Gazeti la umma linapoegemea chama flani...

Kwame Nkrumah

JF-Expert Member
Dec 2, 2008
886
376
UONGOZI wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(Tucta) umeamua kuingilia uhuru wa wafanyakazi kwa kupanga kuwashawishi kumchagua mtu unayemtaka awe Rais wa Tanzania.

Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholaus Mgaya, jana alitangaza kwamba mwezi ujao, Kamati ya Utendaji ya Tucta, itakutana kujadili wafanyakazi wampe kura mgombea gani.

Mgaya alisema hayo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Utafiti, Sayansi, Teknolojia na Habari (Raawu) unaofanyika Dar es Salaam.

Sambamba na hayo pia Tucta ililalamikia kima cha chini cha mishahara ikisema nyongeza haijatosheleza na kupendekeza posho za wakurugenzi na viongozi wengine wa juu, ambazo ilisema ni asilimia 59 ya fedha yote ya mishahara nchini, ipunguzwe ili kujazia kwenye mishahara ya wafanyakazi.

Mgaya jana aliendelea kutumia propaganda potofu inayoenezwa na Chadema juu ya kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwa wafanyakazi, inayodai kuwa alikataa kura za wafanyakazi 350,000.

Akizungumza na wafanyakazi katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Mei mwaka huu, kuhusu madai ya nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma, Rais aliweka bayana kuwa uwezo wa Serikali kuongeza mshahara kwa kiwango wanachokitaka Tucta ni mdogo.

Hata hivyo, kutokana na shinikizo la wafanyakazi lililokuwa likijaribu kumtisha Rais kwamba atakutana nao kwenye uchaguzi, Rais pia aliweka wazi kuwa kama uchaguzi unatumiwa kama kigezo cha kuifanya Serikali ilipe mishahara ambayo haina uwezo nayo, bora azikose kura hizo.

“Kwa hilo Rais angepongezwa kuwa ana ujasiri wa kuwa muwazi na kueleza hali halisi kuliko kupokea vitisho akatoa mambo ambayo hayana ukweli na kudanganya wananchi, lakini bahati mbaya hili linapotoshwa na hata kutengenezewa fulana,” alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo ambaye hakutaka kutajwa jina.

Lakini Mgaya katika kusisitiza hilo la kura alikaririwa akitoa mfano:

“Mtu akikualika kwenye karamu halafu akakataa kula chakula utamlazimisha kula? Huwezi, hivyo na sisi tutamtafuta yule anayeweza kula tutampa kura zetu asiyetaka basi, kwani wahenga walisema ukisusa wenzio wala.”

Alisema tayari wameanza maandalizi ya kikao hicho cha kamati ya utendaji ambacho ndicho kitakachotoa jibu la nani apigiwe kura na wafanyakazi wote nchini, ambapo pia shirikisho hilo limesema lina uwezo wa kumwita mgombea yeyote katika vikao vyao, aeleze namna atakavyoshughulikia maslahi ya wafanyakazi.

Akizungumzia madai ya wafanyakazi, alisema hadi sasa hayajatekelezwa kwa kuwa kiwango kilichoongezwa na Serikali ambacho ni Sh 125,000 ni cha chini na hakiendani na msimamo wao katika katika kikao cha majadiliano ambao walikubali kushusha kima cha chini mpaka Sh 160,000.

Alisema awali madai halisi ya Shirikisho hilo yalikuwa ni Sh 315,000 kwa mshahara wa kima cha chini lakini juzi Serikali ilitangaza kuongeza Sh 125,000 na kupunguza asilimia moja ya kodi ya mshahara (PAYE) tofauti na matakwa yao kuwa kodi hiyo ipunguzwe kwa asilimia 15.

“Haya yote hayaridhishi wala hakuna kitu cha kujivunia, vita yetu iko palepale na katika kikao chetu pia tutajadili suala la mgomo,” alisema Mgaya.

Alidai kuwa katika utafiti uliofanywa na Shirikisho hilo, walibaini kuwa fedha nyingi za mshahara zinaishia katika posho za wakurugenzi na viongozi wa juu ambapo Waziri akifungua mkutano analipwa Sh milioni 1.2, Naibu Waziri Sh 900,000 na Katibu Mkuu Sh 600,000 na hivyo kupendekeza posho hizo zipunguzwe kwa manufaa ya wafanyakazi.

“Tunavyofahamu sisi asilimia 59 ya fedha za mishahara nchini ni posho na asilimia 41 ndio mishahara, ambayo kati yake takribani asilimia 30 inapotea, tunaomba fedha hizo za posho angalau Sh bilioni 55 ziongezwe kwenye mishahara

ili iboreshwe na si kung’ang’ania kuwa fedha hakuna,” alisema.

Aidha, alisema kuhusu pensheni kwa wafanyakazi wastaafu, bado haijashughulikiwa na bado wastaafu wanalipwa pensheni ndogo inayoanzia Sh milioni mbili hadi nne, wakati amefanyakazi kwa zaidi ya miaka 30.

“Hii si haki, mbunge anayekaa kwa miaka mitano bungeni analipwa Sh milioni 40 na zaidi, lakini mfanyakazi anayetumikia nchi kwa miaka 30 analipwa Sh milioni mbili,” alihoji.

Alisema kutokana na masuala yote kutoshughulikiwa ipasavyo, bado shirikisho hilo halijakata tamaa hivyo katika kikao hicho pamoja na kutafakari mgombea wa kumpa kura, pia litajadili suala zima la mgomo ili wafanyakazi wapate haki yao.

Juhudi za kumpata Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya kuzungumzia suala hilo hazikuzaa matunda kutokana na simu yake kutopatikana.


MY TAKE: Kuna kamati ya Bunge ya Mashirika ya umma, ambayo kama sikosei inaongozwa na mbunge wa upinzani. Huu ni wakati muafaka wa kuonyesha demokrasia ya kweli kupitia kamati hiyo.
HabariLeo | Wafanyakazi kuchaguliwa mgombea urais



 
Kwame, Naona umechakachuliwa uwezo wa kufikiria. Mbona ya CCM kwenye magazeti hayo hayo uyaoni? LOL
 
Hivi ni lazima kuwa mwanachama wa chama cha wafanyakazi? Maana haya si katika yale tuliyowatuma. Hawa jamaa wanachukua pesa zetu nyingi saana lakini accountability hakuna. Na km ni lazima kuwa mwanachama na kama upo serikalini ni lazima uwe TUCTA??? Maana wanaropoka tu ilhali maoni yao wengine tunayaona yanakiuka malengo ya kuwa mwanachama. Msaada pls kwa mwenye ujuzi.
 
Kwame, Naona umechakachuliwa uwezo wa kufikiria. Mbona ya CCM kwenye magazeti hayo hayo uyaoni? LOL

Sijakuelewa unamaanisha nini, au wewe haujanielewa.
Ukisoma habari hii, inaonekana wazi kabisa ina lengo la kummaliza Slaa. Siyo kweli kwamba TUCTA imewaagiza wafanyakazi kumchagua fulani kuwa raisi , au kuwa na mpango wa kufanya hivyo. Wanachotaka kufanya TUCTA kama "pressure group" ni ku 'endorse" mtu atakayewafaa wao kama TUCTA. Lakini gazeti hili halijaandika hivyo kabisa. Wanaonekana lengo lao kubwa [tena bila kificho] ni kuitetea serikali iliyopo madarakani.

sasa hebu soma MWANANCHI ilivyoripoti habari hiyo hiyo

Tucta: Pilau yetu ni kwa anayeihitaji Send to a friend Tuesday, 10 August 2010 12:52 0diggsdigg

Fredy Azzah
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) limedokeza sifa ya mgombea anayetakiwa wa urais wa Jamhuri ya Tanzania baada ya kuwaeleza wafanyakazi kuwa wasilazimishe "kumpa pilau mtu asiyetaka, bali wampe yule anayetaka".

"Kuna ile kauli ya 'kama ni hivyo, na kura zao sizitaki'," alisema katibu mkuu wa Tucta, Nicolas Mgaya wakati akiongea na wafanyakazi kwenye ukumbi wa Urafiki jana. "Kwani jamani kama una karamu nyumbani kwako; mtu akaja ukampa pilau; akalikataa, utamlazimisha ama utampa yule anayekwambia anaihitaji?”

Alikuwa akirejea kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati akizungumza na wazee wa Dar es salaam kuhusu mgomo uliopangwa kufanyika Mei 5 mwaka huu kuishinikiza serikali kuongeza kima cha chini cha wafanyakazi wa sekta ya umma, kupunguza kodi inayokatwa kwenye mishahara na kuboresha mafao ya wastaafu.

Siku hiyo, Rais Kikwete alisema serikali haiwezi kulipa kima cha chini cha Sh315,000 kama Tucta inavyotaka na kuongeza kuwa "kama ni hizo kura za wafanyakazi, basi niko tayari kuzikosa".

Wakati fulana zimeanza kusambazwa zikiwa na picha ya JK ambayo chini yake kuna maandishi yasemayo "sizitaki kura za wafanyakazi", mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa amekuwa akijinadi kwenye mikutano yake ya hadhara ya kuomba udhamini akisema yeye anazihitaji sana kura za wafanyakazi kwa kuwa zina wengi walio nyuma yake.

Kauli hizo za Dk Slaa na fulana hizo za njano zimeshaikera CCM na imetangaza kuwa itawasilisha malalamiko rasmi Tume ya Uchaguzi (Nec) ikidai kuwa Chadema imeshaanza kampeni.
Jana, akifungua mkutano mkuu wa nne wa Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu na Utafiti (RAAW), Mgaya alisema ni vizuri kumpa kura mtu anayezihitaji na kuahidi kuwa uongozi wa Tucta utakutana kuamua wafanyakazi wampe kura mgombea gani.

“Wewe ukisusa, wenzio wanakula, lazima kamati ya utendaji (ya Tucta) tukae mwezi ujao ili tutoe tamko la uchaguzi mkuu kama wafanyakazi... tuone nani wa kumpa kura zetu. Hata wakifanya nini, lazima tukae... mimi mwenyewe nina watu 15 katika familia yangu watakaopiga kura,” alisema Mgaya, ambaye jina lake lilitajwa na Rais Kikwete takriban mara sita wakati akizungumza na wazee wa Dar es salaam.
“Sisi ni wafanyakazi bwana... tuna uwezo wa kumwita mgombea atueleze atatufanyia nini. tukiona haeleweki, tunamwita mwingine.”
Dk Slaa amekuwa akieleza kwenye mikutano yake ya kuomba udhamini kuwa wafanyakazi wanategemewa na watu wengi na hivyo hawezi kudharau kura zao na kuwasihi wampigie kura wakati wa uchaguzi mkuu ili ashughulikie malalamiko yao.

Tayari CCM imeshaanza kulalamika ikidai kuwa Chadema inacheza rafu kwa kuanza kampeni mapema huku ikikituhumu chama hicho kuwa ndicho kilichochapisha fulana hizo za njano zilizo na picha ya JK zikinadi kuwa hataki kura za wafanyakazi.

Mgaya pia alisema kuwa serikali pia haijafikia malengo ya nyongeza ya kima cha chini cha mishahara na punguzo la kodi katika mishahara kama walivyoafikiana katika vikao.

Alisema kuwa katika vikao hivyo, Tucta ilikubali kushuka kutoka Sh315,000 walizokuwa wakizidai awali mpaka Sh160,00 lakini serikali ilitangaza kima cha chini cha Sh135,000.
Alisema pia shirikisho hilo lilikuwa likitaka serikali ipunguze kodi kwenye mishahara ya wafanyakazi kutoka asilimia 15 mpaka asilimia sita kabla ya kukubaliana kuwa kodi hiyo ipunguzwe kwa asilimia mbili, lakini serikali ikatangaza punguzo la asilimia moja.

“Kwa hiyo viongozi mtakaowachagua leo lazima wawe jasiri; si watu wa kuambiwa acha na wao wanakimbia, kazi bado sana,” alisema Mgaya wakati akifungua mkutano huo ambao pia ni wa uchaguzi.
Aliwataka wanachama hao kuchagua viongozi makini na walio jasiri kutokana na kile alichosema watu wanaopambana nao ni watu wanaotegemea posho na hivyo kilio cha mshahara hawakisikii.
“Kuna siku nilikuwa katika mkutano ambao ulifunguliwa na waziri... kile kitendo cha cha kufungua mkutano analipwa Sh1.2 milioni; akienda naibu wake anachukua Sh600,000 na kama ni katibu mkuu Sh700,000. Kwa hiyo vita hii yetu ni kubwa mno lazima tujipange,” alisema Mgaya akiamsha hisia kali kutoka kwa wanachama.
Mgaya alisema serikali ina fedha za kulipa wafanyakazi mishahara wanayohitaji, lakini karibu asilimia 59 ya fedha za wizara zinatumiwa na viongozi kuanzia makatibu wakuu na kuendelea juu.

Alisema shirikisho hilo limekuwa likiishauri serikali kuwa asilimia 50 ya posho hizo pamoja na asilimia 30 ya kodi inayopotea, zielekezwe katika mishahara ili kuboresha maisha ya wafanyakazi.

Mgaya kifafanua jinsi ya kujua ni mgombea gani atakaye wajali wafanyakazi alisema
Kuhusu kutoweka kwa mgomo wa Mei, Mgaya alisema tishio la mgomo huo liliwasaidia kuwatambua watu ambao ni wasaliti na kuwa safari hii watakuwa makini nao kwa kuwa mkutano huo wa Septemba pia unatarajiwa kutoa hatima ya mgomo wa wafanyakazi ambao awali uliahirishwa.
Kabla ya Mgaya kuanza kuwahutubia wanachama hao, muasisi na mwenyekiti wa kwanza wa Raaw, Joel Juma Kajula aliwataka wafanyakazi nchi nzima kuwa wamoja na kuwa hiyo ndiyo siri ya ushindi.
“Kuna huu wimbo wa mshikamano daima, unaimbwa duniani kote na vyama vya wafanyakazi, sasa mimi nawaomba mshikamano huu uwe wa vitendo,” alisema.


KAULI ya Rais Jakaya Kikwete ya kuwa haitaji kura za wafanyakazi, imeingia katika sura mpya baada ya Shirikisho la Wafanyakazi Nchini (Tucta), kupanga kukutana Septemba mwaka huu kujadili ni mgombea gani anayefaha kupewa kura hizo.


Kauli hiyo ya Tucta imekuja, wakati kambi ya upinzani tayari imeanza kumkaanga kwa kutumia kauli yake ya mapema mwaka huu aliyotoa kwa wafanyakazi, akisema hata wasipompigia kura hapo Oktoba hana shida na kura zao.


Kauli hiyo pia inakuja wakati kukiwa na fulana zinazotajwa kutengezwa na, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zikiwa na picha ya Rais na nukuu ya kauli yake hiyo kwa wafanyakazi.


Mbali na fulana hizo kuonekana kuvaliwa na baadhi ya watu wanaodhaniwa ni wanachama wa Chadema, pia watu mbalimbali wamezipiga picha na kuziweka katika mtandao wa maarufu dunini wa facebook.


Msimamo huo wa Tucta juu ya kauli hiyo ya Rais Kikwete, ulitolewa jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolas Mgaya, alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa nne wa Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu na Utafiti Nchini (RAAW).


“…kuna ile kauli ya kama ni hivyo na kura zao sizitaki, kwani jamani kama una karamu nyumbani kwako, mtu akaja ukampa pilau akalikataa, utamlazimisha ama utampa yule anayekwambia anaihitaji,” alihoji Mgaya huku akiwa anashangiliwa na mamia ya wanachama wa chama hicho waliokuwa wamekusanyika katika ukumbi wa mikutano wa Urafiki Social Hall.


“Wewe ukisusa wenzio wanakula, lazima tukae kamati ya utendaji mwezi ujao tutoe tamko la uchaguzi mkuu kama wafanyakazi na tuone nani wa kumpa kura zetu, hata wakifanya nini lazima tukae, mimi mwenyewe nina watu 15 katika familia yangu watakaopiga kura,” aliongeza Mgaya na kuamsha shangwe zaidi kwenye ukumbi huo.

Mgaya alifafanua kuwa, mbali na hatua hiyo kuchangia na kauli hiyo, Rais Kikwete pia inatokana na serikali kutofikia malengo ya nyongeza ya kima cha chini cha mishahara na punguzo la kodi katika mishahara kama walivyoafikiana katika vikao.

Alisema kuwa katika vikao hivyo Tucta ilikubali kushuka kutoka Sh315,000 walizokuwa wakizidai awali mpaka Sh160,00 lakini serikali ilikuja kutangaza kima cha chini cha Sh135,000.
Alisema pia shirikisho hilo lilikuwa likitaka serikali ipunguze kodi kwenye mishahara ya wafanyakazi kutoka asilimia 15 mpaka sita kabla ya kukubaliana kuwa kodi hiyo ipunguzwe kwa asilimia mbili, ingawa serikali ilikuja kutangaza punguzo la asilimia moja.

“Kwa hiyo viongozi mtakaowachagua leo lazima wawe jasiri; si watu wa kuambiwa acha na wao wanakimbia, kazi bado sana,” alisema Mgaya.
Aliwataka wanachama hao kuchagua viongozi makini na walio jasiri kutokana na kile alichosema watu wanaopambana ni watu wanaotegemea posho na hivyo kilio cha kishahara hawakisikii.
“Kuna siku nilikuwa katika mkutano ambao ulifunguliwa na waziri, kile kitendo cha cha kufungua mkutano analipwa Sh1.2 milioni, akienda naibu wake anachukua Sh600,000 na kama ni katibu mkuu 700,000. Kwa hiyo vita yetu hii ni kubwa mno lazima tujipange,” alisema Mgaya huku akiamsha hisia kali kutoka kwa wanachama.
Mgaya alisema serikali ina fedha za kulipa wafanyakazi mishahara wanayohitaji, karibu asilimia 59 ya fedha za wizara zinatumiwa na viongozi kuanzia makatibu wakuu na kuendelea juu.

Alisema shirikisho hilo limekuwa likiishauri serikali kuwa asilimia 50 ya posho hizo pamoja na asilimia 30 ya kodi inayopotea, zielekezwe katika mishahara ili kuboresha maisha ya wafanyakazi.

Mgaya kifafanua jinsi ya kujua ni mgombea gani atakaye wajali wafanyakazi alisema “Sisi ni wafanananchi bwana, tuna uwezo wa kumwita mgombea atueleze atatufanyia nini, nikio haeleweki tunamwita mwingine,”.
Aliwahamasisha wanachama hao kwa kuwaeleza kuwa hatima ya taifa hili iko mikononi mwao na kuwa, wakiboronga sasa, watoto pamoja na wajukuu zao watakuja kuwacheka.


Alisema, tishio la mgomo uliositisha uliwasaidia kuwatambua watu ambao ni wasaliti na kuwa, safari hii watakuwa makini nao kwani mkutano huo wa Septemba pia unatarajiwa kutoa hatima ya mgomo wa wafanyakazi ambao awali uliahirishwa.


Kabla ya Mgaya kuanza kuwahutubia wanachama hao, mwasisi wa Raaw na Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho Joel Juma Kajula aliwata wafanyakazi nchi nzima kuwa wamoja na kuwa hiyo ndiyo siri ya ushindi.


“Kuna huu wimbo wa mshikamano daima, unaimbwa duniani kote na vyama vya wafanyakazi, sasa mimi nawaomba mshikamano huu uwe wa vitendo,” alisema.

Tucta: Pilau yetu ni kwa anayeihitaji
 
Kwame kumbe RAngi ya kijani na njano imekuingia barabara

watu wanataka mabadiliko, na Raisi aliyepo madarakani kayaanzisha mabadiliko KWA KUTAMKA KWA KINYWA CHAKE MWENYEWE AKIWA NA AKILI ZAKE TIMAMU NA BILA KUSHAWISHIWA NA MTU, "KUWA AHITAJI KULA ZA WAFANYAKAZI" SASA MGAYA KUYASISITIZIA HAYO MANENO KUNA UBAYA GANI?

VYOMBO VYOTE VYA HABARI VIMESHIKWA NA CCM, NA HAKUNA USAWA KABISA LAKINI KWAKO HILO NI SAWA TU, TAMBWE HIZA KUONGELEA MAMBO YA SERIKALI ILI HALI YEYE NI MTU WA CHAMA TU, NALO KWAKO NI SAWA TU
 
Kwame kumbe RAngi ya kijani na njano imekuingia barabara

watu wanataka mabadiliko, na Raisi aliyepo madarakani kayaanzisha mabadiliko KWA KUTAMKA KWA KINYWA CHAKE MWENYEWE AKIWA NA AKILI ZAKE TIMAMU NA BILA KUSHAWISHIWA NA MTU, "KUWA AHITAJI KULA ZA WAFANYAKAZI" SASA MGAYA KUYASISITIZIA HAYO MANENO KUNA UBAYA GANI?

VYOMBO VYOTE VYA HABARI VIMESHIKWA NA CCM, NA HAKUNA USAWA KABISA LAKINI KWAKO HILO NI SAWA TU, TAMBWE HIZA KUONGELEA MAMBO YA SERIKALI ILI HALI YEYE NI MTU WA CHAMA TU, NALO KWAKO NI SAWA TU

Malalamiko yako ni kama yangu, tupo upande mmoja, that's why nimesema kamati ya bunge ya mashirika ya umma ichunguze shirika la umma kuibeba CCM. Kwa maoni yangu gazeti la Mwananchi limetoa habari hii kwa jinsi ilivyotakiwa na siyo gazeti la Habari Leo.
 
Kwame kumbe RAngi ya kijani na njano imekuingia barabara

watu wanataka mabadiliko, na Raisi aliyepo madarakani kayaanzisha mabadiliko KWA KUTAMKA KWA KINYWA CHAKE MWENYEWE AKIWA NA AKILI ZAKE TIMAMU NA BILA KUSHAWISHIWA NA MTU, "KUWA AHITAJI KULA ZA WAFANYAKAZI" SASA MGAYA KUYASISITIZIA HAYO MANENO KUNA UBAYA GANI?

VYOMBO VYOTE VYA HABARI VIMESHIKWA NA CCM, NA HAKUNA USAWA KABISA LAKINI KWAKO HILO NI SAWA TU, TAMBWE HIZA KUONGELEA MAMBO YA SERIKALI ILI HALI YEYE NI MTU WA CHAMA TU, NALO KWAKO NI SAWA TU

Mkuu umeshinwa kumuelewa Kwame. Point yake ni chimbo cha umma kuegemea upande mmoja (hayo ya magazeti yaweza kuwa mada nyingie). Kumbuka bado hawaja taja nani wata msupport. Je wakitoka na wakisema wata msupport mgombea wa CCM uta semaje? Maana sasa unaonge hivi kwa sababu una tegemea baada ya kilicho tokea TUCTA watamsupport mgombea wa upinzani lakini kumbuka Tanzania ni zaidi ya iuijuavyo. Leo wakitoka na kusema wameongea na Kikwete na wameamua kumendorse bado uta kuwa na attitude hii hii? Kumbuka mdomo waweza tumika kumbusu mtu ama kumsonya. Waki msupport msiyo tegemea msiseme mmesonywa maana Kwame ana advocate usawa.
 
Mkuu Kwame nime kusoma vizuri tu. Majibu ya watu ndiyo maana nasemaga Watanzania wengi ni wanafiki. Wana kilalamikia kitu pale tu ambapo haiwa faidishi wao. Lakini kitu hicho hicho kikiwa na faida kwao hawa kawii kuki kumbatia na kubadilisha mawazo. Watu wengi hapa wana kupinga kwa sababu wana assume mmoja kwa moja kwamba TUCTA itamsupport mgombea wa upinzani na ndiyo maana wana kuja na hoja ya kwamba mbona magaeti ya umma au vyombo vya dola vinaipendelea CCM. Lakini waulize watu hao je wata lionaje hili swala iwapo TUCTA wakiamua kumendorse mgombea wa CCM? Wata lalamika kwamba CCM ime pendelewa na chombo cha umma?
 
Inachekesha kuona ni jinsi gani Habari leo wanasahau kabisa au wanaamua kwa makusudi kupotosha historia ya Tanzania especially Tanganyika na vyama vya wafanyakazi.

Kwa kumbukumbu tu vyama vya wafanyakazi siku zote vilikuwa mstari wa mbele kumkomboa mfanyakazi na mwananchi wa kawaida as such aligning with a political party that has some sort of a compromise na matakwa yao.
 
hivi ni lazima kuwa mwanachama wa chama cha wafanyakazi? Maana haya si katika yale tuliyowatuma. Hawa jamaa wanachukua pesa zetu nyingi saana lakini accountability hakuna. Na km ni lazima kuwa mwanachama na kama upo serikalini ni lazima uwe tucta??? Maana wanaropoka tu ilhali maoni yao wengine tunayaona yanakiuka malengo ya kuwa mwanachama. Msaada pls kwa mwenye ujuzi.

kajiunge fibuka tuache na tucta yetu
 
It is a normal, democratic and a widely accepted practice for trade unions and other groups to ENDORSE a particular candidate. Ni tumaini langu kwamba TUCTA itatoa endorsement yake mapema. CCM wameshaogopa kwani wanajua wafanyakazi watamtaka nani.

Wananchi wengi wa Tanzania wamepata matumaini kutokana na Slaa kujitokeza kuwapigania. Viongozi wa CCM wameogopa mno! Na wana kila sababu ya kuogopa. Wamezoea kuhodhi madaraka, lakini sasa hata wao wameanza kusoma alama za nyakati.

Kaza buti Kamanda Wetu Slaa. Tuko nawe. Wananchi 4,103 wa Wadi ya Orkolili huko Siha ambao wamekihama CCM na kujiunga nasi ni mwanzo tu wa matokeo ya kujitolea kwako kukomboa Tanzania.
 
1. Si sawa kwa vyombo vya umma kama magazeti ya serikali kupendekeza au kumpendelea mgombe au chama fulani.

2. Vyama vya wafanyakazi si vyombo vya umma, ni vyombo vya wafanyakazi vyenye "special interest" za wafanyakazi na vina uhuru wa kupendelea / kupendekeza chama au mgombea fulani ambaye vinaona atawafaa wafanyakazi wake. Sitegemei chama cha wlimu kipiganie interests za madaktari kabla ya za walimu. Idea nzima ya vyama vya wafanyakazi ni kupata bargaining power, so what is the use ya kuwa na chama cha wafanyakazi weeengi nchi nzima bila kuitumia hiyo bargaining power kuhakikisha maslahi ya wafanyakazi yanawekwa mbele ? Kama hukubaliani na maoni ya chama cha wafanyakazi kimoja jiunge na kingine, au anzisha chako.It's not like tuna chama kimoja tu cha wafanyakazi.
 
Inachekesha kuona ni jinsi gani Habari leo wanasahau kabisa au wanaamua kwa makusudi kupotosha historia ya Tanzania especially Tanganyika na vyama vya wafanyakazi.

Kwa kumbukumbu tu vyama vya wafanyakazi siku zote vilikuwa mstari wa mbele kumkomboa mfanyakazi na mwananchi wa kawaida as such aligning with a political party that has some sort of a compromise na matakwa yao.

Zuma,Kawawa,Chiluba.....wooote ni kama Mgaya...wahts wrong now?
 
Someni hii...............

Maoni ya Mhariri

Kauli ya Rais Kikwete isipotoshwe
Imeandikwa na Mhariri; Tarehe: 10th August 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 28; Jumla ya maoni: 0


TUMEMSIKIA Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Nicholaus Mgaya, akihamasisha wafanyakazi kumnyima kura Rais Jakaya Kikwete, mgombea wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao Oktoba 31 mwaka huu. Katika kuhakikisha hilo linafanyika, Mgaya akihutubia juzi Mkutano Mkuu wa Nne wa Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu na Utafiti (RAAW) Dar es Salaam, alisema Kamati ya Utendaji ya Tucta itakutana mwezi ujao kutoa tamko hilo.

Kisa, alisema ni kauli (inayopotoshwa) ya Rais Kikwete alipozungumza Mei mwaka huu na wazee wa Dar es Salaam, kwamba hazitaki kura za wafanyakazi kutokana na wao kudai kima cha chini kuwa Sh 315,000.

Ni dhahiri kuwa kila mwenye nia njema na aliyesikia hotuba ile ya Rais vizuri, ataelewa kuwa kinachoenezwa sasa si tu na Mgaya bali pia na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Wilbrod Slaa, ni upotofu wa alichokisema.

Rais alibainisha wazi kuwa Serikali yake haina uwezo wa kulipa kiasi hicho cha fedha, lakini kama wafanyakazi wanatumia kigezo cha kura kwenye uchaguzi ili alipe asichoweza, basi yuko radhi kukosa kura hizo, lakini si kuwadanganya wafanyakazi.

Kwa anayeelewa vizuri lugha ya Kiswahili, kauli hiyo haimaanishi kwamba hataki kura za wafanyakazi, ila atajikuta hana la kufanya kutokana na shinikizo hilo ambalo litaisuta nafsi yake kwa kuwadanganya Watanzania, kuwa uwezo upo kumbe sivyo.

Ni sawa na mtu kukualika kwenye shughuli akakuahidi kukupa pilau ukaandaa njaa, lakini baada ya hapo pilau usilione, huyo mtu atakuwa katika kundi gani, je, akisema karibu shughulini lakini utakula muhogo na ukaukuta, hatakuwa mwaminifu na mkweli kwako?

Pengine Mgaya angebaki na haki yake ya msingi ya kuzungumzia nafsi yake hasa linapokuja suala la upigaji kura ambao ni haki na siri ya kila mtu, akaamua anavyoamua kama ni kumnyima kura Kikwete afanye hivyo kwa hiari na haki yake, badala ya kutaka kukampeni na kushawishi wafanyakazi.

Aelewe pia kuwa si wafanyakazi wote wasiomwelewa Rais Kikwete na kauli yake hiyo, walioelewa waachwe waendelee kuelewa na hata ukifika uchaguzi watumie haki, hisia na fikra zao kuamua katika sanduku la kura na wasilazimishwe kuelewa vinginevyo.

Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta awaache akina Slaa waendelee na siasa za propaganda ambazo zinaruhusiwa, lakini tunaamini nao wanaelewa alichokuwa akikimaanisha Rais na hivyo kuitumia kauli inayopotoshwa kama silaha, hatudhani kama itasaidia kwani mwamuzi ni mwananchi mwenyewe.
 
Na habari yenyewe hii hapa....Mwongo nani sasa?

Tuesday, May 4, 2010
Rais Kikwete:TUCTA waongo
"TUCTA ni waongo! Tucta ni wanafiki! Tucta wana hiana!... wafanyakazi watakaogoma tarehe 5, watakuwa wamekiuka sheria na watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria na kanuni za Serikali. Na wale wafanyakazi wataokwenda kazini lakini wasifanye kazi, pia watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

"Kiongozi bora ni yule anayewaeleza wananchi wake ukweli hata kama ukweli huo utakuwa unauma."

Hiyo ni kauli nzito ya Rais Jakaya Kikwete, alipozungumza na Taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam jana, kuhusu mgomo ulioitishwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kuanzia kesho, kwa madai kuwa Serikali imepuuza mapendekezo ya kuongezwa kwa kima cha chini ya mshahara kufikia Sh 315,000 kwa mwezi.

Rais alisema Serikali haiwezi kulipa kima cha chini cha Sh. 315,000 kutokana na mapato inayopata.

"Nimewasikia Tucta, wanasema huu ni mwaka wa uchaguzi, hawatanipigia kura kama sitalipa kima cha chini wanachokitaka, nipo tayari kuzikosa kura za wafanyakazi kuliko kuwadhulumu Watanzania walio wengi, wakakosa dawa, maji, barabara, elimu, pembejeo za kilimo na huduma nyingine," alisisitiza Rais akionesha dhdhiri kukerwa na msimamo wa Shirikisho hilo.

Alisema pamoja na mazungumzo yanayoendelea sasa kwa lengo la kuboresha maslahi ya wafanyakazi ikiwamo mishahara, viongozi wa Tucta kwa makusudi, wameamua kuitisha mgomo wa wafanyakazi huku wakitoa madai ya uongo, kwamba Serikali haisikii na viongozi wa Serikali hawawajali wafanyakazi.

Alieleza kushangazwa na kauli za viongozi wa Tucta wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), kauli ambazo kimsingi alisema zinajenga taswira kwamba hakuna mazungumzo yoyote yanayoendelea baina ya Serikali, waajiri na wafanyakazi, kupitia vyama vyao ya kushughulikia maslahi yao na kujenga hisia mbaya kwa wafanyakazi kwamba Serikali haiwathamini.

"Si kweli, Serikalii inawajali na kuwathamini sana wafanyakazi. Zipo hatua ambazo imechukua na inaendelea kuchukua katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

"Tuliingia madarakani kima cha chini ya mshahara kikiwa Sh 65,000 lakini sasa ni Sh 104,000. Kwa makusudi viongozi wa Tucta wanawadanganya wafanyakazi kwamba Kikwete ameongeza Sh 4,000 tu tangu amekuwa Rais wa nchi, jambo ambalo ni uongo mkubwa," alisema Rais Kikwete.

Alitoa mfano wa mazungumzo yaliyofanyika mwezi uliopita, ambapo pande hizo tatu; Serikali, waajiri na wafanyakazi, walikutana mara tatu Aprili 6, Aprili 26 na Aprili 27 kujadiliana kuhusu kima cha chini ya mshahara na wakashindwa kuafikiana kutokana na viongozi wa Tucta kuleta mapendekezo ya viwango vitatu vya kima cha chini cha mshahara baada ya Serikali kukataa kima cha chini cha awali cha Sh 315,000.

Alisema mazungumzo hayo yakapangwa kuendelea Mei 8 mwaka huu. "Wakati mazungumzo yamepangwa kufanyika tena Mei 8, ili wao waje na mapendekezo yao mengine ya kima cha chini cha mshahara, na sisi Serikali tulete mapendekezo yetu ili tujadiliane, viongozi hawa wa Tucta wanashindwa kusema ukweli na wanakana hata kile walichokisema na kupendekeza wao wenyewe ndani ya vikao halali," alisema.

Rais alisistiza kuwa Serikali kwa upande wake, imekuwa ikiheshimu mapendekezo ya nyongeza ya kima cha chini cha mshahara katika sekta binafsi kupitia bodi nane za kisekta, na ndiyo maana kutokana na mazungumzo hayo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, alitangaza kima kipya kwa sekta binafsi Aprili 30, mwaka huu, ambacho kilianza kutumika Mei Mosi.

Alisema pia Serikali kupitia majadiliano hayo, imekubali kuongeza kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma, ongezeko ambalo litatangazwa katika bajeti ijayo ya mwaka wa fedha wa 2010/11, tofauti na kauli zinazotolewa na viongozi wa Tucta kwa wafanyakazi.

Aliongeza kuwa Serikali ina wafanyakazi 350,000 na endapo italipa kima cha chini cha mshahara cha Sh 315,000 italazimika kutumia Sh bilioni 6,852.93, fedha ambazo ni nyingi kuliko mapato ya Serikali, kwani katika bajeti ijayo, Serikali imepanga kukusanya Sh bilioni 5,757.3, na ili iweze kulipa kiasi hicho, italazimika kukopa jambo ambalo ni kichekesho.

"Kama tutalipa mishahara hii kama wafanyakazi wanavyotaka maana yake ni kwamba tutawaridhisha wafanyakazi hawa 350,000, lakini tutawadhulumu Watanzania milioni 39,650,000.

Hatutakuwa na pesa ya kuwanunulia dawa, kuwajengea barabara, kununua madaftari, kununua pembejeo za kilimo wala kuwapa maji safi na salama jambo ambalo siwezi kukubali litokee," alisema.

Rais Kikwete katika hotuba hiyo iliyorushwa moja kwa moja na baadhi ya vituo vya redio na televisheni, alizungumzia pia mkutano mkubwa wa uchumi kwa Bara la Afrika, utakaofanyika kwa siku tatu Dar es Salaam kuanzia kesho, kwamba utasaidia kukuza na kutangaza jina la Tanzania.

Alisema viongozi na wakuu wa nchi 11 wamethibitisha kushiriki mkutano huo utakaoshirikisha zaidi ya watu 959 kutoka nchi 85 Duniani.

Alisema Tanzania kwa upande wake itanufaika kutangaza fursa ilizonazo katika vivutio vya utalii na uwekezaji
 
Mimi niongezee wandugu KAMA KUNA MTU ANA GAZETI LA TAZAMA TANZANIA LA TAREHE 10-16 AUGUST 2010 ATAKUBALIANA NAMI JINSI VYOMBO VYA HABARI VINAVYOTUMIWA NA CCM!!! Mwandishi wa Makala hii anakwenda kwa emaila mpakia@yahoo.com na simu 0718279346 kwa kweli anapotosha sana kuhusu Dr slaa... Kichwa cha makala yake kinasema TUMWANGALIE SLAA UPANDE ALIOUEGEMEZA UKUTANI?
Ndani ya makala yake kuna mambo kama
>> Dr Slaa kakimbilia urais kuogopa jinsi atakavyo garagazwa ubunge kama angegombea ubunge Karatu!
>> Dr Slaa ni Mwongo!
>> Dr Slaa ni Kigeugeu!
>> Dr Slaa ni Mkosa Subira!
 
Back
Top Bottom