Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

Gen. Mrisho Sarakikya aliwahi kuhusishwa na Uhaini?

......... na Kambona alikuwa ndiye chanzo. Alilazimika kuutuliza kwa vile wanajeshi walikuwa wameanza kuwauwa wazungu na wahindi, jambo ambalo halikuwa zuri;

Mkuu imenipita hiyo ya wanajeshi kuanza kuwaua wazungu na wahindi. nakumbuka looting ya hali ya juu sana ya maduka ya wahindi ikiratibiwa na wanajeshi na wananchi wakiimba "HARAMBEEEEEE" katika hiyo looting.

mauwaji ninayokumbuka ni yale ya mwarabu na familia yake yote pale magomeni ambapo mtoto mdogo sana wa mwarabu ndie aliepona. siku inayofuata warabu walilipuka na majambia kutaka kulipiza kisasi. kwa kweli hali ilikuwa tete na ya sintojua dar. Katika hili mwarabu ndo chanzo cha chokochoko. yeye aliwaamuru pale kwake wasitoke nje kuhofia wanajeshi kusaka waasia. sasa mtumishi wake mweusi alitoka nje na akamtwanga risasi wakati askari wakiwa maeneo hayo. inasemekana ndipo wakahisi kuna adui yao katika nyumba ile na kuanza kuishambulia hadi ikawa almost Ground zero.
 
Kweli mkuu wangu.....

I real Miss JF of the Old Days, watu walikuwa wanarusha Nondo tu, tena wanachangia kwa upendo, maarifa, references na kwa kuheshimiana sana, no personal attacks, na blah blah blah. I was a Guest by then.
The Platinum JF of the Golden Days will be missed to be true.
 
Mkuu Gustanza_the,heshima mbelesoma makala hii iliyoandikwa na joseph mihangwa wa gazeti la raia mwema mnamo tarehe 11 februari 2009 kuhusu maslahi na vyeo kwa wazawa vilivyochochea uasi jeshini 1964................. Alifukuza pia asilimia 10 ya askari Polisi 5,000 waliokuwapo kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao.

Polisi wangefanya nini mbele ya KAR kuushika mji wa dar hostage kwa takriban siku 5. Kuna baadhi ya hao polisi walifukuzwa kwa mere kushabikia maasi. ulitakiwa usitoe comment yako yeyote inayoashiria kufurahia yale maasi. naturally polisi walikuwa na expectation ya wao pia kunufaika na matokeo ya maasi - kwa suala la africanization na ongezeko la maslahi. zoezi hili la kuwalopoa askari polisi lilifanikiwa aidha kwa njia ya kuchongeana au kwa njia ya mashushu.
 
Npo, nimemuacha joka kuu asongeshe, haya mawe ndo ilibidi vijana wawe wanasoma waone tulitoka wapi..,

But just need to know if its true...pale alipojenga huyu General mwenye uso wa chuma na kuamua kuishi Bukoba, ndio pale alipoweka tent za kwanza na kuandaa mipango ya mapigano ya kuwasogeza mbali na daraja askari wa nduli ili daraja liweze kujengwa?
 
But just need to know if its true...pale alipojenga huyu General mwenye uso wa chuma na kuamua kuishi Bukoba, ndio pale alipoweka tent za kwanza na kuandaa mipango ya mapigano ya kuwasogeza mbali na daraja askari wa nduli ili daraja liweze kujengwa?

Comrade Ndahani,

Hapana, pale palikua hapakaliki, kyaka, mtukula ndo zilikua frontlines,,, vijana wetu wa signal centers za border walituma taarifa mpaka hauko salama, na inajulikana SITREP(situation report) ikisoma mpaka hauko salama basi ni kwamba jeshi zima linakua STAND-BY, hizi SITREP hutumwa kila siku kutoka vikosi vyote tanzania kuelekea kamandi zao eventually makao makuu, huelezea hali ya usalama wa eneo, askari na silaha.

Sasa huyu mkuu sura ya chuma asingeweza kukaa hapo, zingatia pia tulikua invaded,,, sio kwamba ss tulikua aggressors.

Comrade, pia kuna conflicting info kuhusu nani hasa alivunja ile bridge,, kuna thread nilianzisha hapa kuhusu nani hasa alivunja lile daraja, ila ni kwamba field engineers wetu walijenga temporary movable bridge ili kupitisha zana na askari...,

Na hii ilifanyika haraka kwa sababu tayari tulikua tume-gain momentum ya advance baada ya kumuangushia adui mvua kubwa sana ya mizinga ya howitzer na rocket kutoka kwenye bm21 kwenye strategic border areas zake.., hizi zilichangia sana kumrudisha nyuma adui wakati mobilization ya infantry na silaha nzito kule kagera ikifanyika.., silaha zilitolewa brigade zote na kuelekeza nguvu brigade ya kaskazini
 
Comrade Ndahani,

Hapana, pale palikua hapakaliki, kyaka, mtukula ndo zilikua frontlines,,, vijana wetu wa signal centers za border walituma taarifa mpaka hauko salama, na inajulikana SITREP(situation report) ikisoma mpaka hauko salama basi ni kwamba jeshi zima linakua STAND-BY, hizi SITREP hutumwa kila siku kutoka vikosi vyote tanzania kuelekea kamandi zao eventually makao makuu, huelezea hali ya usalama wa eneo, askari na silaha.

Sasa huyu mkuu sura ya chuma asingeweza kukaa hapo, zingatia pia tulikua invaded,,, sio kwamba ss tulikua aggressors.

Comrade, pia kuna conflicting info kuhusu nani hasa alivunja ile bridge,, kuna thread nilianzisha hapa kuhusu nani hasa alivunja lile daraja, ila ni kwamba field engineers wetu walijenga temporary movable bridge ili kupitisha zana na askari...,

Na hii ilifanyika haraka kwa sababu tayari tulikua tume-gain momentum ya advance baada ya kumuangushia adui mvua kubwa sana ya mizinga ya howitzer na rocket kutoka kwenye bm21 kwenye strategic border areas zake.., hizi zilichangia sana kumrudisha nyuma adui wakati mobilization ya infantry na silaha nzito kule kagera ikifanyika.., silaha zilitolewa brigade zote na kuelekeza nguvu brigade ya kaskazini

Asante mkuu...imekaa vizuri. Unajua nilipata kusikia yeye ndio aliongoza strategies za makomandoo wa kwanza kuvuka mto kwenda upande wa pili wa daraja akiwemo retire Brig. Gen Kabunda...na yeye ndio aliweka tent la kwanza la gen kwenye kuongoza vita hivyo vya kumtoa Nduli....sijui Himid Hemedi alikuwa wapi maana that was his area.
Moshe dayan, historia hii nzuri mbona inafanywa siri bado? Muda haujawa muafaka wa kuiandiaka kwa vizazi vyetu vyote kujua nini kilitokea?
 
Moshe Dayan, Ndahani,

..my reading ni kwamba Maj.Gen.Kiwelu na Brig.Kitete ndiyo walio-mobilize majeshi na kutengeneza plan ya kumuondoa Amin ktk ardhi ya Tanzania.

..kuna mahali nimesoma kwamba vikosi ambavyo vilikuwa tayari kimapigano vilikuwa ktk mpaka wetu wa kusini. mpaka wetu na Uganda ulikuwa na kikosi kidogo kilichokuwa chini ya Lt.Col.Singano, ambaye alikuwa chini ya Brig.Yussuf Himid.

..zaidi inasemekana kipindi tulichovamiwa ilikuwa majira ya mvua, hivyo kazi kubwa ilifanyika kusafirisha askari pamoja na vifaa toka sehemu nyingine za Tanzania kuelekea eneo la mapigano ktk mkoa wa Kagera.

..baada ya majeshi yetu kukomboa ardhi yetu ndipo Maj.Gen.Kiwelu akarejea makao makuu kama Chief of Staff, na Maj.Gen.David Musuguri akachukua jukumu la kamanda mkuu wa vikosi vya Tanzania ndani ya Uganda.

.. Moshe Dayan, gobore, Kudi Shauri, Kichuguu, Ndahani, na wengine, sijui mna kumbukumbu gani kuhusu zoezi zima la kumuondoa Amin toka ktk ardhi yetu, na baadaye kumuondosha madarakani.

NB:

..Brig.Ahmed Kitete alikuja kufariki ktk ajali ya gari jijini D'Salaam. iliripotiwa kwamba alikuwa ni "mshauri wa kijeshi" wa mkuu wa majeshi.
 
Last edited by a moderator:
comrade joka kuu,

Uko sahihi kabisa, brigade ya kusini 401, ilikua ndio brigade yenye nguvu kubwa ya askari na silaha nzito nzito na mara nyingi ilikua STAND-BY..,

Hii ilitokana na threat kipindi kile cha vita za ukombozi wa africa, kaburu alikua threat kubwa sana kwetu,

Kutokana na jwtz kushiriki katika covert operations nyingi huko kusini na kufanya sabotage nyingi kwenye miundombinu ya kaburu, ilitegemewa kwamba somehow, somewhere, oneday, kaburu ange-retaliate.., na kwa sababu hakuwa na mahusiano mazuri na uganda, kenya, zaire, zambia na malawi, ilionekana the possible route ni through mozambique ambapo na yeye alikua ana-conduct covert ops agaisnt machel, hyo ilikua moja ya sababu ya kuiimarisha ile brigade

Pia kulikua na eneo ambalo kaburu alitaka sana kulifanyia sabotage, hii ni kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kipindi hicho..., hilo eneo liliitwa farm 17, lipo mtwara, pale, ilikua ni training camp ya wapiganaji wa msumbiji, zimbabwe na south africa(anc)..., walifundishwa sabotage (kuharibu miundombinu kama bridges, powerlines, communication centers, dams etc kwa namna yoyote lakn mostly explosives), pia walifunzwa propaganda, skills za gorilla warfare, etc, kaburu alipata shida sana na wapiganaji waliotoka pale na mazimbu. Its a painful truth tulipoteza wengi tu kwenye covert-ops, kuna mahali sitasema wapi, tulipoteza a shocking number of commandos baada ya local "double agent" kuwaingiza kwenye trap...,

pia nakumbuka hali ya usalama wa nchi ilikua tense ilifkia na sisi kila infrastructure muhimu ililindwa na wanajeshi, nadhani mtakumbuka kipindi kile hata madaraja makubwa hasa ya reli tazara yalikua na ulinzi wa jeshi.., hata selander bridge lilikua linalindwa.., brigade zilikua haupiti mwezi lazma stand-by za kutosha

Na ukitaka jua kuhusu ule mpaka wa kusini ulivyokua unalindwa, ule ndio mpaka pekee wenye aerial radar stations nyingi kuliko mpaka wowote kwa ratio ya distance,,, kuanzia ile ya mtwara hadi itungi kyela, zilikua tano (kwa sasa ni classified, taifa kwanza)

Joka kuu, kuhusu kagera, si tulishaweka elimu hapa?
 
Asante mkuu...imekaa vizuri. Unajua nilipata kusikia yeye ndio aliongoza strategies za makomandoo wa kwanza kuvuka mto kwenda upande wa pili wa daraja akiwemo retire Brig. Gen Kabunda...na yeye ndio aliweka tent la kwanza la gen kwenye kuongoza vita hivyo vya kumtoa Nduli....sijui Himid Hemedi alikuwa wapi maana that was his area.
Moshe dayan, historia hii nzuri mbona inafanywa siri bado? Muda haujawa muafaka wa kuiandiaka kwa vizazi vyetu vyote kujua nini kilitokea?

Mkuu, kabla hata ya hiyo recce-part ya makomandoo kulikua na (as they like to be called) "guardian angels" waliofanya kazi kubwa..., ni hivi, baada ya chokochoko za idi amini za mwaka 1972, nyerere alikaa na washauri wake wa mambo ya ulinzi na usalama, ikaonekana kua idi amini sio short-term problem na hivyo ilihitajika long-term solution,

therefore, walitumika majasusi ku-infiltrate deep inside uganda ilu kupata taarifa muhimu from the people in the system, ugandans love women, walitumwa wanawake, walitumwa wafanyabiashara, and all other spy covers za kipindi kile, siku ile nyerere ana-declare war kwamba nguvu tunayo, uwezo tunao na sababu tunayo, he was confident kwamba alikua anaenda kushinda vita, kwa sbb alijua nguvu ya adui(idadi ya wanajeshi) na silaha zake na mambo mengine muhm na hii ilitokana na intel gathering ya miaka takriban 7..,

Kuhusu historia ya mambo kufanywa siri, naomba nijibu ni ndio na hapana, ndio kwa sababu ni kweli kuna mambo yanafanywa siri kwa kusudi kabisa kwa sababu "maalum" na mengine ni kwa sababu kuna mambo hayakuwekewa kumbukumbu sawasawa ingawa ukienda pale kwenye makumbusho ya kijeshi utapata mwanga wa mambo mengi sana
 
Moshe Dayan, Ndahani,

..my reading ni kwamba Maj.Gen.Kiwelu na Brig.Kitete ndiyo walio-mobilize majeshi na kutengeneza plan ya kumuondoa Amin ktk ardhi ya Tanzania.

..kuna mahali nimesoma kwamba vikosi ambavyo vilikuwa tayari kimapigano vilikuwa ktk mpaka wetu wa kusini. mpaka wetu na Uganda ulikuwa na kikosi kidogo kilichokuwa chini ya Lt.Col.Singano, ambaye alikuwa chini ya Brig.Yussuf Himid.

..zaidi inasemekana kipindi tulichovamiwa ilikuwa majira ya mvua, hivyo kazi kubwa ilifanyika kusafirisha askari pamoja na vifaa toka sehemu nyingine za Tanzania kuelekea eneo la mapigano ktk mkoa wa Kagera.

..baada ya majeshi yetu kukomboa ardhi yetu ndipo Maj.Gen.Kiwelu akarejea makao makuu kama Chief of Staff, na Maj.Gen.David Musuguri akachukua jukumu la kamanda mkuu wa vikosi vya Tanzania ndani ya Uganda.

.. Moshe Dayan, gobore, Kudi Shauri, Kichuguu, Ndahani, na wengine, sijui mna kumbukumbu gani kuhusu zoezi zima la kumuondoa Amin toka ktk ardhi yetu, na baadaye kumuondosha madarakani.

NB:

..Brig.Ahmed Kitete alikuja kufariki ktk ajali ya gari jijini D'Salaam. iliripotiwa kwamba alikuwa ni "mshauri wa kijeshi" wa mkuu wa majeshi.

Niliwahi kuandika hapa kumbukumbu zangu kuhusu vita ile wakati wa kutoa rambirambi zetu kutokana na kifo cha ama General Marwa au General Mayunga. Ni karibu miaka mitano iliyopita; nitaitafuta post hiyo nikupe link yake
 
Moshe Dayan,

..mimi nina maoni tofauti na kuhusu kutoa details za covert operations zilizopata kufanyika.

..Makaburu wanaweka kumbukumbu zao ktk maandishi. kwa mfano, waliwahi kushambulia D'Salaam kwa manowari na tayari kuna kitabu wanaeleza tukio hilo.

..kwa msingi huo, kama wa-Tanzania hatutaweka kumbukumbu za michango yetu ktk maandishi, Makaburu watafanya hivyo IN THEIR OWN WORDS. sasa wakiwapotosha vijana wetu tusijilaumu wenyewe.

..nimewahi kukutana na Wamarekani walioshiriki Operation Eagle Claw, ile operation ya kuokoa mateka wa Marekani waliokuwa wakishikiliwa Iran ambayo ili-fail. Operation hiyo, pamoja na kwamba ilifeli, ndiyo chimbuko la Navy Seals waliokuja kumuua Osama Bin Laden. Sasa Wamarekani hawafichi kumbukumbu zao hata pale ambapo hawakufanikiwa.
 
Last edited by a moderator:
unachosema ni kweli, inahitajika kumbukumbu kwa kweli, maana kunaweza tokea upotoshaji wa historia,

Ila nadhani mengine hayawekwi wazi kwa sababu kuna maeneo tulipoteza significant number of fighters, si unakumbuka biafra? ila all in all truth must said, kama tulipigwa au la, history must be kept..,

Hizi kumbukumbu kwa jeshi lenyewe linaweka, maana report lazma ziandikwe after each ops/mission kwa madhumuni ya kuboresha future tasks..., ila kwa public domain upotoshaji unaweza tokea, yaani ilibidi hata vifo vya wale askari wetu darfur wananchi waelezwe what happened, au hata ya yule rubani(although uchunguzi bado haujakamilika) ila ukikamilika wananchi waelezwe.., hii itaondoa speculations na conspiracy theories
 
Moshe Dayan, Ndahani,

..my reading ni kwamba Maj.Gen.Kiwelu na Brig.Kitete ndiyo walio-mobilize majeshi na kutengeneza plan ya kumuondoa Amin ktk ardhi ya Tanzania.

..kuna mahali nimesoma kwamba vikosi ambavyo vilikuwa tayari kimapigano vilikuwa ktk mpaka wetu wa kusini. mpaka wetu na Uganda ulikuwa na kikosi kidogo kilichokuwa chini ya Lt.Col.Singano, ambaye alikuwa chini ya Brig.Yussuf Himid.

..zaidi inasemekana kipindi tulichovamiwa ilikuwa majira ya mvua, hivyo kazi kubwa ilifanyika kusafirisha askari pamoja na vifaa toka sehemu nyingine za Tanzania kuelekea eneo la mapigano ktk mkoa wa Kagera.

..baada ya majeshi yetu kukomboa ardhi yetu ndipo Maj.Gen.Kiwelu akarejea makao makuu kama Chief of Staff, na Maj.Gen.David Musuguri akachukua jukumu la kamanda mkuu wa vikosi vya Tanzania ndani ya Uganda.

.. Moshe Dayan, gobore, Kudi Shauri, Kichuguu, Ndahani, na wengine, sijui mna kumbukumbu gani kuhusu zoezi zima la kumuondoa Amin toka ktk ardhi yetu, na baadaye kumuondosha madarakani.

NB:

..Brig.Ahmed Kitete alikuja kufariki ktk ajali ya gari jijini D'Salaam. iliripotiwa kwamba alikuwa ni "mshauri wa kijeshi" wa mkuu wa majeshi.


Haya, nimeipata link hiyo: ni hii hapa

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...hacha-marwa-kambale-afariki-2.html#post122570
 
Mkuu, kabla hata ya hiyo recce-part ya makomandoo kulikua na (as they like to be called) "guardian angels" waliofanya kazi kubwa..., ni hivi, baada ya chokochoko za idi amini za mwaka 1972, nyerere alikaa na washauri wake wa mambo ya ulinzi na usalama, ikaonekana kua idi amini sio short-term problem na hivyo ilihitajika long-term solution,

therefore, walitumika majasusi ku-infiltrate deep inside uganda ilu kupata taarifa muhimu from the people in the system, ugandans love women, walitumwa wanawake, walitumwa wafanyabiashara, and all other spy covers za kipindi kile, siku ile nyerere ana-declare war kwamba nguvu tunayo, uwezo tunao na sababu tunayo, he was confident kwamba alikua anaenda kushinda vita, kwa sbb alijua nguvu ya adui(idadi ya wanajeshi) na silaha zake na mambo mengine muhm na hii ilitokana na intel gathering ya miaka takriban 7..,

Kuhusu historia ya mambo kufanywa siri, naomba nijibu ni ndio na hapana, ndio kwa sababu ni kweli kuna mambo yanafanywa siri kwa kusudi kabisa kwa sababu "maalum" na mengine ni kwa sababu kuna mambo hayakuwekewa kumbukumbu sawasawa ingawa ukienda pale kwenye makumbusho ya kijeshi utapata mwanga wa mambo mengi sana

Unfortunately, mmoja wa majasusi hao alikuwa ni ndugu yangu!!!

Jamaa huyo alishikwa na watu wa Amin akaonekana gazetini akiwa amefungwa kitambaa cheusi tayari kwa kupigwa risasi pamoja na wale waliopigwa risasi hadharani mwaka 1973, lakini hata sisi hatujui alitorokaje. Amefariki miaka ya tisini tu baada ya kusumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo.
 
Mwaka jana Wizara ya Mambo ya Nje ilianza kutoa tuzo za kwa mabalozi wanaoitangaza Tanzania vizuri ambayo inaitwa tuzo ya Mrisho Sarakikya...

Unajua ukweli ni kwamba Jenerali Sarakikya wakati huo alikuwa ni mmoja mwa wasomi watatu waliokuwepo jeshini kwa wakati huo, yeye alikuwa ni kidato cha sita, mwingine ambaye alitimuliwa mapema alikuwa na degree ya hesabu toka chuo kikuu cha makerere, na mwingine alikuwa ni kidato cha nne tu naye alikuwa wakati huo ameshatimuliwa. Kimsingi ni kwamba Jenerali Sarakikya kutokana na usomi wake kwa wakati huo alikuwa na uwezo wa kuchanganua mambo ya kitaifa na kimataifa na hivyo akawa kiongozi mzuri sana. Wenzake ambao elimu yao ilikuwa darasa la saba kama ilivyoada wakawa wanamuonea wivu wa kishenzi, wakawa wanampiga majungu kwa nyerere kila kukicha na hatimaye wakabuni ajenda ya uhaini. Nyerere hakuamini kabisa ajenda ya kwamba eti sarakikya anataka kumpindua lakini kwa kuwa majungu hayo yalikuwa yanatoka jeshini hukohuko aliamua kusawazisha mambo kwa kumtoa sarakikya jeshini na kumpatia appointment ya uwaziri na baadaye ubalozi, kitu ambacho ni kawaida tu kwa mwanajeshi kupangiwa kazi nyingine kulingana na hali. Kwa hiyo sarakikya hakuwahi kuwa mhaini, na mhaini hufikishwa mahakamani siyo kupangiwa kazi nyingine tena nono.
 
Unajua ukweli ni kwamba Jenerali Sarakikya wakati huo alikuwa ni mmoja mwa wasomi watatu waliokuwepo jeshini kwa wakati huo, yeye alikuwa ni kidato cha sita, mwingine ambaye alitimuliwa mapema alikuwa na degree ya hesabu toka chuo kikuu cha makerere, na mwingine alikuwa ni kidato cha nne tu naye alikuwa wakati huo ameshatimuliwa. Kimsingi ni kwamba Jenerali Sarakikya kutokana na usomi wake kwa wakati huo alikuwa na uwezo wa kuchanganua mambo ya kitaifa na kimataifa na hivyo akawa kiongozi mzuri sana. Wenzake ambao elimu yao ilikuwa darasa la saba kama ilivyoada wakawa wanamuonea wivu wa kishenzi, wakawa wanampiga majungu kwa nyerere kila kukicha na hatimaye wakabuni ajenda ya uhaini. Nyerere hakuamini kabisa ajenda ya kwamba eti sarakikya anataka kumpindua lakini kwa kuwa majungu hayo yalikuwa yanatoka jeshini hukohuko aliamua kusawazisha mambo kwa kumtoa sarakikya jeshini na kumpatia appointment ya uwaziri na baadaye ubalozi, kitu ambacho ni kawaida tu kwa mwanajeshi kupangiwa kazi nyingine kulingana na hali. Kwa hiyo sarakikya hakuwahi kuwa mhaini, na mhaini hufikishwa mahakamani siyo kupangiwa kazi nyingine tena nono.

Ni kweli kabisa,
 
comrade kichuguu,

Huo uzi niliupenda sana, "kambale"..., makamanda kipindi kile walikua intimidating bwana,,, akitoa order imetoka, hairudiwi, ni utekelezaji tu.
 
Wakuu, nani anafahamu [kiundani] kuhusu uhaini wa aliyewahi kuwa the first Chief of Defence Forces, General Mrisho Sam Hagai Sarakikya...? Niliwahi kusimuliwa zamani kuwa huyu jamaa alipanga kuipindua nchi/ua Nyerere enzi hizo[Lugalo], na kwamba mtu pekee aliyeokoa hayo mapinduzi alikuwa ni General David Musuguri. Je, ni kweli?

P.S. Kuna paper ninayoaandika kuhusu hali aya kisiasa nchini Tanzania tangu tulipopata uhuru mwaka 61 mpaka leo hii, hivyo I want to get the facts straight kabla sija-submit hiyo paper. So help me by posting down anything you know about uhaini wa huyu jamaa. Just anything.
Peace!

anaitwa Mirisho sio Mrisho
 
Moshe Dayan,

..mimi nina maoni tofauti na kuhusu kutoa details za covert operations zilizopata kufanyika.

..Makaburu wanaweka kumbukumbu zao ktk maandishi. kwa mfano, waliwahi kushambulia D'Salaam kwa manowari na tayari kuna kitabu wanaeleza tukio hilo.

..kwa msingi huo, kama wa-Tanzania hatutaweka kumbukumbu za michango yetu ktk maandishi, Makaburu watafanya hivyo IN THEIR OWN WORDS. sasa wakiwapotosha vijana wetu tusijilaumu wenyewe.

..nimewahi kukutana na Wamarekani walioshiriki Operation Eagle Claw, ile operation ya kuokoa mateka wa Marekani waliokuwa wakishikiliwa Iran ambayo ili-fail. Operation hiyo, pamoja na kwamba ilifeli, ndiyo chimbuko la Navy Seals waliokuja kumuua Osama Bin Laden. Sasa Wamarekani hawafichi kumbukumbu zao hata pale ambapo hawakufanikiwa.

JokaKuu, nakubaliana kabisa na wewe. Jeshi letu lazima liwe jeshi endelevu na kama mambo yote ni siri, inawezekana chance hiyo ya kuwa endelevu ikawa finyu.Operations za miaka mingi iliyopita, zile zisizo hatarisha usalama wetu, si vibaya zikaandikwa vema kwa manufaa ya vizazi vingi vijavyo. Lazima wajue jinsi gani ambavyo jeshi letu limeweza kuwa na historia iliyotukuka
 
comrade joka kuu,

Uko sahihi kabisa, brigade ya kusini 401, ilikua ndio brigade yenye nguvu kubwa ya askari na silaha nzito nzito na mara nyingi ilikua STAND-BY..,

Hii ilitokana na threat kipindi kile cha vita za ukombozi wa africa, kaburu alikua threat kubwa sana kwetu,

Kutokana na jwtz kushiriki katika covert operations nyingi huko kusini na kufanya sabotage nyingi kwenye miundombinu ya kaburu, ilitegemewa kwamba somehow, somewhere, oneday, kaburu ange-retaliate.., na kwa sababu hakuwa na mahusiano mazuri na uganda, kenya, zaire, zambia na malawi, ilionekana the possible route ni through mozambique ambapo na yeye alikua ana-conduct covert ops agaisnt machel, hyo ilikua moja ya sababu ya kuiimarisha ile brigade

Pia kulikua na eneo ambalo kaburu alitaka sana kulifanyia sabotage, hii ni kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kipindi hicho..., hilo eneo liliitwa farm 17, lipo mtwara, pale, ilikua ni training camp ya wapiganaji wa msumbiji, zimbabwe na south africa(anc)..., walifundishwa sabotage (kuharibu miundombinu kama bridges, powerlines, communication centers, dams etc kwa namna yoyote lakn mostly explosives), pia walifunzwa propaganda, skills za gorilla warfare, etc, kaburu alipata shida sana na wapiganaji waliotoka pale na mazimbu. Its a painful truth tulipoteza wengi tu kwenye covert-ops, kuna mahali sitasema wapi, tulipoteza a shocking number of commandos baada ya local "double agent" kuwaingiza kwenye trap...,

pia nakumbuka hali ya usalama wa nchi ilikua tense ilifkia na sisi kila infrastructure muhimu ililindwa na wanajeshi, nadhani mtakumbuka kipindi kile hata madaraja makubwa hasa ya reli tazara yalikua na ulinzi wa jeshi.., hata selander bridge lilikua linalindwa.., brigade zilikua haupiti mwezi lazma stand-by za kutosha

Na ukitaka jua kuhusu ule mpaka wa kusini ulivyokua unalindwa, ule ndio mpaka pekee wenye aerial radar stations nyingi kuliko mpaka wowote kwa ratio ya distance,,, kuanzia ile ya mtwara hadi itungi kyela, zilikua tano (kwa sasa ni classified, taifa kwanza)

Joka kuu, kuhusu kagera, si tulishaweka elimu hapa?

Nafikiri Major Gen Muhidin Kimario played a major role katika kuanzishwa kwake, kama sijakosea. Sasa hivi imefanywa kuwa shule or something!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom