Hadaa ya Mihimili ya Serikali

Hadaa ya Mihimili ya Serikali

Nimetoa mfano kuwa wananchi wengi walitaka muungano wa mkataba ila mbona Warioba aliweka serikali 3 na sio suala la mkataba? Mbona issue ya serikali za majimbo lilipigwa chini? Maana yake maoni yote walichukua ila walichakata na mengine kuyatoa na baadhi kubakiza.
Waliotaka Muungano wa Mkataba ni wachache sana wakiongozwa na Marhum Seif.

Swali waliloshindwa kujibu ni moja, ni mkataba wa mambo gani! Tume ya Warioba ilibaini mkataba ulilenga kuafikiana mambo yenye manufaa kwa Zanzibar. Kwa mfano, Wazanzibar wanajua soko kubwa la biashara lipo bara. Wanatambua ili kufikia masoko mengine lazima wapitie bara. Kwamba, ajira za vijana wao ni bara. Gharama za ulinzi na mambo ya ndani ni kubwa kwao. Hivyo walitaka kuchagua baadhi ya mambo wanayonufaika nayo yawe ni ya mkataba ikiwemo umiliki wa ardhi.

Katika Mkataba Tanganyika hainufaiki na chochote, Mzee Warioba kapiga chini wazo hilo kwasababu halikuwa na mantiki (logic) bali nia ovu iliyojificha miongoni mwao
Mwananchi kumsikiliza ni muhimu ila kuchukua au kuacha maoni yake ni suala jingine kuliko kutomsikiliza kabisa.
Yes ili kuchukua na kuacha lazima ufanye analysis katika hoja, ndio msingi wa Tume ya Warioba kukataa upuuzi wa mkataba kwasababu waliotaka hawakuweza kutetea hoja zao zenye hila.
 
Mkuu Mkandara with all due respect kuna eneo hulifahamu kabisa au unafanya makusudi kupotosha

Katiba ya Warioba inasema kutakuwa na Wabunge 75 wa Federal Government. Serikali washirika zitatafuta namna ya kuwapata. Mfano wa sasa ni Wabunge 5 kutoka Baraza la Wawakilishi wanavyopatikana Dodoma

Kuhusu majimbo 314 kwamba Bunge litakuwa na mara mbili ni upotoshaji au kutojua jua.

Zanzibar wana Baraza la Wawakilishi lenye wajumbe 50 tu. lakini Wabunge wao ni zaidi ya 100.
Sababu kubwa ni moja, Wabunge wanaokuja Dodoma wanalipiwa na Tanganyika hata kama watakuja 1000 haihusu uchumi wa Zanzibar. Wale 50 wanaolipiwa na SMZ ndio maana ni wachache

Leo ukiwaambia Wazanzibar walipie Wabunge wao wanaokuja Dodoma idadi itapungua kwasababu ni mzigo kwa SMZ. Kwabile wanalipiwa na fedha za Watanganyika basi wanagawa mitaa ya watu 3000 kuwa jimbo.
Kwa upuuzi hu urakosaje wabunge 314.

Kukiwa na Serikali ya shirikisho, Zanzibar watakuwa na utaratibu wao wa kupata Wabunge wa Muungano na BLW.
Tanganyika itakuwa na utaratibu wake. Kuna uwezekano kuwa 100 au 200 kwasababu ni utaratibu tu wa kugawa majimbo.

Watanganyika wataamua Bunge lao liwe na Wabunge wangapi si suala la kusema sasa ni 314 wakati huo watakuwa 628.

Marekani ina Wabunge wa majimbo 400 ikiwa na population ya watu milioni 300. Kwanini Tanzania iwe na Wabunge 300. I mean ni ulafi tu wa kujigawiwa majimbo si suala la utendaji au gharama.

Katika hao 314 unaosema wapo kutoka Zanzibar wanaowakilisha watu 3,500 na Wapo wanaowakilisha Watu 800,000 huku bara. Najaribu kulkuelewesha kwamba hakuna Formula ni ulafi tu, serikali za nchi husika zinapaswa kuamua zenyewe. Angalia mfano wa Kenya, seneti na Wabunge wanavyopatika
Nguruvi3, Naomba kitu kimoja. Unaponitaja katika hoja yako, vema na ustaarabu ukasubiri kwanza Majibu yangu unisome na unielewe vizuri badala ya kuweka maneno ambayo pengine wewe ndio hukuniewa.

Naomba nafasi nikujibu hoja yako ya kwanza.
 
Hii haiwezekani mpka katiba mpya iwepo na automatically itapunguza mamlaka ya Rais.

Mfano huwezi sema Bunge liwe huru ilihali kwenye katiba rais ana mamlaka ya kuvunja bunge kama likipinga bajeti au kusema huwezi kubaki bungeni bila chama maana yake ukipinga serikali wakikuvua uanachama sio mbunge tena maana hatuna wagombea binafsi. Maana yake hakuna bunge huru, sasa rasimu ya warioba iliondoa hizo clauses.

Pia Rais kuteua majaji moja kwa moja kunaondoa uhuru wa mahakama sasa ili kutenganisha mihimili lazima katiba mpya ili ipunguze hizo mamlaka za rais kuingilia mahakama. Imagine mpaka bajeti yao wanamlilia rais unategemea itakuaje? Ila katiba mpya inaweza demarcate authority, independence and accountability of the judiciary arm.

Hapa ni mutual exclusive, huwezi kuwa na mihimili huru na wakati huo huo Rais awe na mamlaka makubwa!!
Kuna mambo mawili nakubaliana na Mkandara
1. Kwamba kukiwa na separation of power automatic kuna checks and balances. Unajua kwanini siku hizi hatusikii kesi za uchaguzi! Ni kwasababu hakuna Imani na Mahakama na hiyo inaondoa pia legitimacy ya Bunge.
Matatizo ya October chanzo chake ni kutokuwa na Iman na utoaji haki, Wananchi wakawa desperate!

2. Nakubaliana pia kwamba haiwezekani kufanya mabadiliko na kupata separation of power kwa katiba iliyopo
Katiba ya sasa imeandikwa kumllinda na kumpa nguvu Rais. Nyerere aliwahi kusema ''kwa katiba hii ninaweza kuwa Dikteta'' akimaanisha Katiba inampa uwezo wa kufanya lolote. Katika mazingira hayo huwezi kufanya separation of power, unahitaji Katiba mpya.

3. Ghana wamefanikiwa katika suala la Mahakama. Mahakama inachagua Majaji na Watendaji wake na kumpeleka Rais majina ya walioteuliwa. Kazi ya Rais si kupitia au kuhojia, ni kua ''assent'' katika maana ya ''bless'' na siyo ''agree''. Katika ku bless Rais hana say yoyote, ni wino wake tu ! wala hana veto au nini.
Kenya walitambua hilo na jambo waliloanza nalo ni kuifanya Mahakama iwe huru kabisa. Wapo vizuri kuliko sisi
 
Waliotaka Muungano wa Mkataba ni wachache sana wakiongozwa na Marhum Seif.

Swali waliloshindwa kujibu ni moja, ni mkataba wa mambo gani! Tume ya Warioba ilibaini mkataba ulilenga kuafikiana mambo yenye manufaa kwa Zanzibar. Kwa mfano, Wazanzibar wanajua soko kubwa la biashara lipo bara. Wanatambua ili kufikia masoko mengine lazima wapitie bara. Kwamba, ajira za vijana wao ni bara. Gharama za ulinzi na mambo ya ndani ni kubwa kwao. Hivyo walitaka kuchagua baadhi ya mambo wanayonufaika nayo yawe ni ya mkataba ikiwemo umiliki wa ardhi.

Katika Mkataba Tanganyika hainufaiki na chochote, Mzee Warioba kapiga chini wazo hilo kwasababu halikuwa na mantiki (logic) bali nia ovu iliyojificha miongoni mwao

Yes ili kuchukua na kuacha lazima ufanye analysis katika hoja, ndio msingi wa Tume ya Warioba kukataa upuuzi wa mkataba kwasababu waliotaka hawakuweza kutetea hoja zao zenye hila.
Nianze kwanza na Mada yenyewe. Mada hii ilihusu hadaa ya muundo wa Serikali (Dola) na nikaeleza jinsi usivyokuwa huru nanhakuna separation of Power. Tukamaliza huko vizuri tu.

Ikaunganishwa na hitaji la Katiba Mpya ambapo mimi kwa mtazamo wangu ni kuchelewesha mabadiliko chanya tunayoyahitaji sasa hivi.l, kwa sababu Rasimu ya Warioba ilishindikana na tulianza vibaya kukusanya maoni ya Wananchi ambao naweza sema 50/50 hatutakubaliani kama zilivyo Siasa zenyewe.
Nakumbuka mwanzo tu, niliulizwa kama Rasimu ya Warioba inaweza kubadilisha mfumo mzima nikajibu, rasimu ni nzuri sana lakini ina changamoto zake. Na nikaelewa wapi ina utata. Likaja swala la Serikali 3, hivyo tumetoka kwenye muundo wa Serikali Kuu tukaingia kwenye Muungano.

Nikajibu kwa mawazo na Mtazamo wangu kwamba Serikali 3 zina gharama kubwa nikichukua Uhalisia wa hali tunayo kwenda nayo sasa hivi. Ndio nikaenda kutazama Bunge letu lina Wawakilishi wangapi kutoka Bara, nikakuta 314, na ndio nikaweka mara 2 ya hesabu ya Wabunge kutoka Bara itakayo kuwa katika kuunda Serikali 3 za Jamhuri.

Upande mwingine zitto junior, yeye akasema Wabunge watakuwa 75 tu, kwanza sikunuelewa na alipofafanua kwamba hesabu hiyo katimia Rasimu ya Wariba. Nikahoji kama Wabunge 75 wataweza kweli kuwakilisha Wananchi Mil.60 ikiwa leo tuna Wabunge 314 hakuna kinachoeleweka!

Kwa hiyo kama Rasimu ya Warioba ilitazama umuhimu wa kupunguza Majimbo ilihali nia na dhamira ya Wabunge ni kupeleka Maendeleo kwa wananchi hadi vijijini, sioni kama hiili litawezekana japo tutakuwa timekata gharama lakini tuta fail upande wa Maendeleo. Nikitambua uwezo, nia na uhalisia wa mazingira yetu tokana na Wabunge katika Uwakilishi wa Wananchi. Kwa hiyo, binafasi yangu sikubaliani na Wabunge 75 na nimeeleza kwa nini kulingana na muundo wa Mabunge duniani.

Inayofuata, labda nieleze kwankina kwa nini tena sikubaliani na maelezo uloyaweka hapo juu kuhusoana na Mapendekezonya Rasimu ukitaja jinsi gani muundo utakuwa. Nipe muda kidogo nikusanye data zangu, nitakujibu soon.

Naomba tena nafasi, unless kuna hoja hapa inayokizana na ulichoandika.
 
Ok, Naomba kitu kimoja kutoka kwenu nyote maana yawezekana mimi sikufuatilia rasimu ya Warioba ambayo imezungumzia Serikali 3.

Ni Sura au ibara gani ya Rasimu hiyo inazungumzia Muundo wa Serikali ya Tanganyika ikiwa mpaka sasa tunavyo jadiliana hapa hakuna Katiba ya Tanganyika!

Nikiisoma Sura au ibara hiyo itanisaidia kujenga hoja zangu maana napowasoma nashindwa kuelewa mmepata wapi huo muundo wa Serikali ya Tanganyika.

Haya please, ukumbi wako..
 
Hili ni swali kwa wahenga wa jukwaa hili la Siasa. Naomba pia ufafanuzi wake.

Ni Sura au Ibara gani ya Katiba ya JMT inayosema hivi: -

Serikali ina Mihimili mitatu.
1. Bunge -Parliament
2. Mahakama - Judicial
3. Serikali - Executive
Serikali Ina muhimili mmoja tu Executive
 
Ok, Naomba kitu kimoja kutoka kwenu nyote maana yawezekana mimi sikufuatilia rasimu ya Warioba ambayo imezungumzia Serikali 3.

Ni Sura au ibara gani ya Rasimu hiyo inazungumzia Muundo wa Serikali ya Tanganyika ikiwa mpaka sasa tunavyo jadiliana hapa hakuna Katiba ya Tanganyika!

Nikiisoma Sura au ibara hiyo itanisaidia kujenga hoja zangu maana napowasoma nashindwa kuelewa mmepata wapi huo muundo wa Serikali ya Tanganyika.

Haya please, ukumbi wako..
Kama ulimsikiliza Mzee Warioba , kulikuwa na miaka 4 ya kipindi cha mpito toka 2014 hadi 2018 kutoa muda
Huu ndio uliokuwa muda wa Tanganyika kutengeneza serikali yake kwasababu ya Zanzibar ipo.

Rasimu ya Warioba ilizungumzia mgawanyo wa Serikali 3 na muundo wa Serikali ya shirikisho. Rasimu haikuzungumzia muundo wa Serikali ya Tanganyika kwasababu katika kipindi cha mpito Watanganyika watatengeneza Katiba yao .

Muundo wa Serikali ya Tanganyika tunaousema ni MIFANO, ndio maana kila sentensi hasa mimi huanza kwa kuandika ''mfano''. Hakuna mtu anayejua muundo kwasababu haujajadiliwa

SI kazi ya Rasimu kujadili muundo wa Serikali Washirika, kilichotokea ni kutoa muundo wa Serikali kuu
Ilikuwa ni makusudi ili kulinda Muungano. Laiti Rasimu isingetoa muundo wa Serikalia kuu, maana yake kungekuwa na mvutano kati ya Tanganyika na Zanzibar. Rasimu ili 'pre empty contentious matter'' ili kulinda muungano.
 
Kama ulimsikiliza Mzee Warioba , kulikuwa na miaka 4 ya kipindi cha mpito toka 2014 hadi 2018 kutoa muda
Huu ndio uliokuwa muda wa Tanganyika kutengeneza serikali yake kwasababu ya Zanzibar ipo.

Rasimu ya Warioba ilizungumzia mgawanyo wa Serikali 3 na muundo wa Serikali ya shirikisho. Rasimu haikuzungumzia muundo wa Serikali ya Tanganyika kwasababu katika kipindi cha mpito Watanganyika watatengeneza Katiba yao .

Muundo wa Serikali ya Tanganyika tunaousema ni MIFANO, ndio maana kila sentensi hasa mimi huanza kwa kuandika ''mfano''. Hakuna mtu anayejua muundo kwasababu haujajadiliwa

SI kazi ya Rasimu kujadili muundo wa Serikali Washirika, kilichotokea ni kutoa muundo wa Serikali kuu
Ilikuwa ni makusudi ili kulinda Muungano. Laiti Rasimu isingetoa muundo wa Serikalia kuu, maana yake kungekuwa na mvutano kati ya Tanganyika na Zanzibar. Rasimu ili 'pre empty contentious matter'' ili kulinda muungano.
Shukran, Rasimu ya Katiba Mpya ni muundo wa Katiba ya JMT kwa hiyo zile hesabu mlokuwa mkitoa sii za kweli ila mnadhani Katiba ya Tanganyika inge au itakuwa hivyo sio?. Mpaka hapa tupo pamoja.

Sasa basi mlitakiwa mnisikilize miye kwa makini kwa sababu nina ufahamu muundo ya Serikali washirika na ndio maana nikatumia pia mifano yangu kwa lengi kama lenu. Haikuhitaji kubishana bali kuelimishana. Tuache hizi dhana palipo Ukweli.

Sasa tuanze na Ukweli sio mifano au dhana. On records Majimbo ya Tanzania Bara ni 272 na idadi ilofanya Wabunge kufikia 314 ni pamoja na wale walio chaguliwa na rais pamoja na viti maalum.

Na kule Zanzibar kuna majimbo 50 na kuna Wabunge wengine 5 wanao chaguliwa na baraza la wawakilishi hivyo idadi kamili ya Wabunge wa Zanzibar ni 55.

Na Bunge la Zanzibar linawakilishwa pia na Wabunge 50 halafu kuna wa rais na viti maalum kufikia idadi ya Wabunge 66+ Spika ni 67.

Kwa hiyo Zanzibar Wabunge wa majimbo ni 50 kwao na kwenye Jamhuri wana Wabunge 50 pia wa Majimbo. Hivuo hivuo kama tungekuwa na Tanganyika basi tungekuwa na Wabunge 272 wa Tanganyika katika Serikali ya Bara. Hivi ndio nilikuwa nikielezea

Na maadam Rasimu ya Warioba imetaja Bunge la Jamhuri kuwa na Wabunge 50 toka Bara na 20 toka Zanzibar halafu viti v5 nadhani vya viti maalum (walemavu n.k), ndio nikasema hilo halitapita wala halitawezekana. Sasa ndio umenifunua akili kwa nini Rasimu ilikataliwa wakati Bunge la Katiba likijadili Serikali 3. Hizi namba hazisomi kabisa..

Wee kwa akili ya Kawaida unadhani Viongozi wetu ambao wanapigania nafasi 272 za Ubunge wangekubali kuona Bunge litakuwa na viti 50 tu? Au Zanzibar kutoka viti 50 mpaka 20! Nanhuo Wabunge 50 Tanganyika na 20 Zanzibar mgawanyo wa Majimbo yake ungekuwaje?

Tuna mikoa chini ya 50 na tuna wilaya zaidi ya 50! Je, tungeandika upya jata mikoa na wilaya zake? Au ndio tutaelekeo kwenye Serikali za Majimbo?

Halafu mkuu wangu hoja ya wingi wa watu kwa jimbo tunayo sisi tu, nikupe mfano Wa Ontario ambayo kwa ukubwa wake karibu saaana sawa na Tanzania lakini Ontario ina Watu Mil. 16 na kuna Wabunge 124. Tanganyika yenu ina watu mil. 60 na Wabunge 272. Angalia tofauti hii.

Sasa nenda Ontario mpaka nje porini mashambani kuna barabara za lami, umeme na maji, huduma za Elimu na Afya za kumwaga.

Kwetu pamoja na wabunge kuwa 272 wanadai majukumu ni makubwansananfedha wanazolokea ndogo. Wabunge wenyewe wanaishi miji au mikoa mingine huenda tu majimbo wakati wa kampeni za Uchaguzi.

Kwa analysis hii ndogo tu ndio nasema hivi vitu haviwezekani tunapoteza muda badala ya kuchukua hatua za harala na muhimu Ibara ya 4 ya Katiba ya Jamhuri.

Mwisho, sijui kama unajua wenzetu wanatazama Ubunge katika Uwakilishi wao kama vile walimu wa Shule. Kwao wanatazama Mwalimu mmoja kwa Wanafunzi wachache max 45, ilihali sisi tunataka mwalimu mmoja kwa wanafunzi wengi max 100. Kwa haya mazoea yetu ndio maana tumeshindwa kufuta Ujinga. Na mnataka kuyapeleka kwenye Ubunge mtafutaje Umaskini?

Narudia kusema tena kama kweli mnataka kuuvunja Muungano wetu basi leteni hii habari ya Serikali 3 na mtakuja juta pia gharama zake. Tanganyika inabeba mIgo ambao hata kuutua itakuwa haiwezekani. 'cause I know how the system works.

Maasalaam
 
Shukran, Rasimu ya Katiba Mpya ni muundo wa Katiba ya JMT kwa hiyo zile hesabu mlokuwa mkitoa sii za kweli ila mnadhani Katiba ya Tanganyika inge au itakuwa hivyo sio?. Mpaka hapa tupo pamoja.
Tuelewane kwamba mifano tuliyotoa ilikuwa na maana moja, kwamba, Bunge unaloliona sasa halitakuwa hivyo
Sababu ni kwamba kutakuwa na Bunge la Shirikisho lenye viti 75 tu. Viti hivyo vitatoka kwa serikali washirika

Serikali washirika zitaamua kwa mujibu wa katiba zao mabunge yao yatakuwa na ukubwa gani.
On records Majimbo ya Tanzania Bara ni 272 na idadi ilofanya Wabunge kufikia 314 ni pamoja na wale walio chaguliwa na rais pamoja na viti maalum.
Kumbuka wa viti maalumu pia wanagawanywa kwa Zanzibar 1 usisahu hili
Na kule Zanzibar kuna majimbo 50 na kuna Wabunge wengine 5 wanao chaguliwa na baraza la wawakilishi hivyo idadi kamili ya Wabunge wa Zanzibar ni 55.
Viti maalumu ni wangapi?
Na Bunge la Zanzibar linawakilishwa pia na Wabunge 50 halafu kuna wa rais na viti maalum kufikia idadi ya Wabunge 66+ Spika ni 67.
Spika ana jimbo ni sehemu ya Wabunge namba si sahihi.
Kwa hiyo Zanzibar Wabunge wa majimbo ni 50 kwao na kwenye Jamhuri wana Wabunge 50 pia wa Majimbo. Hivuo hivuo kama tungekuwa na Tanganyika basi tungekuwa na Wabunge 272 wa Tanganyika katika Serikali ya Bara. Hivi ndio nilikuwa nikielezea
Hapa ndipo tunaachana! Zanzibar wana Wabunge kwasababu kuna structure. Tanganyika haijawa na structure hivyo si lazima kufanyia reference kile Wazanzibar walichoamua. Kuna Uwezekano Katiba ya Tanganyika ikaamua kuwa na Wabunge 100 au 500 ! Unapokosea wewe ni kudhani kwamba Tanganyika ni hii ya JMT! Kumbuka kwamba hakuna Katiba ya Tanganyika hivyo hatujui wangeamua nini. Ndio maana kukawa na kipindi cha mpito cha miaka 4 ili Tanganyika iwe na structure
Na maadam Rasimu ya Warioba imetaja Bunge la Jamhuri kuwa na Wabunge 50 toka Bara na 20 toka Zanzibar halafu viti v5 nadhani vya viti maalum (walemavu n.k), ndio nikasema hilo halitapita wala halitawezekana. Sasa ndio umenifunua akili kwa nini Rasimu ilikataliwa wakati Bunge la Katiba likijadili Serikali 3. Hizi namba hazisomi kabisa..
Unasahau kwamba ni serikali ya shirikisho. Nikupe mfano, Marekani kuna watu milioni 300 na Seneta 100
Kila state inawakilishwa na seneta 2 ili kuhakikisha uwakilishi sawa. Hatuhitaji kuwa na Wabunge 400 kwasababu serikali ya shirikisho ina mambo 7 tu kwa mujibu wa Warioba.

Serikali za nchi Washirika ndizo zitakuwa na Wabunge wengie kutokana na mipango yao.
Hata Marekani serikali kuu ina majukumu muhimu ndio maana Wizara kama ya Elimu wanasema ifutwe
Kazi za Elimu ni za state.
Wee kwa akili ya Kawaida unadhani Viongozi wetu ambao wanapigania nafasi 272 za Ubunge wangekubali kuona Bunge litakuwa na viti 50 tu? Au Zanzibar kutoka viti 50 mpaka 20! Nanhuo Wabunge 50 Tanganyika na 20 Zanzibar mgawanyo wa Majimbo yake ungekuwaje?
Hapana! ni hivi viti 50 ni vya shirikisho kama vile tunavyokuwa na viti 9 vya EAC.
272 Wangekaa kama Watanganyika wapange kwamba ni sawa> Ni pungufu ?

Tuna mikoa chini ya 50 na tuna wilaya zaidi ya 50! Je, tungeandika upya jata mikoa na wilaya zake? Au ndio tutaelekeo kwenye Serikali za Majimbo?
Katina ya Tanganyika ingeamua kama vile ya Zanzibar ilivyoamua. Leo SMZ inaweza kupunguza viti au kuongeza na hakuna wa kuhoji. Tanganyika ikiwa na katiba yake itaamua pia idadi ya viti. Ni suala la Katiba
 
Tuelewane kwamba mifano tuliyotoa ilikuwa na maana moja, kwamba, Bunge unaloliona sasa halitakuwa hivyo
Sababu ni kwamba kutakuwa na Bunge la Shirikisho lenye viti 75 tu. Viti hivyo vitatoka kwa serikali washirika

Serikali washirika zitaamua kwa mujibu wa katiba zao mabunge yao yatakuwa na ukubwa gani.

Kumbuka wa viti maalumu pia wanagawanywa kwa Zanzibar 1 usisahu hili

Viti maalumu ni wangapi?

Spika ana jimbo ni sehemu ya Wabunge namba si sahihi.

Hapa ndipo tunaachana! Zanzibar wana Wabunge kwasababu kuna structure. Tanganyika haijawa na structure hivyo si lazima kufanyia reference kile Wazanzibar walichoamua. Kuna Uwezekano Katiba ya Tanganyika ikaamua kuwa na Wabunge 100 au 500 ! Unapokosea wewe ni kudhani kwamba Tanganyika ni hii ya JMT! Kumbuka kwamba hakuna Katiba ya Tanganyika hivyo hatujui wangeamua nini. Ndio maana kukawa na kipindi cha mpito cha miaka 4 ili Tanganyika iwe na structure

Unasahau kwamba ni serikali ya shirikisho. Nikupe mfano, Marekani kuna watu milioni 300 na Seneta 100
Kila state inawakilishwa na seneta 2 ili kuhakikisha uwakilishi sawa. Hatuhitaji kuwa na Wabunge 400 kwasababu serikali ya shirikisho ina mambo 7 tu kwa mujibu wa Warioba.

Serikali za nchi Washirika ndizo zitakuwa na Wabunge wengie kutokana na mipango yao.
Hata Marekani serikali kuu ina majukumu muhimu ndio maana Wizara kama ya Elimu wanasema ifutwe
Kazi za Elimu ni za state.

Hapana! ni hivi viti 50 ni vya shirikisho kama vile tunavyokuwa na viti 9 vya EAC.
272 Wangekaa kama Watanganyika wapange kwamba ni sawa> Ni pungufu ?


Katina ya Tanganyika ingeamua kama vile ya Zanzibar ilivyoamua. Leo SMZ inaweza kupunguza viti au kuongeza na hakuna wa kuhoji. Tanganyika ikiwa na katiba yake itaamua pia idadi ya viti. Ni suala la Katiba
Mkuu nadhani unasahau kwamba Rasimu ya Warioba sio Katiba, ni Mapendekezo ya awali ya Katiba Mpya ambayo yalikwama. Kuna kukubalika ama kukataliwa kwa sura, ibara au hata vipengele vyake. Hii sio Katiba wala Hatujafika huko na hatutafika kweli, kama mkiendelea kulazimisha vitu visivyowezekana.

Nimesema Yaonyesha sasa, Muundo wa Serikali 3 ulipigwa chini kutokana na Bunge litakuwa na viti 75 tu! nikasema hili haliwezekani na ndio sababu pendekezo hili la Serikali 3 haikufanikiwa Bunge la Katiba.
Viongozi hawatakubaliana nalo na hauakisi uhalisia kuwakilishinwa Wananchi mil.60 kwa Uchache kiasi hiki. Watu wenyewe sijui kama kweli unatujua?

2. Kuhusu Spika wa Zanzibar, sii maneno yangu, imeandikwa kwenye mfumo wa Bunge lao kwamba Wabunge wa Majimbo wa kuchaguliwa ni 50, 7 Wa rais, 18 viti maalum na 1 Spika . Kosa langu ni jumla yao wote ni 76 sio 67 kama nilivyoandika awali.

3. Umesema Zanzibar wana structure kwa sababu wana Serikali yao, unashindwa kuelewa kwamba Wabunge 272 ndio wawakilishi wa Bara na Serikali Kuu. Kwa hiyo Bunge hili Bara inapiga ndege wawili kwa jiwe moja.

Asilimia 99 ya Bunge la Jamhuri ni maswala ya Bara aidha tuwe na Serikali yetu au hii ya Muungano. Technically, Bunge hili kwa Asilimia 99 ni mfumo wa kusimamia maswala ya Serikali ya Bara.

4. Kuhusu Senate ya Marekani, hawa sio sawa na Wabunge ni baraza jingine kabisa, kama nilivyosema katika mapendekezo yangu kwamba nasi tuwe na Baraza la Wazee (senate). Hakuna Sheria wala mikataba itapitishwa na Bunge pekee, lazima Baraza na Wazee nao wapitishe. Nadhani nimeeleza vizuri huko nyuma hakuna sababu ya kurudia rudia

5. Sielewi kwa nini bado hunielewi, nasema hivi kupendekeza Serikali ya Bara kuwakilishwa na Wabunge 50 tu Bungeni, pendekezo hili haliwezi kupita popote kwa sababu 2.

Ya kwanza Ubunge ni mradi wa Utajiri kwa viongozi, huwezi kuwaambia watoke 273 hadi 50 wakapitisha. Sawa nankumpa mwajiliwa mamlaka ya kufanya layoff akiwepo yeye mwenyewe. Pili, Ujue maswala ya Kitaifa hubeba mzigo wote wa Serikali shirikisho. Huko ndio kuna mijadala mizito sana kuliko Serikali shirikisho. Kawaida ilitakiwa Bara we care less what's happening in Zanzibar lkn sisi ndio wa kwanza kuitazama Zanzibar kisha tunajilinhanisha nao.

Wewe kama upo Marekani, utataka kusikia zaidi sera za Serikali ya Trump zaidi kuliko unapoishi. Na utapenda kuona mijadala mikali na Usimamizi "Check and Balance" toka Serikali Kuu kuliko Serikali shirikisho. Kwa sababu juu kukilega lega huku chini kunafuata tu. States unaweza kuhama lakini huwezi ikimbia Marekani.

Serikali Kuu ndio huleta impact kubwa kwenye maisha ya Wananchi. Policies za Kitaifa zinabeba taaswira ya nchi.

Mwisho, Zanzibar hawaamui wao idadi ya Wabunge wa Kuchaguliwa. Majinbo nfio hutoa Wabunge wa Kuchaguliwa. Ukisema Zanzibar itakuwa na Wabunge 20 ina maana Zanzibar itakuwa na Majimbo 20 ya kupiga kura, Bara nako Wabunge = Majimbo 50. Hizo nyongeza za sijui nafasi za Rais na viti maalum hazina Upande. Wanaweza fhaguliwa toka upande wowote wa Muungano.

Ok. Mkuu wangu naishia hapa. Uwe na Siku njema..
 
Mkuu nadhani unasahau kwamba Rasimu ya Warioba sio Katiba, ni Mapendekezo ya awali ya Katiba Mpya ambayo yalikwama. Kuna kukubalika ama kukataliwa kwa sura, ibara au hata vipengele vyake. Hiinsio Katiba wala Hatujafika huko na hatutsfika kweli mkiendelea kulazimisha vitu visivyowezekana.
Exactly! ni framework . Kitu kilichokuwa dhahiri ni kwamba 2 tier government system is unsustainable
Nimesema Muundo wa Serikali 3 ulipigwa chini kutokana na Bunge litakuwa na viti 75 tu! nikasema hili haliwezekani na ndio sababu pendekezo hili la Serikali 3 haikufanikiwa. Viongozi hawatakubaliana nalo na hauakisi uhalisia kuwakilishinwa Wananchi mil.60 kwa Uchache kiasi hiki. Watu wenyewe sijui kama kweli unatujua?
Si kweli, nadhani hukufuatilia mchakato. Kilichokwamisha ni muundo wa Serikali 3 siyo contents za Serikali 3
CCM Unguja hawakutaka Serikali 3. Vurugu zilianzia NEC CCM walipomtisha JK. Unakumbuka ' Zanzibar siyo nchi ya machotara" the rest is history
3. Umesema Zanzibar wana structure kwa sababu wana Serikali yao,
Zanzibar wana structure kamili kwasababu kila jambo la muungano lina 'parallel' structure
Ndio maana wanakataa miswada ya JMT hadi ipitie BLW
Hivi unajua hivi karibuni wameanzisha Jeshi lao. Nenda you tube uone
unashindwa kuelewa kwamba Wabunge 272 ndio wawakilishi wa Bara na Serikali Kuu. Kwa hiyo Bunge hili Bara inapiga ndege wawili kwa jiwe moja.
Ni makosa! na hapo ndipo shida inapoanzia. Huwezi kuwa Tanganyika na Tanzania at the same time! dude!
Hata kama utakubali ni la Tanganyika, kwanini Wabunge 77 wanaamua mambo ya Tanganyika
Kwanini Wabunge wa Zanzibar wafanye shughuli za kamati za Bunge maeneo ya Tanganyika.
Wabunge wa Zanzibar wana athiri kura ndani ya Bunge la Tanganyika
Asilimia 99 ya Bunge la Jamhuri ni maswala ya Bara aidha tuwe na Serikali yetu au hii ya Muungano. Technically, Bunge hili kwa Asilimia 99 ni mfumo wa kusimamia maswala ya Serikali ya Bara.
Serikali ya Tanganyika haikwepeki kwa sasa, it's a matter of time. I can bet kama SSH hatakubali Tanganyika iwepo, muungano utafia mikononi mwake. In fact ni dhaifu sana kuliko wakati mwingine
5. Sielewi kwa nini bado hunielewi, nasema hivi kupendekeza Serikali ya Bara kuwakilishwa na Wabunge 50 tu Bungeni, pendekezo hili haliwezi kupita popote kwa sababu 2.
Ya kwanza Ubunge ni mradi wa Utajiri kwa viongozi, huwezi kuwaambia watoke 273 hadi 50 wakapitisha.
Ni hivi wabunge 50 ni wa Federal kama wale 9 wa EAC.
273 ni Watanganyika labda iniambia hawatakubali kwa muundo wa Tanganyika.

Ili uelewe na kutochanganya mambo: Serikali 3 ina Tanganyika, Zanzibar na Shirikisho(Federal)
Federal ina mambo 7 tu ambayo ukiondoa Katiba na Msajili wa vyama yanabaki 5 ikiwemo Ulinzi, mambo ya ndani, mambo ya nje, Fedha na jingine moja. Serikali kuu inashughulika na mambo yenye common interest

Serikali za washirika zitakuwa na mamlaka zake na hizo ndizo zitaamua structure ya mabunge yao kutokana na uzito wa shughuli zao.




Mwisho, Zanzibar hawaamui wao idadi ya Wabunge wa Kuchaguliwa. Majinbo nfio hutoa Wabunge wa Kuchaguliwa. Ukisema Zanzibar itakuwa na Wabunge 20 ina maana Zanzibar itakuwa na Majimbo 20 ya kupiga kura, Bara nako Wabunge = Majimbo 50. Hizo nyongeza za sijui nafasi za Rais na viti maalum hazina Upande. Wanaweza fhaguliwa toka upande wowote wa Muungano.
Narudia tena, Zanzibar inaweza kuamua idadi ya Wawakilishi katika BLW kwa kadri inavyotaka. Hakuna chombo au taasisi inayoweza kuzuia kwasababu BLW lipo kwa mujibu wa Katiba ya SMZ 1984 toleo 2010.
Tofautisha kati ya Wabunge na Wawakilishi.

Pili, Serikali kuu kwa mujibu wa Warioba itakuwa na Wabunge 75. 50 kutoka Bara na 25 kutoka visiwani kama sikosei. Uchaguzi wa hawa 50 utazingatia matakwa ya Katiba ya Tanganyika, na hao 25 wa Zanzibar utazingatia katiba ya SMZ. Kila upande utaamua njia za kupata Wabunge wake!

Mfano, EAC imetoa nafasi za kila nchi kupeleka Wabunge Arusha,, haikusema wapatikane vipi. Kila nchi ina utaratibu wake wa kupata hao 9. Tanzania tunawachagua kupitia Bunge , Kenya , Uganda na Rwanda wana utaratibu wao.

Usichanganye upatikanaji wa Wabunge wa serikali za shirikisho na Wabunge wa serikali kuu.
 
Exactly! ni framework . Kitu kilichokuwa dhahiri ni kwamba 2 tier government system is unsustainable

Si kweli, nadhani hukufuatilia mchakato. Kilichokwamisha ni muundo wa Serikali 3 siyo contents za Serikali 3
CCM Unguja hawakutaka Serikali 3. Vurugu zilianzia NEC CCM walipomtisha JK. Unakumbuka ' Zanzibar siyo nchi ya machotara" the rest is history

Zanzibar wana structure kamili kwasababu kila jambo la muungano lina 'parallel' structure
Ndio maana wanakataa miswada ya JMT hadi ipitie BLW
Hivi unajua hivi karibuni wameanzisha Jeshi lao. Nenda you tube uone

Ni makosa! na hapo ndipo shida inapoanzia. Huwezi kuwa Tanganyika na Tanzania at the same time! dude!
Hata kama utakubali ni la Tanganyika, kwanini Wabunge 77 wanaamua mambo ya Tanganyika
Kwanini Wabunge wa Zanzibar wafanye shughuli za kamati za Bunge maeneo ya Tanganyika


Serikali ya Tanganyika haikwepeki kwa sasa, it's a matter of time. I can bet kama SSH hatakubali Tanganyika iwepo, muungano utafia mikononi mwake. In fact ni dhaifu sana kuliko wakati mwingine

Ni hivi wabunge 50 ni wa Federal kama wale 9 wa EAC.
273 ni Watanganyika labda iniambia hawatakubali kwa muundo wa Tanganyika.

Ili uelewe na kutochanganya mambo: Serikali 3 ina Tanganyika, Zanzibar na Shirikisho(Federa)
Federal na mambo 7 tu ambayo ukiondoa Katiba na Msajili wa vyama yanabaki 5 ikiwemo Ulinzi, mambo ya ndani, mambo ya nje, Fedha na jingine moja. Serikali kuu inashughulika na mambo yenye common interest

Serikali za washirika zitakuwa na mamlaka zake na hizo ndizo zitaamua structure ya mabunge yao kutokana na uzito wa shughuli zao.





Narudia tena, Zanzibar inaweza kuamua idadi ya Wawakilishi katika BLW kwa kadri inavyotaka. Hakuna chombo au taasisi inayoweza kuzuia kwasababu BLW lipo kwa mujibu wa Katiba ya SMZ 1984 toleo 2010.
Tofautisha kati ya Wabunge na Wawakilishi.

Pili, Serikali kuu kwa mujibu wa Warioba itakuwa na Wabunge 75. 50 kutoka Bara na 25 kutoka visiwani kama sikosei. Uchaguzi wa hawa 50 utazingatia matakwa ya Katiba ya Tanganyika, na hao 25 wa Zanzibar utazingatia katiba ya SMZ. Kila upande utaamua njia za kupata Wabunge wake!

Mfano, EAC imetoa nafasi za kila nchi kupeleka Wabunge Arusha,, haikusema wapatikane vipi. Kila nchi ina utaratibu wake wa kupata hao 9. Tanzania tunawachagua kupitia Bunge , Kenya , Uganda na Rwanda wana utaratibu wao.

Usichanganye upatikanaji wa Wabunge wa serikali za shirikisho na Wabunge wa serikali kuu.
Exactly! ni framework . Kitu kilichokuwa dhahiri ni kwamba 2 tier government system is unsustainable

Si kweli, nadhani hukufuatilia mchakato. Kilichokwamisha ni muundo wa Serikali 3 siyo contents za Serikali 3
CCM Unguja hawakutaka Serikali 3. Vurugu zilianzia NEC CCM walipomtisha JK. Unakumbuka ' Zanzibar siyo nchi ya machotara" the rest is history

Zanzibar wana structure kamili kwasababu kila jambo la muungano lina 'parallel' structure
Ndio maana wanakataa miswada ya JMT hadi ipitie BLW
Hivi unajua hivi karibuni wameanzisha Jeshi lao. Nenda you tube uone

Ni makosa! na hapo ndipo shida inapoanzia. Huwezi kuwa Tanganyika na Tanzania at the same time! dude!
Hata kama utakubali ni la Tanganyika, kwanini Wabunge 77 wanaamua mambo ya Tanganyika
Kwanini Wabunge wa Zanzibar wafanye shughuli za kamati za Bunge maeneo ya Tanganyika.
Wabunge wa Zanzibar wana athiri kura ndani ya Bunge la Tanganyika

Serikali ya Tanganyika haikwepeki kwa sasa, it's a matter of time. I can bet kama SSH hatakubali Tanganyika iwepo, muungano utafia mikononi mwake. In fact ni dhaifu sana kuliko wakati mwingine

Ni hivi wabunge 50 ni wa Federal kama wale 9 wa EAC.
273 ni Watanganyika labda iniambia hawatakubali kwa muundo wa Tanganyika.

Ili uelewe na kutochanganya mambo: Serikali 3 ina Tanganyika, Zanzibar na Shirikisho(Federal)
Federal ina mambo 7 tu ambayo ukiondoa Katiba na Msajili wa vyama yanabaki 5 ikiwemo Ulinzi, mambo ya ndani, mambo ya nje, Fedha na jingine moja. Serikali kuu inashughulika na mambo yenye common interest

Serikali za washirika zitakuwa na mamlaka zake na hizo ndizo zitaamua structure ya mabunge yao kutokana na uzito wa shughuli zao.





Narudia tena, Zanzibar inaweza kuamua idadi ya Wawakilishi katika BLW kwa kadri inavyotaka. Hakuna chombo au taasisi inayoweza kuzuia kwasababu BLW lipo kwa mujibu wa Katiba ya SMZ 1984 toleo 2010.
Tofautisha kati ya Wabunge na Wawakilishi.

Pili, Serikali kuu kwa mujibu wa Warioba itakuwa na Wabunge 75. 50 kutoka Bara na 25 kutoka visiwani kama sikosei. Uchaguzi wa hawa 50 utazingatia matakwa ya Katiba ya Tanganyika, na hao 25 wa Zanzibar utazingatia katiba ya SMZ. Kila upande utaamua njia za kupata Wabunge wake!

Mfano, EAC imetoa nafasi za kila nchi kupeleka Wabunge Arusha,, haikusema wapatikane vipi. Kila nchi ina utaratibu wake wa kupata hao 9. Tanzania tunawachagua kupitia Bunge , Kenya , Uganda na Rwanda wana utaratibu wao.

Usichanganye upatikanaji wa Wabunge wa serikali za shirikisho na Wabunge wa serikali kuu.
Daaah mimi naona.hatutaelewana. Kuna pahala nimesema ni Bara ndio walokataa Serikali 3? Kifupi mkuu wana CCM wote hawakubaliani na Serikali 3 kwa sababu ni harakati za wafuasi wa Hizbu (ZNP na ZPPP) kutaka Serikali ya Zanzibar huru. Walipewa nusu mkate sasa wanadai mkate mzima.

Hakuna mtu asojua hizi ndio zilikuwa Siasa za Maalim Seif na hata UKAWA wakaingizwa choo cha Kike, kiasi kwamba Lissuakaanza kudai kuwa hata Muungano wetu sio halali bali matakwa ya Nyerere aliye zoea vya Kunyonga! Nakumbuka vizuri sana.

Kifupi Mkuu wangu sitopenda kuendelea na Maswala ya Muungano kwa sababu nyie vijana wengi hamuijui Historia yetu. Hata nikijaribu vipi bado hamtanielewa..

Nakutakia siku njema.
 
Kifupi Mkuu wangu sitopenda kuendelea na Maswala ya Muungano kwa sababu nyie vijana wengi hamuijui Historia yetu. Hata nikijaribu vipi bado hamtanielewa.
Mkuu , unamkumbuka Nicodemus Banduka! Requiestcat in pace ni miongoni mwa Waanzilishi 20 wa CCM waliokaa Motel Agip. Kama sitakosea kadi yake ya CCM ni number 09.

Ahsante
 
Kifupi Mkuu wangu sitopenda kuendelea na Maswala ya Muungano kwa sababu nyie vijana wengi hamuijui Historia yetu. Hata nikijaribu vipi bado hamtanielewa
Kuna historia nyingine zaidi ya hii mliotuwekea kwenye mitaala ya shule?..
 
Mkuu , unamkumbuka Nicodemus Banduka! Requiestcat in pace ni miongoni mwa Waanzilishi 20 wa CCM waliokaa Motel Agip. Kama sitakosea kadi yake ya CCM ni number 09.

Ahsante
Sujakuelewa, inahusianaje?
Kuna historia nyingine zaidi ya hii mliotuwekea kwenye mitaala ya shule?..
Aaah mbona mmefichwa mengi sana! Imefika mpaka mnajifunza kwa Mohamed Said. Wa kulaumiwa ni Waasisi wetu kina Mwalimu, Karume na hata kina Haruub, Shivji, Warioba na wengine wengi tu hawakuandika true historia badala yake tunapigwa historia za kiimani kama Wayahudi.

Kama mngefundishwa ya Pan Africanism ungeyajua mengi.mfano, je unajua kwamba Uchaguzi mkuu wa Zanzibar, ASP ndio ilokuwa mshindi lakini Muingereza akawapa mshindi wa 2 kuungana na mshindi wa 3 kuunda Serikali ya Zanzibar na wakapewa Uhuru!

Kawaida ya chaguzi zote duniani, Mshindi wa kwanza kama ushindi wake haukufikia asilia 50 basi ni yeye hupewa nafasi kuunda Coalition. Akishindwa kupata wa kuungana naye Utawala utakuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (Minority rule) lakini PM anatoka Chama kilichoshinda. Laa utaratibu mwingine ni Uchaguzi unarudiwa kati ya Mshindi wa kwanza na Mshindi wa pili. Winner take all. Kwa Zanzibar haikuwa hivyo.

Mshindi ASP alitupwa nje, halafu kiongozi PM akawa mshindi wa 3 (Mohammed Shamte) chini ya Utawala wa Kifalme wa Sultan mshindi wa 2.

So, obvious Pan Africanism walisha jiandaa kwa ukombozi wa nchi zote kusini mwa jangwa. 1958 waliunda chombo kinaitwa PAFMESCA (Pan African Freedom Movement for East, South and Central Africa). John Okello hakuwa tu mpasua kokoto Kule Pemba, alikuwa Che wa East Africa. Trained for that porpose - Liberation of Zanzibar.

Je katika mitaala yenu, mmefundishwa niloyasema? halafu watu wanakaa kujadili Muungano wetu kwa hadith za wajukuu wakisema sijui CIA sijui Muingereza wakati hao ndio maasimu wakubwa walotugawa na kutugabaza..

Niishie hapa kwa leo..
 
Mkandara suala la Muungano sijui tunaliachaje kwa asili ya mada husika
Kama ikiwezekana kurekebisha sheria ikawepo ''checks and balances'' je, hiyo inatosha kumaliza tatizo la Muungano, na kama ndivyo ni kwa njia zipi. Na je muundo wa sasa wa Muungano ni sustainable?
 
Mkandara suala la Muungano sijui tunaliachaje kwa asili ya mada husika
Kama ikiwezekana kurekebisha sheria ikawepo ''checks and balances'' je, hiyo inatosha kumaliza tatizo la Muungano, na kama ndivyo ni kwa njia zipi. Na je muundo wa sasa wa Muungano ni sustainable?
Leo kidogo nimebanwa na majukumu, ila nitakujibu vizuri baadae. Maswala ta Muungano ukiyatazama vizuri ni KERO tu zinatusumbua hakuna jambo kubwa la Kiutendaji zaidi ya Uzanzibar na Utanganyika. Kero huleta karaha tofauti kabisa na Utawala bora.
 
Mkandara suala la Muungano sijui tunaliachaje kwa asili ya mada husika
Kama ikiwezekana kurekebisha sheria ikawepo ''checks and balances'' je, hiyo inatosha kumaliza tatizo la Muungano, na kama ndivyo ni kwa njia zipi. Na je muundo wa sasa wa Muungano ni sustainable?
Ok, nirudi kwenye Swali lako la Muundo wa Serikali za Muungano. Sio kwa asilimia 100 sustainable, Serikali Moja ingekuwa Sustanable lakini ndio haikuwa japokuwa Karume alitaka tuwe na nchi moja.

Lakini kati ya Serikali Mbili na Tatu, hii ya Mbili tulonayo ni bora zaidi ya Seeikali 3 kwa sababu, at least hii kuna vitu hutukera lakini bado tumefumgwa Kikatiba na Muungano wa nchi mbili (Unitary State) badala ya Shirikisho (Federal Union).

Serikali 3 ni sawa na wanandoa wanataka Separation wee kaa.chumba chako na mimi na kwangu.tutatumia wote sebule, choo na jiko as long nyimba ni yetu sote. Easier said, lakini Utakubali kuishi maisha kama haya? And for how long?

Makubaliano kama haya matokeo yake ndoa kuvunjika kirahisi kabisa kwa sababu within hizo separation days kutazaa Uhasama baina yao na the only option ni kutarakiana. Sijui kama unanielewa?

Nirudi kwenye hoja, watunwenfi wame doubt muundo huu kutolana na Kero za Muungano ambazo haziishi. Leo utasikia hili kesho lile ili mradi ni vijembe tu tunarushiana kama nyimbo za Taarab.

Na Hizi Kero za Wazanzibar tumekuwa nazo toka 1993 baada ya kufanya marekebisho ya Katiba yetu mwaka 1992, kupitisha mfumo wa Vyama Vingi na tuliongeza Mambo ya Muungano toka 11 na kuwa 22 ili kuboresha mshikamano wa nchi yetu kwani toka 1964 hadi 1992, Kero zilikuwa zetu sisi Bara maana kulikuwa na Vikwazo vingi kwa Watanganyika. Ilikuwa hata Mbara akitaka kwenda Zanzibar lazima ubebe Passport yake.

Baada ya kupitishwa kwa Vyama vingi na nyongeza ya Mambo ya Muungano, Kero zikageukia upande wa Wazanzibar ambao kwa Asili yao ni zao la Wabaguzi. Kama kuna Mzanzibar hapa ananisoma natanguliza radhi, lakini ntasema Ukweli daima.

Ukikutana na Mzanzibar hana Ubaguzi basi elewa huyo malezi yake hayakuwa Zanzibar ama mmoja wa Wazazi wake ni Mbara. Walizaliwa kwenye Ubaguzi wakakulia kwenye Ubaguzi sii rahisi kwao kuona dhambi katika Kugabuana.

Na sisi Wabara tukilamizika kuingia katika Ubaguzi basi ni Wabaya kuliko Wazanzibar kwa sababu ubaguzi wao husema sana huku wamejitenga nasi, Wabara watawakufuata popote ulipo na kwa vitendo.

Na kilichowakera zaidi Wazanzibar ni marekebisho ya KATIBA ya Jamhuri kutoka Mambo 11 ya Muungano hadi kufikia 22 na kiini cha Kero zao kimetokana na Uzawa wa Vyama vingi. CUF ilichangia sana kuzalisha Chuki ya Kisiasa baina ya Bara na Zanzibar.

Deep down adui na mgonvi mkubwa wa CUF ni ASP lakini hutumia kivuli cha Bara na CCM kwa sababu hawawezi kuwanyooshea kidole ASP moja kwa moja, mziki wake utakuwa mkubwa na Zanzibar hakutakalika.

Kwa hiyo, mkuu wangu wala msikereke na kelele za Wazanzibar, hawa wana possess psychological traits za Kibaguzi sio Political ideologies. Na binadamu wote sisi tuna elements ambazo zina align upande wa Liberali ama Uhafidhina. Sisi tuna nafasi ya kuchambua mambo haya Kisiasa, kwao wao ni Uzanzibar.

Naomba radhi yenu niachie hapa kwa leo..

Maasalaam
 
Back
Top Bottom