Eng. Zezudu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 7,813
- 10,823
Maombi yanajibiwa,
Kule Pemba watasemaje?Mbona ushabiki wa kisiasa unawatoa utu kiasi hiki aisee
Sasa kama mnalijua hlo mbna mnauwa wenzenu???
Hongereni wote mnaoshabikia misiba ya wenzenu na kuwaombea wengine wafe mkiwa nyuma ya keyboards. Mbarikiwe sana kwa kuweza kujipa moyo kwamba mna kibali cha kuishi duniani milele huku mkiwaombea wengine wafe.
Wengine tunaamini kwenye neno hili. "Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye" Mathayo 24:36
Hao walompigia sim kama sio watu wake aweke mawasliano hapa. Hakuna anayetaka kumuua aache kujitisha
Ila kama anapenda kuishi ubalozini vile
Duuh jaman Sky Eclat kweli umeumia kama Mimi .Ila mpk ipite two yrs tutaona mengiMungu ni hakimu anae hukumu kwa haki.
Nitajie wanachama wa siasa wenye utu?Mbona ushabiki wa kisiasa unawatoa utu kiasi hiki aisee
Ndipo tulipofika na ukiona hivyo inabidi ujiongeze kutambua yaliyomo mioyoni mwao, don't panic!Mbona ushabiki wa kisiasa unawatoa utu kiasi hiki aisee
Wanaouwawa na polisi piani mipango ya Mungu mkuu?.Poleni sana wafiwa, kifo ni mpango wa Mungu, mwanadamu usije ukakejeli
Si bora ushabiki wa Hawa waliyo fariki kwa njia zilizo zoeleweka?Vipi ushabiki wa wale walio katizwa maisha yao kwa Risasi?Napo ulikemea hivi hivi?Mbona ushabiki wa kisiasa unawatoa utu kiasi hiki aisee
Kwenye uzi wa Lisu uliandika hivyo.
Ni halali pia wengine kufurahia Vifo vya Madiwani wa CCM kama wewe ulivyofurahia Lisu kutishwa
Haya sasa, uchaguzi mdogo kabla hata ya uapisho.
---
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita kimepata pigo baada ya madiwani wake wawili wateule kufariki dunia kwa nyakati tofauti wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumamosi Novemba 7, 2020 katibu mwenezi wa CCM mkoani Geita, David Azaria amewataja madiwani hao wateule kuwa ni Masalu Luponya (Bugalama) na Magomamoto Zanziba (Buziku).
Azaria amesema Luponya aliugua wakati wa kampeni na hata siku ya uchaguzi Oktoba 28, 2020 alipigiwa kura na wananchi akiwa amelazwa hospitali ya Bugando.
Amesema Magomamoto aliugua ghafla juzi na alipelekwa Bugando lakini alifariki saa chache baadaye.
Amesema Luponya atazikwa leo nyumbani kwake Bugalama huku taratibu za mazishi ya Magomamoto zikiendelelea kufanywa na chama hicho kwa kushirikiana na familia yake.
Magomamoto alikuwa diwani wa Buziku kuanzia 2010 hadi 2020 na mwaka 2010 hadi 2015 alikuwa makamu mwenyekiti wa baraza la madiwani.
Katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Geita, Jonathan Masele amesema kifo cha Luponya ni pigo kwa CCM na jamii iliyokuwa ikimzunguka.
Luponya wakati wa uhai wake alikua akisomesha wanafunzi 50 wa sekondari na 20 wa ualimu sambamba na kutoa huduma mbalimbali za kijamii kwenye kata hiyo.
Chanzo: Mwananchi
Mama uliandamana?Mungu ni hakimu anae hukumu kwa haki.
Ulitaka afe ili ushangilie vizuri ?Kwani Tundu amekufa nikafurahia???
Huoni kama hao wanaomtishia ni sawa wawekwe hadharani ili washughulikiwe?
Acha kujichanganya utachanganyikiwa bure
Mimi huwa sishangilii vifoUlitaka afe ili ushangilie vizuri ?
Ila huwa unashangilia wakipigwa watu risasi ?Mimi huwa sishangilii vifo
Ila huwa unashangilia wakipigwa watu risasi ?