Kutokana na watu wengi kuwa na kiu na hadithi hii, leo tena nimeamua kuileta mapema kabla hata kufika Jumatatu, nadhani umeburudika vya kutosha, ni miye mtumishi wenu Mommadou Keita.
HISIA ZANGU-16
ILIPOISHIA...
Nakuhakikishia, akasema Pam.
Lilian akajivuta kwa Pam, akalala kifuani mwake. Penzi jipya lilifumuka kwa wawili hao.
Waliamka kwa pamoja na kuelekea bafuni kuoga kisha wakavaa na kuondoka. Pam alimrudisha Lilian mpaka chuoni.
Lilian alikuwa na jambo moja tu kichwani mwake; angemwambia nini Edo kuhusu usichana wake? Hakuwa na jibu!
Huo ndiyo mtihani mgumu uliokuwa mbele yake.
SASA ENDELEA...
ULIKUWA zaidi ya mtihani. Siku zote alimwambia alikuwa na usichana wake, jambalo lilikuwa la kweli tupu. Ahadi yao ilikuwa ni kukutana faragha mara baada ya kufunga ndoa.
Ni msimamo ambao yeye ndiye aliyeushikilia zaidi. Kilichomuuma ni kuja kuutoa usichana wake kirahisi kiasi kile. Alijua wazi kuwa, hakuwa na mapenzi hata kidogo na Pam, ni fedha ndizo zilizomchanganya.
Moyoni alikuwa na majuto makubwa, tamaa ya fedha ndiyo mwanzo wa matatizo yote hayo. Hata hivyo moyoni alikiri kuwa, hakuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo.
Isingekuwa rahisi awe na Pam, ampe fedha zake bila chochote kuendelea. Hilo lingekuwa jambo la ajabu sana.
Sina namna, tayari nimeshaingia kwenye mambo ya kikubwa, siamini kama imekuwa rahisi kiasi hiki, alijisemea wakati akitembea taratibu kuelekea hosteli.
Akiwa anatembea, simu yake ikaita, alipotupa macho yake kwenye kioo cha simu, akakutana na namba za mpenzi wake, Edo. Mara moja akapokea.
Haloo!
Haloo mpenzi wangu, habari za huko?
Salama. Wewe je?
Mimi ni mzima, nashukuru naendelea vyema na masomo. Nimekupigia simu hii kwa ajili ya mambo mawili muhimu.
Mambo gani?
Kwanza kukuomba msamaha.
Msamaha?
Ndiyo mpenzi, kukuomba wewe msamaha.
Kwa kosa gani tena mpenzi? akauliza Lilian akionekana kuwa na mashaka kidogo.
Alijaribu kuwaza kuhusu msamaha aliosema, akashindwa kuelewa kabisa. Kwa namna ilivyokuwa, yeye ndiye aliyetakiwa kuomba msamaha kutokana na kuvunja ahadi yao.
Kichwa kikamuuma, akawaza kuwa huenda Edo alikuwa akizungumza mambo kinyume. Kwamba huenda alikuwa akimaanisha yeye.
Hata kama alikuwa akimaanisha mimi, itawezekanaje basi hata ajue? Yeye yupo Malaysia, mimi Tanzania, wapi na wapi? Hili ni jambo gumu kutokea bwana, akazidi kuwaza.
Lilian, Edo akaita.
Nakusikia Edo.
Nisamehe mpenzi.
Baby niambie bwana.
Jana ilikuwa siku yako ya kuzaliwa!
Najua Edo.
Kosa langu ni kutokupongeza mapema tangu jana, lakini nina sababu za msingi ingawa sipendi kukueleza, ila naomba ufahamu kuwa ninajua umuhimu wa siku yako hiyo na thamani yangu kwako kama mwanaume wako. Happy birthday Lilian, akasema Edo kwa msisitizo sana.
Thanks. Usijali, najua huko utakuwa na majukumu mengi, kwa hiyo kawaida tu, isikupe shida sana mpenzi wangu, akasema Lilian.
Nashukuru.
Ila kuna jambo kubwa sana nitakufanyia siku chache zijazo, akasema Edo.
Mh! Bwana unanitisha sasa. Ni jambo gani hilo?
Surprise, siwezi kusema chochote kwa sasa, muda ukifika utajua tu. Vuta subira mpenzi wangu, akasema Edo.
Poa mpenzi.
Wakakata simu zao.
Lilian wakati akizungumza na simu alikuwa amesimama, hivyo alivyokata tu simu akaanza kutembea tena. Chumbani kwao aliwakuta Lucy, Latifa na Leila wakiwa bado wamejilaza. Hata hivyo hawakuwa kwenye usingizi.
Mama lao nakuona! akasema Lucy kwa sauti iliyoonyesha alikuwa akijua kilichoendelea.
Mambo zenu, akasalimia.
Poa, pole mwaya! akadakia Latifa.
Pole ya nini tena? Lilian akauliza akiwa ameukunja uso kidogo.
Naona mwenzetu hujarudi kabisa jana! akasema Latifa.
Sasa ndiyo unipe pole?
Wote wakacheka.
Ungepewa nini sasa, maana wenzako wote kweli tuna mambo hayo, lakini hadi asubuhi?
Mh! Kweli mtu hawezi kuona tatizo lake, Latifa wewe hukulala na Big siku ile ukarudi kesho yake mchana? Bora hata mimi nimerudi asubuhi, akasema Lilian kwa kujiamini.
Wakacheka tena.
Lilian akaamua kuingia bafuni, akaoga haraka kisha akatoka na kujitupa kitandani.
Sitaki usumbufu leo, hata darasani sitakwenda, nahitaji kupumzika siku nzima ya leo, akasema Lilian.
Sawa mama, umesomeka! Lucy ndiye aliyejibu.
Lilian akavuta shuka, kama vile alikuwa amelala usiku. Akajitahidi kuvuta usingizi.
***
WIKI MOJA BAADAYE
Lilian hakuamini macho yake, aliendelea kukaza macho yake kwenye kioo cha simu yake ili kupata uhakika wa alichokuwa akikiona, lakini bado kiliendelea kuwa vilevile.
Namba iliyokuwa ikimpigia ndiyo iliyomchanganya Lilian. Namba ya mpenzi wake Edo ya nchini Tanzania.
Mh! Inamaana Edo yupo Bongo? akajiuliza.
Alijiuliza sana, lakini baadaye akagundua maswali yake yasingekuwa na maana kama asingepokea simu na kuujua ukweli. Mara moja akabonyeza kitufe cha kupokea.
Haloo, akaita Lilian.
Surprise! Surprise! akasema Edo.
Baby really? akauliza Lilian.
Yeah baby, nipo jijini Dar es Salaam, akasema Edo kwa furaha.
Uko wapi nikufuate mpenzi wangu?
Ha! Ha! Ha! Huo ni wimbo wa Ray C! Sikia nipo hapa chuoni.
Lilian alihisi kuzimia!
Itaendelea wiki ijayo.
ILIPOISHIA...
Nakuhakikishia, akasema Pam.
Lilian akajivuta kwa Pam, akalala kifuani mwake. Penzi jipya lilifumuka kwa wawili hao.
Waliamka kwa pamoja na kuelekea bafuni kuoga kisha wakavaa na kuondoka. Pam alimrudisha Lilian mpaka chuoni.
Lilian alikuwa na jambo moja tu kichwani mwake; angemwambia nini Edo kuhusu usichana wake? Hakuwa na jibu!
Huo ndiyo mtihani mgumu uliokuwa mbele yake.
SASA ENDELEA...
ULIKUWA zaidi ya mtihani. Siku zote alimwambia alikuwa na usichana wake, jambalo lilikuwa la kweli tupu. Ahadi yao ilikuwa ni kukutana faragha mara baada ya kufunga ndoa.
Ni msimamo ambao yeye ndiye aliyeushikilia zaidi. Kilichomuuma ni kuja kuutoa usichana wake kirahisi kiasi kile. Alijua wazi kuwa, hakuwa na mapenzi hata kidogo na Pam, ni fedha ndizo zilizomchanganya.
Moyoni alikuwa na majuto makubwa, tamaa ya fedha ndiyo mwanzo wa matatizo yote hayo. Hata hivyo moyoni alikiri kuwa, hakuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo.
Isingekuwa rahisi awe na Pam, ampe fedha zake bila chochote kuendelea. Hilo lingekuwa jambo la ajabu sana.
Sina namna, tayari nimeshaingia kwenye mambo ya kikubwa, siamini kama imekuwa rahisi kiasi hiki, alijisemea wakati akitembea taratibu kuelekea hosteli.
Akiwa anatembea, simu yake ikaita, alipotupa macho yake kwenye kioo cha simu, akakutana na namba za mpenzi wake, Edo. Mara moja akapokea.
Haloo!
Haloo mpenzi wangu, habari za huko?
Salama. Wewe je?
Mimi ni mzima, nashukuru naendelea vyema na masomo. Nimekupigia simu hii kwa ajili ya mambo mawili muhimu.
Mambo gani?
Kwanza kukuomba msamaha.
Msamaha?
Ndiyo mpenzi, kukuomba wewe msamaha.
Kwa kosa gani tena mpenzi? akauliza Lilian akionekana kuwa na mashaka kidogo.
Alijaribu kuwaza kuhusu msamaha aliosema, akashindwa kuelewa kabisa. Kwa namna ilivyokuwa, yeye ndiye aliyetakiwa kuomba msamaha kutokana na kuvunja ahadi yao.
Kichwa kikamuuma, akawaza kuwa huenda Edo alikuwa akizungumza mambo kinyume. Kwamba huenda alikuwa akimaanisha yeye.
Hata kama alikuwa akimaanisha mimi, itawezekanaje basi hata ajue? Yeye yupo Malaysia, mimi Tanzania, wapi na wapi? Hili ni jambo gumu kutokea bwana, akazidi kuwaza.
Lilian, Edo akaita.
Nakusikia Edo.
Nisamehe mpenzi.
Baby niambie bwana.
Jana ilikuwa siku yako ya kuzaliwa!
Najua Edo.
Kosa langu ni kutokupongeza mapema tangu jana, lakini nina sababu za msingi ingawa sipendi kukueleza, ila naomba ufahamu kuwa ninajua umuhimu wa siku yako hiyo na thamani yangu kwako kama mwanaume wako. Happy birthday Lilian, akasema Edo kwa msisitizo sana.
Thanks. Usijali, najua huko utakuwa na majukumu mengi, kwa hiyo kawaida tu, isikupe shida sana mpenzi wangu, akasema Lilian.
Nashukuru.
Ila kuna jambo kubwa sana nitakufanyia siku chache zijazo, akasema Edo.
Mh! Bwana unanitisha sasa. Ni jambo gani hilo?
Surprise, siwezi kusema chochote kwa sasa, muda ukifika utajua tu. Vuta subira mpenzi wangu, akasema Edo.
Poa mpenzi.
Wakakata simu zao.
Lilian wakati akizungumza na simu alikuwa amesimama, hivyo alivyokata tu simu akaanza kutembea tena. Chumbani kwao aliwakuta Lucy, Latifa na Leila wakiwa bado wamejilaza. Hata hivyo hawakuwa kwenye usingizi.
Mama lao nakuona! akasema Lucy kwa sauti iliyoonyesha alikuwa akijua kilichoendelea.
Mambo zenu, akasalimia.
Poa, pole mwaya! akadakia Latifa.
Pole ya nini tena? Lilian akauliza akiwa ameukunja uso kidogo.
Naona mwenzetu hujarudi kabisa jana! akasema Latifa.
Sasa ndiyo unipe pole?
Wote wakacheka.
Ungepewa nini sasa, maana wenzako wote kweli tuna mambo hayo, lakini hadi asubuhi?
Mh! Kweli mtu hawezi kuona tatizo lake, Latifa wewe hukulala na Big siku ile ukarudi kesho yake mchana? Bora hata mimi nimerudi asubuhi, akasema Lilian kwa kujiamini.
Wakacheka tena.
Lilian akaamua kuingia bafuni, akaoga haraka kisha akatoka na kujitupa kitandani.
Sitaki usumbufu leo, hata darasani sitakwenda, nahitaji kupumzika siku nzima ya leo, akasema Lilian.
Sawa mama, umesomeka! Lucy ndiye aliyejibu.
Lilian akavuta shuka, kama vile alikuwa amelala usiku. Akajitahidi kuvuta usingizi.
***
WIKI MOJA BAADAYE
Lilian hakuamini macho yake, aliendelea kukaza macho yake kwenye kioo cha simu yake ili kupata uhakika wa alichokuwa akikiona, lakini bado kiliendelea kuwa vilevile.
Namba iliyokuwa ikimpigia ndiyo iliyomchanganya Lilian. Namba ya mpenzi wake Edo ya nchini Tanzania.
Mh! Inamaana Edo yupo Bongo? akajiuliza.
Alijiuliza sana, lakini baadaye akagundua maswali yake yasingekuwa na maana kama asingepokea simu na kuujua ukweli. Mara moja akabonyeza kitufe cha kupokea.
Haloo, akaita Lilian.
Surprise! Surprise! akasema Edo.
Baby really? akauliza Lilian.
Yeah baby, nipo jijini Dar es Salaam, akasema Edo kwa furaha.
Uko wapi nikufuate mpenzi wangu?
Ha! Ha! Ha! Huo ni wimbo wa Ray C! Sikia nipo hapa chuoni.
Lilian alihisi kuzimia!