HHP ameondoka mwenyewe kwenye system. Huwezi kusema anaongea haya kwa vile upepo hauko upande wake.
Siku anaandika barua ya kujiuzulu na kwachana upepo ulikuwa upande wake.
Kitu ambacho huna control nacho ndio upepo umekuendea vibaya. Kwa saab hatuna control na hali ya hewa. Usitumie metaphors and idioms usizozielewa vizuri, zinakufanya uonekane wa ovyo.
Polepole ametuma shock waves nchini kwa saab amewaonyesha CCM na serikali kwamba kumbe nguvu ya hela na vyeo ina mahala huwa inakwama.
Si kila mtu, si watumishi wote na makada na wajumbe wa NEC za wilaya mpaka Taifa, na wabunge na mawaziri na watunza siri za nchi wooooote nchini unaweza kuwanunua on demand, pale unapotaka, kwa kuwapa vyeo na hela na landcruiser la serikali na diplomatic passport na kuitwa mheshimiwa kila ukiingia msibani na harusini na kanisani watu wanasimama.
Kumbe sio wote watakubali uwaburuze kama nguruwe na kuwaagiza wauze nchi yao na kusaliti wenzao kwa vyeo na hela za kuhonga wajumbe na wabunge. Kuna siku waziri au mwanajeshi mtunza siri atasanuka mabaya zaidi na atakinukisha pakubwa zaidi.