Hadithi: Gamboshi

Hadithi: Gamboshi

SEHEMU YA SABA (7)

Alitoka mpka nje alikuta watu wakiwa wamejaa wamezunguka maiti ya binti yule ambae wamemaliza kumtoa mtoni mda si mrefu, afande baraka na mzee walikuwa wamesimama pembeni wakiwa wanamsubiri
“Nini kinaendelea”
“Familia ya marehemu imekuja inataka mwili wa binti yao”
“Hicho kitu hakiwezekani”
“Kimila na desturi ni vema mngewapa mwili wa binti yao” yule mzee alimwambia afande mwita bila kupepesa macho huku afande baraka akibaki kimya
Sababu ya afande mwita kukataa alikuwa anahitaji kufanya upepelezi wa nani kafanya hivi na kwa nini kama ilivokuwa kawaida akipata kazi kipindi cha nyuma
“Naombeni tuskilizane”
“Naomba nifahamu familia ya huyu binti” alinyoosha kidole na kuuliza
Walijitokeza mama mmoja akiwa na binti mdogo wa miaka 17 kwa pembeni yake
“Samahan we ndo familia ya huyu binti aliyelala hapo”
“Ndio”
“Ni nani yako”
“Ni mwanangu mimi mama yake mzazi “
“Kwanza mama nikupe pole”
“pili mimi naitwa mwita ni askari wa jeshi la polisi nimekuja na mwenzangu”
“Baraka” afande Baraka alijitambulisha
“Lengo la kuja hapa ni kurudisha amani na pamoja haki na uhuru wenu kama wanakijiji”
“Pia kutokomeza vitendo vya kikatili kama hivi, Kwahiyo nakuomba tubaki na mwili wa binti yako” akaongezea huku akimtzama mama yule machoni.
“Sawa” alijibu na kugeuka akiwa na binti yake bila kuongezea chochote na kuondoka pale
Afande mwita alishusha pumzi tena na kumwita afande baraka waweze kurudisha ule mwili kwenye gari yao ya jeshi la polisi, Afande mwita alimfata yule mzee na kumuuliza ni wapi wanaenda kufungua kituo chao basi mzee yule alikubali na kuwapeleka mpka eneo lenyewe kilikuwa ni chumba ambacho kilitumika kama sungu sungu miaka ya nyuma lakini mazingira yalionesha hakijatumika kwa muda mrefu sana walikuta uchafu kwa wingi sana huku panya zikiwa zimekufa kila mahari na wadudu wengine
“Hii sehemu inanuka kama buka man” Afande baraka alikuwa akijiuliza
“BUKA MAN NDO NANI”yule mzee aliuliz
“Ni kitabu tu hata sio hadithi ya kweli”Afande mwita alimjibu
“Mnamanisha BUKAKILAMA SIO BUKA MAN”
“Na alikuwa sio mwanaume alikuwa ni mwanamke” akaozengea
“Inaonesha unamjua ni nani” Afande baraka alishangaa badaa ya yule mzee kuongea lile neno
“Sijui chochote “ yule hakutaka kuendelea na mazungumzo na aliondoka na kuacha wafanye usafi kwenye hilo eneo
“Wanawake wa hivo huwa wanafaa w apatane na bishoo kama wewe”
“Nani?”
“Bukakilama”
“Me nioe mchawi”
“Ata ivyo mapenzi uchawi”
“Kwahiyo we umerogwa”
“ Na nani sasa Veronica au Janeth “ afande baraka aliuliza na kumwacha afande mwita akimtazama tu huku akitabasamu, sababu afande mwita alikuwa anafaham afande baraka ni mtu wa matani sana kwahiyo hakujibu swali lake
“Embu tufanye kazi iliyotuleta hapa”Afande alimjibu na kuendela na shughuli zingine akiwa anaendelea kufanya usafi alikota karatasi moja ambayo ilikiwa imekunjwa na kuikunjua alikuta ilikuwa ni ramani flani ambayo kwa wakati huo akuielewa lakini aliona kuna rangi ya mduara mwekundu ulikuewa umezungushiwa kwenye ramani ile aliikunya kama alivo ikuta na kuiweka mfuko wa nyuma
Aliendelea kufanya usafi lakini simu yake ya mfukoni iliita alitoa na kuangalia alikuwa mkuu wa kituo cha polisi mkoa wa simiyu akifahamika kama Njegele kulwa alipokea
“Hello”
“Habari yako Afande” Alikuwa ni mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa simiyu bwana
Huku mwita kiendelea kuongea na maongezi simu ya afande baraka pia iliita alitoa mfukoni na kuangalia alikuwa ni veronica alipokea
“Hello”
“Mambo Vp shem”
“Acha basi masihara baraka”
“Haya safi nambie”
“Mbona napiga simu ya mwita hapokei”
“Yupo anaongea na simu nyingine”
“Ooh okay”
“Na mnaendeleaje hapo”
“Tupo tunafanya usafi, japo tulikuwa na changamoto kidogo”
“changamoto gani?”
“Tumepata maiti kipindi tunarudi kijijini”
“Mungu wangu”
“Ndio na Familia ilikuwa inataka kuchukua mwili ikazike leo lakini na sisi tunafata sheria”
“Lazima maiti ifanyiwe uchunguzi”Veronica alimalizia
“Ndio”
Maongezi yakiendelea kwenye simu baina yao wawili Afande baraka aliskia akiitwa ivyo alimwaga na kukata simu kwenda kuskiliza alikuwa akiitiwa nini
“ulikuwa unaongea na nani”
“Dem wako!”
“NANI?”afande mwita alitahamaki
“Veronica” Afande baraka alijibu bila wasiwasi
“kapiga akitaka kujua unaendeleaje akaona aulizie tunaendeleaje”akaongezea
“Ukamjibuje?”
“Tunaendelea vizuri sana”
“Na wewe ulikuwa ukiongea na nani”
“Njegele”
“Anasemaje”
“Alikuwa anaulizia maendeleo nikamwomba aniongezee askari wawili”
“Kakubali”
“Ndio”
Walimaliza maongezi hayo mafupi na kuendelea na kazi hadi saa moja jion wakiwa wamefika asalimia 90 ya marekebisho na usafi ukiwa umeenda vizuri mzee yule ambae mpaka saa hamna kati yao anaemjua jina alifika na kupeleka mpka mgahawani kwenda kupata chakula walipofika mgahawani waliagiza na kukaa lakini akiwa amekaa anasubiri chakula afande mwita aliangalia kwa njee na kuona dada mrembo sana na kutokewa kuvutiwa sana alijikuta akimtazama mdada hakika alikuwa mrembo sana akiwa kasuka rasta rangi yake kama mtoto wa uchagani lakini hakupata nafasi ya kusemesha sababu yeye alikuwa kwa ndani na mdada alikuwa kwa nje.
Walimaliza kupata chakula na mzee yule kuwaambia waende moja kwa moja kula na wao walimskiliza ikiwa ni siku yao ya kwanza wamemaliza wakiwa kijijini gamboshi walikuwa wachovu sana ivyo kila mmoja alipata maji ya kuoga na kwenda kupumzika kitanda
“Huwezi kuamini kipindi naambia watu watawanyike pale mtoni nilikuwa na hofu labda wanaweza kupinga”afande mwita akimwelezea afande baraka huku akiwa amelala chali
“Hata kipidi naongea na yule mama nilikuwa na hofu sana, nilikuwa nikimtazama machoni naona kama anahasira sana na mimi au dunia nilikuwa sielewi” aliendelea kuongea huku afande baraka akimskiliza kwa makini sana akiwa yupo kitandani pia
“Hawa watu wameumia kwa mda mrefu na wanaitaji matuamini tena labda wewe unaweza kuwa shujaa wao”afande baraka akimwelezea mwita kwa nini hao watu wako hivo
“Siku zote umekuwa shujaa kwenye kila kitu, unakumbuka ulisadia maisha yangu “
“Siwezi kusahau iyo siku”
“hata hawa unaweza wasaidia”
Mda wote afande akiwa anaongea afande mwita alikuwa kimya
“Unajua nini siku zote nimekuwa shujaa kwenye mambo yote kumbuka na wewe ulikuwa nyuma nyangu, na saizi upo na mimi kwenye kufanya hili jingine”
Walisamama na kugonga tano huku wakihadi kusaidia hiki kijiji ,Afande mwita alipo rudi kitandi alikumbuka kuna zawadi alipewa na mke wake kipindi anaondoka nyuma alikulupuka na kutoka nje huku afande baraka akiwa tayaru kashapitia na usingizi baada ya maongezi yale alifika kwenye gari kufungua ilikuwa kwenye dashboard alichukua na kurudi ndani alifika na kukifungua kile kiboski alikuta kuna rozari ya wakristu ambayo imetengenezwa na madini ya shaba alifurahi sana huku ndani kukiwa na ujumbe mfupi wa maandishi “NI BUSU KABLA HUJALALA” hakika alibusu huku tabasamu likiwa limetawala uwo wake aliwaza kumpigia mke wake lakini aliona mda umeshaenda hivyo aliahid asubuhi atakuwa mtu wa kwanza kumpigia.
 
Sehemu ya saba iko tayari karibuni msome wapendwa na wapenzi wa gamboshi aisee poleni sana kwa kusubiri naona wafuatiliaji mmekuwa wengi sana nashukuruni sana
 
Picha ndo kama limeanza hivi afande mwita kama namwona shusha like na comment yako niendelee kuweka kazi nzuri
 
UTANGULIZI

Ni hadithi inayohusu kijiji kilichopo mkoa wa simiyu wilaya ya bariad ambacho kiko umbali wa takribani kilometa 12 za mlaba kutoka simiyu mjini, kama hili jina litakuwa geni kwako na hujawahi kuliskia kabisa basi ngoja nikufamishe kidogo.

Gamboshi ni kijiji kinachofahamika kwa uchawi nchi Tanzania kikifahamika ni makao makao makuu ya wachawi ukiachana na mkoa wa sumbawanga basi kwa lugha nyingine unaambiwa ni kitovu cha wachawi yani mizimu yote inapatikana huko, ndo kijiji pekee unaambiwa mchana giza usiku ulaya.

Julai mwaka 1999 serikali ilichukua maamuzi ya kukitenga kijiji hicho baada ya vifo vya zaidi ya watu hamsini [50] vilivoketea ndani ya siku moja ikiaminika ilikuwa na uhusiano na mambo ya kishirikina basi watu waliambiwa kuhamaka makazi na kutafuta sehemu zingine za kuishi.

Kwa muda wa takribani miaka ishirini [20] hamna ambae amekuwa na taarifa zozote kuhusu eneo hilo basi ndo mda serikali kutoka kwenye ofisi ya rais, ilitumwa barua kwa mkuu wa mkoa wa simiyu barau ya agizo la kukifungua kijiji hicho kwa upya ikiwezekana atume maaskari mara moja na kufunguliwe kituo kidogo cha polisi nae mkuu wa mkoa wa simiyu alitii maagizo yaliyo kuwa yametoka kwa rais na kuitisha kikao cha maaskari wa jeshi la polisi, kutoka wilaya zote za simiyu.

Mkuu wa mkoa kwa kutambua kuwa askari wengi wangekuwa na uonga wa kufanya kazi kijiji kule lakini bado ilikuwa inamlazimu kuchagua sababu pia alikuwa na mamlaka ya kufanya hivyo, basi alifanya maamuzi na kumchagua Mwita Choma na Baraka Kulwa kama maaskari teule kwenda kijijini gamboshi.
Lakini bila kufaham wamejiigiza kwenye shida kubwa nao walikuba kazi ile kwa mikono yote.

SEHEMU YA KWANZA

Tarehe 13 mwezi wa sita mwaka 2019 saa kumi na mbili afajiri [06:00am] akiwa amelala kwake kengele ya mezani [ Alarm] ilikuwa ikipiga kelele kumanisha mda wa kuamka umefika nae taratibu akijinyoosha kutoa uchovu wa usiku, akamudu kufungua macho huku akiwa anatazama aliona mtu akija ghafla kurukia kitandani kama kwa kishindo alishutka sana maana alikuwa na wenge la usingizi lakini hakuwa mwingine bali mke wake Mwita choma

“Habari za asubuhi, mme wangu”. alikuwa ni mke wake mwita akitoa salam huku akilukia kwa kitanda alipo mume wake
“ unajua umenishutua” mwita alimuliza mke na kueka kituo bila kujibu salam yake
“ kumbe umeogopa, basi pole mume wangu”anaomba radhi huku sura yake ikiwa inatabasamu kama anataka kucheka .
“ Umeamkaje kipenzi changu” bado aliuzua huku sura yake ikiwa na tabasamu lilelile
“ salama tu mke wangu.” alijibu salam ya mke wake akaambatanisha na swali,
“mbona umeamka mapema sana leo”
“ kuna kitu konki nimekuandalia kabla ya hujaondoka” alimjibu swali la mume akimtazama kwa ukalibu
“Aah konki” mwita alianza kumtenkenya mke wake huku akirudia neno “konki”
Konki! konk, konki! konki! Mwita aliendelea kumtenkenya huku mke wake akicheka na kumwomba aache anahisi atajikojolea!
Mwita aliacha huku mke wake akiwa ameweka sura ya kununua nae alijirudi na kumwambia
“ kumbe umeumia, basi pole mke wangu” huku sura yake ikiwa inatabasamu kama anataka kucheka

Wakiwa bado wapo kitandani mke wake hakujibu chochote bali alisogeza uso wake karibu na kushika kidevu cha mume wake na kumpiga busu la wakika, na kulikatisha haraka huku akishuka kitandani na kumwambia mume wake amfate bafuni. Nae Mwita alishuka kitandani haraka akiwa na boxer tu na kuelekea bafuni, basi huko kilikuwa ni kitendo cha kuendelea kudumisha ndoa yao ambayo imeishi kwa muda wa miaka mitano sasa wakiwa bado hawajafanikiwa kupata mtoto.

Mwita choma ni kijana wa miaka therathini [30] kabila mkulya urefu wake nin wastani, akiwa na miaka 25 alibahatika kupata mke aitwae ni Janeth. akiwa na miaka 27 aliteuliwa kuwa ofisa msimamizi wa kituo kidogo kilichopo wilaya ya bariadi mkoani simiyu alifanya kazi kwa waminifu huku sifa zikimndondokea kama kijana jasiri. Badaa ya kutumikia jeshi la polisi kwa kipindi wa muda mrefu akiwa ofisa msimamizi alipewa kazi ya kwenda kuwa mkuu wa kituo kijijini gamboshi kama ilivotoka kwa ofisi ya raisi kuwa wateuliewe askari wawili waende wakafanye kazi kijijini huko.

Na ndo ilikuwa siku yenyewe akiwa ameamka salama akiwa nyumbani kwake na mke wakiwa bafuni wanamlizia kuoga. Akiwa amejifunga taulo kiunoni alisikia sauti ya simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita aliishika na kuangalia jina lilikuwa ni rafiki yake Baraka kulwa alikuwa anapiga alikuwa amemsave [ Partern in crime] alipokea na kuongea nae

“Kaka, habari yako” ndo kitu cha kwanza aliskia alipo pokea simu ilikuwa ni salam kutoka kwa rafiki yake
“ salama kaka, kwema?”
“uko wapi”
alijibu salam huku akikaa kitandani. Akaongezea swali jingine
“Kwema! Niko nyumbani napata breakfast” baada ya kujibu swali mwita alicheka na kuuliza
“Haha haha”
“Hivi mdogo wangu huna mpango wa kuoa kabisa!”
“Maana kila siku ujipikie mwenyewe ufue kwa nini usioe?”
Aliuliza na kubaki kusubiri atasema nini
“Mimi ntaoa tu kaka ata usijali ni mipango tu”
“Sawa, wahi kituo sababu tutakuwa tunaondoka mapema si unalewa sehemu tunayoenda unaambiwa usiku ni ulaya” alikubali kisha kumpa taarifa nyingine
“Haha haha, sawa kaka” alicheka kidogo kwa taarifa mwita aliyompa kisha akakubali na kukata simu maongezi yakawa yameishia hapo
Mwita akaweka simu kitandani iliavae nguo za jeshi la polisi ambazo zilikuwa zinamkaa vizuri sana sababu pia ya mwili wake uliokuwa umekaa kimtindo wenye mpangilio na kwenda kupata chai ambayo mke alikuwa kamwandalia, alikuta janeth akiwa anamsubiri seblen akiwa tayari kashaweka chai mezan alikuwa kavaa kitenge tu.
“Karibu chai mme wangu” alimkaribisha chai mme wake kwa tabasamu nzuri kabisa huku akimtengenezea kiti aweze kuketi
“Ahsante mke wangu” alishukuru na kuketi kwenye kiti huku mke wake akiwa ubavu wake wa kushoto
Hakika kilikuwa chakula kitamu ambacho hata mwita alishambulia kama hana akili timamu
“wewe umeshakula mke wangu” aliuliza huku akiendelea kula
“ hapana babo ntakula baadae kidogo, saivi nataka nikae karibu na wewe” alimjibu mme wake na kuongezea shida yake kwa huo mda
Mwita alitambua kwa nini mke wake alisema maneno yale na alikuwa hana jinsi zaid ya kumfariji
“ usijali mama angu, mimi ni wako siku zote “ alimwambia maneno mazuri akiwa anambembeleza kwa kumshika shavu akitumia mkono wake wa kushoto
Janeth alisimama na kumwambia mme wake asuburi na kuelekea chumbani alipo rudi alikuwa na kiboski kidogo ambacho kilikuwa kimefungwa vizuri
“ Kwa ajili yako mme wangu” alimpatia kwa mikono miwili likiabatinishwa na taabasam kama ilivyo kawaida yake kutabasamu
“Ahsante mke wangu” mwita alifurahi alionesha kabisa kashukuru alisamama na kumpatia busu mke wake, alipo jaribu kufungua mke wake alikataa na kumwambia utaifungua baadae
“kuna nini kwani “ akaongezea na swali
“ utaona tu, lakini usikifungue hapa” alimwambia akiwa anamtazama machoni bila kupepesa
“ sawa” mwita alikubali lakini alibaki na maswali kutakuwa na nini kwenye boski maana kilikuwa kidogo sana chenye urefu wa 5 na upata wa 3
tayari kamaliza kupata chai alichukua begi lake la mgongoni lilokuwa mezani na kuelekea nje akiwa anatoka alimgeukia mke wake na kumwambia
“ usisahau kufunga milango mda wa kulala na ukiwa unatoka”
“ na ukiwa na shida yoyote nipigie mimi kwanza”akaongezea huku akiwa anafungua mlango
“sawa , mme wangu” alikubali huku akimtazama mme wake akielekea kupanda gari la jeshi la polisi aina ya toyota landa cruiser ikiwa inafahamika kama [ Defender ]
Mwita aliwasha injini ya gari na kushusha vioo huku mke wake akiwa bado anasubiri aondeke
“ kwaheri, ubaki salama” alimwaga akiwa anamtazama kwa mbali
“ sawa, safari njema mme wangu” alimjibu na kuingia ndani
Mwita alipandisha vioo na kuondoa gari kuelekea kituoni.
Huu uandishi mbona unaboa sana kuelewa jamani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom