Gharama zinatoka wapi? Wakati walikua wanapunguza positions na departments zinazo overlap. Mfano sahivi mbona matumizi mfano gharama za serikali kama mishahara, posho, magari, safari yaani recurring budget zinapanda kila mwaka ilihali ni serikali mbili? Maana yake hakuna correlation kati ya idadi ya serikali na gharama kuongezeka au kupungua.
Mkandara haelewi suala la gharama. Kwasasa hivi kila Wizara na idara hadi jeshi zina mbadala Zanzibar.
Maana yake, Wizara kama Afya , Elimu , Utalii , mifugo n.k. ni za JMT kwa ubatizo , kiuhalisia ni za Tanganyika. Kama sivyo, kwanini tuna mbadala huo kule Zanzibar?
Mfano anaotoa wa Bunge anajichanganya sana, sina uhakika kama alielewa Rasimu ya Warioba.
Kwa mfano, Warioba anasema kutakuwa na Bunge la Shirikisho lenye Wabunge 75. kama sikosei 35 kutoka Zanzibar 40 kutoka Tanganyika. Kila mshirika ataweka utaratibu wa kupata Wabunge hao.
Mfano , Tanganyika itaweka utaratibu katika Wabunge 40 kila mkoa utachagua Mbunge mmoja. Watakaobaki 10 watapatikana kwa utaratibu kutoka Taasisi kama vyama vya Wafanyakazi, wakulima na makundi maalum. Gharama za Wabunge 40 zitalipiwa na zile za sasa za Wabunge 100 wa Zanzibar wanaokuja Dodoma kulala tu kwasababu 97% hayawahusu. Gharama zitaongezeka au kupungua!!!
Kuhusu Bunge la Tanganyika, nalo litakuwa na Wabunge kulingana na mgawanyo utakaowekwa si huu wa sasa. Ukiondoa Wabunge 100 wanaokuja kula na kula kutoka Zanzibar, Wabunge wa Tanganyika leo hii ni 300
Kuna uwezekano wa kuPunguza Wabunge kama tutazingatia population na si maeneo.
Gharama zitaongezeka vipi?
Ukiondoa Wabunge 100 kutoka Zanzibar unapunguza mzigo kwa Mtanganyika. Mbona Baraza la wawakilishi lina Wawakilishi 50 kwa Zanzibar ile ile.
Kwasasa Wabunge wa Zanzibar wanachaguliwa na watu 3,500 yaani Mbunge anakuja Dodoma anawakilisha watu wachache kuliko Faculty of law au CoE pale Chang'ombe wala si UDOM au MUHAS!
Pili, Wizara haziwezi kuongeza gharama kwasababu hadi sasa tunazo zile zile! Serikali ya shirikisho itachangiwa na Washirika katika Wizara zisizodi 3. Wizara zingine kama kilimo ni za Washirika
Labda gharama anayosema ni kwa Zanzibar kwasababu free ride ya kuleta Wabunge wanaochaguliwa na watu 3,500 haitakuwepo. Dezo la gharama za Muungano halitakuwep pia
Kitakachoua muungano ni mzigo anaobeba Mtanganyika. Mtanganyika analipa kodi kumlipa Mbunge kutoka Zanzibar aliyechaguliwa na watu wachache kuliko Diwani wa Tanganyika.
Mbunge huyo wa Zanzibar akija Dodoma hana mchango wowote ni haya ya YUDA.
Mbunge wa Znz anayechaguliwa na Watu 3,500 ana kura sawa na Mbunge wa Ubungo anayechaguliwa na watu 400,000. Mkandara anachanganya Umma eti kutakuwa na ongezeko la gharama.
Tena Mbunge wa Zanzibar anaweza kukwamisha Bajeti ya mambo ya Tanganyika yasiymhusu kama atakuwa amemaliza hoja ya YUDA.
Katika umasikini, ujinga na maradhi anayozungumzia Mkandara yupo aliyevuka bahari na idea moja tu YUDA! Gharama zake zinabebwa na Mtanganyika!