pili halikuwa sahihi

bali tamaa ya macho ndiyo iliyompoteza. Cecy baada ya kumaliza kuoga alirudi ndani na kubadili nguo kwa kujipamba kwa vazi la kitenge lililompendeza, alionekanamwanamke wa Kiafrika hasa.

Alisimama mbele ya Colin na kutabasamu. “Colin tunaweza kwenda.” “Duh!” Colin alisema akiwa haamini.

“Ndiye mimi Cecy,mwafrika asilimia mia moja ninayejivunia rangi yangu nyeusi.” “Basi mama inatosha,” Colin alisema huku akinyanyuka na kumshika mkono. “Mama tunaomba tukukimbie,” Colin alimuaga mama Cecy.

“Haya baba,Mungu awatangulie mfike salama.” “Amina.” Walishikana mikono na kutoka nje kuelekea kwenye gari,mama Cecy aliwasindikiza kwa macho na kunyanyua mikono juu na kurudi

kuomba dua yake ya Colin kumuoa mwanaye ili roho itulie. Hakuteremsha jicho mpaka gari lilipopotea machoni mwake. Ndani ya gari,Cecy moyo wake ulikuwa na furaha nusu kwa vile aliamini lazima Colin atumie nguvu nyingi kupigania penzi lao

bila hivyo hakuna mapenzi kwa vile mama yake alishajenga uadui mapema. Alionekana mtu mwenye mawazo mengi kitu kilichomfanya Colin amshtue. “Vipi mpenzi?”

“Colin bado moyo wangu una wasiwasi.” “Wa nini?” “Jinsi mama yako atakavyonipokea.” “Ondoa wasi kila kitu niachie mimi.”

Colin alisimamisha gari mbele ya geti na kupiga honi,mlango ulifunguliwa na kuliingiza gari ndani. Alizunguka upande wa pili

na kumfungulia Cecy na kumshika mkono kuteremka kwenye gari kwa heshima kisha alielekea naye ndani. Walitembea taratibu kama mtu na mkewe, angetokea mtu na kuwaona angejua ni wapenzi wa muda mrefu wanaopendana sana.

Walipofika mlango wa kuingia sebuleni,Colin alisema kwa sauti ya unyenyekevu: “Karibu malkia wangu.” “Asante mfalme wangu,” Cecy naye alijibu kwa unyenyekevu.

Sauti zile zilimfanya mama Colin aliyekuwa ameinama akisoma biblia kunyanyua macho na kumuona mwanaye na msichana mrembo

ambaye aliamini ndiye aliyeondoka muda mfupi uliopita. “Shikamoo ma’mkwe!” Cecy alimsalimia mama Colin kwa unyenyekevu huku akipiga magoti ya heshima. “Marahaba mama,karibu.”

“Asante,” Cecy alijibu huku akinyanyuka na kumfuata Colin aliyekuwa amesimama pembeni yake na kumshika mkono.

Colin alimuongoza Cecy mpaka kwenye sofa na kumkaribisha tena: “Karibu.” “Asante,” Cecy alijibu huku akikaa.

“Unatumia kinywaji gani?” “Chochote utakachonichagulia mfalme wangu.” “Colin si ungemwita dada wa kazi awahudumie,” mama Colin aliingilia kati. “Hapana huyu ni mgeni wangu,kila kitu chake nitafanya mimi.”

“Mmh! Haya.” Muda wote mama Colin alikuwa bado hajaipata picha ya yule msichana mrembo, alituliza macho kwa wizi ndipo alipogundua kuwa ni

Cecy,msichana muuza ndizi. Alikunja uso kwa hasira na kuamini kabisa lile si chaguo sahihi kwa mwanaye bali ni papara ya kuachwa na Mage.

Alinyanyuka na kuelekea chumbani kwake, alipotoka eneo la sebule alimwita Colin. “Colin.” “Naam mama.” “Njoo mara moja.”

“Nakuja,” Colin alisema huku akimuwekea juisi Cecy kwenye glasi na kunywa kidogo kisha kumkaribisha. “Karibu malkia wangu.” “Asante mfalme wangu.”

“Samahani namsikiliza mama mara moja.” “Nenda mpenzi kamsikilize mama.”

Colin alimfuata mama yake kwenye korido alipokuwa amesimama,alimsogelea karibu na kumuuliza: “Unasemaje maana ulivyotoka kama kuna kitu?” “Yule nani?” aliuliza huku akinyoosha kidole sebuleni.

“Mke wangu mtarajiwa,chaguo sahihi la moyo wangu.” “Colin…Colin una tatizo gani? Wanawake wote wameisha mpaka umfuate huyu maskini mbumbumbu asiyejua kitu. Mwanangu tuna fedha,

tunaweza kumuoa msichana yeyote mzuri mwenye elimu yake kwa fedha yoyote na popote duniani.” “Mama naomba kwa hili usizungumze chochote uniache kabisa,umetafuta mwanamke ambaye leo katuvua nguo kwa vile ulimfuata

msomi mwenye uwezo.” “Lakini suala la Mage bado tulikuwa tunalishughulikia,lilikuwa halijafika mwisho. Hivi leo Mage aje na mama yake wakikute

kinyago hiki kuna ndoa kweli?” “Penzi langu na Mage liliishia Bagamoyo.” “Lakini bado wazazi hatujabariki uamuzi wenu.”

“Mama si uamuzi wetu bali wa Mage, kasema ukweli ana mtu anayempenda tatizo lipo wapi?” “Basi Cecy si chaguo langu.” “Mama mimi ni mwanao,umenizaa na kunilea na kunifundisha kila kitu,lakini suala la kumpenda mtu ni matakwa ya moyo wangu.

Nilikukubalia kwa Mage kwa vile ni mzazi wangu zoezi lako lilifeli sasa huu ni muda wangu.” “Lakini siyo kwa Cecy.” “Mama Cecy ni zaidi ya mwanamke ndiye mwenye nafasi moyoni mwangu zaidi ya hapo sitakuwa na mwanamke mwingine.”

“Colin,Cecy umemjulia wapi kama siyo mimi?” “Basi hili ndilo chaguo lako lililokuwa sahihi hujui tu.”

“Nilikuwa namtania tu lakini si kwa ajili ya kuwa mkeo.” “Basi imekuwa hivyo bila kutegemea.” “Basi mimi simtaki.”

“Kwa hiyo unatafuta aibu nyingine?” Colin alisema huku akifungua simu upande wa picha na kumuonesha mama yake.

Itaendelea
 
Mizambwa amerudi kwahiyo namuachia hili gurudumu aendelee kulisongesha . Aliniachia vifaa vyake kwa muda tu ili msiboeke.
buchooooo......asante umetufurahisha kuendeleza story...umemfuma wapi Mizambwa??alituacha solemba aisee...mwambie mizambwa akupe makabrasha uendelee kama yeye yuko buzy...
 
Last edited by a moderator:
bucho pokea hiyo :A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Last edited by a moderator:
mizambwa mbona kimya tena wakati nilisikia umerudi...??

naona kama vipi bucho endelea bhana tupate utamu......
 
Last edited by a moderator:
Watoto wa kike wana mitihani mikubwa sana hapa duniani.
 
Watoto wa kike wana mitihani mikubwa sana hapa duniani.

Kweli kabisa..hebu mwangalie Mage yaliyompata hadi sasa.mwangalie Cecy nae sijui anaelekea wapi... Na haya yapo sana tuu tumeyashuhudia yakiwapata watoto wetu jamani..eee mungu wasaidie
 
Wakili wa moyo 44



ILIPOISHIA:

“Basi mimi simtaki.” “Kwa hiyo unatafuta aibu nyingine?” Colin alisema huku akifungua simu upande wa picha na kumuonesha mama yake. SASA ENDELEA… “Umeonaunayempenda?” Aliangalia picha za Mage na kuuliza: “Hizi picha za nani?”

“Mage na mpenzi wake,” Colin alimjibu huku akimtazama usoni. “Picha hizi zimepigwa lini?” “Leo.” “Wapi?”

“Wapo Afrika ya Kusini wanakula raha katika Hoteli ya Hilton jijini Durban,sasa naomba uniache na Cecy wangu.” “Colin bado hujanieleza kitu,tafuta msichana mwingine lakini kwa Cecy sipo radhi kuingiza uchafu katika familia yangu.”

“Mama nakupenda,nakuheshimu sana, naomba kuhusu Cecy usiniingilie kabisa zaidi ya hapo nitaondoka na kukuacha na fedha zako.” “Colin mwanangu mbona umefika mbali,” mama alishtuka.

“Kwa sababu umeingilia haki ya moyo wangu,wewe ni mzazi gani usiye na huruma nimeumizwa badala ya kunihurumia bado unataka kuniongezea maumivu,” Colin alisema kwa uchungu. “Lakini kumbuka wewe ni msomi unawezaje kuoa mwanamke mbumbumbu?” “Mama mapenzi si cheo,elimu wala fedha, Cecy ni zaidi ya vyote hivyo kwangu.” “Sawa,lakini utakuja kunikumbuka na uamuzi wako hata nikifa.”

“Ni kweli mama nitakukumbuka kwa kunitafutia mchumba aliye bora kuliko Mage. Cecy ni lulu iliyokuwa imejificha kwenye matope.” “Nimekuelewa mwanangu,naomba unisamehe kwa kukukwaza.” “Nilikusamehe kabla hujatenda.” “Basi naomba ya huku yaache hukuhuku.” “Sawa mama.”

Baada ya makubaliano,Colin alirudi kwa Cecy na mama yake kwenda chumbani, alipofika alimpigia simu mama Mage kutaka kupata ukweli wa kauli ya mwanaye. Baada ya simu kuita ilipokelewa upande wa pili: “Haloo,dada vipi?”

“Mmh! Yaani bado nachanganyikiwa ulisema Mage kaenda wapi?” “Nilikuambia amekwenda kwa shoga yake.” “Wapi?’ “Aliniaga anakwenda Kibaha,” mama Mage alidanganya. “Mmh! Mbona Colin anasema katumiwa picha za Mage akiwa na mwanaume Afrika ya Kusini wakila raha kwenye Hoteli Hilton?”

“Mmh! Labda maana ametoka toka jana, dada wee hebu tuachane na Mage tufanye mambo mengine.” “Sawa dada nimekuelewa.” Baada ya kukata simu alitulia kwa muda akiwaza,alijikuta akimchukia Cecy na kuuapia moyo wake hatakuwa tayari kuona mwanaye akioa mwanamke asiye na hadhi. Alipanga kuhakikisha anauvunja uhusiano ule kwa hali na mali ili Colin aoe mwanamke mwingine mwenye elimu na kutoka familia yenye uwezo.

Alitoka chumbani na kujifanya kujichekesha kwa Cecy huku akimtania. “Jamaniii mmependezaje wapenzi!” “Asante mkwe,” alijibu Cecy kwa furaha huku Colin akiuona unafiki wa mama yake uliojificha moyoni ambao mpenzi wake hakuujua. Kwa vile mama Colin hakupenda Cecy kuwa pale,aliondoka na kwenda chumbani kwake na siri yake nzito moyoni.

JIJINIDURBAN AFRIKAKUSINI Katika ufukwe wa Hoteli ya Hilton,wapenzi wawili walikuwa wakila raha,Mage alikuwa amelala kifuani kwa Hans huku akichezea kidevu chenye ndevu chache. “Hans nikuambie kitu?” “Niambie mpenzi.”

“Ningebugi vibaya kuolewa na mrugaruga kama yule (Colin).” “Si haraka zako,nilikueleza piga ua lazima mke wangu utakuwa wewe pamoja na wazazi kunilazimisha kumuoa yule mwanamke.”

“Nilichanganyikiwa baada ya kuona umepata mtoto.” “Ilikuwa lazima iwe vile ili wasijue nimepanga nini mbeleni.” “Asante Hans kwa kuponya majeraha ya moyo wangu.” “Nami nashukuru kukubali kurudi mikononi mwangu.” “Kwa hiyo ndoa lini?”

“Tukirudi tu nyumbani mipango inaanza mara moja.” “Nitafurahije mpenzi wangu.” “Usijali nipo kwa ajili yako.”

“Basi naomba turudi nyumbani ili tukalisema hili mbele ya wazazi wetu wote.” “Hakuna tatizo nakusikiliza wewe.” “Nataka kesho jioni tuwe mbele ya wazazi wako ukiwaeleza kwa mdomo wako kuwa mimi ndiye mkeo baada ya hapo twende kwetu nikamueleze mama kuwa wewe ndiye mume wangu.”

“Hakuna tatizo mpenzi wangu.” Walikubaliana kuondoa Afrika ya Kusini siku ya pili mchana warudi Tanzania ili kwenda mbele ya wazazi wao kuthibitisha mapenzi yao ya dhati. *** Colin na Cecy baada ya kutoka nyumbani walikwenda Bagamoyo katika Hoteli ya Malaika ambako alipanga kukaa kwa siku moja. Majira ya jioni wakiwa wamejilaza mchangani huku wakipepewa na upepo mwanana wa bahari,Colin aliyaangalia mawimbi ya bahari na mitumbwi ya wavuvi waliokuwa wakivua samaki.

Baada ya kugandisha macho baharini, alijikuta akitokwa na machozi baada ya kukumbuka sehemu kama ile ndiyo iliyotumika kuvunja uchumba wake na Mage japokuwa ilikuwa hoteli tofauti lakini ni Bagamoyo ileile. Machozi yalimdondoka bila kujua na kuangukia kwenye paji la uso la Cecy aliyekuwa amejilaza mapajani kwa mpenzi wake na kumfanya anyanyue macho kumuangalia. Alishtuka kumuona akibugujikwa machozi kitu kilichomfanya amuulize.

“Vipi mpenzi wangu mbona unalia?” “Nimekumbuka kitu ambacho kimesababisha nitokwe machozi.” “Kitu gani mpenzi wangu?” Cecy alimuuliza huku akimfuta machozi kwa upande wa mtandio aliojifunga. “Ni juzi tu maeneo hayahaa yaliujerudi moyo wangu lakini,leo hii maeneo yaleyale yameujenga upya na kujiona kama nimezaliwa upya.” “Kwa nini unasema hivyo?” “Juzi tulikuja huku na Mage kuvunja uchumba wetu ambao ulinishtua sana na kuumiza moyo wangu japokuwa haikuwa hoteli hii,lakini ni hukuhuku Bagamoyo. Itaendelea
 
Sema mkuu Bucho kuna kitu mmeruka kati ya sehem ya 41 na 42
 
bucho oooooooooo!!!!!!!!!?????????????
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom