Gharama za imported goods kuwa chini kati ya Tanganyika na Zanzibar sio jambo jipya

Planet FSD

JF-Expert Member
Oct 24, 2019
455
938
Leo nimeona mjadala mkubwa umekuwa ukiendelea kuhusiana na utofauti wa bei ya lita moja ya mafuta kati ya Zanzibar na Tanganyika.

Na picha zikisambaa mitandaoni kuonesha Zanzibar lita moja ni 2600+ TZS wakati Tanganyika ni 3100+ TZS, huku swali kubwa likiwa inakuaje bei iko chini Zanzibar kuliko Tanganyika.

Lakini kubwa hasa ambalo limenifanya niandike uzi huu ni kuwa, swali hili linaulizwa kwa insinuation ya kwamba huenda Zanzibar wanalipa kidogo kwa lita kwa sababu ndiko anakotokea Hangaya. Kusema ukweli sifurahishwi na jinsi Hangaya anavyotupeleka, lakini hapa naomba nimtetee.

Kabla hata hajawa rais wote tunajua gharama za kuingiza bidhaa kutoka nje kwa Zanzibar ziko chini kuliko Tanganyika. Iwe gari iwe TV, Zanzibar unavipata kwa gharama ndogo kuliko Tanganyika. Imekuwa hivyo miaka nenda rudi, sio jambo jipya.

Ukweli ni kwamba kinachotuletea tabu watanganyika ni msururu na lundo la kodi na tozo zisizo na kichwa wala miguu. Bidhaa ndogo tu ila ina utitiri wa kodi. Jaribu kununua gari kutoka Japan halafu peleka Zanzibar, na jaribu kuleta model ya gari hiyo hiyo Tanganyika ndiyo utajua hujui. Unaweza kujipatia kitv chako cha bei rahisi kule kisiwani, wazenji hawana tabu na wewe, balaa litakukuta pale bandarini utakapokutana na watanganyika wenzako.

Kwahiyo kama lita ya mafuta mpaka ifike bandari zetu za Tanzania CIF yake ni 1162 TZS, yakiingizwa Zanzibar na Tanganyika, hayawezi kuwa sawa. Na wenzetu wanajaliana, wanapeana relief muda huu wa mgogoro huko ulaya mashariki.

Kwahiyo watanganyika tusimtafute mchawi. Hangaya asilaumiwe kabisaaaa. Tumuache atukune na kutupuliza fuuu!
C2F9F013-D848-432E-B2F5-64AC5A2DB448.jpeg


372B6776-D5CA-43B0-BF20-345C1A20816E.jpeg
 
KaTV Zenji bei rahisi ukiingia nako bara mpaka utajuta kwa nini uliinnunulia Zanzibar. Bara tuna ujinga mwingi sana
Umeona mkuu😂😂sasa hapa mafuta tusitake kujifanya kuna mkono wa Hangaya. Hii tabia ya kukomoana tunayo upande wetu huku
 
Waulize ZNZ kuna miradi ya REA kama ilivyo bara ambapo kuna tozo kwenye mafuta ili kuiwezesha REA.

Waulize tena ZNZ kuna reli? Kwasababu bara tunatoza kodi ya maendeleo ya Reli kwenye mafuta.

Waulize tena ZNZ kuna KM ngapi za barabara zinazohitaji kujengwa kulinganisha na bara?
Ni mtu punguani tu anayeweza kulinganisha kodi ya ZNZ na Bara
Bajeti ya SMZ ni bajeti ya wizara moja tu hapa mnafikiri hizo pesa Mama Samia atalima nyanya azipate?
 
Leo nimeona mjadala mkubwa umekuwa ukiendelea kuhusiana na utofauti wa bei ya lita moja ya mafuta kati ya Zanzibar na Tanganyika.

Na picha zikisambaa mitandaoni kuonesha Zanzibar lita moja ni 2600+ TZS wakati Tanganyika ni 3100+ TZS, huku swali kubwa likiwa inakuaje bei iko chini Zanzibar kuliko Tanganyika.

Lakini kubwa hasa ambalo limenifanya niandike uzi huu ni kuwa, swali hili linaulizwa kwa insinuation ya kwamba huenda Zanzibar wanalipa kidogo kwa lita kwa sababu ndiko anakotokea Hangaya. Kusema ukweli sifurahishwi na jinsi Hangaya anavyotupeleka, lakini hapa naomba nimtetee.

Kabla hata hajawa rais wote tunajua gharama za kuingiza bidhaa kutoka nje kwa Zanzibar ziko chini kuliko Tanganyika. Iwe gari iwe TV, Zanzibar unavipata kwa gharama ndogo kuliko Tanganyika. Imekuwa hivyo miaka nenda rudi, sio jambo jipya.

Ukweli ni kwamba kinachotuletea tabu watanganyika ni msururu na lundo la kodi na tozo zisizo na kichwa wala miguu. Bidhaa ndogo tu ila ina utitiri wa kodi. Jaribu kununua gari kutoka Japan halafu peleka Zanzibar, na jaribu kuleta model ya gari hiyo hiyo Tanganyika ndiyo utajua hujui. Unaweza kujipatia kitv chako cha bei rahisi kule kisiwani, wazenji hawana tabu na wewe, balaa litakukuta pale bandarini utakapokutana na watanganyika wenzako.

Kwahiyo kama lita ya mafuta mpaka ifike bandari zetu za Tanzania CIF yake ni 1162 TZS, yakiingizwa Zanzibar na Tanganyika, hayawezi kuwa sawa. Na wenzetu wanajaliana, wanapeana relief muda huu wa mgogoro huko ulaya mashariki.

Kwahiyo watanganyika tusimtafute mchawi. Hangaya asilaumiwe kabisaaaa. Tumuache atukune na kutupuliza fuuu!View attachment 2213167

View attachment 2213168
Nimependa ulivyo itambua Tanzania mainland kama Tanganyika kunahoja ndani ya uzi imefichwa pengine ni kwa uoga au unatuchora wadanganyika na hapo ndipo tunaona KATIBA mpya inahitajika kwa upana mkubwa mbali na siasa za majitaka za upinzani uchwara.
 
Waulize ZNZ kuna miradi ya REA kama ilivyo bara ambapo kuna tozo kwenye mafuta ili kuiwezesha REA.

Waulize tena ZNZ kuna reli? Kwasababu bara tunatoza kodi ya maendeleo ya Reli kwenye mafuta.

Waulize tena ZNZ kuna KM ngapi za barabara zinazohitaji kujengwa kulinganisha na bara?
Ni mtu punguani tu anayeweza kulinganisha kodi ya ZNZ na Bara
Bajeti ya SMZ ni bajeti ya wizara moja tu hapa mnafikiri hizo pesa Mama Samia atalima nyanya azipate?
Sasa kama tunatambua haya kuwa kodi iko juu Tanganyika, watu waache kelele za kuuliza kwanini lita moja ya mafuta iko chini Zanzibar. Maana huu mjadala umekuwa na kaharufu ka kutaka kumsingizia Hangaya kuwa huenda Zanzibar wana unafuu kwa sababu yake.
 
Nimependa ulivyo itambua Tanzania mainland kama Tanganyika kunahoja ndani ya uzi imefichwa pengine ni kwa uoga au unatuchora wadanganyika na hapo ndipo tunaona KATIBA mpya inahitajika kwa upana mkubwa mbali na siasa za majitaka za upinzani uchwara.
Hapana siko huko mkuu. Mi nachojua kuna Tanzania ambayo ni matokeo ya Zanzibar na Tanganyika, sasa kama nikiispecify Zanzibar kutoka kwenye muunganiko huko si kinabaki Tanganyika au? Ni simple mathematics

Tanganyika + Zanzibar = Tanzania
Hence,
Tanzania - Zanzibar = …? Sina lengo lingine zaidi ya kujadili mafuta.
 
Zanzibar wana akili ya maisha, bara wana akili za kukariri darasani.

Zanzibar wataitwa wavivu kwasababu akili zinafanya kazi hawalali njaa, bara utafanya makazi mazito zito ili mkono uende kinywani 😄😄

Eti muungano 😂😂
 
Waulize ZNZ kuna miradi ya REA kama ilivyo bara ambapo kuna tozo kwenye mafuta ili kuiwezesha REA.

Waulize tena ZNZ kuna reli? Kwasababu bara tunatoza kodi ya maendeleo ya Reli kwenye mafuta.

Waulize tena ZNZ kuna KM ngapi za barabara zinazohitaji kujengwa kulinganisha na bara?
Ni mtu punguani tu anayeweza kulinganisha kodi ya ZNZ na Bara
Bajeti ya SMZ ni bajeti ya wizara moja tu hapa mnafikiri hizo pesa Mama Samia atalima nyanya azipate?
Na vipi kuhusu rasilimali asilia, kiwango cha natural resources kwa zanzibar na bara zinalingana?

Tusitafute mchawi, watawala wetu wanapenda shortcut katika kupata pesa kupitia kodi na tozo, na ndipo wamezijaza kwenye mafuta sababu mafuta ni bidhaa ya lazima kila mwananchi kuitumia directly or indirectly kila siku. Kwa rasilimali tulizonazo hatukutakiwa kujaziwa kodi na tozo katika mafuta.
 
Back
Top Bottom