Hadithi tamu: Hisia zangu

Hadithi tamu: Hisia zangu

Sory ni nzuri na inafundisha lol hawa watu wa it watatumaliza.
 
Mpaka hapo alikuwa hajui anachokitaka Pam au zuga tu!
 
mi lily ananiboaaaaa....ahaaaa.momma hebu fanya mambo edo atabasam kidogo...ananiumaaaaaaa
 
Aahahahahh, nimeishia kucheka tu
Huyu lily sikujui katoka mkoa gani, badala apokee simu ya eddo angalau amshushe pressure kijana wa watu kang'ang;ana na pam,halafu eti anajifanya hajui pam anataka nini, lol!

lily unaniuziiiiii ahaaaaaa.....hebu pokea simu uko upewe mashitaka yako.pesa zisikufanye uuze utu wako..thamani ya penzi lako ni kubwa kuliko pesa ambazo ukitumia zinaisha...mxxxuuuuuuuuuu...
 
Aahahahahh, nimeishia kucheka tu
Huyu lily sikujui katoka mkoa gani, badala apokee simu ya eddo angalau amshushe pressure kijana wa watu kang'ang;ana na pam,halafu eti anajifanya hajui pam anataka nini, lol!
ram kwani Pam anataka nini kwa Lily?
 
Last edited by a moderator:
Lilian kwisha habari....................

Ujanja hakuna tena kitumbua kimeshaliwa hicho.

Na mapenzi ya kuweka pesa mbele ipo siku atakuja jutia Lilian atakapoachwa kwenye mataa na atamkumbua EDOO wake.

Chezea pesa weye.........
 

Hisia Zangu – 11
ILIPOISHIA...
LILIAN alikuwa akimsifia msichana aliyekuwa ndani ya kioo mbele yake. Alikuwa akiangalia taswira yake mwenyewe kwenye kioo. Hakuwa na shaka kuwa, eneo lote la Mlimani City, jioni hiyo kusingekuwa na mwanamke mzuri aliyependeza kama yeye!
Mara simu ikaita!
Ni Pam alikuwa anampigia!
Akapokea...
“Nimeshafika mama, upo tayari?” Pam akamwuliza.
“Bila shaka, dakika mbili tu nitakuwa hapo barabarani,” akasema Lilian kisha akakata simu.
Mara moja akatumbukiza miguu yake kwenye viatu virefu kiasi. Akachukua mkoba na kuubamiza mlango!
Akatembea kama Twiga!
Sasa endelea...

Ni saa 10:00 alasiri, muda ambao kipindi kilikuwa kimemalizika. Kama walioambiana, Lucy na Latifa walitoka kwa pamoja darasani. Wakashuka ngazi taratibu wakianza kutembea kuelekea hosteli.
Tangu wanatoka darasani mpaka wanafika barabara kubwa ya lami, hakuna cha maana walichozungumza zaidi ya stori za hapa na pale.
Lakini baadaye, Latifa akaamua kuvunja ukimya. Akaanza kumzungumzia Lilian...
“Vipi mwenzangu, ulimuona Lilian alivyotoka darasani?” akauliza akionekana kuwa na shauku ya kusikia jibu kutoka upande wa pili.
“Nilimuona sana.”
“Unadhani ana nini?”
“Anajua mwenyewe lakini kwa vyovyote vile, mapenzi ya Pam yatakuwa yameshaanza kumkolea. Unafanya mchezo na pesa?”
“Lakini kweli...”
“Si unamuona Leila, si alijifanya mjanja na mwenye msimamo, yuko wapi sasa? Si aling’ang’ania kuondoka na Big jana. Kuna mjanja kwenye pesa?” akasema.
Wote wakacheka!
Ilikuwa dili!
Kwao ilikuwa furaha, maana fedha ilikuwa inaingia kama kawaida.
“Lakini Pam amenitumia ujumbe nikiwa darasani,” Lucy akasema.
“Amesemaje?”
“Mambo mazuri, leo ana mtoko na Lilian. Watajuana wenyewe. Unajua ninachompendea Pam, hana papara na anajua anachokifanya.”
“Kweli kabisa.”
“We subiri, siku mbili hizi usikie kama utamsikia Lilian akizungumza habari za Edo tena. Kila kitu kitafunikwa na fedha za Pam, niamini mimi.”
“Kwa nini nisiamini wakati dalili zinaonekana wazi?”
“Umeanza kuwa mjanja sasa, unaona maneno hayo?”
“Wewe! Kwani tangu lini nikawa mshamba?”
“Haya bwana, ratiba ya leo vipi?”
“Kiukweli sitaki hata kujichosha sana. Tukapumzike, usiku twende tu hapo Udasa tukale mbuzi choma na ndizi, kisha tushushie na wine, nadhani itakuwa poa!”
“Sawa.”
Wazo likapita!
Fedha kwa wasichana hao ilikuwa jambo dogo sana. Walikuwa na uhakika wa kufanya chochote bila kutegemea fedha zinazoingizwa kwenye akaunti zao na serikali kwa ajili ya matumuzi ya kawaida.
Walitumia usichana wao kujipatia fedha na kufanya kila aina ya anasa za mjini. Ni jambo moja tu walijua, pamoja na yote hayo, vichwani mwao walikuwa na madini ya ajabu.
Walikuwa wakifanya vizuri sana kiasi kwamba, wengine waliamini walikuwa wakitoa rushwa ya ngono kwa wahadhiri ili wawafaulishe. Haikuwa hivyo.
Ukweli ni kwamba, walijua vizuri kujisomea na kujadiliana katika kundi lao. Cha kushangaza ni kwamba, hawakutaka mtu yoyote aungane nao kwenye kundi zaidi ya wao wanne tu; Leila, Lucy, Latifa na Lilian.
Ndivyo msimamo wao ulivyokuwa!
***
Hakutaka lakini alijishangaa akitaka kuingia kwenye anwani pepe yake. Hiyo ni baada ya kuamua kujisomea kwa nguvu na kuachana kabisa na mawazo ya Lilian.
Edo alishaamua kuachana na mambo ya mapenzi. Kichwani mwake aliamini kuwa, Lilian hakuwa mwanamke sahihi kwake, hivyo alijipa muda kutafakari na pengine kutafuta mwingine ambaye angekuwa na penzi la dhati.
Lakini sasa uamuzi huo aliupinga ghafla. Kuna kitu alihisi kikizunguka kichwani mwake. Alitakiwa kujiridhisha tena kupitia maandiko yale kwenye email yake.
“Lilian anaweza kunitusi mimi? Anaweza kunikejeli? Napata shaka na jambo hili. Kuna kitu kipo nyuma kinafanyika. Kipo, naamini kipo,” akawaza.
Muda huo huo akafungua email yake, kisha akaenda kwenye ujumbe wa mwisho kutoka kwa Lilian. Kwa uchungu moyoni, akarudia tena kuusoma. Sasa aliamua kusoma kwa sauti kabisa.
Hakuna kilichobadilika. Maneno yalikuwa ni yaleyale. Alihisi kupasuka kichwa kwa mawazo. Akapata wazo lingine la haraka. Alitakiwa kuzungumza na Lilian muda uleule ili amwulize vizuri kuhusu email alizokuwa akimtumia.
Ni Lilian pekee ndiye angemaliza utata uliokuwa umemzunguka kichwani mwake. Akachukua simu yake mezani kisha akampigia. Simu ikaita kwa muda mrefu sana, lakini haikupokelewa!
Akarudia kupiga kwa mara nyingine, bado haikupokelewa!
“Shiiiiit!” akasema kwa sauti na kuishusha simu hiyo kwa hasira.
Hakuweza tena kuendelea kusoma, alibadilisha nguo, akavaa suti za michezo, akatoka na kwenda uwanjani kwa ajili ya mazoezi ya viungo.
***
Alifungua mlango na kuingia ndani ya gari. Alikutana na tabasamu pana lililodhihirisha fedha kutoka kwa Pam. Lilian akakaa, huku akijishangaa namna woga ulivyoanza kumuondoka kwa kasi.
“Karibu mrembo!” Pam akasema.
“Ahsante. Pole na kazi.”
“Nashukuru, nawe pole kwa masomo.”
“Ahsante sana. Siku yangu haijawa nzuri sana leo, kichwa kimekuwa kizito sana.”
“Usijali, amini kwamba utaimaliza siku vizuri sana.”
“Nashukuru Pam.”
Gari likaungurumishwa!
Walikuwa wanaelekea Mlimani City. Hapakuwa mbali, dakika tatu tu Pam alikuwa anaegesha gari kwenye maegesho eneo hilo. Akashuka, kisha akazunguka upande wa pili haraka na kumfungulia mlango Lilian.
Akashuka!
Wakaongozana hadi Samaki Samaki. Wakapata chakula cha jioni kisha vinywaji vikafuata. Kwa mara ya pili Lilian alikunywa mvinyo. Kidogo alianza kuuzoeazoea!
Hawakukaa sana, saa nne usiku, Pam alimrudisha Lilian chuoni. Akiwa ameegesha gari nje ya jengo la hosteli anayoishi, Pam alitoa bahasha na kuchomoa maburungutu matatu ya fedha na kumkabidhi.
Zilikuwa milioni tatu!
Lilian akasita kupokea.
“Chukua tu!”
“Hapana Pam. Kwa nini unanifanyia yote haya? Hebu niambie ukweli, unataka nini kwangu?” Lilian akamwuliza.
“Unataka kujua ukweli?” Pam akamwuliza akiwa amemkazia macho.
“Ndiyo niambie ukweli Pam, kuwa wazi...” akasema Lilian akionekana kukolea kwa kilevi kidogo.
Itaendelea ...
 
Hisia Zangu – 11
ILIPOISHIA...
LILIAN alikuwa akimsifia msichana aliyekuwa ndani ya kioo mbele yake. Alikuwa akiangalia taswira yake mwenyewe kwenye kioo. Hakuwa na shaka kuwa, eneo lote la Mlimani City, jioni hiyo kusingekuwa na mwanamke mzuri aliyependeza kama yeye!
Mara simu ikaita!
Ni Pam alikuwa anampigia!
Akapokea...
"Nimeshafika mama, upo tayari?" Pam akamwuliza.
"Bila shaka, dakika mbili tu nitakuwa hapo barabarani," akasema Lilian kisha akakata simu.
Mara moja akatumbukiza miguu yake kwenye viatu virefu kiasi. Akachukua mkoba na kuubamiza mlango!
Akatembea kama Twiga!
Sasa endelea...

Ni saa 10:00 alasiri, muda ambao kipindi kilikuwa kimemalizika. Kama walioambiana, Lucy na Latifa walitoka kwa pamoja darasani. Wakashuka ngazi taratibu wakianza kutembea kuelekea hosteli.
Tangu wanatoka darasani mpaka wanafika barabara kubwa ya lami, hakuna cha maana walichozungumza zaidi ya stori za hapa na pale.
Lakini baadaye, Latifa akaamua kuvunja ukimya. Akaanza kumzungumzia Lilian...
"Vipi mwenzangu, ulimuona Lilian alivyotoka darasani?" akauliza akionekana kuwa na shauku ya kusikia jibu kutoka upande wa pili.
"Nilimuona sana."
"Unadhani ana nini?"
"Anajua mwenyewe lakini kwa vyovyote vile, mapenzi ya Pam yatakuwa yameshaanza kumkolea. Unafanya mchezo na pesa?"
"Lakini kweli..."
"Si unamuona Leila, si alijifanya mjanja na mwenye msimamo, yuko wapi sasa? Si aling'ang'ania kuondoka na Big jana. Kuna mjanja kwenye pesa?" akasema.
Wote wakacheka!
Ilikuwa dili!
Kwao ilikuwa furaha, maana fedha ilikuwa inaingia kama kawaida.
"Lakini Pam amenitumia ujumbe nikiwa darasani," Lucy akasema.
"Amesemaje?"
"Mambo mazuri, leo ana mtoko na Lilian. Watajuana wenyewe. Unajua ninachompendea Pam, hana papara na anajua anachokifanya."
"Kweli kabisa."
"We subiri, siku mbili hizi usikie kama utamsikia Lilian akizungumza habari za Edo tena. Kila kitu kitafunikwa na fedha za Pam, niamini mimi."
"Kwa nini nisiamini wakati dalili zinaonekana wazi?"
"Umeanza kuwa mjanja sasa, unaona maneno hayo?"
"Wewe! Kwani tangu lini nikawa mshamba?"
"Haya bwana, ratiba ya leo vipi?"
"Kiukweli sitaki hata kujichosha sana. Tukapumzike, usiku twende tu hapo Udasa tukale mbuzi choma na ndizi, kisha tushushie na wine, nadhani itakuwa poa!"
"Sawa."
Wazo likapita!
Fedha kwa wasichana hao ilikuwa jambo dogo sana. Walikuwa na uhakika wa kufanya chochote bila kutegemea fedha zinazoingizwa kwenye akaunti zao na serikali kwa ajili ya matumuzi ya kawaida.
Walitumia usichana wao kujipatia fedha na kufanya kila aina ya anasa za mjini. Ni jambo moja tu walijua, pamoja na yote hayo, vichwani mwao walikuwa na madini ya ajabu.
Walikuwa wakifanya vizuri sana kiasi kwamba, wengine waliamini walikuwa wakitoa rushwa ya ngono kwa wahadhiri ili wawafaulishe. Haikuwa hivyo.
Ukweli ni kwamba, walijua vizuri kujisomea na kujadiliana katika kundi lao. Cha kushangaza ni kwamba, hawakutaka mtu yoyote aungane nao kwenye kundi zaidi ya wao wanne tu; Leila, Lucy, Latifa na Lilian.
Ndivyo msimamo wao ulivyokuwa!
***
Hakutaka lakini alijishangaa akitaka kuingia kwenye anwani pepe yake. Hiyo ni baada ya kuamua kujisomea kwa nguvu na kuachana kabisa na mawazo ya Lilian.
Edo alishaamua kuachana na mambo ya mapenzi. Kichwani mwake aliamini kuwa, Lilian hakuwa mwanamke sahihi kwake, hivyo alijipa muda kutafakari na pengine kutafuta mwingine ambaye angekuwa na penzi la dhati.
Lakini sasa uamuzi huo aliupinga ghafla. Kuna kitu alihisi kikizunguka kichwani mwake. Alitakiwa kujiridhisha tena kupitia maandiko yale kwenye email yake.
"Lilian anaweza kunitusi mimi? Anaweza kunikejeli? Napata shaka na jambo hili. Kuna kitu kipo nyuma kinafanyika. Kipo, naamini kipo," akawaza.
Muda huo huo akafungua email yake, kisha akaenda kwenye ujumbe wa mwisho kutoka kwa Lilian. Kwa uchungu moyoni, akarudia tena kuusoma. Sasa aliamua kusoma kwa sauti kabisa.
Hakuna kilichobadilika. Maneno yalikuwa ni yaleyale. Alihisi kupasuka kichwa kwa mawazo. Akapata wazo lingine la haraka. Alitakiwa kuzungumza na Lilian muda uleule ili amwulize vizuri kuhusu email alizokuwa akimtumia.
Ni Lilian pekee ndiye angemaliza utata uliokuwa umemzunguka kichwani mwake. Akachukua simu yake mezani kisha akampigia. Simu ikaita kwa muda mrefu sana, lakini haikupokelewa!
Akarudia kupiga kwa mara nyingine, bado haikupokelewa!
"Shiiiiit!" akasema kwa sauti na kuishusha simu hiyo kwa hasira.
Hakuweza tena kuendelea kusoma, alibadilisha nguo, akavaa suti za michezo, akatoka na kwenda uwanjani kwa ajili ya mazoezi ya viungo.
***
Alifungua mlango na kuingia ndani ya gari. Alikutana na tabasamu pana lililodhihirisha fedha kutoka kwa Pam. Lilian akakaa, huku akijishangaa namna woga ulivyoanza kumuondoka kwa kasi.
"Karibu mrembo!" Pam akasema.
"Ahsante. Pole na kazi."
"Nashukuru, nawe pole kwa masomo."
"Ahsante sana. Siku yangu haijawa nzuri sana leo, kichwa kimekuwa kizito sana."
"Usijali, amini kwamba utaimaliza siku vizuri sana."
"Nashukuru Pam."
Gari likaungurumishwa!
Walikuwa wanaelekea Mlimani City. Hapakuwa mbali, dakika tatu tu Pam alikuwa anaegesha gari kwenye maegesho eneo hilo. Akashuka, kisha akazunguka upande wa pili haraka na kumfungulia mlango Lilian.
Akashuka!
Wakaongozana hadi Samaki Samaki. Wakapata chakula cha jioni kisha vinywaji vikafuata. Kwa mara ya pili Lilian alikunywa mvinyo. Kidogo alianza kuuzoeazoea!
Hawakukaa sana, saa nne usiku, Pam alimrudisha Lilian chuoni. Akiwa ameegesha gari nje ya jengo la hosteli anayoishi, Pam alitoa bahasha na kuchomoa maburungutu matatu ya fedha na kumkabidhi.
Zilikuwa milioni tatu!
Lilian akasita kupokea.
"Chukua tu!"
"Hapana Pam. Kwa nini unanifanyia yote haya? Hebu niambie ukweli, unataka nini kwangu?" Lilian akamwuliza.
"Unataka kujua ukweli?" Pam akamwuliza akiwa amemkazia macho.
"Ndiyo niambie ukweli Pam, kuwa wazi..." akasema Lilian akionekana kukolea kwa kilevi kidogo.
Itaendelea ...

Mkuu hii Episode ya 11 naona umeirudia...
 
HISIA ZANGU -12
ILIPOISHIA...
“Ni wewe kweli ndiye unayenitumia meseji mbaya kwenye email yangu?” Edo akauliza kwa utulivu.


Lilian akashtuka!
“Meseji mbaya?”
“Ndiyo meseji mbaya. Hebu nijibu na uwe mkweli, ni wewe?”
Lilian akazidi kuchanganyikiwa!
Hakukumbuka kumwandikia ujumbe wowote mbaya zaidi ya kumtumia mara moja tu, akitaka kujua kuhusu ukimya wake!
Hiyo ilikuwa ni ukimya baada ya kuingia nchini Malaysia mara walipoachana Uwanja wa Ndege jijini Dar es Salaam.
Taa nyekundu iliwaka kichwani mwake.
Ulikuwa mchezo!
Hata hivyo, hakuna aliyeujua. Si yeye wala Edo.
SASA ENDELEA...
LILIAN alitulia kwa muda akiiacha simu hewani bila kuzungumza kitu. Alitakiwa kutulia kwa muda ili aweze kutafakari japo kwa muda mfupi kuhusu mambo yaliyokuwa yakitokea wakati huo.
Yalikuwa mambo mageni kabisa. Edo hakuwa yule aliyemzoea. Japokuwa moyoni alikiri wazi kuwa alishachafua penzi lao kwa kumwingiza Pam lakini kwa kiasi kikubwa, Edo alichangia.
Swali la Edo likaendelea kugonga kichwani mwake. Kwa nini anamwambia asimfiche. Ni wazi kuwa isingekuwa rahisi kwa Edo kugundua kuwa alikuwa na mpenzi mwingine na tayari mapenzi yalishaanza kuchanua.
Ilikuwa vigumu sana!
Angejuaje?
Malaysia na Tanzania wapi na wapi? Kuala Lumpur na Dar es Salam, wapi na wapi? Ni nchi mbili tofauti. Majiji mawili tofauti, tena yaliyotenganishwa na nchi nyingi katikati.
“Hawezi kujua kuhusu Pam,” akajipa moyo.
“Ndiyo....hawezi jua. Atajuaje sasa? Nani wa kumwambia? Siamini kama anaelewa kuhusiana na Pam. Lakini bado nachanganywa na jambo moja. Kwa nini anasema nimemtumia email yenye maneno machafu?
“Ni lini mimi nimemtumia email? Kuna kitu kinaendelea hapa. Lazima kuna mchezo mchafu unafanyika. Napaswa kuwa makini sana, lakini ngoja kwanza nimsikilize. Nitaujua ukweli tu,” akazidi kuwaza Lilian.
Ni kweli Lilian alikuwa katika mawazo sahihi kabisa. Kila kitu ni kama kilikuwa kimejificha ndani. Hakuwa na uwezo wa kuona lakini alijiahidi kuupata ukweli.
“Lilian...” Edo akaita baada ya kimya cha muda mrefu.
“Nakusikia Edo.”
“Hutaki kuniambia ukweli?”
“Unataka ukweli gani mwingine? Mimi nimekuambia nimekuandikia email mara moja tu. Tena nilikuuliza kama umefika salama na kwa nini hukunijulisha. Hivyo tu, hakuna email nyingine niliyokutumia mpenzi.”
“Una hakika?”
“Ndiyo.”
“Naanza kupata picha sasa.”
“Picha gani?”
“Hapo ulipo si unayo laptop?”
“Ndiyo.”
“Sawa...naomba uingie kwenye akaunti yako mara moja, halafu unijulishe.”
“Mh! Haya bwana. Kwani kuna nini?”
“Fanya hivyo.”
“Sawa.”
Wakakata simu.
Mara moja Lilian akaivuta laptop yake, akaingia kwenye mtandao wa google.com kisha akaenda moja kwa moja kwenye anwani pepe ya gmail. Akaandika jina la akaunti yake ambayo ilisomeka; lilygirldsm, kisha akaenda mahali pa kuandika neno siri, akaandika.
Haikuwa ngumu, ilikuwa ni muunganiko wa majina yake na Edo. Aliandika lilianed, kisha akaingia. Alitumia muda kidogo kuperuzi, akaangalia email zilizoingia na kutoka.
Akagundua ni ileile ya mwisho aliyomtumia Edo. Hapakuwa na nyingine. Lilikuwa jambo lililomshangaza sana. Muda huo huo akampigia Edo.
Edo hakupokea, alimkatia na baadaye akampigia yeye...
“Tayari?” Edo akamwuliza haraka baada ya Lilian kupokea simu.
“Ndiyo mpenzi.”
“Sasa fanya hivi, nenda kwenye sehemu ya kuandika ujumbe, andika neno lolote hata kama ni fupi tu, kisha nitumie. Ukishafanya hivyo naomba unijulishe kwa simu,” akasema Edo.
“Sawa baba.”
Lilian akafanya hivyo. Kwake yalikuwa majaribio ya kushangaza sana. Hakuelewa ni kwa nini alikuwa akimwambia afanye hivyo. Hata hivyo hakuwa na la kufanya zaidi ya kutekeleza maagizo yale.
Akaenda kwenye sehemu ya kuandika ujumbe, akamwandia maneno manne tu kwa herufi kubwa; I LOVE U EDO! Mara moja akamtumia. Alipokamilisha zoezi hilo, akamtumia sms kupitia simu yake, kumjulisha kuwa tayari alishamtumia.
Ilipita dakika moja bila Edo kujibu kitu, kisha simu yake ikaita. Alipotupa macho yake kwenye kioo cha simu yake, akakutana na namba za Edo. Mara moja akapokea.
“Una hakika umenitumia?”
“Ndiyo mpenzi.”
“Kwenye email yangu ileile?”
“Ndiyo baby.”
“Unaweza kunitajia?”
“Kabisa, ni eddyhb@yahoo.co.uk
“Sasa nimeanza kupata picha.”
“Ni nini mpenzi?”
“Hakuna email iliyofika huku.”
“Kivipi sasa wakati nimekutumia?”
“Ndiyo maana nimekuambia nimeshaanza kupata picha. Kifupi kuna mtu ameyateka mawasiliano yako. Bila shaka ni mtu wako wa karibu na anayekujua sana. Lengo lake kubwa ni kuharibu uhusiano wetu.
“Sasa nimeshajua cha kufanya. Najua unao marafiki zako wa karibu. Kuna mmoja wao anajaribu kufanya huu ujinga. Sasa mimi sijali wala wewe usijali na usijaribu kumshirikisha mtu yeyote kuhusu hili jambo.
“Unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kufungua akaunti nyingine ya email. Hiyo ya zamani achana nayo na usiitumie tena. Lakini usiwaambie rafiki zako kuwa umeamua kubadilisha akaunti,” akasema Edo.
“Lakini baby...” akasema Lilian lakini kabla hajamalizia, Edo alikuwa ameshadakia.
“Hakuna cha lakini hapo, fuata maelekezo yangu.”
“Sawa baba, nimekuelewa.”
Wakakata simu.
Lilian alizima kila kitu pale mezani. Alizima mpaka simu, kisha akajitupa kitandani kulala. Kichwa kilikuwa kizito kuliko kawaida. Mawazo mengi yalimtawala.
Bado alikuwa hajaelewa, ni nani aliyeteka mawasiliano yake na kwa nini aliamua kumgombanisha na mwanaume wa maisha yake. Jambo hilo lilisababisha usiku huo uwe mgumu, mzito na mrefu kuliko kawaida!
Alikesha akiwaza!
Usingizi angeupata wapi?
“Hakuna marefu yasiyo na ncha,” akajisemea.
Angalau maneno hayo yalimtia faraja, kidogo akajihisi mwepesi na macho yake sasa yakaanza kumlemea kwa uzito. Bila uamuzi wake, aliyafumba,mara usingizi mzito ukamchukua!
Itaendelea wiki.



 
Back
Top Bottom