Kamanda hujamuelewa mleta uzi. Swala sio kuwa hawapo, bali wameleta mafanikio gani ya kimaendeleo katika majimbo yao zaidi ya maandamano?
Nyie kuna maendeleo gani yaloletwa na Wabunge wenu?
Kamanda hujamuelewa mleta uzi. Swala sio kuwa hawapo, bali wameleta mafanikio gani ya kimaendeleo katika majimbo yao zaidi ya maandamano?
Hivi sugu anawezaje kuwa na ujasiri wa kumtukana Waziri mkuuu lakini kakosa ujasiri wa kukaa na mke?
Najiuliza siasa za hawa wabunge zimeishia wapi ambapo mmojawao alishafikishwa katika vyombo vya usalama kwa kumtolea raisi maneno ya kichochezi na mwingine alifikishwa kwa kumtolea waziri mkuu maneno ya kichochezi wakati wa mijadala bungeni.
Ukimya huu bila shaka unaonyesha walikamilisha kazi walizotumwa na chama chao na sasa wameingia msituni kujipanga.
Ama kweli debe tupu haliachi kuvuma! Sijui wanajipanga na uwongo gani kwa sasa hao watumwa wa chama walioingia mafichoni. Hii inadhihirisha ni jinsi gani wananchi wanafanya makosa katika chaguzi. Kwa tasfsiri makini ni kwamba Jimbo La Arusha Mjini lipo wazi tangu 2010 maana mbunge hakuna alichokifanya cha maendeleo kwa jimbo lake. Wananchi tusirudie makosa. Kuna mshirika mmoja wa G. Lema ameachana na siasa ameaanza kulaghai kwa kivuli cha Uchungaji. Tuwe makini na watu wenye njaa kali.
sugu mbeya tumemchoka kabisa.. tunasubiri uchaguzi mwakani tumtimue