Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

Kwa wanaomjua huyu Baba Sarakikya, nawaomba wachangie hoja hii - Kama kuna mtu ambaye kweli leo hii inafaa kuwa rais basi huyu Baba Ni mmoja wao..Ikisikia Mzalendo, mchapakazi na mtu mwenye nidhamu ya juu huyu baba nii kiboko yao..Sijui yuko wapi mara ya mwisho nakumbuka mwaka 2002 alikuwa balozi wetu Kenya.
 
Hii forum kuna kitu kikubwa imekibeba kwa ajiri ya Taifa hili. Time will tell, maana I am a beliver of the fact that there is a space between stimulus and response


Nimeguswa na post yako mjomba, mara nyingi forum hii imekuwa mtetezi wa wanyonge ikisema mambo ambayo yalidhaniwa ni siri na watawala wa dunia/inchi hii. Forum hii imekuwa ikitimiza andiko fulani katika biblia linalosema
3
[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Kwa hiyo, lo lote mlilosema gizani litasikiwa nuruni na kile mlichonong’ona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa. Luka 12:3[/FONT][/FONT]
[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Wanyoke sasa wana sehemu ya kupasulia kile kinachowachoma moyoni, Pia nawatieni moyo Watanzania wote walioteswa na kundi la watu wchache ambao wamejimilikisha inchi kama mali yao kwa sababu kuna andiko lingine lazima litimie nyakati hizi andiko hili liko katika kitabu Wakorinto wa kwwanza 12:26 to 31
26
[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi waliokuwa na nguvu, si wengi waliozaliwa katika jamaa zenye vyeo. [/FONT][/FONT]27[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Lakini Mungu alichagua vitu vipumbavu vya ulimwenguni ili aviaibishe vyenye hekima, Mungu alichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili aviaibishe vyenye nguvu. [/FONT][/FONT]28[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko, [/FONT][/FONT]29[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]ili mtu ye yote asijisifu mbele za Mungu. [/FONT][/FONT]30[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]Mungu ndiye chanzo cha uzima wenu katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu na haki na utakaso na ukombozi, [/FONT][/FONT]31[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]ili kama ilivyoandikwa: "Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana." [/FONT][/FONT]
[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][/FONT][/FONT]
[FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]
[/FONT]
[/FONT][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow][FONT=Arial Narrow,Arial Narrow]
[/FONT][/FONT]
[/FONT]
[/FONT]
 
Nadhani C flat bado ni juu sana. Huyu mwanafunzi anapaswa kupewa F katika hiyo paper. Huwezi kunakili data/info toka JF na kuziweka kwenye academic paper. Mtafute General Sarakikya halafu muombe akupe muda wa kuyajibu maswali yako. Kwenye paper utapaswa kumquote yeye. The report will then be authentic.
 
Thread hii ni nzuri Kabisa. Sasa nina swali. Vipi Captain Alfred Milinga kutoka Treason trial bado yupo hai? Nimesoma ameuawa na Idi Amin baada ya treason trial. asante!
 
Thread hii ni nzuri Kabisa. Sasa nina swali. Vipi Captain Alfred Milinga kutoka Treason trial bado yupo hai? Nimesoma ameuawa na Idi Amin baada ya treason trial. asante!
 
Kuna 'conspiracy' nyingine kuhusu Sarakya amabyo haitofautiani na wachangiaji waliopita. Inasemwa Sarakya alijenga umaarufu sana jeshini kiasi cha kuonekana ana ushawishi mkubwa kuliko Amiri jeshi. Hii ndiyo inaunganishwa na dhana ya uhaini.

Nchi 'ilitikisika' siku alipondolewa CDF. Imeelezwa kuwa pamoja na njama haikuwa rahisi kumuacha mtu anayeijua nchi azurure mitaani. Kumtengenezea kesi ingeleta matatizo kutokana na ushawishi wake jeshini. Kwahiyo aliteuliwa kuwa waziri ili kumweka vema katika 'rada' za mambo yake ya kila siku na baada ya hapo akawa balozi ili kumuondoa katika ulimwengu wa mambo nyeti.

Conspiracy ya umaarufu inaelezwa kutumika kwa Lt Gen T.Kiwelu. Huyu naye alikuwa maarufu sana hasa kwa kusimamia masilahi ya askari na misimamo kama ile ya kusaidia vita msumbiji. Naye alipelekwa ubalozini na kisha kurudishwa nyumbani kama mkuu wa mkoa.

Kuna maarufu mwingine marehemu Gen Walden( mti mkavu). Alishiriki vita ya Kagera na akina Mayunga(mti mkavu), Musuguri n.k.
Uteuzi wa musuguri ukisemwa kuwa ulikuwa na uhusiano na undugu. Gen Musuguri na Nyerere ni watu wa karibu sana nyumbani.
Hata hivyo ikisemwa kuwa Walden hakuridhia sana kwasababu ukiangalia darsa yeye lilipanda. Walden alikuwa ni Chotara na nashangaa msiba wake haukuwa katika hadhi iliyotarajiwa.

Kuhusu upandaji wa vyeo, nadhani pia kabla hatujalaumu kwanini hapakuwepo na cheo fulani wakati fulani, inabidi tuangalie ukubwa wa jeshi. Katika jeshi kila cheo kina uzito na majukumu yake kuanzia private hadi general.
Huwezi kuwa na brigadier anayeongoza kikosi. Brigadier inatokana na brigade na brigade inaundwa na idadi kadhaa ya vikosi vyenye askari kadhaa. Sasa wakati wa akina Sarakya tulikuwa na jeshi lenye ukubwa wa kuunda brigade na brigade za kutosha ili ziweze kuwa na brigadier ambao watahitaji Lt general kwa mkusanyiko fulani?

Ninachotaka kusema ni kuwa jeshi limepanuka sana sasa hivi ukilinganisha na miaka 30 iliyopita. Limepanuka kwa idadi na ubora hasa viwango vya elimu. Hii inakidhi mahitaji ya vyeo husika.

Kuhusu Cleopa Msuya, amekuwa waziri katika utawala wa Nyerere na Mwinyi mfululizo akiwa waziri wa viwanda, fedha, biashara na kufikia uwaziri mkuu. Hakuna shaka kuwa kipato chake kinachochagizwa na nyadhifa kama alizo nazo sasa, ni cha kawaida kabisa na sijui anawezaje kuitwa tajiri.

Huyu ni mmoja wa watoto wa Mwalimu ndiyo maana kuna wakati huwa na nyodo za kukemea haya tunayoyaona bila woga.
Sifa ya Msuya kama mbunge si upendeleo kama wanavyodai watu. Msuya ni 'organizer' mzuri sana wa watu wake. Na watu wake walimsikiliza sana.
 
Nguruvi3,

..ingependeza sana kama tungeweza kupata details za jaribio lililo-fail wa kumpindua Iddi Amin.

..jaribio hilo ilikuwa lihusishe mashambulizi ya askari wa majini na nchi kavu, pamoja na kuivamia Entebe kwa kutumia askari waasi watakaotua na ndege ya kiraia.

..something went terrible wrong, ambapo ilishindikana kuwarusha askari kwa ndege, na wale waliokuwa nchi kavu waligundulika na Amini na kusambaratishwa vibaya.

..hii habari imefanywa siri Tanzania, lakini waandishi mbalimbali wa Kiganda wameandika kuhusu tukio hili.

NB:

..Wamarekani walipo-fail kuwaokoa mateka wao Teheran hawakufanya siri.

..They went back to the drawing board na kikosi kilichomuua Osama Bin Laden, asili yake ni kikosi kilichoshindwa wakati wa operation eagle claw.
 
Rev.Kishoka,Gustanza-The,kichuguu,Jasusi,

.........

NB:

..binafsi napinga sana hujuma za kiuchumi zilizotokea wakati wa Mkapa. lakini kuna shutuma dhidi yake hapa ambazo hazina msingi kabisa.

..kitendo cha Mkapa "kumfuta jasho" Chief Fundikira, au Bibi Mohamed Titi, naamini kilikuwa cha kiungwana.

..siyo kweli kwamba Mkapa alikuwa akisaidia "maadui" wa Mwalimu. Mkapa alifikia mpaka kumsaidia Mzee Timothy Apiyo[chief secretary wa Mwalimu] aliyekuwa amesahaulika akiugua kule Ukonga.

..Mkapa huyo huyo akamsaidia Mzee Mourice Nyunyusa ambaye RTD ilitumia midundo yake bila kumpa malipo yoyote.

..Mkapa kwa misaada yake mpaka akapewa heshima ya kuwa mwana-ukoo wa kina Nyerere.

Hapo kwenye bold, jee adui ni yule aliyetafautiana na Nyerere? Na ndiyo maana kulikuwa na 'zidumu fikra sahihi za Mwalimu Nyerere', alikuwa hapendi kupingwa.
 
Nguruvi3,

..ingependeza sana kama tungeweza kupata details za jaribio lililo-fail wa kumpindua Iddi Amin.

..jaribio hilo ilikuwa lihusishe mashambulizi ya askari wa majini na nchi kavu, pamoja na kuivamia Entebe kwa kutumia askari waasi watakaotua na ndege ya kiraia.

..something went terrible wrong, ambapo ilishindikana kuwarusha askari kwa ndege, na wale waliokuwa nchi kavu waligundulika na Amini na kusambaratishwa vibaya.

..hii habari imefanywa siri Tanzania, lakini waandishi mbalimbali wa Kiganda wameandika kuhusu tukio hili.

NB:

..Wamarekani walipo-fail kuwaokoa mateka wao Teheran hawakufanya siri.

..They went back to the drawing board na kikosi kilichomuua Osama Bin Laden, asili yake ni kikosi kilichoshindwa wakati wa operation eagle claw.

jokaKuu,
Ameeleza vizuri kisa hicho David Martin katika kitabu chake Idi Amin.
 
Kwamba JWTZ hawakushirikishwa ktk operation ya kwanza ya kumg'oa Idd Amin inaweza kuwa kweli iliwaudhi hasa madhara ambayo yangetokea kutokana na uwezo wa Uganda wakati ule huku wao wakiwa ndio walinzi wakuu wa nchi.
Binafsi nilisikia walipelekwa wanamgambo ambao kikosi kizima kiliteketea.hofu ni kuwa kuna uwezekano mkubwa JWTZ kuhujumu mpango ule kwa jinsi mipango yote ya JKT ilivyofeli tena wakati wapiganaji wakiwa ktk uwanja wa mapambano!
Inawezekana hujuma ilikuwa kuzuia wanamgambo kuvuka mpaka au kupunguza madhara ambayo yangetokea kwa nchi hasa Idd Amin akijibu mapigo huku wao hawajajiandaa,kweli Amin alijibu mapigo na Bukoba na Mwanza walikiona cha mtemakuni ingawa JWTZ walijitahidi kujibu mapigo kujihami bila kuzidi kumchokonoa Amin aliyekuwa tayari kwa lolote!
Tunashukuru wakuu wote mliochangia ktk thread hii,mmetoa elimu kubwa na hakika thread hii itakuwa ya kufunga mwaka.
 
Hivi Kikwete anapenda kupingwa?

Jee kuna slogan ya 'zidumu fikra sahihi za mwenyekiti JK'? Na ndiyo maana unaona kila leo anatukanwa shiba ya waandishi na wanaopenda lakini ni mara chache sana huwa anachukuwa hatua.

Enzi za Mwalimu kweli ungeweza kufanya robo ya wanayofanya watz hivi sasa?

Give the devil his due bwana.
 
Asante kwa shule Jobo...



First of all, hii paper sio ya ki-shule. Ni paper ambayo inaelezea hali ya ki-siasa ya Tanzania tangu tupate uhuru mpaka leo hii. So, nikuondoe wasiwasi mkuu, haitakuwa graded.

Also, I know that these are confidential info, ndo' maana nikaamua kuweka hii issue hapa JF. Kwasababu, nimekusanya baadhi ya info toka kwa watu waliokuwa serikalini kipindi hicho, lakini maelezo yao yanaonyesha kama kuna kitu hawataki kufichua...

JF ni chama kubwa, na ninaimani kuwa kuna watu wanafahamu hii issue vizuri, wenye uwezo wa kutupatia info nzuri kuliko wengi wenu mnavyodhani/underestimate. So, ninachotafuta hapa ni leads. Plus, nikishakusanya hizo unazoziita "substantive facts," nitazifanyia vetting tena na tena na tena.

Mkuu naomba katika research yako ufuatilie na issue hii nadhari akuna mahali popote ambapo imezungumzwa au kuandikwa lakini kwa kweli iliumiza watu wengi sana katika miaka ya 1978 ambapo watu wengi ambao walikuwa wasomi (elite) jeshini na Usalama wa Taifa waliachishwa kazi bila sababu yeyote ya msingi na wakatakiwa warudi Vijijini kwao walipo zaliwa. Wengi wa watu walioachishwa walikufa kwa msongo wa mawazo kwa sababu waliachishwa kazi bila sababu na hawakupewa staili zao wanazostahili baada ya kuachishwa kazi, wengi walikuwa wasomi wakubwa tu kwenye Taasisi ya Jeshi na Usalama wa Taifa na wengine ndo kwanza walikuwa kwanza wametoka kwenye masomo katika nchi za Ulaya (Romania, Urusi, East Germany) na ata wengine waliachishwa kazi wakiwa huko huko masomoni. Mchakato wote huu ulisimamiwa na Sokoine. Mkuu huu si uzushi ni ukweli mtupu, fuatilia hii issue na utabaki mdomo wazi. Na mbaya zaidi wale wote walioachishwa kazi walikuwa wanafuatiliwa huko Vijijini na watu wa Usalama, wengi wa watu hawa (Elite) walikufa kwa mawazo, so fuatilia hii ili watanzania waelewe ukweli watakaposoma "PAPER" yako.
 
I have read this thread and discovered that JF OF THOSE DAYS IS NOT THE SAME AS THE ONE OF TODAY.WAKUU, the depth and the content in each comment is amazing. I wish the veterans like Kundi and Fieldmarshal could maintain the spirit. There is a lot we "the new comers" can learn from this thread. Hope the coming 2012 will bring in depth contributions to flouted threads. Happy New Year (2012) to all Pioneers, veterans and members of this Great Great forum
 
I have read this thread and discovered that JF OF THOSE DAYS IS NOT THE SAME AS THE ONE OF TODAY.WAKUU, the depth and the content in each comment is amazing. I wish the veterans like Kundi and Fieldmarshal could maintain the spirit. There is a lot we "the new comers" can learn from this thread. Hope the coming 2012 will bring in depth contributions to flouted threads. Happy New Year (2012) to all Pioneers, veterans and members of this Great Great forum
Bado vichwa kibao vipo active kama FMes,Jasusi,Joka kuu,Mwanakijiji n.k tatizo watu wanataka stori za ma godfather ENL,RA! Hatuibui mada kama hizi zinazotaka ufahamu wa historia uone nondo zitavyoshuka mkuu!
 
Kudokoa kidogo nje ya mada:

Katika jeshi kuna platoon yenye askari kati ya 16-50, halafu combania inayoundwa na platoon 3,4 au 5, na kombania ndizo zinaunda kikosi chenye askari kati ya 1000 na kadhaa. Mkusanyiko wa vikosi ndio unaunda brigade. Hata hivyo inaweza kubadilika kutoka muundo mmoja wa jeshi hadi mwingine.

Jeshini kuna kitu kinaitwa 'sleeping general' kwa hiyo ustaafu wa hawa ma-general sio ustaafu wa kawaida

Kama mlifuatilia mwaka jana(kama si huu) kuna sherehe kubwa ilifanyika kumuaga General mmoja anaitwa Msuya. Ukifuatilia vita vya Kagera katika kwa umakini jina la Msuya halikosekani na wakati huo akiwa kanali. Moja ya mambo aliyoyafanya ni kuongoza kikosi kilichoiteka Kampala. Huyu bwana ni moja ya 'unsang heroes' lakini historia ina hukumu ya kweli kwani jina lake linajitoleza sana hasa katika vita. Katika hao unsang yupo pia brigadier general Ambrose Bayeke

Nadhani jina la general anayetajwa katika mada hii ni Mirisho na si Mrisho kama sijakosea. Upandaji wa wake wa vyeo kutoka captain hadi CDF unafikirisha kidogo.

Happy new year 2012
 
Nguruvi3,

..tatizo letu liko kulekule kwamba hatuna utamaduni wa kuweka kumbukumbu zetu za kihistoria wazi.

..kwenye nchi za wenzetu ungekuta tayari kuna vitabu vya maisha na experiences za makamanda wote waliopigana vita kubwa kama ile ya Kagera, au ya Msumbiji.

..juu ya hayo pia kungekuwa na kumbukumbu ya matukio au mapigano muhimu kama yale ya Lukaya, au urejeshaji wa eneo la daraja la kagera, etc etc.

..wakati wa vita vya Kagera, Major General.Ben Msuya[then Lt.Col] alikuwa chini ya kamandi iliyokuwa ikiongozwa na General.David Musuguri[then Major.Gen]. sasa Lt.Col.Msuya ndiye inaripotiwa kuwa ndiye kamanda wa kwanza wa Kitanzani kuingia Kampala!!

..unapozingatia kwamba wakati huo serikali moja ilianguka, na ikabidi kusimikwe serikali nyingine, ndiyo utagundua uweledi na ufanisi wa askari wetu pamoja na makamanda waliokuwa wakiwaongoza.

..hata hii habari tunaweza kuizungumzia kwasababu wapo waandishi wa Kiingereza waliokuwa embedded na vikosi vya JWTZ vilivyokuwa mstari wa mbele kuiteka Kampala. Waandishi na wanahistoria wa Tanzania have never shown any interest kuli-document tukio lile. Kitu cha kusikitisha ni kwamba sasa hivi makamanda wengi walioongoza vita ya Kagera wametangulia mbele ya haki.

NB:

..jina kamili la mhusika mkuu wa mada hii ni MIRISHO SAM HAGGAI SARAKIKYA.

..wakati wa maasi ya 1964 alikuwa na cheo cha Captain. wakati huo hakukuwa na Mtanganyika aliyekuwa na cheo kikubwa zaidi ya hicho.

..sasa kwasababu Tanganyika Riffles ilikuwa chini ya Afisa wa Kiingereza aliyekuwa na cheo cha Brigadier. Cheo cha Brigadier General nimeanza kukisikia miaka ya karibuni.

..baada ya Tanganyika Riffles kuvunjwa na kuanzishwa JWTZ/TPDF, Mirisho Sarakikya aliteuliwa kuwa Chief of Defence Forces, na kupandishwa ngazi kuwa Brigadier.

..Mkuu wa utawala wa Jeshi, au Chief of Staff, wa kwanza wa JWTZ alikuwa ni Major.Elisha Kavana ambaye alikuwa na cheo cha 1st Lieutenant.
 
Sarakikya hajawahi kuhusishwa na kesi ya uhani.Kwa kifupi wanajeshi wa vyeo vya chini walitishia kupindua nchi punde tu baada ya uhuru wakikwera na uongozi wa Brigedia mwingereza na mshahara mdogo.Kuchaguliwa kwa Brigedia mwingereza kulitokana na ukweli kuwa kulikuwa hakuna mtanzania aliyefikia cheo cha kuweza kuwa CDF maana mkoloni ali-limit vyeo kwa watu weusi.Wakati huo Sarakikya alikuwa kapteni na hakuhusika ndio maana alikamatwa na kutiwa ndani na wanajeshi wenzake waongoza mgomo maana alichukuliwa kama mmoja wa wasaliti kwa kuwa umande hakukimbia kawa wengi wao wakati huo.Nyerere alidharau mgomo huo mpaka aliposhauriwa na kawawa kuwa hali si nzuri na ikabidi afichwe kwa muda.Mpaka leo sehemu alipojificha inabakia kuwa siri iliyofichwa vizuri katika historia ya nchi hii?Oscar Kambona ndie aliyekuwa mediator kati ya serikali na wanajeshi hao wenye hasira na alifanikiwa kuwatuliza baada ya purukushani za hapa na pale ambazo sitaweza kuziweka hapa kwa sababu ya muda.Inasemekana Kambona alikuwa na lengo moja na wanajeshi waasi ila alibadili mawazo baada ya kuona wanajeshi hao wana akili ya kibangi bangi na hasira zilizopitiliza.Baada ya fujo kutulia Nyerere aliibuka kutoka mafichoni akifikiria mambo shwari.Mwalimu akatumia ujanja wa kutoa amri kuwa atafika lugalo kukagua gwaride kwa hiyo kila askari awe tayari.Wanajeshi waasi walikataa kama mwanafunzi mtukutu anapokataa kutii amri ya mwalimu ya kufanya usafi.Inasemekana kila askari aliendelea na shughuli zake kama amri hiyo haijatoka kwa amiri mkuu.Jaribio lingine la mwalimu lilishindwa na ndipo alipogundua kuwa jeshi limekosa utii kwakwe na kugundua mpango wa kumpindua huko pale pale.Aliomba msaada wa Majeshi ya Uingereza na Malikia akatuma makomando wachache na helikopta.Ndani ya masaa machache sana wanajeshi wa Tanzania walisalimu amri pasipo umwagaji wa damu baada ya ACTION ndogo tu kutoka kwa vijana wa malikia.Ndipo nyerere alipomrudisha nyumbani Brigedia mwingerez,kuunda jeshi jipya la JWTZ,kuongeza mshahara na KUMRUSHA CHEO SARAKIKYA KUTOKA KAPTENI MPAKA BRIGEDIA NA KUMTEUA KUWA CDF wa kwanza wa jwtz mzawa wa Tanganyika.Sarakikya alistaafu kishujaa kama Meja Jenerali na kutokana na mchango wake mkubwa Mkapa alimpandisha kwa hesima mpaka Jenerali kamili cheo hata baada ya kuwa alishastaafu.Mtiririko wa yeye kupanda vyeo haujawahi tokea Tanzania na sidhani kama itajirudia.

Nikusahihishe kidogo, Sarakikya alipandishwa cheo kwanza kuwa generali ndipo akastaafu, hakupandishwa cheo akiwa amestaafu.
 
Nguruvi3,
..tatizo letu liko kulekule kwamba hatuna utamaduni wa kuweka kumbukumbu zetu za kihistoria wazi.

..kwenye nchi za wenzetu ungekuta tayari kuna vitabu vya maisha na experiences za makamanda wote waliopigana vita kubwa kama ile ya Kagera, au ya Msumbiji.

..juu ya hayo pia kungekuwa na kumbukumbu ya matukio au mapigano muhimu kama yale ya Lukaya, au urejeshaji wa eneo la daraja la kagera, etc etc.

..wakati wa vita vya Kagera, Major General.Ben Msuya[then Lt.Col] alikuwa chini ya kamandi iliyokuwa ikiongozwa na General.David Musuguri[then Major.Gen]. sasa Lt.Col.Msuya ndiye inaripotiwa kuwa ndiye kamanda wa kwanza wa Kitanzani kuingia Kampala!!

..unapozingatia kwamba wakati huo serikali moja ilianguka, na ikabidi kusimikwe serikali nyingine, ndiyo utagundua uweledi na ufanisi wa askari wetu pamoja na makamanda waliokuwa wakiwaongoza.

..hata hii habari tunaweza kuizungumzia kwasababu wapo waandishi wa Kiingereza waliokuwa embedded na vikosi vya JWTZ vilivyokuwa mstari wa mbele kuiteka Kampala. Waandishi na wanahistoria wa Tanzania have never shown any interest kuli-document tukio lile. Kitu cha kusikitisha ni kwamba sasa hivi makamanda wengi walioongoza vita ya Kagera wametangulia mbele ya haki.

NB:
..jina kamili la mhusika mkuu wa mada hii ni MIRISHO SAMA HAGGAI SARAKIKYA.
..wakati wa maasi ya 1964 alikuwa na cheo cha Captain. wakati huo hakukuwa na Mtanganyika aliyekuwa na cheo kikubwa zaidi ya hicho.
..sasa kwasababu Tanganyika Riffles ilikuwa chini ya Afisa wa Kiingereza aliyekuwa na cheo cha Brigadier. Cheo cha Brigadier General nimeanza kukisikia miaka ya karibuni.
..baada ya Tanganyika Riffles kuvunjwa na kuanzishwa JWTZ/TPDF, Mirisho Sarakikya aliteuliwa kuwa Chief of Defence Forces, na kupandishwa ngazi kuwa Brigadier.
..Mkuu wa utawala wa Jeshi, au Chief of Staff, wa kwanza wa JWTZ alikuwa ni Major.Elisha Kavana ambaye alikuwa na cheo cha 1st Lieutenant.
Joka kuu, nashukuru sana umenikumbusha hili la Mirisho. Ni kweli kama ulivyosema.
Pili, upo sahihi sana kwamba hatuna utamaduni wa kuweka kumbu kumbu. Ingekuwa ni kwa wenzetu vita kama ya Kagera ingekuwa na vitabu kama 10 au zaidi. Yupo ambaye angeandika kuhusu Maandalizi ya vita tu, mwingine kutangazwa vita, Kukomboa daraja, Lukaya, mbarara, Kampala n.k.

Inasikitisha sana kuona mtu kama Gen Mayunga na Gen Walden wametangulia mbele ya haki na sidhani kama zipo kumbu kumbu za kina kuhusu wao.

Mtu kama Lt Gen Tumaini Kiwelu ni muhimu sana katika kumbu kumbu. Inasemwa kuwa ndiye aliyewahi kuhoji kwanini RENAMO na FRELIMO mtu na mjomba wake wapigane halafu askari wetu washiriki vita. Kauli yake ilibadili sana mtazamo wa Tanzania kuhusu msumbiji na ikatia msukumo zaidi wa mazungumzo badala ya silaha

Labda tutoe changamoto kwa wana historia na waandishi wa habari kwenda kuongea na watu kama kina Kiwelu, Bayeke, Ben Msuya, Musuguri, Kiyaro, Mahufudhi, na wengine ili kuweka kumbu kumbu sawa.
Ukiangalia kwa makini kuna ajira nzuri sana hapo.

Waandishi wa habari hivi hamuwezi kuandika documentary. Kama kuna watu wana documentary ya 80-100 years na inaleta hisia kwanini ishindikane kitu cha miaka 30 tu iliyopita.

Mleta mada chukua dondoo ziwe 'lead' katika kazi yako na fanyia kazi kupata details na facts, wazo lako zuri sana keep it up.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom