Hadithi tamu: Hisia zangu

Hadithi tamu: Hisia zangu

Sasa nimeamini kweli swaumu kali... daaa! nisameheni waungwana.
 
mi lilian ananiboa ujueeeeee..ahaaaaa...momma ebu mfanye edo alud bwana achukue chake asepe......
 
Liian ana mtihani mzito;

PAM na EDDO atachagua nani??

Je EDDO akijua kuwa alikuwa anaruka viwanja na PAM, EDDO atafanya nini?

Je, kama akimmwaga PAM, reaction gani atakuja nayo PAM kwa Lilian??
 
Ilipoishia ya 11 na ilipoanzia ya 12 tofauti kabisa
 
Liian ana mtihani mzito;

PAM na EDDO atachagua nani??

Je EDDO akijua kuwa alikuwa anaruka viwanja na PAM, EDDO atafanya nini?

Je, kama akimmwaga PAM, reaction gani atakuja nayo PAM kwa Lilian??

Mzee hadi humu upo
 
Liian ana mtihani mzito;

PAM na EDDO atachagua nani??

Je EDDO akijua kuwa alikuwa anaruka viwanja na PAM, EDDO atafanya nini?

Je, kama akimmwaga PAM, reaction gani atakuja nayo PAM kwa Lilian??

Wapi Wakili Wa moyo
 
Mmmmh huyu mommsdou mbona kauchuna sana? Au anaumwa? Mmmmh ngoja nimwite mommadou keitaaaaaaaaaaaaaa
 
ILIPOISHIA...14

Bado alikuwa hajaelewa, ni nani aliyeteka mawasiliano yake na kwa nini aliamua kumgombanisha na mwanaume wa maisha yake. Jambo hilo lilisababisha usiku huo uwe mgumu, mzito na mrefu kuliko kawaida!
Alikesha akiwaza!
Usingizi angeupata wapi?
“Hakuna marefu yasiyo na ncha,” akajisemea.
Angalau maneno hayo yalimtia faraja, kidogo akajihisi mwepesi na macho yake sasa yakaanza kumlemea kwa uzito. Bila uamuzi wake, aliyafumba mara, usingizi mzito ukamchukua!
SASA ENDELEA...

ALIAMKA mapema sana. Saa 11 alfajiri Lilian alikuwa macho. Ilikuwa vigumu sana kuufaidi usingizi wa asubuhi. Hakuwa na kipindi cha asubuhi, zaidi alitakiwa kuingia darasani saa nane mchana, hivyo alikuwa na uhuru wa kuendelea kulala.
Kichwa chake kiliendelea kuwaza juu ya mtu aliyeteka mawasiliano yake. Ni nani mtu huyo na kwa nini afanye hivyo? Alijiuliza bila kupata majibu yakinifu.
Aliamini kwa vyovyote vile, aliyehusika kumfanyia kitendo kile alikuwa kati ya rafiki zake anaolala nao bweni moja. Ndivyo ukweli wenyewe ulivyokuwa.
Aliwafikiria rafiki zake wote na tabia zao, hakujua ni nani angekuwa amefanya tukio hilo. Mawazo yake yalimpeleka kwa Lucy lakini baadaye akayaondoa.
Pamoja na yote alikuwa na amani kidogo moyoni mwake kuona kuwa, sasa mpenzi wake alielewa kuwa hakuwa amemfanyia kitu chochote kibaya.
Changamoto ilikuwa moja tu; uhusiano mpya aliouanzisha na Pam. Jambo hilo pekee ndilo lililousumbua ubongo wake.
***
Pam alipanda ngazi kama anakimbizwa! Zilikuwa ngazi fupi katika Hoteli ya Tarahan iliyokuwa Mikocheni katika eneo lililotulia mno.
Alifika moja kwa moja Mapokezi ambapo alipokelewa na tabasamu mwanana la msichana mrembo sana.
“Mambo vipi?” Pam akamsalimia.
“Poa, shikamoo.”
“Acha hizo mtoto mzuri, shikamoo siyo muhimu sana...sema mambo poa.”
Yule msichana akacheka, kisha akamjibu: “Haya poa.”
“Hayo ndiyo mambo!” akasema Pam.
“Mh! We’ baba una mambo! Niambie...naomba nikusikilize.”
“Nahitaji makazi ya muda hapa kwako. Nataka chumba kizuri, chenye hadhi ya juu kuliko vyote. Kifupi nataka chumba cha gharama kuliko vyote!
“Nina mgeni muhimu ambaye ana tukio lake leo, nataka lifanyike ndani ya chumba. Naamini inawewezekana maana wewe unajua vyumba vyote ndani ya hoteli hii,” akasema Pam akitabasamu.
Tabasamu lake lilisababisha hata yule msichana naye ashindwe kujizuia na kuachanua midomo yake akitabasamu.
“Umepata.”
“Bei gani?”
“Laki mbili ndiyo kizuri zaidi, kinachofanana na wewe kwa kila kitu.”
“Sawa. Unaweza kunipeleka?”
“Bila shaka.”
Yule msichana, akamwita mhudumu ambaye alipanda na Pam hadi ghorofa ya nne kilipokuwa chumba alichohitaji. Aliingia ndani na kukikagua.
Kilikuwa kizuri sana, chenye hadhi na ubora zaidi ya ule ambao alikuwa akiufikiria. Pam alimwangalia yule msichana aliyeongozana naye, akatabasamu...
“Panafaa kabisa,” akasema wakitoka nje ya chumba kile na kukifunga.
Aliposhuka chini alilipa kisha akamwambia: “Nasisitiza, kuna tukio muhimu sana. Kama kuna uwezekano, mnaweza kuongeza manjonjo zaidi kwenye kile chumba.”
“Hakuna shida kaka, nadhani ukirudi utafurahi zaidi. Tutajitahidi kuongeza nakshi.”
“Nitafurahi sana.”
“Unatarajia kuja saa ngapi kwa ajili ya hiyo shughuli?”
Pam akacheka kidogo, kisha akajibu: “Jioni. Sina hakika sana na muda lakini itakuwa zaidi ya saa moja usiku.”
“Karibu sana.”
“Nashukuru.”
Pam akaondoka zake.
***
Ilikuwa saa nane kasoro mchana. Lilian, Leila, Latifa na Lucy walikuwa wakitembea taratibu kuelekea kwenye kipindi. Wakiwa njiani, Lilian akaanzisha mjadala. Hakuona sababu ya kuendelea kuishi na mawazo kichwani wakati kulikuwa na uwezekano wa kudodosa ili kupata ukweli.
“Hivi ni nini kinaendelea kati yetu?” alianza kuuliza Lilian.
Wote walipigwa na butwaa.
“Unamaanisha nini?” Lucy alikuwa wa kwanza kuuliza.
“Hujui ninachomaanisha? Huu ni urafiki gani sasa jamani? Kwa nini tunatibuliana mambo?” akasema tena Lilian.
Ilikuwa vigumu sana yeyote kati yao kuelewa alichokuwa akimaanisha. Wote walionekana kama wanasikia habari mpya kabisa kutoka kwa Lilian.
“Kwani kuna nini? Si useme ukweli? Hebu kuwa wazi tuelewe unachomaanisha,” akasema Leila.
“Anayejua alichofanya anajijua na anatakiwa kufahamu tu kuwa nimeshagundua mchezo wake ila mambo hayaendi hivyo kwa sisi marafiki, hayo ni mambo ya kinafiki!” akasema Lilian akionekana kukasirika sana.
Muda huohuo simu yake ikaita, alipotazama kwenye kioo, akakutana na jina la Pam. Akasimama na kuwaacha wenzake waendelee mbele kidogo ili apate kumsikiliza.
Walipofika mbali kidogo, akabonyeza kitufe cha kupokea, kisha akaanza kuzungumza: “Haloo.”
“Niambie mrembo wangu.”
“Poa.”
“Nahitaji kutoka na wewe leo jioni, ni muhimu sana mpenzi wangu.”
“Utanifuata?” akauliza Lilian kwa haraka.
“Haina shida, saa moja kamili usiku nitakuwa hapo chuoni au kama vipi uchukue taksi nikueleze pa kunikuta?”
“Hapana bwana...wewe njoo unichukue tu!”
“Hilo limepita.”
“Poa Pam, ngoja mimi niingie kwenye kipindi.”
“Masomo mema mama.”
“Ahsante.”
***
Pam alifungua mlango wa gari, Lilian naye akafanya hivyo. Wakashuka na kuibamiza kwa nguvu. Wakatembea wakiwa wameshikana mikono hadi Mapokezi ambapo Pam alichukua funguo.
Waliamua kutumia ngazi kupanda hadi ghorofa ya nne kilipokuwa chumba alichochukua Pam. Pam akafungua mlango. Lilian alishangazwa sana na namna chumba kile kilivyokuwa kimepambwa vizuri na kuvutia.
Zaidi alishangaa kuona kadi zikiwa zimezagaa kitandani. Pam akasimama nyuma yake kisha akamshika kiuno, akasema: “Happy Birthday Lilian, Happy Birthday to you!”
Lilian akashtuka sana!
“Siamini Pam mpenzi wangu, leo ni birthday yangu?”
“Ndiyo mpenzi wangu. Hongera sana!” akasema tena Pam.
“Ahsante kwa kunijali. Yaani nilikuwa nimeshasahau kabisa,” akasema Lilian huku akimwaga machozi.
Yalikuwa machozi ya furaha.
Itaendelea wiki ijayo.
 
mara hii ashamsahau mzee wa malasya au Edo nae amecrash na ile ndege ilodunguliwa kule ukrane
 
Hisia Zangu-15
Pam alifungua mlango wa gari, Lilian naye akafanya hivyo. Wakashuka na kuibamiza kwa nguvu. Wakatembea wakiwa wameshikana mikono hadi Mapokezi ambapo Pam alichukua funguo.
Waliamua kutumia ngazi kupanda hadi ghorofa ya nne kilipokuwa chumba alichochukua Pam. Pam akafungua mlango. Lilian alishangazwa sana na namna chumba kile kilivyokuwa kimepambwa vizuri na kuvutia.
Zaidi alishangaa kuona kadi zikiwa zimezagaa kitandani. Pam akasimama nyuma yake kisha akamshika kiuno, akasema: “Happy Birthday Lilian, Happy Birthday to you!”
Lilian akashtuka sana!
“Siamini Pam mpenzi wangu, leo ni birthday yangu?”
“Ndiyo mpenzi wangu. Hongera sana!” akasema tena Pam.
“Ahsante kwa kunijali. Yaani nilikuwa nimeshasahau kabisa,” akasema Lilian huku akimwaga machozi.
Yalikuwa machozi ya furaha.
MARA zote huwa hakumbuki siku yake ya kuzaliwa. Aliyekuwa akimkumbusha kuhusu siku yake ya kuzaliwa alikuwa ni mpenzi wake Edo na wakati mwingine rafiki zake akina L (Latifa, Lucy na Leila) ambao humnunulia kadi na kumwimbia nyimbo za Birthday.
Siku hiyo Edo hakumkumbuka, wala hakumwambia kuwa ni siku yake ya kuzaliwa. Kitendo cha Pam kuonyesha kuikariri haraka ingawa penzi lao lilikuwa bado changa kulimchanganya sana Lilian na kuzidisha mapenzi kwa mwanaume huyo.
Lilian alimwangalia sana Pam kisha akamsogelea na kumbusu tena. Mashavu yake yalikuwa yamejaa machozi. Hakuamini macho yake.
“Inanipasa nifanye hivi kwako, maana nakupenda kwa moyo wangu wote. Kwa nini unashangaa baby, mimi ndiye mwanaume wako,” akasema Pam.
“Unaniahidi Pam?”
“Ndiyo.”
“Nimefurahi sana kusikia hivyo.”
Kilikuwa chumba nadhifu sana, kisafi chenye nakshi za kila aina ndani. Macho yao kwa pamoja yalifurahishwa na kila kilichokuwa ndani ya chumba kile.
Ingawa walikuwa wawili tu, Pam alikuwa ametayarisha shampeni. Alichukua chupa kisha akaifungua kwa ustadi, iliporuka ilikwenda kumlowanisha Lilian alipokuwa amesimama.
Wakamimiana kisha wakaanza kunywa kwa furaha. Baada ya kunywa glasi moja moja, kwa kuwa haikuwa yenye kilevi, Pam alifungua mvinyo mwekundu ambao ulikuwa na kilevi kisha akajaza glasi mbili.
Akampatia Lilian moja na moja akaishika yeye. Wote kwa pamoja wakagonganisha glasi zao na kuanza kunywa kwa furaha. Walikunywa taratibu, hadi walipoanza kuchangamka!
“Baby sasa inabidi tupate chakula, utapenda kula nini?” Pam akamwuliza Lilian.
“Utakachokula wewe, nami nitakula hichohicho.”
“Sawa, natamani sana tule samaki, wewe unaonaje?”
“Samaki ni sawa, samaki gani lakini?”
“Unapenda wa ziwani au baharini?”
“Ziwani ni wa watamu zaidi, itakuwa vyema kama watakuwa sato na chipsi...” akasema Lilian akitabasamu.
“Sawa mpenzi, ni chaguo langu pia.”
Pam akasogea kwenye meza ndogo iliyokuwa na simu, akanyanyua mkonga wa simu kisha akabonyeza namba za mapokezi na kuunganishwa na jikoni, akatoa oda yake.
Waliendelea kuzungumza mengi mle chumbani, Lilian akijihisi kuzidi kumpenda Pam kuliko awali.
“Najisikia kukupenda sana Pam,” akasema Lilian.
“Unamaanisha kuwa mwanzoni hukuwa ukinipenda?”
“Siwezi kusema hivyo ila ukweli ni kwamba, kwa sasa nahisi kukupenda zaidi ya mwanzo. Nakupenda sana.”
“Ahsante sana Lilian, mimi nilikupenda kwa dhati tangu mwanzo.”
“Sasa nakukaribisha rasmi kwenye moyo wangu, uwe mwanaume wangu wa kweli,” akasema tena Lilian.
“Nimefurahi kusikia hivyo, nakuhakikishia nitakuwa mwanaume mwema kwako. Nitahakikisha unakuwa mwenye furaha siku zote. Narudia kukuambia tena, nilikupenda tangu mwanzo, tangu naonana na wewe mara ya kwanza nilikupenda na ninauamini moyo wangu,” akasema Pam akiachia tabasamu.
“Ahsante my love,” akasema Lilian.
Mlango uligongwa, Pam akasimama na kwenda kufungua. Alikuwa ni mhudumu amefika na vyakula walivyoagiza. Pam akapokea na kuingia navyo ndani.
Waliketi mezani kisha wakaanza kula kwa furaha. Kama walivyotarajia ndivyo ilivyokuwa, chakula kilikuwa kitamu sana na wote walikifurahia sana.
Baada ya chakula wakaendelea na vinywaji. Lilian hakujua kitakachotokea baadaye, kilevi kilivyomkolea alijikuta akijiachia kihasarahasara, michezo ya kimapenzi ya hapa na pale ikaanza.
Hapo ukawa mwanzo wa kuelekea kwenye dimbwi la mahaba. Kwa ushawishi wa Pam, Lilian akajikuta akiharibiwa usichana wake. Kwa mara ya kwanza alikutana na mwanaume.
Alipata maumivu makali sana. Lilian alivunja ahadi aliyokuwa amewekeana na mpenzi wake Edo. Maumivu makali aliyopata, ukichanganya na ulevi aliokuwa nao, alijihisi mchovu sana.
Pam na Lilian walilala hadi asubuhi hotelini hapo.
***
Lilian aliamka asubuhi na mapema. Alipojigeuza na kufumbua macho, akamuona Pam amelala pembeni yake, hapo akagundua kuwa kweli alilala na Pam.
Akili za pombe zilimtoka, sasa akagundua thamani ya usichana wake. Alimkumbuka Edo na ahadi walizowekeana. Alimtingisha Pam aliyekuwa bado amelala pembeni yake.
Akashtuka!
“Vipi mpenzi wangu?” Pam akauliza mara baada ya kushtuka usingizi.
“Pam, kwa nini umenifanyia hivi?” akauliza Lilian kwa hasira.
“Tuliza hasira basi, kwani kuna nini kibaya mpenzi wangu?”
“Huoni kama ni vibaya siyo? Huoni ubaya? Ona sasa umeharibu usichana wangu!” akasema Lilian.
“Wasiwasi wako ni nini wakati wewe ni mpenzi wangu? Nipo kwa ajili yako mpenzi. Mimi ni wako na wala si kwamba nimekuwa na wewe kwa siku moja tu, umeshakuwa wangu na utandelea kuwa wangu milele.”
“Hayo ni maneno ya wanaume, siku zote wamekuwa na maneno ya kudanganya tu baada ya kupata wanachotaka, wanaondoka!”
“Mimi nikuache wewe? Nani kasema? Sibahatishi, naujua moyo wangu. Najiamini kuwa nakupenda kwa dhati,” akasema Pam.
“Kweli?”
“Nakuhakikishia,” akasema Pam.
Lilian akajivuta kwa Pam, akalala kifuani mwake. Penzi jipya lilifumuka kwa wawili hao.
Waliamka kwa pamoja na kuelekea bafuni kuoga kisha wakavaa na kuondoka. Pam alimrudisha Lilian mpaka chuoni.
Lilian alikuwa na jambo moja tu kichwani mwake; angemwambia nini Edo kuhusu usichana wake? Hakuwa na jibu!
Huo ndiyo mtihani mgumu uliokuwa mbele yake.
Itaendelea.
 
Aaaaah aaaaah, najua watu wangu watashangaaa, wiki hii nimeamua kuwahisha stori nisaidaiwe wakati wa Sikukuu ya Eid el Fitr... aaaah aaaah.
 
Rich Pol, njoo huku uone, Lilian kwisha habari yake
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom