Majaliwa: Tusikubali kushawishiwa na Mtanzania yeyote anayetumiwa na watu wenye lengo la kutaka kuja kututawala

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka Watanzania hususani vijana wasikubali kurubuniwa na makundi ya watu wasio na mapenzi mema na nchi yetu ambao watataka kuwatumia kwa maslahi yao binafsi na hatimaye kuhatarisha usalama na amani ya nchi yao.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Desemba 10, 2020) wakati akifungua mkutano Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma. Amewasisitiza Watanzania wawe wazalendo kwa nchi yao.

“Uzalendo ndio utalifanya Taifa liendelee kujitegemea, hivyo ni muhimu suala hilo likapewa kipaumbele. Tusimkubali kushawishiwa na Mtanzania yeyote anayetumiwa na watu wenye lengo la kutaka kuja kututawala, tusikubali lazima tuendelee kuwa huru na tulinde rasilimali kwa manufaa ya wote.”

Waziri Mkuu amesema uzalendo ni muhimu sana katika kujenga umoja wa kitaifa na Vijana ni zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wa Tanzania, hivyo wakipata misingi mizuri ya uzalendo tutajenga Taifa imara, lenye mshikamano, nguvu na kuendelea kudumisha Amani nchini.

Amesema Serikali kwa kutambua hilo, kupitia Ilani ya CCM 2020-2025, imeweka msisitizo wa kuhamasisha na kuelimisha wananchi juu ya masuala ya uzalendo wa Kitaifa. “Suala la uzalendo ni muhimu sana kwa mustakabali na maendeleo ya Taifa lolote.”

Waziri Mkuu amesema amefurahi kuona skauti wenye umri mdogo katika mkutano huo na kwamba wanachama wa chama cha skauti huanzia umri wa miaka mitano na kuendelea, ni dhahiri kuwa malezi na makuzi ya uzalendo kuanzia utotoni yatawezesha ujenzi wa Taifa imara lenye wananchi wenye kuipenda nchi yao, kuilinda na kuithamini.
 
Akili za kushikiwa hizi. Hakuna Mtanzania yeyote anatumiwa na mtu yeyote yule duniani. Watanzania tunataka haki na demokrasi ya kweli ili tuweze kuchagua watu wanaostahili kuiongoza Nchi yetu bila ya uhuni na wizi unaosimamiwa na polisiccm na tume FAKE ya uchaguzi.
 
Kuhusu uzalendo mh yupo sahihi,kwani ni wazi kabsa wapo watanzania ambao wametanguliza maslahi ya mabeberu kuliko sisi watanzania (mtu anayeandika barua eti tusipewe misaada huyo sio mzalendo kabisa, na adhabu yake ameshaipata) na wengine wa karba hiyo.
Lakni mh jiwe na kundi lako sisi vijana wako hatuna ajira mkuu, hivyo nijambo jema sana kama ungekuwa unalifikiria hili kwa kina🤔

#jr
 
SIsi tumruhusu jiwe tu atutawale na si mwengine. Kwa vile tusikubali kutawaliwa na mkoloni mweupe, bora tubaki na kukoloniana wenyewe kwa wenyewe ndio mtindo wa kisasa!
 
Kuhusu uzalendo mh yupo sahihi,kwani ni wazi kabsa wapo watanzania ambao wametanguliza maslahi ya mabeberu kuliko sisi watanzania (mtu anayeandika barua eti tusipewe misaada huyo sio mzalendo kabisa, na adhabu yake ameshaipata) na wengine wa karba hiyo.
Lakni mh jiwe na kundi lako sisi vijana wako hatuna ajira mkuu, hivyo nijambo jema sana kama ungekuwa unalifikiria hili kwa kina

#jr
Mitano tenaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Sidhani kama hawa watu watafanikiwa kuturudisha enzi za Chama kimoja kushika hatamu yaani turudi mwaka enzi za mwaka 1977 Zudumu kifra za Mwenyekiti wa Chama.... turudi kuitii sauti ya mtu mmoja bila kuhoji hata kuuliza .

Maana ya Uzalendo kwa sasa ni kukubali bila kuhoji chochote toka kwa viongozi wa CCM.
 
😂😂 Tayari tunatawaliwa na wachache kimabavu na kura hazina kazi sasa Watanzania sio wajinga wanajua nani ni mzalenso wa kwelina nani wanataka masaraka tu. Waziri mkuu mpaka mgombea wake mpinzani kazuiwa asigombee sasa huyu anapenda Tanzania au anajipenda mwenyewe.
 
😂😂 Tayari tunatawaliwa na wachache kimabavu na kura hazina kazi sasa Watanzania sio wajinga wanajua nani ni mzalenso wa kwelina nani wanataka masaraka tu. Waziri mkuu mpaka mgombea wake mpinzani kazuiwa asigombee sasa huyu anapenda Tanzania au anajipenda mwenyewe.
Uzalando ni kutimiza malengo yao
 
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka Watanzania hususani vijana wasikubali kurubuniwa na makundi ya watu wasio na mapenzi mema na nchi yetu ambao watataka kuwatumia kwa maslahi yao binafsi na hatimaye kuhatarisha usalama na amani ya nchi yao.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Desemba 10, 2020) wakati akifungua mkutano Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango jijini Dodoma. Amewasisitiza Watanzania wawe wazalendo kwa nchi yao.

“Uzalendo ndio utalifanya Taifa liendelee kujitegemea, hivyo ni muhimu suala hilo likapewa kipaumbele. Tusimkubali kushawishiwa na Mtanzania yeyote anayetumiwa na watu wenye lengo la kutaka kuja kututawala, tusikubali lazima tuendelee kuwa huru na tulinde rasilimali kwa manufaa ya wote.”

Waziri Mkuu amesema uzalendo ni muhimu sana katika kujenga umoja wa kitaifa na Vijana ni zaidi ya asilimia 60 ya wananchi wa Tanzania, hivyo wakipata misingi mizuri ya uzalendo tutajenga Taifa imara, lenye mshikamano, nguvu na kuendelea kudumisha Amani nchini.

Amesema Serikali kwa kutambua hilo, kupitia Ilani ya CCM 2020-2025, imeweka msisitizo wa kuhamasisha na kuelimisha wananchi juu ya masuala ya uzalendo wa Kitaifa. “Suala la uzalendo ni muhimu sana kwa mustakabali na maendeleo ya Taifa lolote.”

Waziri Mkuu amesema amefurahi kuona skauti wenye umri mdogo katika mkutano huo na kwamba wanachama wa chama cha skauti huanzia umri wa miaka mitano na kuendelea, ni dhahiri kuwa malezi na makuzi ya uzalendo kuanzia utotoni yatawezesha ujenzi wa Taifa imara lenye wananchi wenye kuipenda nchi yao, kuilinda na kuithamini.
Kuna wakati fulani inafikirisha kuona watu tuliowategemea wangesmamia ukweli utakaojenga Taifa imara. Wanapindisha ukweli kua uongo and vice versa.!! MAKUNDI wanaoasisi ni wao lakini wakiwa majukwaani huvaa ngozi ya kondoo. Tutapata wapi Viongozi imara wa kuirudisha Taifa hili katika mshikamano?

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Akili za kushikiwa hizi. Hakuna Mtanzania yeyote anatumiwa na mtu yeyote yule duniani. Watanzania tunataka haki na demokrasi ya kweli ili tuweze kuchagua watu wanaostahili kuiongoza Nchi yetu bila ya uhuni na wizi unaosimamiwa na polisiccm na tume FAKE ya uchaguzi.
Anataka wao ndio wawatumie Watanzania kwa maslahi yao.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom