Ghorofa latitia mtaa wa Mchikichini, Kariakoo jijini Dar

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Sep 6, 2014
6,170
7,661
Nipo nasikiliza Radio nimeikuta habari katikati sijaelewa ni nini Kinachoendelea huu mtaa wa Livingston karibu na bank ya NBC hapa Kariakoo.

Nilichosikia ni kwamba Ghorofa ndo limeleta kashi kashi na ninasikia wahindi wakilalamika kuwa hio sio haki kabisa wanapewa Milion Moja na Laki nane iwapeleke wapi na wameshtukizwa usiku tuu na watu wenyewe hawana vibali.

Watu nasikia ni wengi wamekusanyia na nasikia wahindi wakilalmika kuwa wameibiwa na ni adhari hio ( nasema wahindi kutokana na rafudhi walio kuwa wanaongea).

Mwisho nikasikia Mtangazaji wa Radio One kasema watamtafuta Afisa ardhi Ilala kupata ufafanuzi.

Tafadhali mwenye kujua hili atupe taarifa kamili hicho ndo kidogo nilicho sikia ngoja na mimi nitafute habari kamili.

Inavoonekana serikali imeenda tofauti hapa au wamiliki wa gorofa au kuna kingine sijakielewa.

======

Wakuu habari Zenu! ITV wametangaza mchana huu kuna ghorofa linalotitia taratibu Kariakoo kutokana na ujenzi mbovu jirani na ghorofa hilo na kusababisha nyufa kwa jengo hilo..

Wananchi na wapangaji wa jengo linalotitia wameomba wahusika kuchukua hatua stahiki kwani wao wamejitahidi kufatilia lakini jitihada zao zinaonyesha kugonga mwamba.

Rai: Polisi wawahi eneo hilo ili waweke tape kuzunguka eneo la hatari. Walioko ndani wengi wametoka ila watakaoathirika ni wale wanaoshangaa pale nje jirani na hapo na wapita njia.

Naamini wahusika watalifanyia kazi.
 
Wakuu habari Zenu! ITV wametangaza mchana huu kuna ghorofa linalotitia taratibu Kariakoo kutokana na ujenzi mbovu jirani na ghorofa hilo na kusababisha nyufa kwa jengo hilo..

Wananchi na wapangaji wa jengo linalotitia wameomba wahusika kuchukua hatua stahiki kwani wao wamejitahidi kufatilia lakini jitihada zao zinaonyesha kugonga mwamba.

Rai: Polisi wawahi eneo hilo ili waweke tape kuzunguka eneo la hatari. Walioko ndani wengi wametoka ila watakaoathirika ni wale wanaoshangaa pale nje jirani na hapo na wapita njia.

Naamini wahusika watalifanyia kazi.
 
During vasco da gama reign every engineer was never an engineer any more.
 
..mkuu kutititia mie sijui maana yake mi najua kutitia ndio kubonyea kwa kwenda chini

Ulivyoongezea kwa kwenda chini umekaribia maana, make ukisema tu kubonyea haileti maana, mfano gari inaweza kuwa imebinyea bila kutitia.

Kutitia inaendana na ardhi mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom