Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

JokaKuu
NB:

..jina kamili la mhusika mkuu wa mada hii ni MIRISHO SAM HAGGAI SARAKIKYA.

..wakati wa maasi ya 1964 alikuwa na cheo cha Captain. wakati huo hakukuwa na Mtanganyika aliyekuwa na cheo kikubwa zaidi ya hicho.

..sasa kwasababu Tanganyika Riffles ilikuwa chini ya Afisa wa Kiingereza aliyekuwa na cheo cha Brigadier. Cheo cha Brigadier General nimeanza kukisikia miaka ya karibuni.

..baada ya Tanganyika Riffles kuvunjwa na kuanzishwa JWTZ/TPDF, Mirisho Sarakikya aliteuliwa kuwa Chief of Defence Forces, na kupandishwa ngazi kuwa Brigadier.

..Mkuu wa utawala wa Jeshi, au Chief of Staff, wa kwanza wa JWTZ alikuwa ni Major.Elisha Kavana ambaye alikuwa na cheo cha 1st Lieutenant.

Mkuu kuna uvumi uliokuwepo katika kipindi cha maasi ya 1964 kuwa kulikuwa na ushindani wa vyeo kati ya Elisha Kavana na Sarakikya kiasi kwamba Mnyamwezi Kavana akachongewa kuwa alikuwa ndie engineer wa maasi. Kavana tokea pale hakusisikika tena na sijui yuko wapi msomi machachari huyu aliye pata first class ya units 9 - akifanya masomo 9 na kila somo unit 1 ambayo ilikuwa ndo VERY GOOD.

Pili
: historia inataka potoshwa hapa kwamba Jeshi la Wananchi (JWTZ) liliundwa na waingereza waliokuja kuwa disarm wale wa KAR walioasi. Si kweli hapa lazima tujivune waafrika kuwa jeshi letu lilifundishwa na wa NIGERIA baada ya Mwalimu kuziomba nchi za kiafrika zijitoe kuchukua nafasi ya kuilinda tanganyika badala ya majeshi ya Mwingereza wakati tulikuwa tunaonekana kuunga kwa vitendo ukombozi wa africa.

Tatu: si kweli kabisa kuwa askari waasi walisalimu amri kirahisi kwa jeshi la uingereza. pale carito walipambana na mkurya aliewachachafya sana na resistance kubwa waliipata Tabora kwani walishapata taarifa hivyo wakawa na muda wa kujiandaa kuukabili uvamizi. kwa vyovyote vile walishindwa ukichukulia uduni wa vifaa vya kivita. wale wa carito walifanyiwa mbinu ya kuleweshwa usiku uliotangulia kwa kile kilichoelezwa ni tafrija ya kusheherekea mafanikio ya maasi baada ya "MAKUBALIANO" na Serikali kuhusu madai yao.

Nne
: nchi hii ilikuwa na idadi ya watu takriban 9 milioni - na dar ilikuwa ndogo kiasi cha habari watu kupasiana kirahisi. watu watakumbuka hata Mwalimu aliweza isoma orodha ya watu "waongo" na TBC ikawa inayasoma majina hayo kila baada ya taarifa ya habari. inawezekana sarakikya kuhusika na moja ya uasi ambapo inasemekana nyerere alimwita na kumpa bunduki ampige yeye kuliko kuiharibu nchi. swala hapa ni je uasi katika phase ipi - baada ya maasi ya 1964 kulikuwa na phases za uasi au majaribio ya kuiangusha serikali ya mzanaki sio chini ya tatu mojawapo ikiishia kuhukumiwa Mahakama kuu. kina Ilonsi wako wapi jamani.
 
Ni kweli Sarakikkya hakuhusika na jaribio la mapinduzi yoyote yale. Oscar Kambona(Waziri wa ulinzi na mambo ya nje) alihusishwa pamoja na Job Malecela Lusinde(Waziri wa mambo ya ndani na Usalama wa Taifa na kaka wa John Samuel Malecela aka Tingatinga) Hata hivyo, studies zinaonyesha uchunguzi unaonyesha Mzee Lusinde(ambaye bado yuko hai) hakuhusika hata kidogo. Kuanzia hapo mahusiano ya Mr Handsome guy Oscar Kambona(Son of an Anglican priest Salatiel Kambona) na Julius Nyerere yalianza kuharibika. Tamaa ya kupenda madaraka na rafiki zake akina Sajenti Ilogi ikamtumbukia nyongo.
 
Kwa idadi ya askari iliyokuwa nayo Tanzania wakati wa Sarakikya protocol hazikuruhusu kuwa na askari wa cheo cha jenerali. Hivyo, akastaafu jeshi akiwa si jenerali. Mkapa na washauri wake wakaona si busara mtu aliyewa train askari wengi kuwa brigedia wakati wanafunzi wake wakiwa ndio majenerali. Walichofanya ni kumpa ujenerali na kumstaafisha siku hiyo hiyo ili angalau CV yake isomeke alistaafu akiwa jenerali.
 
Machief waliondolewa mamlaka nchini na kubaki na prestigious status. Hapo ni km Nyerere alijua alichokuwa anafanya kwani akateuliwa Chief Mazengo kuwa mwenyekiti wa machief wote nchini. Kuanzia hapo Chief Mazengo akawa rafiki na mtu wa karibu na Nyerere hadi kupewa heshima ya kuwakilisha machief wote kwenye siku ya Muungano tarehe 26.04.1964.
 
General Sarakikya alihamishwa JWTZ sometime in early 1974 na akafanywa waziri wa utamaduni na michezo. Sababu za kutolewa JWTZ hazikutangazwa lakini nafasi yake kama CDF ilichukuliwa na Gen Twalipo ambaye alikuwa RC wa Kagera nafikiri. Mwalimu pia alicreate new strcture kama nafasi ya Chief of Staff ambayo alimteua Brig. Nkwera au Mkwera na Western and Eastern Brigades ambapo aliwateua Col. Mayunga na Musuguri na kuwapandisha vyeo kuwa Ma-Brigediar. Pamoja na Sarakikya pia walihamishwa toka JWTZ quite a number of officers -Col. Marealle; Lt. Col Metili & Kibola; Ma-Major Ndosi & Mrema pamoja na several officers at Captain and Lieut. level e.g. Mushi; Nkya; Ihula; Bob Nasser etc. Most of them were from the Kilimanjaro/Arusha regions. They were transferred to senior positions in parastatals and the civil service. It was this transfer which led to rumours that there was something brewing in the JWTZ aganst the government.

It is important to recognize kuwa mabadiliko haya yalitokea baada ya the first invasion of Uganda by Uganda rebels based in TZ through Mutukula. Invasion hii ambaye ilitokea July 1972 failed very badly and the invaders were routed by Idi Amin who also bombed Bukoba and Mwanza. This routing of the rebels led to the Mogadishu peace agreement between TZ na Idi Amin - John Malecela was the Foreign Minister and he led the TZ delegation to Mogadishu and he did an excellent job in getting this agreement from the ugandans as legally Tanzania was in the wrong as she had allowed the guerillas to invade Uganda kutoka kwenye ardhi yake against the provisions of OAU charter.

According to David Martin's book Idi Amin - the 1972 invasion of Uganda had been superintended by the National Service and JWTZ were not involved but when it failed it was the JWTZ who were in the trenches defending the country. National Service then was being led by lawrence Gama - ambaye aliyekuwa amemuoa dadake yake mwalimu.

The whole invasion created some dis-quiet in the JWTZ especially among the educated officer corp most of whom had been trained in Canada & Britain. In fact the JWTZ had two types of officers those who had come through the NCO route - like Musuguri; Kyaro; Twalipo; Chacha etc and those who had come through the cadet route like Marealle; Kombe, Mayunga; Kiwelu; Mwakandalile; Wolden etc. These two groups of officers were not often talking the same language as they had very different educational backgrounds. Further given the Ujamaa policies being pursued then the educated officers labda uaminfu wao kwa siasa hiyo ulitiliwa mashaka.
QUOTE]

Sasa naamini maneno ya Mtei kwamba Tanzania hatukupaswa kupigana vita ya Kagera ila kwa sababu ya ushikaji wa Nyerere na Obote.
Jambo lingine linalojitokeza wazi hapa ni kuwatenga wasomi kwenye nafasi za maamuzi nyeti kwa taifa letu ili kutoa mwanya kwa kuruhusu maamuzi ya kijinga yafanyike. Kwa vyovyote vile wasomi hawakuona sababu ya kuliingiza taifa letu changa kwenye vita ya kiushikaji wakati taifa lina mambo mengi ya msingi ya kufanya ili kuliondoa taifa katika umasikini. Si ajabu taifa letu kuendelea kuwa taifa omba omba baada ya zaidi ya miaka 50 ya uhuru kwani hakuna taifa lolote lile duniani lililoendelea kwa kuwatenga wasomi wake.
Lakini vilevile kuna hii conspiracy theory ya CCM kuhakikisha kwamba Raisi wa Tanzania hatokei maeneo ya kaskazini. Ni wazi kwamba muendelezo huo hapo juu una confirm dhana hii na kwamba CCM wamechiwa mikoba hii ya kuwatenga watu wa kaskazini kwenye utawala wa nchi na Nyerere.
Mungu ibariki Tanganyika. Mungu ibariki Africa.
 
Sarakikya alikuwa ni askari wa ukweli. alisomea sandhursrt
huko uingereza. Lakini hakujihusisha na uhaini. Hata HIVYO tANZani NI NCHI ya majungu kwa hiyo wapo wliomuhusina uhaini kwa malengo yao.​
 
Sarakikya alikuwa ni askari wa ukweli. alisomea sandhursrt
huko uingereza. Lakini hakujihusisha na uhaini. Hata HIVYO tANZani NI NCHI ya majungu kwa hiyo wapo wliomuhusina uhaini kwa malengo yao.​

Vijana waliotoka Africa na kusoma Sandhurst ni kama walilishwa bangi kule walivyorudi nyumbani kukatokea milipuko ya majaribio ya mapinduzi karibu Africa yote - baadhi yalifanikiwa na mengine kushindwa yakiwemo ya Afrika Mashariki. Sarakikya si pekee aliepitia Sandhurst - kina Kavana na badae kina Mboma na kina Munthali etc..

Huyu mtafiti katika thread hii ajaribu pia kuwatafuta watangazaji wa TBC enzi hizo kama kina Suleiman Hegga na wandishi wa habari wa enzi hizo - hawa walikuwa karibu sana na habari za kila siku za nchi hii ambayo haikuwa so complex kama ilivyo hivi sasa.
 
Hivi nani alihusika na vipeperushi toka angani na kuzagaa mitaani kuonyesha picha ya huzuni ya Mwalimu nyerere na picha ya Kambona aliekuwa na furaha na bashasha?
Vipeperushi hivi vilifuatiwa na msururu wa magari ya kivita yaliyokuwa yakipita mitaani kila siku utadhani nchi ilikuwa ktk vita!
 
Sasa naamini maneno ya Mtei kwamba Tanzania hatukupaswa kupigana vita ya Kagera ila kwa sababu ya ushikaji wa Nyerere na Obote.
Jambo lingine linalojitokeza wazi hapa ni kuwatenga wasomi kwenye nafasi za maamuzi nyeti kwa taifa letu ili kutoa mwanya kwa kuruhusu maamuzi ya kijinga yafanyike. Kwa vyovyote vile wasomi hawakuona sababu ya kuliingiza taifa letu changa kwenye vita ya kiushikaji wakati taifa lina mambo mengi ya msingi ya kufanya ili kuliondoa taifa katika umasikini. Si ajabu taifa letu kuendelea kuwa taifa omba omba baada ya zaidi ya miaka 50 ya uhuru kwani hakuna taifa lolote lile duniani lililoendelea kwa kuwatenga wasomi wake.
Lakini vilevile kuna hii conspiracy theory ya CCM kuhakikisha kwamba Raisi wa Tanzania hatokei maeneo ya kaskazini. Ni wazi kwamba muendelezo huo hapo juu una confirm dhana hii na kwamba CCM wamechiwa mikoba hii ya kuwatenga watu wa kaskazini kwenye utawala wa nchi na Nyerere.
Mungu ibariki Tanganyika. Mungu ibariki Africa.[/QUOTE]



Kwa hiyo unatuambia kuwa sasa ni wakati wa Chadema kuachiwa nchi ili nao wapendelee Kaskazini na kutawala kimajimbo kwa mujibu wa sera zao? Mimi binafsi simuamini Mzee Mtei kwani aliasisi Chadema kwa misingi ya ukabila wee angalia maana ya neno CHADEMAA ni kuchechemea kwa maana ya lugha za kichaga!
Sasa Mtei alikosa jina la kiswahili mpaka atuanzishie chama kwa jina la kichaga? huo sio ukabila?

Mbowe ni Mkwe wake kamuolea Mwanae!, ndio maana kila anachotamka Mbowe, Mtei anamuunga mkono! Mbona Zito akisema anataka kugombea Urais Mzee Mtei anakuja juu! lakini Mbowe akisema Slaa tosha! Mtei nae vivyo hivyo!

Mwalimu Nyerere alipohutubia UN kudai uhuru 1958, Mangi Mareale nae akaenda kuhutubia na kusema wa TZ bado hawajaiva kujitawala! huyu alikuwa Mchaga alieonyesha undumilakuwili! Sasa wanataka kuongoza nchi huku wanaukabila kihivyo!

We angalia wenyeviti wote wa vyama vikuu vya upinzani ni Wachaga, Lyatonga Mrema, James Mbatia, Freeman Mbowe nk. Kaskazini kuna maendeleo na upendeleo wa makusudi huko mchango wao kwa pato la taifa ni mdogo! lakini hawana shukrani badala yake wanapinga kila kitu!
 
zubeda, Kisindika,

..Mzee Edwin Mtei ni member wa JF.

..alieleza hapa kwamba akiwa waziri wa fedha wakati wa vita vya kagera hakuwahi kutoa ushauri wa kupinga vita ile.

..hoja ya Mzee Mtei ilikuwa kwamba, mzalendo yeyote yule wa Tanzania asingeweza kutoa ushauri kwamba wa-Tanzania wasijilinde kutokana na uvamizi wa Iddi Amin na majeshi yake.
 
Last edited by a moderator:
JokaKuu


Mkuu kuna uvumi uliokuwepo katika kipindi cha maasi ya 1964 kuwa kulikuwa na ushindani wa vyeo kati ya Elisha Kavana na Sarakikya kiasi kwamba Mnyamwezi Kavana akachongewa kuwa alikuwa ndie engineer wa maasi. Kavana tokea pale hakusisikika tena na sijui yuko wapi msomi machachari huyu aliye pata first class ya units 9 - akifanya masomo 9 na kila somo unit 1 ambayo ilikuwa ndo VERY GOOD.

Pili
: historia inataka potoshwa hapa kwamba Jeshi la Wananchi (JWTZ) liliundwa na waingereza waliokuja kuwa disarm wale wa KAR walioasi. Si kweli hapa lazima tujivune waafrika kuwa jeshi letu lilifundishwa na wa NIGERIA baada ya Mwalimu kuziomba nchi za kiafrika zijitoe kuchukua nafasi ya kuilinda tanganyika badala ya majeshi ya Mwingereza wakati tulikuwa tunaonekana kuunga kwa vitendo ukombozi wa africa.

Tatu: si kweli kabisa kuwa askari waasi walisalimu amri kirahisi kwa jeshi la uingereza. pale carito walipambana na mkurya aliewachachafya sana na resistance kubwa waliipata Tabora kwani walishapata taarifa hivyo wakawa na muda wa kujiandaa kuukabili uvamizi. kwa vyovyote vile walishindwa ukichukulia uduni wa vifaa vya kivita. wale wa carito walifanyiwa mbinu ya kuleweshwa usiku uliotangulia kwa kile kilichoelezwa ni tafrija ya kusheherekea mafanikio ya maasi baada ya "MAKUBALIANO" na Serikali kuhusu madai yao.

