mwanakwetu
Member
- Mar 30, 2008
- 89
- 14
Global Publishers kwa kushirikiana na Clouds group wanaanda tamasha la kuwahamasisha wananchi kuwa wazalendo kwa kile walichodai kuchafuliwa kwa hali ya hewa kulikosabaishwa na maandamano na kauli za wanasiasa dhidi ya serikali hivyo wananchi kupoteza imani kwa serikali yao. Tamasha litafanyika viwanja vya Biafra, tarehe 19/03/2011 kuanzia saa 5 asubuhi na kingilio ni bure.
Swali langu wametumwa na nani kuwafundisha wananchi uzalendo? wakati wote walikuwa wapi wakashindwa kufundisha wananchi uzalendo wa kupinga ufisadi na unyonyaji kwa wananchi? Kuna haja ya kuwaangalia hawa wanaojiita vijana wazalendo wa taifa hili.