Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

Nguruvi3,

..talk about MSUMBIJI!??

..hawa ndugu zetu ni kati ya mataifa marafiki waliotusaidia wakati wa vita vya Kagera.

..if I am not mistaken ndiyo nchi pekee iliyotuma askari wake kupigana bega kwa bega na vijana wetu ndani ya Uganda.

..sijui kwanini UNDUGU wetu na MSUMBIJI nao hauko documented vijana wetu wakajua.

..sasa vita ya Msumbiji unayoiongelea wewe iliitwa "Operesheni Safisha". Hii ilikuwa ni baada ya Samora kufariki, na majeshi ya Frelimo yalikuwa na hali mbaya sana.

..ushiriki wetu ktk vita hiyo ulifanywa siri. hata askari wetu waliopoteza maisha huko miili yao ilikuja kurudishwa wakati wa utawala wa Mkapa na kuzikwa kwa heshima za kijeshi Mtwara eneo la Naliendele.

..Gen.Tumainieli Kiwelu made the right observations kuhusu masuala ya Frelimo vs Renamo. Inawezekana kabisa alifanya hivyo kutokana na ripoti za askari wake on the battle field.

..kuna mahali nilisoma kwamba UFISADI ulitamalaki ktk jeshi la Msumbiji kiasi kwamba askari wa Frelimo walianza kushirikiana na magaida wa Renamo ktk biashara haramu kama pembe za ndovu na magendo mengine.

..katika mazingira hayo ndiyo maana utaona msaada wowote ule uliokuwa ukitolewa na TANZANIA na ZIMBABWE haukufanikiwa kuleta hali ya AMANI na USALAMA kwa wananchi wa MSUMBIJI.

NB:

..Tumainieli Kiwelu alitumikia mara mbili kama Afisa Mnadhimu Mkuu[Chief of Staff] wa JWTZ. Mara ya kwanza alikuwa chini ya Abdalah Twalipo, na mara ya pili alitumikia chini ya Gen.Ernest Mwita Kiaro.

..baadaye Raisi Mkapa alimpandisha cheo na kuwa Generali na kumteua kuwa Balozi wa Tanzania Ufaransa. Kati ya Chief of Staff wote ni Kiwelu peke yake ndiye ametunukiwa cheo cha General, ngazi ambayo iko reserved kwa Wakuu wa Majeshi tu.
 
Ukisoma uchangiaji wa watu kwenye hii thread, ni kama unasoma kitabu kizuri sana cha Historia...Nampongeza mtoa mada, nawapongeza wachangiaje kwa detailed information...na nimefurhishwa sana na kutokuta michango ya kipuuzi, nkimaanisha huwa kuna thread zinatolewa humu alafu utakuta mtu anachangia tu ili mradi....for the sake of knowledge ni bora kama kitu unakijua basi kichambue vizuri kama walivyofanya watu humu ili tuweze kupata Elimu na kama huna cha kuchamgia unaweza uka-like au kusoma tu na si kupoteza muda kuchangia vitu visivyo vya msingi... Asanteni sana wanajamii
 
Brutus,
Good to see you back. Usipotee sana mazee.
Naam Comrade! Kaisari alibana sana!
Ndio tumerudi na kuanza kupekua hazina zilizofichika... maana hii mijadala ilikuwa mitamu sana. Nowadays kuna uhaba wa threads kama hizi! Haya mambo huwezi kupata darasani!
Siku hizi threads zimejaa name callings tu, mara huyu kamuita mwenzake 'gamba' sababu katofautiana hoja, na mwingine anamjibu ' na wewe gwanda' LOL! Field Marshal ES, Joka Kuu, Phillemon, Ndahani, Masatu, Zanaki .. where are you guys?
 
Jf ni kisima cha maarifa,mambo niliyojifunza hapa sijui kama ningeweza kuyapata sehemu nyingine,thanks alot Jf veterans kwa yale mnayotufundisha wadogo zenu na kuweka kumbukumbu zetu sawa kuhusu tulipotokea.
 
Mtoto wa .Com nimekula darasa la bure ambalo hata babu yangu hakuwai nisimulia!Thanks Jf na wazee wote Mungu aendelee kuwapa uhai mtupe haya madude UNLIMITED!...
 
I have read this thread and discovered that JF OF THOSE DAYS IS NOT THE SAME AS THE ONE OF TODAY.WAKUU, the depth and the content in each comment is amazing. I wish the veterans like Kundi and Fieldmarshal could maintain the spirit. There is a lot we "the new comers" can learn from this thread. Hope the coming 2012 will bring in depth contributions to flouted threads. Happy New Year (2012) to all Pioneers, veterans and members of this Great Great forum
Lets Keep ob mourning..! The old is Gold dear. Can u believe Field Marshall Es ni Le Mutuz,ambaye sasa hivi ni coward na propagandist wa CCM- mafisadi? Wacha tule mipasho tu. Jf Ya wakai huo si hii.
 
Nguruvi3,

..talk about MSUMBIJI!??

..hawa ndugu zetu ni kati ya mataifa marafiki waliotusaidia wakati wa vita vya Kagera.

..if I am not mistaken ndiyo nchi pekee iliyotuma askari wake kupigana bega kwa bega na vijana wetu ndani ya Uganda.

..sijui kwanini UNDUGU wetu na MSUMBIJI nao hauko documented vijana wetu wakajua.

..sasa vita ya Msumbiji unayoiongelea wewe iliitwa "Operesheni Safisha". Hii ilikuwa ni baada ya Samora kufariki, na majeshi ya Frelimo yalikuwa na hali mbaya sana.

..ushiriki wetu ktk vita hiyo ulifanywa siri. hata askari wetu waliopoteza maisha huko miili yao ilikuja kurudishwa wakati wa utawala wa Mkapa na kuzikwa kwa heshima za kijeshi Mtwara eneo la Naliendele.

..Gen.Tumainieli Kiwelu made the right observations kuhusu masuala ya Frelimo vs Renamo. Inawezekana kabisa alifanya hivyo kutokana na ripoti za askari wake on the battle field.

..kuna mahali nilisoma kwamba UFISADI ulitamalaki ktk jeshi la Msumbiji kiasi kwamba askari wa Frelimo walianza kushirikiana na magaida wa Renamo ktk biashara haramu kama pembe za ndovu na magendo mengine.

..katika mazingira hayo ndiyo maana utaona msaada wowote ule uliokuwa ukitolewa na TANZANIA na ZIMBABWE haukufanikiwa kuleta hali ya AMANI na USALAMA kwa wananchi wa MSUMBIJI.

NB:

..Tumainieli Kiwelu alitumikia mara mbili kama Afisa Mnadhimu Mkuu[Chief of Staff] wa JWTZ. Mara ya kwanza alikuwa chini ya Abdalah Twalipo, na mara ya pili alitumikia chini ya Gen.Ernest Mwita Kiaro.

..baadaye Raisi Mkapa alimpandisha cheo na kuwa Generali na kumteua kuwa Balozi wa Tanzania Ufaransa. Kati ya Chief of Staff wote ni Kiwelu peke yake ndiye ametunukiwa cheo cha General, ngazi ambayo iko reserved kwa Wakuu wa Majeshi tu.

Where is this old soldier? Moshe Dayan, he made a nest for himself where the tent for battle to liberate Kagera started?
 
Hapa naomba nikusahihishe kidogo. Baada ya Sarakikya kutumikia nchi kama balozi nchini Kenya kwa muda mrefu sana akiwa na cheo cha Major-General na akiwa bado ni askari, kwa mujibu wa taratibu cha kijeshi alitakiwa awe amepandishwa cheo kwenda General. Hivyo, baada ya kuona kwamba hakupandishwa cheo, kabla ya kustaafu rasmi aliomba kupandishwa cheo kama stahili yake halali na CDF aliyekuwepo wakati huo kutoa ushauri unaofaa kwa rais, na ndo maana alipandishwa cheo kuwa Generali na akastaafu akiwa Generali. Kwa hiyo Sarakikya alistaafu na akiwa na cheo cha Generali na siyo Major-General.


So far, kuna Conspiracy theory inayomhusisha Sarakikya na njama za kumpindua Nyerere zilizofichuliwa na Marehemu Abdallah Twalipo wakati huo akiwa Kanali ambaye alimjulisha kawawa kwa siri na kawawa kumjulisha Mwalimu. Hiki ndo chanzo cha Sarakikya kupelekwa nje kuwa Balozi kwa kipindi chote cha utumishi wake kilichosaria, na pia Chanzo cha marehemu Abdallah Twalipo kuwa CDF.

Tuendelee na conspiracy theories zingine kama zipo...............

Toka Major General to General
au Major General to Lieutenant General?
Sababu General ni mkuu wa majeshi!
 
I real Miss JF of the Old Days, watu walikuwa wanarusha Nondo tu, tena wanachangia kwa upendo, maarifa, references na kwa kuheshimiana sana, no personal attacks, na blah blah blah. I was a Guest by then.
The Platinum JF of the Golden Days will be missed to be true.
 
Where is this old soldier? Moshe Dayan, he made a nest for himself where the tent for battle to liberate Kagera started?
Ndahani,

..Tumainieli Kiwelu alipandishwa cheo toka Lt.Gen na kuwa General halafu akaondolewa jeshini na kuteuliwa kuwa balozi wetu Ufaransa.

..kabla hajaripoti ubalozini Ufaransa akateuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga.

..wakati yuko Shinyanga ndiyo ile kashfa ya "mauaji" ya Bulyankulu ilipotokea. sijui ni kwa kiasi gani alihusika lakini "mauaji" hayo yalitokea akiwa mkuu wa mkoa.

..baadaye alihamishiwa mkoa wa Kagera na huku ndipo alipostaafu kazi. nilisoma kwenye magazeti kwamba amebakia huko huko Kagera akijishughulisha na kilimo cha kahawa.

cc: Mwawado
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom