tinkanyarwele
JF-Expert Member
- Dec 30, 2016
- 2,008
- 1,954
Siku wasomi mkijua kwanini mnaenda shule basi mtaacha kuona baadhi ya vyuo ni dhaifu na vingine ni imara, kuna chuo kinaaminika na kuheshimiwa sana hapa nchini ila niliwahi kustaajabu kuona baadhi ya mazao yake(wahitimu) kwenye kada ya ualimu hawajui hata kuandaa Andalio la Somo wala Azimio la Somo huo ulikuwa mwaka 2013. Nilidhani ni madhaifu ya mtu mmoja mmoja, lakini mwaka 2014 nikakutana na zao lile lile kutoka chuo kile kile hapa ndo niliona maajabu. Mwaka 2015 nilibahatika kuanza kuishi na wahitimu wa hicho chuo pendwa, hapa sote tukiwa kikazi na kimaisha zaidi, maajabu ya miaka hiyo ikajirudia, vijana hawana lolote, ulevi mwanzo mwisho, hana hawana muda na kuifikiria kesho yao ila wanajitambua kuwa walitoka chuo kikikuu cha TAIFA . Lakini kwa makusudi zaidi wale wanao sadikika kuwa wametoka vyuo vya kata TEKU au UDOM wamekaa pembeni maisha yananyooka kila uchao. Kumbuka si wote wa chuo kile cha TAIFA wako vizuri au si wote wako vibaya, pia si kwamba wale wa TEKU na UDOM wako vizuri au vibaya. Kumbuka baada ya chuo the next step ni maisha so kwa elimu za Kiafrika Jina la chuo, hadhi, majengo, maprofesor, G. P.A, umri wa chuo n.k havina uhusiano kabisa na maisha yako baada ya shule. I stand to correct taka usitake. Pia huyu wa GPA 3.9 kama hujakosea baadhi ya hatua za kufuata ktk kuomba basi ushindani ulikuwa mkubwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app