Hadaa ya Mihimili ya Serikali

Hadaa ya Mihimili ya Serikali

Mkandara

Platinum Member
Joined
Mar 3, 2006
Posts
15,904
Reaction score
9,244
Hili ni swali kwa wahenga wa jukwaa hili la Siasa. Naomba pia ufafanuzi wake.

Ni Sura au Ibara gani ya Katiba ya JMT inayosema hivi: -

Serikali ina Mihimili mitatu.
1. Bunge -Parliament
2. Mahakama - Judicial
3. Serikali - Executive
 
Naona swali limekuwa gumu kujibika kwa sababu Katiba yetu haisemi maneno hayo isipokuwa Ibara ya 4(1-3) inasema Shughuli zote za Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na mihimili hiyo kwa pande mbili za Muungano.

Hoja ya msingi hapa ni kujiuliza Serikali ambayo ina Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Inaongozwa na nani? Bila shaka jibu ni Rais wa Jamhuri, kisha ukienda kwanye Mhimili wa Serikali pia kiongozi wake ni rais.

Kwa hiyo, ile dhana ya kwamba Serikali ina mihimili mitatu inayojitawala ni dhana Potoshi kwa sababu neno Mihimili ni sawa na kusema MATAWI ya Serikali, na matawi haya hayapo huru kwa sababu yote yapo chini ya Mamlaka ya rais.

Huwezi kuwa na Bunge huru ikiwa rais na mawaziri wake ni sehemu ya Bunge, na huwezi kuwa na Mahakama huru ikiwa majaji wa Mahakama ni wateule wa rais. Huu ni muundo nadhani wa Kiingereza ambao Serikali yao Kifalme yenye mihimili mitatu chini ya Ufalme huo.

Tanzania ni nchi huru inayofuata misingi ya Utawala wa Kidemokrasia, hatuwezi kuwa na rais sawa na Mfalme. Hii ndio sababu ilonifanya niweke mjadala huu hapa kwenu kuujadili kwa kina kama kweli tunataka suluhisho la kudumu aidha kwa kuchukua muundo wa Marekani ambao Serikali kwao ni KATIBA ya nchi. Na wameipa Mamlaka kamili mihimili hii KUSIMAMIANA.

Bunge lao lina Wajumbe walochguliwa Ubunge na UMaseneta chini ya Uongozi wa Spika, mamlaka yake ni kutunga Sheria na kuisimamia Serikali. Hakuna mtumishi yeyote wa Serikali ndani ya Bunge lao.

Mhimili wa Serikali inaongozwa na rais ikiwajibika katika kutekeleza Sheria. Hakuna Mbunge yeyote ndani ya mhimili wa Serikali. Na Mahakama yao ikiongozwa na jaji mkuu mamlaka yake ni Kusimamia haki na kutafsiri Sheria za Bunge na Katiba. Hakuna mwakilishi wa Wananchi Bungeni wala mtumishi wa Serikali ndani yake. Ndio maama Mihimili yote hii ni HURU yenye Mamlaka kamili sawa (co-equal) hakuna alo juu ya mwenzako ili kudhibiti viongozi kulewa madaraka.

Haya miye nakaa pembeni nawaachia mjadala.. Samahani kama kuna makosa ya Kiuandishi
 
Huwezi kuwa na Bunge huru ikiwa rais na mawaziri wake ni sehemu ya Bunge, na huwezi kuwa na Mahakama huru ikiwa majaji wa Mahakama ni wateule wa rais. Huu ni muundo nadhani wa Kiingereza ambao Serikali yao Kifalme yenye mihimili mitatu chini ya Ufalme huo.
Sahihi,
Ufafanuzi kuntu..
Tanzania ni nchi huru inayofuata Utawala wa Kidemokrasia hatuwezi kuwa na rais sawa na Mfalme.
Utawala wa kidemokrasia kwa Tanzania hakuna, ni nadharia tu, kiuhalisia tuna mfumo wa kidikteta au kifalme.

Kurekebisha huo mkwamo ni vigumu kwa sababu unanufaisha watawala kibinafsi dhidi ya umma, ndiyo maana wapo tayari kufanya lolote, hata kuteka na kuua maelfu ya wananchi ili mfumo uendelee kubaki hivyo
 
Sio Serikali ni Dola inaundwa na mihimili mitatu ambayo ni.
1. Serikali.
2. Bunge
3. Mahakama
Haya maneno sikutunga mie, yapo kwa maandishi sehemu nyingi, isitoshe mkuu wangu neno Serikali na Dola fasihi yake ile ile, ukitafsiri Serikali utaambiwa ni Dola na Ukitafsiri Dola utaambiwa ni Serikali. Labda ule mhimili wa Serikali ndio ungeitwa Utawala kwa maana ya utelelezaji wa Sheria.

Kubwa zaidi niiojifunza kutoka Katiba ya Marekani utaona kwamba kila Mhimili utakuta lengo kuu ni SHERIA iwe utunzi, utekelezaji ama Uimamizi ambayo ndio huongoza Taifa lao. (Huwa tunasema -Kwa mujibu wa Sheria)

Nikafikiri kwa kina na kugundua kwamba hata kampuni au taasisi utaona jina lake lakini kinachowapa haki ya kuendesha shughuli zake ni Katiba yake. Hivyo kinachosimama juu ni Katiba ambayo ndio umetupa nchi yetu kuitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Je, ile Rasimu ya Katiba ya Warioba ingeweza kuleta suluhisho?
Mkandara
Katika Sura kama hii nadhani wameweka vema isipokuwa pale kwenye kumpunguzia rais Madaraka sijui abakie na wizara chache za serikali kusimamia. Tukimpunfuzia mamlaka yake tutayapeleka wapi? Hii itatuvuruga na kupata marais wengine pembeni wenye mamlaka ya juu.

Ukiwa na Bunge na Mahakama huru hakuna sababu ya kupunguza Madaraka ya rais maadam jukumu lake la uongozi unakuwa kwa mujibu wa Sheria. Nisichokubali miye ni rais kuteua viongozi wa Bunge na Mahakama bila Usaili, hii inampa fursa kuweka watu wake kusimamia sehemu ambazo zina mamlaka ya kumwajibisha.

Wabunge wakisha teuliwa majimboni ni jukumu lao kumpata Kiongozi baina yao, Marekani wao Majaji ni nafasi za kudumu haijalishi chama gani kimechukua madaraka moaka akifa mmoja ndio wanatafuta replacement. Bila shaka jawa Majaji huwa wamebobea Elimu ya Sheria na tafsiri zake.
 
Wewe ulishaamua kuwa chawa wa CCM, acha kutupotezea muda
Maadam mmesha nibatiza basi nakuwa Chawa kichwani mwao, wajikune vizuri vizuri halafu wajua Chawa huambikiza mpaka majirani.

Dhumuni hasa la Mada hii ni kuonyesha Mapungufu ndani ya Katiba yetu hasa sehemu nyeti ambayo watu wengi huwa hawaitazami wakilaumu Bunge na Mahakana kuwa mihimili hii halina meno bila kutafakari kwa nini hayo mapengo wanayo.

Na kama hatutarekebisha muundo tulonao, basi yeyite atakae kuwa rais wa JMT ataendelea kuwa Dikteta kwa mujibu wa Katiba hii. Nyerere aliwahi kutuasa juu ya Katiba hii ya mwaka 1977 lakini wengi hawakumuelewa.

Ni lazima Mihimili iwe Huru na haiweza kuwa Huru ikiwa Mawaziri watatokana na Ubunge. Rais kuwa sehemu ya Bunge na pia rais kuchagua Majaji ambao anaweza kuwaondoa kwa mamlaka alokuwa nayo. Hapa chini nitaweka Muundo wa Serikali ya Marekani ambao binafsi naupendekeza kulingana na mazingira yetu.

Maasalaaam
 
Please take your time to read this constitutional design vs our Constitution or of any other countries.

The United States government divides power through a dual system:
Separation of Powers among three co-equal federal branches, and Federalism, which divides sovereignty between the national government and individual states. This constitutional design prevents any single entity from monopolizing control and protects individual liberties.

1. The Three Branches (Separation of Powers)
The U.S. Constitution establishes three distinct branches, each with tailored responsibilities:
  • Legislative Branch: Headed by Congress, which includes the House of Representatives and the Senate. Its primary power is to make laws, declare war, control taxing and spending, and approve or reject presidential appointments.

  • Executive Branch: Headed by the President, and includes the Vice President and the Cabinet. Its primary power is to enforce the laws, command the armed forces, and conduct foreign policy.

  • Judicial Branch: Composed of the Supreme Court and lower federal courts. Its primary power is to interpret the laws and the Constitution, resolving disputes and overturning unconstitutional legislation.

2. Checks and Balances
To ensure one branch does not dominate the others, the system integrates checks and balances. For example, the President can veto legislation passed by Congress, but Congress can override that veto with a two-thirds vote. The President appoints federal judges, but the Senate must confirm them. The Supreme Court can declare laws passed by Congress to be unconstitutional.

3. State and National Power (Federalism)
The division of powers also dictates how the national government and state governments interact:
  • Federal Powers: The national government handles matters of national scale, such as national defense, coining money, and regulating interstate commerce.
  • State Powers: Powers not granted to the federal government are reserved for the states. State governments manage regional concerns like education, public safety (police and fire departments), and intrastate commerce.
  • Shared Powers: Both levels of government can concurrently exercise certain powers, such as collecting taxes and building roads.
 
Please take your time to read this constitutional design vs our Constitution or of any other countries.

The United States government divides power through a dual system:
Separation of Powers among three co-equal federal branches, and Federalism, which divides sovereignty between the national government and individual states. This constitutional design prevents any single entity from monopolizing control and protects individual liberties.

1. The Three Branches (Separation of Powers)
The U.S. Constitution establishes three distinct branches, each with tailored responsibilities:
  • Legislative Branch: Headed by Congress, which includes the House of Representatives and the Senate. Its primary power is to make laws, declare war, control taxing and spending, and approve or reject presidential appointments.

  • Executive Branch: Headed by the President, and includes the Vice President and the Cabinet. Its primary power is to enforce the laws, command the armed forces, and conduct foreign policy.

  • Judicial Branch: Composed of the Supreme Court and lower federal courts. Its primary power is to interpret the laws and the Constitution, resolving disputes and overturning unconstitutional legislation.

2. Checks and Balances
To ensure one branch does not dominate the others, the system integrates checks and balances. For example, the President can veto legislation passed by Congress, but Congress can override that veto with a two-thirds vote. The President appoints federal judges, but the Senate must confirm them. The Supreme Court can declare laws passed by Congress to be unconstitutional.

3. State and National Power (Federalism)
The division of powers also dictates how the national government and state governments interact:
  • Federal Powers: The national government handles matters of national scale, such as national defense, coining money, and regulating interstate commerce.
  • State Powers: Powers not granted to the federal government are reserved for the states. State governments manage regional concerns like education, public safety (police and fire departments), and intrastate commerce.
  • Shared Powers: Both levels of government can concurrently exercise certain powers, such as collecting taxes and building roads.
Lakini still inaonekana ni supporter wa hiki chama kinachokataa mabadiliko, I’m confused 🤔
 
Lakini still inaonekana ni supporter wa hiki chama kinachokataa mabadiliko, I’m confused 🤔
Wee shabiki sio muumini wa Itikadi.i Wanasema kwa Mwana Yanga kumsifia Chama lazima uwe supporter wa Simba!

Mimi nautazama mpira kama umavyochezwa, naweza msifia Chama kulingana na nafasi anayocheza au Pacome kwa sababu hiyo hiyo. Over all Mimi hutqzama uchezaji wa timu inayo utafuta Ubingwa na kwa mbinu gani sio mchezaji.

CCM ina mapungufu yake, Chadema vile vile, ACT, NCCR na wengineo wote wana Mapungufu lakini wote wamegoma kutafuta sababu isipokuwa kutafuta Mchawi nani alofukia kichwa cha mbuzi Uwanjani, matokeo yake wanataka uwanja ubadirishwe.

This is where I come in..
 
Naona swali limekuwa gumu kujibika kwa sababu Katiba yetu haisemi maneno hayo isipokuwa Ibara ya 4(1-3) inasema Shughuli zote za Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na mihimili hiyo kwa pande mbili za Muungano.

Hoja ya msingi hapa ni kujiuliza Serikali ambayo ina Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Inaongozwa na nani? Bila shaka jibu ni Rais wa Jamhuri, kisha ukienda kwanye Mhimili wa Serikali pia kiongozi wake ni rais.

Kwa hiyo, ile dhana ya kwamba Serikali ina mihimili mitatu inayojitawala ni dhana Potoshi kwa sababu neno Mihimili ni sawa na kusema MATAWI ya Serikali, na matawi haya hayapo huru kwa sababu yote yapo chini ya Mamlaka ya rais.

Huwezi kuwa na Bunge huru ikiwa rais na mawaziri wake ni sehemu ya Bunge, na huwezi kuwa na Mahakama huru ikiwa majaji wa Mahakama ni wateule wa rais. Huu ni muundo nadhani wa Kiingereza ambao Serikali yao Kifalme yenye mihimili mitatu chini ya Ufalme huo.

Tanzania ni nchi huru inayofuata misingi ya Utawala wa Kidemokrasia, hatuwezi kuwa na rais sawa na Mfalme. Hii ndio sababu ilonifanya niweke mjadala huu hapa kwenu kuujadili kwa kina kama kweli tunataka suluhisho la kudumu aidha kwa kuchukua muundo wa Marekani ambao Serikali kwao ni KATIBA ya nchi. Na wameipa Mamlaka kamili mihimili hii KUSIMAMIANA.

Bunge lao lina Wajumbe walochguliwa Ubunge na UMaseneta chini ya Uongozi wa Spika, mamlaka yake ni kutunga Sheria na kuisimamia Serikali. Hakuna mtumishi yeyote wa Serikali ndani ya Bunge lao.

Mhimili wa Serikali inaongozwa na rais ikiwajibika katika kutekeleza Sheria. Hakuna Mbunge yeyote ndani ya mhimili wa Serikali. Na Mahakama yao ikiongozwa na jaji mkuu mamlaka yake ni Kusimamia haki na kutafsiri Sheria za Bunge na Katiba. Hakuna mwakilishi wa Wananchi Bungeni wala mtumishi wa Serikali ndani yake. Ndio maama Mihimili yote hii ni HURU yenye Mamlaka kamili sawa (co-equal) hakuna alo juu ya mwenzako ili kudhibiti viongozi kulewa madaraka.

Haya miye nakaa pembeni nawaachia mjadala.. Samahani kama kuna makosa ya Kiuandishi
Uko AG haendi bungeni??
 
Kwa Marekani haendi wao Bunge wanaita Congress. Nchi nyingine chini ya tawala za Kifalme au Waziri Mkuu ndiye kiongozi wa Serikali nadhani AG anakwenda.

Muhimu kwetu sisi ni kutazama Mfuundo gani unatifaa zaidi kutokana na hali ya Urumishu na Kisiasa nyumbani.
 
Hili ni swali kwa wahenga wa jukwaa hili la Siasa. Naomba pia ufafanuzi wake.
Asante kurejea kihenga,
Ni Sura au Ibara gani ya Katiba ya JMT inayosema hivi: -

Serikali ina Mihimili mitatu.
1. Bunge -Parliament
2. Mahakama - Judicial
3. Serikali - Executive
Hili jambo tuliisha lijadili sana humu Nani Zaidi Kati ya Bunge na Mahakama?!. The Doctrine of "Separation of Powers" Nothing, Just a Myth!

Hali hii ni. kufuatia tulipopata uhuru ile 1961, katiba ya uhuru ilitoka UK, Malkia ndie alikuwa the head of State, Waziri Mkuu the head of the Government, Spika the head of the legislature, na CJ the head of the Judiciary,

Kazi zao zilikuwa Bunge kutunga sheria, Mahakama kutafsiri sheria na Serikali kutekeleza sheria. Bunge linaundwa na Malkia na Kuvunjwa na Malkia, CJ anateuliwa na Malkia na kuidhinishwa na Bunge, Spika anachaguliwa na wabunge .

Mfumo huu unalifanya Bunge kuwa na nguvu kuisimamia serikali, CJ ana nguvu ya kulizuia Bunge na serikali.
Mwaka 1962, tukawa Jamhuri, yale madaraka yote ya malkia, akapewa President, na madaraka yote ya PM, akapewa president, hivyo sasa president akawa an executive president mwenye madaraka yote, rais wa kifalme. Rais akawa ndio kila kitu! kama nilivyo eleza hapa Je, wajua kuwa Rais wa JMT ndie Serikali, Bunge na Mahakama? Yuko juu ya Mihimili yote 3. Je, kuna uwezekano Rais wa JMT pia yuko juu Katiba?

Ile siku nimemuuliza JPM swali hili Ikulu,
View: https://youtu.be/Ta0URHvUlko?si=r3IMbnd_90GeZHEu
Akanijibu kuna mhimili, umejichimbia chini zaidi,

Bunge la Tanzania ni Bunge Zuga Tuu!, halitungi sheria, sheria zote zinatungwa na serikali, kisha zinapelekwa bungeni kuwa rubber stamped na Bunge kuzuga limetunga sheria, Je, Bunge letu ni Bunge Butu?. Angalia Bunge la Uingereza lenye meno linavyong'ata Serikali. Je, Kuna ubaya tukiiga?

Nishauri PreGE2025 - Watanzania tusiruhusu tena Bunge Kibogoyo dhaifu kama hili, lisilo na Meno, kukosa Kambi ya Upinzani na kushindwa kuisimamia Serikali kikamilifu!

Nimeandika sana humu kuhusu hili Bunge.
  1. Wabunge Wetu wa Ajabu!, Wanaachaje Bunge Lijipendekeze Kwa Serikali!, Wanajua Wajibu Wao?. Check 'n' Balance Itoke Wapi?
  2. Sehemu ya Pili: Je, Bunge letu tukufu linajipendekeza kwa Serikali?
  3. Bunge letu ni Bunge la ovyo? Bunge linafanya Uhuni? Wabunge Wetu ni Wahuni? Tumshauri Spika naye aanze kuita Watu kwenye Kamati, au waachwe tu?
  4. Watanzania tutaendelea kusubiri mpaka lini Bunge likitunga Sheria batili na kuuchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu? Tufanye nini?
  5. 1780702626727.png Je, wajua kuwa Rais wa JMT ndie Serikali, Bunge na Mahakama? Yuko juu ya Mihimili yote 3. Je, kuna uwezekano Rais wa JMT pia yuko juu Katiba?
  6. Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?
  7. 1780703117368.png
  8. Je, Bunge Litimize Wajibu Wake KikamiliIfu Ikiwemo Kutunga Sheria, Au Liendelee Kuwa "Rubber Stamp" ya Kupitishia Miswada ya Serikali Bila Kuhoji?
P
 
Shukran sana, unajua sikuwepo hapa kijiweni mida na dhumuni langu haswa ni kutafuta suluhisho bora zaidi, na ndio maana nikaanza na kuuliza swali.

Hata nilipokosa majibu nilirudi kuhitimisha dhamira yangu kwa sababu watu wengi wanalilalamikia Bunge kuwa butu wakati hawajui Bunge hilo hilo ni sehemu ya Serikali (Executive). Na nikaeleza pia kuhusu Mahakama zetu huwezi mlalamikia CJ ambaye mhimili wake upo dhani ya Serikali.

Nimepitia muundo wa Serikali nyingi kutazama muindo yao lakini kote nilikutana na hitilafu za Kifalme ama PM pamoja na CJ kuwa sehemu ya Bunge. Hapa huwezi kupata 'Separation of Power' bali ni nchi ambazo wana Utaifa na walindana wenyewe.

Kutokana na experience tulizopitia toka wakati wa Mwalimu hadi Sasa, njia pekee tunayoweza kupata mabadiriko ya kweli ni kuanza na muundo mpya wa Utawala wetu ili tuwe na Separation of Power katika mihimili yetu na muundo pekee unaoswihi kisheria katika mazingira yetu ni huu wa Marekani.

Nilitegemea zaidi kutoka kwenu wakongwe kujadilli muundo huo zaidi ya kuitafuta Katiba Mpya kwa mijadala ya Serikali ngapi, sijui Tume Huru wakati rais wa nchi Ndiye aloshika Mpini. Rasimu ya Warioba ilikwama kwa sababu hii na sidhani kama itakuja kurudishwa mezani while the President is a supreme leader.

Kwa muundo tulonao, katu hatuwezi kuwa na Bunge Huru wala Mahakama huru ikiwa Serikali ina mkono wake ndani ya Mihimili hii. La ziada labda badala ya sisi pia kuwa na Baraza la Senate sisi tuunde Baraza la Wazee kama ilivyo kwa Zanzibar wao.l mbali Baraza la Wawakilishi wana Baraza la Mapinduzi.

Itasaidia sana pale Bungeni haipiti Sheria yeyote kwa kutegemea Wabunge, lazima Baraza la Wazee nao wapitishe na wanaweza ku veto au kumhoji rais kwa maamuzi yeyote yanayoonekana kinyume cha Katiba.

Maasalaam
 
Dola ndo Ina Mihimili Mitatu siyo serikali

Sema serikali inaingilia sana mihimili Mingine
Mara Nyingi Serikali ya Tanzania /Serikali Kuu imeonekana kuingilia mihimili mingine - Bunge na Mahakama. Kumbuka Tanzania ina "separation of powers" kwenye katiba, lakini kwenye vitendo wakati mwingine mistari imekuwa ukungu.

mfano tu hata bila kuchimba sana

1. Kuingilia Bunge
1. 2016-2020 - Kusimamisha wabunge na kufuta hotuba
Spika wa Bunge alipiga marufuku wabunge kadhaa wa upinzani kusema Bungeni kwa kipindi kirefu. Hoja ilikuwa "kutunza heshima ya Bunge". Wabunge kama Tundu Lissu, Zitto Kabwe, Halima Mdee walinyimwa haki ya kuzungumza kwa miezi. Hapa Serikali kupitia Spika ilionekana kudhibiti mjadala wa Bunge.

2. 1992 - Katiba ya Vyama Vingi
Mchakato wa kuleta vyama vingi ulisukumwa sana na Nyerere wakati wa Rais Mwinyi + CCM. Bunge lilipitisha sheria haraka sana baada ya kamati ya Nyalali kutoa mapendekezo. Wakosoaji walisema Bunge lilikuwa "rubber stamp" - lilipitisha tu bila mjadala wa kina. Lakin ndo Mpaka sasa inatutesa

3. 2019 - Sheria za Bunge kuhusu vyombo vya habari na NGOs
Bunge lilipitisha sheria za Media Services Act na sheria za NGOs ambazo zilipa Waziri madaraka makubwa ya kufunga magazeti/kuvuta leseni. Mahakama baadaye ilipinga baadhi ya vifungu, lakini awali Bunge lilikuwa limepitisha kile Serikali ilitaka.

2. Kuingilia Mahakama
1. 1994 - Kesi ya James Mapalala vs AG
Mahakama Kuu iliamua kuwa kifungu cha katiba kinachozuia vyama vya siasa kisipitishe mgombea mmoja ni kinyume na katiba. Serikali ilikasirika sana. Baada ya hapo kulikuwa na mjadala mkubwa wa "Mahakama inakiuka Bunge". Ilionyesha mgogoro wa mihimili.

2. 2017-2018 - Kesi za uhaini na "sedition"
Wanasiasa na wanaharakati kadhaa walipeleka mahakamani kwa kesi za uhaini. Wanaharakati wa haki za binadamu walisema mahakama ilikuwa inatumika "kunyamaza" wakosoaji. Mfano: kesi za Lissu, Freeman Mbowe. Serikali ilikanusha, ikasema ni utekelezaji wa sheria tu. Lakin Samia na Magufuli wana mkono kwenye kesi za Kipuuzi hizo

3. 2006 - Teule la Majaji
Rais ana katiba uteue Jaji Mkuu na majaji wa Rufaa. Wakati mwingine uteuzi huu ulilalamikiwa kuwa "kisiasa". 2006 Rais Kikwete alipoteua majaji kadhaa bila kushauriana sana na Tume ya Huduma za Mahakama. Wanashiria walisema inathiri uhuru wa mahakama.

4. 2020 - Kesi ya Kupinga Matokeo ya Uchaguzi
Baada ya uchaguzi 2020, kesi kadhaa zilizopinga matokeo zilitupiliwa mbali na mahakama kwa "technicalities". Upinzani ulisema mahakama ilikuwa inaogopa Serikali. Jaji Mkuu alijibu kuwa mahakama inafanya kazi kwa mujibu wa sheria.

Mambo 3 ya kuelewa:
1. Katiba inaruhusu kuingiliana kidogo: Rais anateua Jaji Mkuu, Bunge linapitisha bajeti ya mahakama. Hivyo "kuingilia" kabisa na "kuingiliana kwa utaratibu" ni tofauti.
2. Uhuru wa Mahakama umeimarika zaidi: Tangu 2000, mahakama imekuwa ikipinga Serikali kwenye kesi kadhaa kama kesi za ardhi, haki za binadamu. Lakin simu zinapigwa toka juu! Mfano juzi tarehe 2/06/2026 Simu kutoka kwa msaidizi wa Samia alimpigia afisa mkuu wa Magereza na pia akipiga kwa Hakimu kujiridhisha kuwa je Lissu wamuachie kwa Mbinu gani! Mkuu wa Gereza yeye hakuwa na la kusema anasema TUNATEKELEZA MAAGIZO YATOLEWAYO MKUU TUNASUBIRIA

3. Tafsiri inatofautiana: Serikali husema "tunatekeleza sheria", Wakosoaji husema "ni kuingilia". Hivyo serikali ujificha kwenye kutekeleza sheria kumbe wanaingilia mahakama.


Britanicca
 
Back
Top Bottom