Nne
: nchi hii ilikuwa na idadi ya watu takriban 9 milioni - na dar ilikuwa ndogo kiasi cha habari watu kupasiana kirahisi. watu watakumbuka hata Mwalimu aliweza isoma orodha ya watu "waongo" na TBC ikawa inayasoma majina hayo kila baada ya taarifa ya habari. inawezekana sarakikya kuhusika na moja ya uasi ambapo inasemekana nyerere alimwita na kumpa bunduki ampige yeye kuliko kuiharibu nchi. swala hapa ni je uasi katika phase ipi - baada ya maasi ya 1964 kulikuwa na phases za uasi au majaribio ya kuiangusha serikali ya mzanaki sio chini ya tatu mojawapo ikiishia kuhukumiwa Mahakama kuu. kina Ilonsi wako wapi jamani.
MAKAH,

..habari zote nilizoandika hapa nimezipata kwenye kitabu kinachohusu maasi ya 1964.

..kwa uelewa wangu, Kavana aliteuliwa kuwa Chief of Staff wa kwanza wa JWTZ akiwa na cheo cha Major.

..ila sijui Major.Kavana aliondoka jeshini mwaka gani, na katika mazingira gani. labda tumtafute Kudi Shauri, Kichuguu, Moshe Dayan, Nyenyere, wanaweza kutusaidia hapa.

..hata mimi sielewi kwanini mchango wa jeshi la Nigeria ktk kufundisha askari wa mwanzo wa JWTZ hauwekwi wazi. Wanigeria pia wametoa mchango mkubwa sana ktk harakati za ukombozi wa Afrika haswa kupitia ile kamati ya Frontline States.

NB:

..je, uliposema "Ilonsi" ulikuwa unamaanisha Sgt.Hingo Ilogi ambaye alikuwa kiongozi wa maasi ya 1964?
 
Last edited by a moderator:
MAKAH na JokaKuu.


Pamoja na uzalendo wetu; ukweli ni kuwa jeshi la uingereza likiwa na kikosi cha makomandoo wapatao 50 pamoja na kikosi cha mizinga cha majini ndio waliovunja maasi yale na lile jeshi la Tanganyika Rifles kuvunjwa.

Kuna ushahidi mwingi sana kuwa Kambona ndiye aliyechochea askari wale waasi kwa kuwa anapingana na amri za makamanda wa jeshi, na kuwa anawaahidi mambo ambayo hayakuwa yametoka serikalini. Kukawa na mvutano sana baina ya Kambona na mkuu wa majeshi wakati huo Brigadier Douglas kuhusu training za askari, ambapo Douglas alitaka maofisa jeshi wawe trained Sandhurst kama ilivyokuwa kwa Captain Alex Nyirenda (aliyekuwa na cheo cha juu sana wakati huo) pamoja na Lt Sarakikya na 2nd Lt Kavana waliosomea Sandhurst. Wakati huo Alex Nyirenda akiwa Deputy Adjutant wa Colito, alikuwa na masimamo huo huo wa kijeshi ambao Kambona hakupenda, na hivyo kusababisha Nyirenda asipendwe na askari wa kiswahili waliotaka mambo ya kijeshi yaendeshwe kienyejienyeji. Kambona alikuwa analeta maafisa wa jeshi kutoka nchi nyingine kwa mfano aliwahi kuajiri Luteni Kanali mmoja kutoka East German kufanya makao makuu ya jeshi ambayo yalikuwa yanaongozwa na waingereza. Alikuwa anapeleka vijana kwenda kusoma israel ili wakirudi wawe maofisa chini ya command ya waingereza bila ridhaa ya genera Douglas; mipango hiyo ya Kambona ilichangia sana kuweka mvurugano jeshini.

Maandiko mengi yamekuwa yakionyesha kambona na Okelo kuwatuliza askari wale lakini ni kwa sababu Kambona alikuwa ni rafiki yao, na walikuwa wanaamini kuwa Nyerere na Kawawa wameshakaimbia na hivyo, Kambona ndiye atakuwa Rais. Jeshi la Uingereza lilipofika liliwafumua sana na kuwakamata viongozi wote wa maasi yale na kuwashitaki katika court martial.

Wakati wa maasi, Nyerere aliomba msaada wa jeshi la uingereza bila Kambona kujua, na hata yeye mwenyewe aliwahi kukiri hadharani mwaka 1983 wakati alipoulizwa jambo linalomsononesha kuhusiana na maamuzi yake, akasema kuwa kitendo cha kuwaomba waingereza warudi kumsaidia kutuliza nchi lilikuwa ni jambo linalomuumiza sana. Ni baada ya maasis yale uhusiano wa Nyerere na Kambona ukaanza kudorora sana hasa kwa vile Nyerere alipatiwa ripoti kamili na Brigadier Douglas kuhusu mwenendo wa Kambona kabla na baada ya maasi. Kuanzia hapo Nyerere akafukuza askari wote waliokuwa trained na Kambona, na akawa hamchukulii Kambona kwa uzito aliokuwa akimpa mwanzoni; ndiyo maana hata walipopingana kuhusu Azimio la Arusha, Nyerere alimponda wala hakumsikiliza tena kama ambavyo ilivyokuwa siku za nyuma kabla ya maasi.

Baada ya court martial ile, wale viongozi wa maasi waliokuwa karibu sana na Kambona yaakina akina Illogi walifungwa, lakini wale walioonekana kuwa waliunga mkono maasi kwa kulazimishwa na hivyo kuhofia maisha yao kama akina Kavana, Sarakikya, Mayunga, Marwa, Gangis, na wengine waliachiwa. Katika maafisa wakuu wa kijeshi wakati huo, ni Captain Nyirenda tu ndiye hakuwa amehusishwa kabisa na maasi yale kwa vile maafisa wa chini wasingemsogelea na upuuzi huo; alikuwa ni strict military officer aliyekuwa hataki upuuzi.

Hata hivyo, baada ya maaasi kuzimwa, jeshi zima lililokuwa na Battalion mbili tu: Colito, Tabora pamoja na kikosi kidogo huko Nachingwea, lilivunjwa, na maafisa wote wa jeshi waingereza wakarudi kwao; na badala yake tukaletewa jeshi Commonwealth kutoka Nigeria lililokuwa linaongozwa na Major Ojukwu kusaidia shughuli za ulinzi. Huyu Major Ojukwu ndiye ambaye baadaye alikuja ongoza maasi ya Biafra huko kwao. Kuna taarifa zisizothibitishwa zinazodai kuwa Nyerere alimuunga mkono Ojukwu kwenye vita ya Biafra kwa sababu ya urafiki baina yao alipokuwa nchini.


Baada ya kuvunjwa kwa jeshi muundo wa jeshi la kwanza Sarakikya alipandishwa cheo kutoka Luteni kuwa Captain, Kavana akapanda kutoka 2nd Luteni kuwa Luteni na wakawa ndio viongozi wa kwanza kusimamia ujenzi wa jeshi jipya. Sijajua kwa nini Kaptain Nyirenda hakuhusishwa, labda kwa vile alikuwa akichukiwa na askari wa chini. Muda mfupi baadaye, Sarakikya alipanda kuwa Luteni Kanali na kuwa mkuu wa majeshi wa kwanza, na Kavana akawa major na kuwa mnadhimu mkuu wa kwanza. Sina uhakika na madaraka aliyopewa Captain Nyirenda wakati huo.

Mabadiliko makubwa ya muundo wa jeshi yalikuja tokea tena mwaka 1972 wakati tukiwa na mfarakano na Amin, kukawa tena na mpango mwingine wa kumpindua Nyerere; mpango ambao inasemekana ulimhusisha Sarakakikya na baadhi ya maafisa wa karibu naye - nadhani hapo ndipo Kavana alipoondelewa jeshini moja kwa moja ingawa sina uhakika kwani kuanzia hapo sarakikya naye akaondolewa jeshini; kwanza kwa kufanywa waziri wa michezo na baadaye kuwa balozi wa Tanzania huko Nigeria. Mipango ile ya 1972 ilipanguliwa na Luteni Kanali Twalipo aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Kagera, ambaye ndiye aliyepandishwa cheo na kuwa Meja Generali na mkuu wa majeshi akisaidiwa na Brigedia Kiwelu, na jeshi likaundwa upya kuwa katika brigedi tano zikiongozwa na Marwa, Mayunga, Musuguri, Walden na Yusuf Himid. Makao makuu yakawa hayana nguvu sana juu ya bridage hizo, na kila brigade ikiwa na nguvu zake kamili. Muundoa huo ulifanywa makusudi ili iwe vigumu kucoordinate maasi.
 
Kipindi cha nyerere kila mtu alitaka kumpindua

Hapana, siyo kwa sababu alikuwa ni Nyerere bali ilikuwa ni fasheni ya majeshi katika sehemu nyingi Afrika wakati huo hasa yale yaliyokuwa yakiongozwa na wasomi wa Sandhurst. Angalia nchi hizi zilizowahi kushuhudia mapinduzi ya kijeshi katika Afrika: Nigeria, Ghana, Cameroon, Guinea, Libya, Liberia, Ethiopia, Somalia, Congo (Kinshasa), Uganda, Mali, Mauritania, Upper Volta, Rwanda, Burundi, Congo (Libreville), Misri, Gabon, Tunisia na Algeria.

Nni karibu zote zilizokuwa huru wakati huo zilionja hayo mapinduzi!
 
Mkuu Gustanza_the,heshima mbelesoma makala hii iliyoandikwa na joseph mihangwa wa gazeti la raia mwema mnamo tarehe 11 februari 2009 kuhusu maslahi na vyeo kwa wazawa vilivyochochea uasi jeshini 1964 na kuhusika kwa Sarakikya katika uasi huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi wa wakati huo, Oscar Kambona, aliweza kuwashawishi wanajeshi walioasi Januari 21, 1964, kurejea kambini, kwa ahadi ya kushughulikia malalamiko yao. Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere, aliweza kutoroka Ikulu kukwepa shari ya waasi waliokwenda kumtafuta, akaenda kujificha mahali pasipojulikana. Mwalimu alijitokeza ghafla siku mbili baadaye, akashika madaraka tena. Hata hivyo, siku nne baadaye, askari hao waliasi tena. Kwa nini? Siku ya pili baada ya kurejea kambini, askari waasi walionekana kufuraha kuona maofisa wa Kiingereza wakiondoka kama walivyoahidiwa na Kambona. Lakini mtu mmoja kati yao hakuwa na furaha kama wengine: Sajini Francis Higo Ilogi. Wakati wa mazishi ya askari wawili siku hiyo, waliouawa mtaani na Mwarabu mmoja wakati wa maasi, Sajini Ilogi aliacha kuzumgumza na Kambona, wala kumtazama usoni. Je, ni kwa sababu Kambona hakuweza kutekeleza yote aliyoahidi? Je, ni kwa sababu hakupandishwa cheo baada ya kuongoza maasi? Siku hiyo ilipokewa taarifa kwamba Kikosi cha Pili cha Jeshi kilichokuwa Tabora nacho kilikuwa kimeasi, baada ya kupata habari kwamba wenzao wa Colito walikuwa wameasi. Inawezekana ama walikuwa hawajapata taarifa kwamba wa Colito walikuwa wamerejea kambini; au walifahamu, lakini wakataka nao watekelezewe mambo kadhaa kwenye kikosi chao.Wakati Kikosi cha Tabora kikiendelea na maasi, ilipokewa simu ya maandishi kutoka kwa Kambona, kwamba alikuwa amemteua Kapteni Mirisho Sam Hagai Sarakikya, kuwa Mkuu wa Kikosi . Wakati huo Sarakikya na maofisa wengine walikuwa wamekamatwa na kuwekwa mahabusu. Sarakikya akatolewa mahabusu, akaomba simu hiyo isomwe kwa sauti; kisha akatoa amri wasimame “mguu sawa”, wafungue beneti na kutoa risasi. Nao wakamtii. Usiku huo, Sarakikya alifanya mipango ya kuwasafirisha maofisa wa Kiingereza kwenda Dar es Salaam na hatimaye makwao. Tukio la Januari 21, na lile la Tabora pamoja na hali ilivyokuwa huko Kenya, Uganda na Zanzibar, lilifanya Serikali ya Uingereza ichukue tahadhari ya ziada kwa kupeleka askari 2,000 zaidi Afrika Mashariki. Kwa hiyo, manowari iliyoitwa Rhy, ikawa imetia nanga hima Pwani ya Dar es Salaam, na nyingine Centaur; iliyobeba ndege, iliwasili na askari 600. Siku ya tatu baada ya maasi ya Kikosi cha Kwanza, Jumatano, Januari 23 asubuhi, ghafla Nyerere akatokea amepanda gari la wazi akiwa na Mama Nyerere na Waziri wa Mambo ya Ndani, Job Lusinde, akatembelea kila sehemu ya mji iliyoathiriwa na maasi. Alhamisi, Januari 24, ilikuwa shwari; lakini Ijumaa, Januari 25, mazungumzo kati ya Serikali na waasi yalionekana kuanza kuvunjika, wakaasi tena. Ni nani alikuwa kiongozi wa maasi awamu ya pili? Sajini Higo Ilogi tena?. Tofauti na maasi ya Januari 21, ambayo hakushirikisha wanasiasa, wala kuwa na shabaha ya kisiasa, maasi haya mapya yaliingiliwa na wapiga filimbi wa kisiasa. Taarifa za kiusalama zilionyesha kwamba, viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi walikuwa wakikutana na askari walioasi kwenye kambi ya Colito, na kwamba vyama hivyo vilikuwa wimeandaa mgomo mwishoni mwa wiki kuungana na askari hao. Maasi haya ya pili yaliweza kuambukiza majeshi ya Kenya na Uganda, nayo yakaasi vivyo hivyo, siku hiyo hiyo, wakati huo huo, na kwa mtindo huo huo. Jomo Kenyatta na Milton Obote walizisoma alama za nyakati ukutani; wakajiandaa kuita Jeshi la Uingereza kuzima maasi. Nyerere hakutaka. Hakuamini kwamba Jeshi lake mwenyewe lingeweza kumhujumu, yeye na Serikali yake. Alianza kuamini pale Maofisa Usalama walipomuonyesha orodha ya mawaziri watarajiwa, iliyoandaliwa na waasi. Mmoja wa watu wake wa karibu alikwenda mbali zaidi kumwambia kwamba, alikuwa ameombwa akubali kuwa Makamu wa Rais baada ya mapinduzi. Mwalimu akalowa; akayaamini maneno hayo, kwamba Serikali yake ilikuwa hatarini.Ndipo, yapata saa 11:30 siku hiyo, Mwalimu akamwita Ikulu, Naibu Balozi wa Uingereza, Bwana F. Stephen Mills; akamwomba msaada wa kijeshi. Na bila kuchelewa, Mills alipeleka taarifa London na kujibiwa kwamba maombi yalikuwa yamekubaliwa.Naye Oscar Kambona akaenda mbio kwenye Ubalozi wa Uingereza kumtafuta Bregedia Douglas ambaye alikuwa amejificha humo kwa wiki nzima, kumwomba msaada. Usiku wa siku hiyo, Douglas na ofisa mwingine, walinyatia hadi kwenye manowari Centaur iliyokuwa imefichwa Pwani. Jumamosi; Januari 26; saa 12:20 asubuhi, helikopta sita kutoka manowari Centaur zilichukua askari 60 (akiwamo Bregedia Douglas) hadi eneo karibu na kambi ya Colito. Dakika 10 baadaye, saa 12:30, manowari hiyo, na meli nyingine ya vita, Cambrian, iliyokuwa ikisubiri Pwani; zilianza mashambulizi kwa kupiga mizinga kuwatisha waasi.Kutoka umbali wa mita 20 hivi, na kwa ujasiri mkubwa, Douglas akatangaza kwa kipaza sauti, kwamba alikuwa ameshika madaraka yake tena; akatoa amri askari wote watoke kambini na “silaha juu” na kukaa chini barabarani.Baada ya dakika 10 bila kuona kitu, akaanza kuhesabu, “moja, mbili….. kumi”, askari wa Kiingereza wakafyatua roketi hadi kambini. Waasi wakaanza kujisalimisha.Dakika 10 nyingine zilizofuata, askari 150 walijisalimisha, na wengine 150 baada ya saa moja. Kufikia saa 1:30 asubuhi, wote walikuwa wamesalimu amri; maasi yakawa yamezimwa katika zoezi ambalo askari walioasi watano waliuawa, na wengine watano kujeruhiwa. Hakuna askari wa Kiingereza kati ya 60 walioongoza mapambano, aliyedhurika. Na kwa juma lote la maasi, raia wasiopungua 17 waliuawa.Wakati Wanajeshi wa Jeshi la Uingereza wakiwadhibiti askari waasi wa Tanganyika, huko Uganda na Kenya nako, Jeshi hilo lilikuwa linachukua hatua kama hiyo, muda, saa na kwa staili hiyo hiyo kwa askari walioasi Jinja (Uganda), na katika Kikosi cha 11 cha Bark-Lanet (Kenya).Haielezwi ni jinsi gani Sajini Higo Ilogi aliweza kuponyoka, akaonekana mjini asubuhi hiyo kwenye jumba la Simu za Nje za Kimataifa (Extelcoms), akituma simu ya mandishi kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), U Thant, kuomba msaada. Simu hiyo ilisomeka: “Majeshi ya Tanganyika yametekwa na askari wasiojulikana. Saidia haraka kuleta Majeshi ya Umoja wa Mataifa. LUTENI KANALI ILOGI, MKUU WA JESHI”.Turejee kwenye swali letu la msingi: Nani alichochea maasi ya jeshi letu mwaka 1964? Oscar Kambona? John Okello?. Kambona alikuwa waziri mwenye dhamana ya ulinzi wakati huo, ambapo Jeshi lilikuwa chini ya Wizara yake. Kwa sababu hii, kushiriki kwake katika kutuliza maasi ya awamu ya kwanza, hakuwezi kuchukuliwa kwamba alikuwa na hisa au kwamba alikuwa anajua mpango huo.Ni ujasiri wake tu uliomtuma kukabiliana na hali hiyo. Kama kweli angekuwa na nia mbaya kwa Serikali; na kwa kuzingatia jinsi alivyodhibiti hali na askari wakamkubali, angeshindwaje kupindua nchi ambayo ilikuwa mikonini mwa Jeshi kwa siku mbili mfululizo?.Je, ni “Field Marshal” John Okello? Hapana; yeye hakuwa na muda huo, kwa sababu kwa kipindi chote tangu Mapinduzi ya Zanzibar, alikuwa katika hati hati za kulinda na kuimarisha utawala wake Visiwani kutokana na tishio la kuenguliwa na hasimu wake ambao alidai hawakushiriki katika mapinduzi. Okello aliongoza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa miezi miwili mfululizo kabla ya kuenguliwa.Wala haishangazi kwamba, maasi ya askari hawa yaliweza kuambukizwa kwa wenzao wa Kenya na Uganda, ikizingatiwa kuwa majeshi ya nchi hizi tatu yamezaliwa na Jeshi la Wakoloni wa Kiingereza waliotawala nchi hizo. Kwa hiyo, kwa kipindi hicho, na kwa mazingira ya kazi ya wakati huo, malalamiko yao yalifanana kuwafanya wadai haki zao kwa njia na kwa mtindo unaofanana.Nakubaliana na maoni ya Balozi Abbas Kleist Sykes (akinukuliwa mahali fulani mwaka 2001), kwamba, “Maasi ya Jeshi la Tanganyika Rifles (TR) mapema mwaka 1964, yalitokana kwa kiasi kikubwa na kuchelewa kuwaondoa Makamanda wa Kizungu na kuwapandisha vyeo Waafrika”, kama ilivyofanyika kwa Jeshi la Polisi na Watumishi wengine Serikalini. Na ndivyo ilivyokuwa kwa maasi ya Kenya na Uganda.Wala haishangazi kwamba, viongozi wa Vyama Vya Wafanyakazi waliungana na waasi awamu hii ya pili kutaka kuiangusha Serikali, kutokana na ukweli kwamba, tangu Mwalimu alipositisha zoezi la “Africanisation” Januari 1963, walikwishaapa kutolala usingizi “mpaka kieleweke”.Kutokana na maasi hayo, Mwalimu alikifuta Kikosi chote cha Kwanza (Colito Barracks) na kuwafukuza kazi askari 100 wa kikosi cha Pili, Tabora. Alifukuza pia asilimia 10 ya askari Polisi 5,000 waliokuwapo kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao. Watu zaidi ya 400 walikamatwa na kuhojiwa, wakiwamo viongozi wa vyama vya wafanyakazi; na wengine 500 walitiwa nguvuni chini ya Sheria ya kuzuia hatari, lakini wengi waliachiwa. Nalo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TFL) lilifutwa, badala yake kikaundwa Chama cha NUTA kama Jumuiya ya Chama tawala – TANU. Mwalimu alimteua Mirisho Sam Hagai Sarakikya kuwa Mkuu mpya wa Jeshi, na kumpandisha cheo kuwa Bregedia. Mwanzoni mwa April 1964, Majeshi ya Uingereza yaliondoka, na nafasi yake kuchukuliwa na Kikosi cha Tatu cha Jeshi la Nigeria, chini ya Luteni Kanali James Pam. Sajini Francis Higo Ilogi alipatikana na hatia ya uasi wa Jeshi na kufungwa miaka 15, washirika wake 13 wakafungwa kifungo kati ya miaka mitano hadi kumi.Waswahili walisema, “Kila ovu lina baraka zake”. Mwalimu aliongeza kima cha chini cha mshahara kwa wanajeshi, kutoka 105/= hadi 240/= kwa mwezi. Lakini la muhimu kuliko yote ni kwamba, maasi hayo yalitusaidia kujihoji na kufahamu aina ya Jeshi lililotakiwa kwa nchi kama yetu. Yalituwezesha kujenga Jeshi upya kabisa, tukapata “Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania” (JWT), kwa maana halisi ya Jeshi la Wananchi na kwa ajili ya Wananchi.Nawasilisha
 
Hii Record ya Mihangwa haiko kamili; imekaa vipande vipande. Kuna vitabu kadhaa vyenye record kamili sikumbuki authors wake, lakini iwapo ungepata bahati ya kukaa pamoja na General Marwa ukamwuliza historia ya jeshi la wananchi angekusimulia vizuri sana, alikuwa anatoa maelezo yake bila woga. Katika maasi yale yaliyongozwa na Sgt Ilogi Mzee Marwa alikuwa na cheo cha 2nd Lieutenant, hata yeye alivutwa na kupandishwa cheo kutoka 2nd Lieutenant hadi kuwa Major wakati huo ambapo Sgt Ilogi mwenyewe alipojipandisha kuwa Luteni Kanali na kuwapandisha wengine akina akina Kavana Kuwa Brigadier, Gangis kuwa Luteni Kanali na wengineo. Hizi ripoti za mgomo wa kwanza, mgomo wa pili mgomo wa tatu siyo sahihi; ulikuwa mgomo mmoja tu, na Kambona alikuwa ndiye chanzo. Alilazimika kuutuliza kwa vile wanajeshi walikuwa wameanza kuwauwa wazungu na wahindi, jambo ambalo halikuwa zuri; lakini alipofanikiwa kuwatuliza wanajeshi wale, akawa ametowa mwanya kwa Nyerere kupata ukweli na kujizaititi zaid. ndiyo maana wahusika wakuu wote walifungwa na hata Kambona mwenyewe akakosa ile respect aliyokuwa akipata kutoka kwa Nyerere.

Ukisoma ripoti binafsi za Brigadier Douglas, Lt Col Mans, Major Callaghan, na Captain Lammond wambao wakati huo ndio waliokuwa wakiongoza jeshi hapo Makao Makuu na Colito Barracks utajua kuwa ule mgomo haukuwa wa maslahi tu ya askari tu bali ulihamasishwa na Kambona ambaye alikuwa anatembelea sana ile kambi ya Colito karibu kila baada ya siku mbili kabla na baada ya maasi.
 
MAKAH,

..habari zote nilizoandika hapa nimezipata kwenye kitabu kinachohusu maasi ya 1964.

..kwa uelewa wangu, Kavana aliteuliwa kuwa Chief of Staff wa kwanza wa JWTZ akiwa na cheo cha Major.

..ila sijui Major.Kavana aliondoka jeshini mwaka gani, na katika mazingira gani. labda tumtafute Kudi Shauri, Kichuguu, Moshe Dayan, Nyenyere, wanaweza kutusaidia hapa.

..hata mimi sielewi kwanini mchango wa jeshi la Nigeria ktk kufundisha askari wa mwanzo wa JWTZ hauwekwi wazi. Wanigeria pia wametoa mchango mkubwa sana ktk harakati za ukombozi wa Afrika haswa kupitia ile kamati ya Frontline States.

NB:

..je, uliposema "Ilonsi" ulikuwa unamaanisha Sgt.Hingo Ilogi ambaye alikuwa kiongozi wa maasi ya 1964?

You are right nilikosea badala ya "Ilongi" ambae alikuwa gumzo la jiji wakati ule nikasema "Ilonsi"
 
[ Kudi Shauri, Kichuguu, Moshe Dayan, Nyenyere, wanaweza kutusaidia hapa.

..hata mimi sielewi kwanini mchango wa jeshi la Nigeria ktk kufundisha askari wa mwanzo wa JWTZ hauwekwi wazi. Wanigeria pia wametoa mchango mkubwa sana ktk harakati za ukombozi wa Afrika haswa kupitia ile kamati ya Frontline States.
?

Kwa mujibu wa uelewa wangu ni kuwa baada ya maasi ya 1964 kuna timu kubwa tu ya ODA walikuja kutoka Canada(CAFATTT) na ndio walifundisha Jeshi letu la kwanza pamoja na kutengeneza Chain of comand mpya! Kuna Kanali mmoja ndo alikua kiongozi wao pamoja na kina Captain Saunders, Sargent Rogers, Sgt Smith nimemsoma alielezea kwa kirefu sana ikiwa ni pamoja na walivyokuja kuwa na rivaly na Wachina. Hii timu pia ndio ilikuja kuombwa baadaye na Serikali(kupitia Kawawa I think) waje waanzishe Airwing. Na ndio walituletea zile Caribou za mwanzoni mwanzoni kabisa ila tulipofungua ubalozi wa Ujerumani mashariki wakajitoa rasmi. Kwenye historia yake anaelezea kuwa wakati wanaondoka waliacha ndege nyingine ziko kwenye crates bado, zikiwa hazijaunganishwa na kutukomoa waliondoka na manuals zao Ila Kuna Engineers wetu wakajitahidi kuziunganisha na moja ndo iliangukaga Manyara kule.

Ngoja nipekue nitaileta hapa. Pamoja wakuu
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom