ba mdogoo
Member
- Jul 25, 2014
- 68
- 32
Gazeti namba moja tanzania. Lenyekutupa habari za uhakikaMamlaka ya mawasiliano Tanzania kuiptia Kamati ya Maudhui imesitisha leseni ya utoaji wa huduma za maudhui mtandaoni ya Mwananchi Newspaper kwa kipindi cha miezi sita, na kuwapiga faini ya Tshs milioni 5.
Adhabu hiyo imetolewa baada ya kubainika kuwa Aprili 13 kupitia mitandao ya kijamii Mwananchi Newspaper ilichapisha taarifa ya kupotosha kinyume cha Kanuni Na. 5(1)(a) na 12(l) za mawasiliano ya kieletroniki na posta, 2018
Mwananchi Newspaper waliitwa kujieleza kwanini wasifungiwe Aprili 15, na wakakiri kuwa kweli walikiuka kanuni hizo. Kwa kufuata sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Kifungu cha 28(1)(b) na (d) sura ya 172, ya mwaka 2017 wamepewa adhabu hizo
Iwapo Mwananchi Newspaper atashindwa kutekeleza adhabu hiyo TCRA itachukua hatua zaidi
====