Habib Mchange akamatwa na Polisi...!

Habib Mchange akamatwa na Polisi...!

Status
Not open for further replies.
Mkuu Molemo,
Kweli hii ni breaking news? Naona mmeamua kuchafuana.

Ili kukanusha kitu lazima ufanye utafiti upate data zitakazokuwezesha kukanusha sio unabwatuka tuu kama mlevi, taarifa umepewa ndio hiyo sasa unachobisha nini? na una taarifa zingine tofauti na hizo??
 
Hakuna uadilifu hakuna kumbe ndiyo maana ametimuliwa, chama chochote kisiwachukue wale wote wanaotimuliwa na chama kingine ili wakae kijiweni wajifunze.

View attachment Mobile picking.bmp

Wizi mfukoni.jpg
 
Hajaiba wala nini ni chuki binafsi.labda kategeshewa na kununua simu ya wizi

Umejuaje mkuu kwamba hakuiba ila kategeshewa!!?binafsi siamini sana hizi taarifa ila nasimama kwa taarifa ambayo iliyopo.
 
Pole Mchange, sitashangaa akimtuhumu Heche kuwa ndiye kakuchongea polisi.
Mkuu Molemo hiyo simu aliikwiba kwa nani na ina thamani ya shilingi ngapi?
 
Last edited by a moderator:
Wizi wa simu? Haingii akilini hata kama ni masalia! Kuna lingine jambo!
 
Akalitafute janga lenzake li Kisandu au Janga Mwampamba.Laana ya wazee wliomlea.Alidhani anamkomoa nani? Sisi tupo tunasubiri jioni twende kwenye vijiwe vya kahawa na Visheti ye akae huko Nondo.
 
Hajaiba wala nini ni chuki binafsi.labda kategeshewa na kununua simu ya wizi

Tutasikia mengi ila hili nalo linawezekana wakati mwingine watu tunanunua vitu vizuri na vya dhamani kubwa kwa bei nafuu tukijua tumepata kumbe simu iko connected kwenye laptop ukiitumia tuu aliyeibiwa anajua uliko anakukamata na Polisi na wewe unaonekana mwizi.

Kama ni kweli kijana amekamatwa basi nampa Pole.Nafikiri ni kijana mahiri wa kujibu hoja hapa na ninaamini atakuja haraka tuu kutoa maelezo yake japo huwa hanyooshagi kiswahili,naamini mara tuu atakapoachiwa na wadogo zake Kova kama kweli wamemweka chini ya Ulinzi atakuja hapa.Au kina Shoza na Drogba wanaweza kueleza ukweli wa jambo hili kuondoa utata.
 
Vijana waliohukumiwa wote niwale wanaotokea Mbeya, Mbozi na Kibaha. Wakati Vijana wa Kilimanjaro wameachwa kwa madai wao wametoa ushirikiano.

Waliohukumiwa ni:
_Mtela Mwampamba-Mbozi, Mbeya
_Habib Mchange-Kibaha, Pwani
-Juliana Shonza-Mbozi, Mbeya
-Joseph Kasambala – Mbeya mjini (kasimamishwa)
- GWAKISA Mwakasendo –Rungwe, Mbeya (kasimamishwa)

Pamoja na wanachama watatu waliopo Mbeya mjini waliofukuzwa uanachama.

Waliosamehewa ni:
_Ben saanane-Kilimanjaro
_Exaud Mamuya-Kilimanjaro.

Hii ni dhamira ya wazi kabisa kwamba CHADEMA sasa ni chama cha kikanda
, Viongozi wa CHADEMA wanatumika kutangaza ukanda kwa watanzania.

Kwa maana hiyo wale wote wasio wa kaskazini ndani ya Chadema tusitegemee kutendewa haki.

source; juliana shonza
 
Sioni ajabu kwa yeye kufikishwa polisi ila ajabu ninayoipata ni kesi hiyo ya kuiba simu.Kama ni kweli basi ni aibu kubwa sana kwa wote walio karibu nae.
 
Vijana wa CCM hatutaki kuwaona kabisa hawa makahaba wakisiasa hawana nafac kabisa CCM hata ya Balozi wa Nyumba kumi ama ukuu wa Kaya. Kama Viongozi mafisadi watawapokea ama kuwaunga mkono hawa utakuwa ni upuuzi mwingine kwa CCM yangu hawa ni type ya le mutuz hawastahili kabisa kuwa CCM ya Nyerere
Hakuna uadilifu hakuna kumbe ndiyo maana ametimuliwa, chama chochote kisiwachukue wale wote wanaotimuliwa na chama kingine ili wakae kijiweni wajifunze.

View attachment 79514

View attachment 79515
 
Siasa za kuchafuana sio mpenzi hata kidogo
 
Pili naomba kuweka wazi kwambanatarajia kuomba ufafanuzi wa kikatiba juu ya shutuma zilizotolewa kwenye vyombo vya habari dhidi yangu na bwana Wegesa Suguta (John heche) ili aseme ni aminisho lipi la kuthaminisha na kusakidikisha mtazamo wa maono yake ili bongo za watanzania zijue ukweli. Mimi Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA natangaza rasmi Mtela Mwampamba na Habib Mchange ni wanachama hai na halali wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
wewe ndio tatizo kubwa ndani ya chama. unatumika vibaya kijana
Ni lazima niwe Tatizo kwenu...na sina dalili ya kuacha kuwa Tatizo katika siku za usoni
ni aib kwa kijana kama wewe kuwa na akili ya kizee. ukikua utaacha.

Ulipofukuzwa ukapotea underground ukaja ukafungua ID juzi tarehe 11/01/2013 na kujiita Osamamtanzania.Kama kukua ndiyo kukubali kuwa Kuwadi na Msaliti kwa CHADEMA basi sitaki kukua kwa aina hiyo na akili hizi hizi ndizo zinazofaa.Hizo nyingine zizitaki
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom