Mimi najua sababu moja kubwa Tume ya Warioba walipo kosea ni kujadili maoni ya Wananchi kuhusiana na tuunde Serikali ngapi? Kana sikosei
Tume ya Warioba iliundwa kuchukua maoni ya Wananchi. Kumbuka wenye Nchi si viongozi ni Wananchi. Nyerere aliwahi kuonya, msipuuze maoni ya Wananchi hata kidogo. Maoni ya Wananchi ndio nguzo ya Muungano.
Hadi Tume inaundwa ilishapita miaka 40 na viongozi waliona tatizo na kubaini hali si ''sustainable''
Hakuna Tume yoyote iliyoundwa ikaja na proposal tofauti na Warioba. In Fact miaka 20 baada ya Tume ya Nyalali kusema, maoni yale yale yalirudiwa na Tume ya Warioba, Wananchi wanasema
Warioba alimuuliza JK akamwambie go ahead knowing vyovyote itakavyokuwa, yeye atapigilia msumari hapo hapo..
JK alikumbuna na tatizo la Muungano. Katika watu waliodhoofisha ni yeye kwasababu hakutaka kuwa mkweli bali kuwapendeza Wazanzibar! Tatizo sasa ni kubwa kuliko alipokuwa kiongozi
Mtazamo wangu miye hili lisingekuwepo kabisa kwenye Rasimu ile, kwa sababu ni moja ya NGUZO kuu kabisa iloasisiwa na Wazee wetu toka 1922 hata kabla ya Mwalimu
Huwezi kufunika kidonda na taulo ukasema unatibu. Dawa ya kidonda ni kukifunua na kusafisha
Miaka 60 na ushee leo Muungano ni dhaifu kuliko wakati wowote. Uwezekano wa Muungano kuvunjika ni mkubwa kuliko kuimarika hasa zama hizi za ''zamu' yetu.
Kama sikosei swala la Serikali 3, ndilo lilomweka Marehemu Abdul Jumbe kifungo cha nje maisha Kigamboni na kumpelekea Mzee wetu Malecela balaa wakati ule Afro Shiraz ilijaa wana Mapinduzi wa African Association ya Zanzibar ambao hata Salim A Salim walimkataa kuwa rais wa JMT kwa imani yao kwamba hoja ya serikali 3 ni hoja ya wafuasi wa Hizbu na lengo lao ni kutengua Umoja wa Bara na Visiwani ulosababisha Mapinduzi ya 1964. Rasimu nzima ikapigwa vita.
Well, je, Jumbe, SAS n.k. kuwekewa vikwazo kume solve tatizo?
Tuliposimama leo hii, tumekalia kuti kavu. Muungano upo matatani japokuwa Viongozi wote wa mihimili yote wameapa kuitetea na Kuilinda Katiba! Na katika vitu vyote vilopewa kipaumbele zaidi ndani ya Utaifa wetu ni MUUNGANO.
Maadam tumekalia kuti kavu, tunapitia mitihani kama Wa South hawaamini kama walisaidiwa kuupata Uhuru wao. Generation hii ni Chako chako Changu Changu, njaa kali Na viongozi wengi wanavunja miiko yote waziwazi kuwajaza Wananchi CHUKI na HOFU. Leo tunashughulikiana wenyewe badala ya kutafuta suluhu ya matatizo yetu Kitaifa, tunaanza kugawana Kuti.
Hapana! Kwa miaka mingi Watanganyika hawakuwahi kuwa na tatizo na muungano. Tatizo limeanza baada ya Uzanzibar kuwa mkubwa kuliko Utanzania. Watanganyika wanajiuliza kipi hasa wanachonufaika nacho katika muungano walioubeba wenyewe?
Kama umepita mitandaoni leo kuna Mtanganyika analalamika kwamba Leseni yake ya udereva haitambuliwi Zanzibar. Trafiki anayeikataa analipwa na Wizara ya mambo ya ndani inayogharamiwa na Tanganyika. Leseni ya Tanganyika inakubalika Uganda, Kenya, Malawi, Zambia! Vipi ikataliwe Zanzibar
Ujinga kama huu unawafanya watu wajiulize, huu muungano ni wa kitu gani! na Watanganyika wananufaika na nini, na watakosa nini ikiwa haupo!