Godbles Lema video: Nimemmis sana Kikwete

Godbles Lema video: Nimemmis sana Kikwete

Siasa si mchezo wa vichekesho. Siasa ni kazi maalum yenye mchango wake katika maendeleo ya taifa letu kama madaktari, mabwana shamba, wanajeshi nakadhalika. Tunapokwenda kwenye uchaguzi tunakuwa tunatafuta watu watakaofanya kazi maalum kwa maendeleo ya taifa letu.

Tumechagua wabunge ili waweze kufanya kazi kama wabunge na wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia, kuishauri serikali.

Tumeletewa mfumo wa siasa za vyama vingi na kwa kweli wakati wa awamu iliyopita pale serikali ilipokuwa imelala tumeona manufaa yake.

Haya. 2015 tukafanya uchaguzi. Tukampata rais anayeyaangalia matatizo ya wananchi kwa makusudi ya kuyatatua. Tumelitengeneza bunge. Tukaongeza idadi ya wabunge wa vyama vya upinzani. Tukatarajia kuona nguvu ya upinzani ikiisaidia serikali hii inayoonekana kuyaangalia matatizo yanayogusa wananchi.

Ninaanza kuwa na matatizo na mambo ninayoyaona yakiendelea bungeni. Kuna wabunge hawaoni ulimwengu unachoona kikifanywa na serikali. Ndani na nje ya Tanzania kila mwenye akili kamili anaona serikali ya Magufuli inachokifanya na kila kona anapongezwa.

Niongelee moja kama sio mawili: Serikali ilipotangaza kuwa mwaka ujao wa fedha (2016/17) inatarajia kutumia fedha za kitanzania Trilion 29 kutoka trillion 22 za mwaka unaoisha. Viongozi Ukawa walisimama kidete kuikatalia serikali kuwa haiwezi kuzikusanya fedha hizo kwa hiyo bajeti hii ni kiini macho.

Binafsi nilielewa wanalolisema japo niliielewa serikali kuwa kwa juhudi inazoonyesha za kukusanya kodi na kubana matumizi inaweza kuzifikisha. Kilichonitisha ni pale wakati wabunge hao hao wakijadili bajeti za wizara wanaibuka na kutaka budget za wizara zisipitishwe kwa sababu wizara zimetengewa fedha kidogo.

Nashindwa kuwaelewa wawakilishi wetu hawa. Wanapendekeza wizara ziongeze fedha (kwa kuwa hazitoshi) ambazo zinatokana na budget wanayotaka ipunguzwe (kwa kuwa haziwezi kupatikana). Kuna bongo ngapi vichwani mwao? Sielewi.

Lakini mbunge wa mwingine ambaye anaheshimika mhe. Lema sana anasema wabunge watamkumbuka JK. Watamkumbuka kwa sababu hakuwahi kuwazuia kumsema. Kazi ya bunge ni kumsema rais au kuisaidia serikali?

Lema anasema hivyo kwa sababu bunge limemzuia kumbambikiza Magufuli ujinga kuwa aliuza nyumba za serikali. Wabunge hawajui kuwa Magufuli hakuwahi kuuza nyumba hizo bali serikali iliuza nyumba zake kwa uamuzi wake na Waziri (Magufuli) akatekeleza uamuzi wa serikali.

Anaambiwa aondoe neno Magufuli na aweke neno Serikali anasema hawezi kusoma maoni ya kambi ya upinzani. Upumbavu huu naulinganisha na ule ambao watu wazima walifafanuliwa zaidi ya mara nyingi kuwa Dr. Slaa alisema ataanzisha mchakato wa katiba ndani ya siku 100.

Wao wakaendelea kusema alisema atalipatia katiba Taifa ndani ya siku 100. Nauita upumbavu kwa sababu hawakuelewa kabisa licha ya kufafanuliwa. Ni huo ambao watu wanalinganisha uuzaji wa nyumba na kashfa ya Richmond.

Wabunge wa aina ya Lema na Msigwa wanaotaka mijadala ambayo inaisha baada ya kujadiliwa wataua upinzani. Tunatarajia wajadili mambo yatakayoleta matunda baada ya kujadiliwa. Kutaka kujadili nyumba zilizouzwa na serikali kunatarajia kuleta faida gani baada ya mjadala.

Mtu mmoja ameniuliza kuwa sababu ilizotoa serikali kutoonyesha mijadala ya bunge live ni sahihi? Nikamjibu kuwa sio sahihi. Sababu ni kuwa serikali ilitaka kuliondolea taifa aibu kutokana na mijadala kama ambavyo watu fulani huwaficha watoto walemavu ili kuficha aibu za familia.
 
Watu dizaini ya singidadodoma wanaoisapoti ccm ni aibu kuwepo katika uso wa dunia
 
haa haa kwa hiyo wabunge wanaofaa ni aina ya Lusinde, msukuma na Agnes Marwa eti?
 
Wewe ndio hujielewi hamtaki wapinzani waseme ukweli sijui mnashida gani jamani lumumba .kama rais aliuza na hiyo issue ni ya mrada mrefu mbona akiwa waziri wa ujenzi .labda we ulikuwa hujazaliwa .
 
Tumechagua wabunge ili waweze kufanya kazi kama wabunge na wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia, kuishauri serikali.

Siasa ni kazi maalum yenye mchango wake katika maendeleo ya taifa letu kama madaktari, mabwana shamba, wanajeshi nakadhalika. Tunapokwenda kwenye uchaguzi tunakuwa tunatafuta watu watakaofanya kazi maalum kwa maendeleo ya taifa letu.
haya yote uliyoyaelezea sio kwa afrika na tanzania hii tunayoijua sisi wabongo. hayo ni malengo ya siasa safi kwa nchi za wenzetu kama japan ama canada, nchi zinazojua nini maana ya uwajibikaji wa kisiasi.
 
wewe ndo unataka waweke sanamu ya daimond pale posta au ni yule unashikwa na uchungu maana miandiko yenu inafanana sana hadi nashindwa kuwatofautisha.
 
watu wanamiss chai nzito ya palee.bei ya sukari imepiga kote kote.
 
Kwa sisi wenye akili timamu hakika hatuachi kuwacheka na kuwashangaa hawa wabunge wa upinzani kwa huu undumilakuwili na uendawazimu wanaoionesha. Sijajua hasa ni nini kinawapanda vichwani mwao mpaka wanashindwa kutunza kumbukumbu zao vizuri na kusahau nini walifanya jana yake ili waoanishe na wanachofanya leo.

Ameanza Godbless Lema kummiss Rais Jakaya Kikwete ambaye amemaliza muda wake Novemba tano 2015. Wamesahau kuwa ni huyu huyu Kikwete ndiye walimuita Rais dhaifu kuweza kutokea Tanzania.

Sasa wameanza kilio kipya cha kumlilia Spika Job Ndugai wakidai kuwa Naibu Spika Dr Tulia Akson anawakandamiza na kuwaziba midomo ili wasisikike. Hakika madai haya yamenishangaza sana na kuniacha mdomo wazi. Je ni nini hasa wanachokitaka hawa wapinzani? Je wana madai mapya ama ni kuendeleza kile walichofanya miaka iliyopita?

Hebu soma habari hii hapa chini then Uniambie kama Wapinzani wanatumia akili kufikiri ama wanatumia viungo vingine vya miili yao.

WAPINZANI WAUNGANA KUMSUSIA NAIBU SPIKA JOB NDUGAI

KWA mara ya kwanza tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa 2010, wabunge wa vyama vya upinzani Februali Mosi 2013 waliungana pamoja na kumsusia Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, wakipinga hatua yake ya kupindisha hoja binafsi ya Mbunge wa kuteuliwa na Rais, James
Mbatia (NCCR-Mageuzi) na kuitetea serikali bila maelezo yanayoeleweka.
Kwa pamoja, wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), National Convention for Construction and Reform (NCCR- Mageuzi), United Democratic Party (UDP) na Chama cha Wananchi (CUF) walitoka nje ya ukumbi wa Bunge wakaenda ukumbi wa kambi ya upinzani kufanya kikao cha dharura juu ya hatua za kuchukua dhidi ya ubabe wa Ndugai.

Hatua kama hiyo ya kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, imekuwa ikitumiwa na wabunge wa CHADEMA ambayo inaunda kambi rasmi ya upinzani bungeni kupinga baadhi ya masuala kadhaa.
Hata hivyo, kwa mara mbili tofauti CHADEMA waliposusia Bunge, wenzao wa vyama vingine hawakuwaunga mkono, hatua iliyotafsiriwa kama kutokuwapo kwa mshikamano.

Kwa mara ya kwanza, CHADEMA walisusia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ya kufungua Bunge, wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliyomleta madarakani na mara ya pili walitoka nje ya ukumbi wakipinga kupitishwa kwa sheria ya mabadiliko ya katiba mpya.

Hali hiyo ni tofauti na Februari Mosi 2013 ambapo wabunge wa vyama hivyo vya CHADEMA, CUF, UDP, TLP na NCCR-Mageuzi waliungana kwa kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, kupinga hatua ya Ndugai kuwaburuza katika kupitisha hoja ya Mbatia.

Hoja hiyo binafsi iliyoainisha udhaifu katika mfumo wa elimu nchini, iliwasilishwa na kuibua mjadala mzito bungeni, huku kambi ya upinzani ikikubali hoja ya Mbatia kutaka kuunda kamati teule wakati wabunge wa CCM wakipinga.
Mzozo wa jana ulianza baada ya Mbatia kufunga hoja yake na kutaka Waziri wa Elimu na

Kwa muktadha huu, nawaomba wasomaji wa uzi huu muuweke kwenye makabrasha yenu ili tukikutana baada ya uchaguzi wa 2020 tuje tujikumbushe. Kwa hakika hamtaamini. Hawa hawa wanaompinga leo Dr Tulia ndio watakaomlilia. Ni kawaida yao kwani walifanya kazi kubwa ya kunadi ufisadi wa Lowasa na genge lake lakini ni hao hao leo wanamsafisha. Kazi wanayo
 
Hakika wapinzani tunajitakia matusi. Yaani kumbe haya tunayofanya kwa Dr Tulia tulifanya hata kwa Job Ndugai? Hahahahahaaaaa. Tumecurugwa kweli
 
Shikamoo kaka Chabruma. Umerejesha makali yako ya Bunge la Katiba
 
Mkuu Chabruma, muda hubadili mtizamo Na ni Jambo la kawaida mtu kubadili mawazo baada ya muda Fulani kupita, ni Mungu tu(rejea biblia) ndio huwa habadiliki...
 
Mkuu Chabruma, muda hubadili mtizamo Na ni Jambo la kawaida mtu kubadili mawazo baada ya muda Fulani kupita, ni Mungu tu(rejea biblia) ndio huwa habadiliki...
Nakubaliana na wewe Mkuu. Ndo maana sisi wenye akili timamu tunawacheka sana hawa UKAWA. Walichofanya jana wanasahau na wakifanya leo wanadhani sisi tutaona ni kutu kipya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom