Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
"Lowasa ni kama Mohammed"
Tueleze hapo shekhe alimaanisha mini?

Mbona magazeti hayakunukuu habari na kusema "wakristo sasa mashakani lowassa akiteuliwa"?
Ni kwamba waandishi ni wanataaluma na walielewa lipi lilikuwa lengo,sasa Leo imekuwa habari kwasababu ni mfano toka upinzani
Ni kweli gazeti walichosema unategemea kauli ya Mchugaji wa Chadema itakuwa na maana gani mkuu?
 
Kwa mwislamu mwenye akili zake na uelewa wa kutosha, kauli hii ya Mch. Msigwa haiwezi kumkwaza hata kidogo. Ni ya kawaida mno na wala haina hata chembe ya udini kama gazeti hilo linavyotaka kuwaaminisha watu. Gazeti hilo lina nia ovu ya kichonganishi na ni la kupuuzwa tu! Siwezi kujizuia kuamini kuwa mhariri wake ama yeye mwenyewe anapenda mgawanyiko kati ya wakristo na waislamu au anatumiwa na wenye malengo hayo.
 
Huu ndio ulevi tunaoupenda sana.

Wazungu na waarabu walitupatia sana walivyoleta hizi dini!Mkiwashtukia katika njama za ulaji wao wanatafuta choko choko za kidini wanawaingiza huko,watz wrote tunahamia huko,problem solved wenyewe wanaendelea kututafuna kiulainiii!period
 
Unapokuwa umegubikwa na imani au mtazamo fulani bila kutaka kupanua wigo wa kufikiri ni hatari sana,watu wataendelea kulalamikia mfumo kristo pasipo kuhangaikia suala la elimu na kujibidisha ktk maisha.Nchi ambayo inatoa uhuru wa kuabudu ni vigumu kushinikiza kupata jambo kwa misingi ya dini.Muhimu ni kuachana na imani za mawe kwa kusomesha watoto ktk elimu dunia na ahera,kufanya kazi kwa bidii na maarifa huku ukimtumainia Mungu pasipo kushika upanga kumtetea Mungu kama mdoli usio na nguvu wala mamlaka.
 
Chadema ni kama msikiti kila mtu anayetaka kuslimu na kumrudia Mola wake hakataliwi. Naomba makosa ya huo usemi
 
Teh teh teh.
Mgalatia unataka kuleta Ule mchezo wa kiklistu sio?
Mimi nimeshaoa kamanda.
Mjaribu Matola. Nyie wote imani moja. Halafu Mkwala wake anaanza kukuimbia Taarabu kwanza kisha anakufukiza udi. Akimaliza hapo anamwaka Asumini chumba kizima!
Teh teh teh!

Usiniulize hizi habari nimezipata wapi. Muulize lusungo.
Iko siku moja kwenye Jukwaa la Watu wazima nilimkuta lusungo analalamika kuwa Jamaa ana makalio magumu ka Nyani mzee.

Yaani wakitaka kumchoma sindano lzm wampake majivu na Grisi ndio ipite!

Sasa sijui alikuwa anamtibu kitu gani muefeso mwenzake mpk akajua ugumu wa makalio yake.

Kwema Africa sana?
Mbona unawaka sound nyingii, ooh Matola..simba anakimbi km150 kwa SAA lakini anazaa! Nimekusifu unapendeza dogo; sema asante!
 
Last edited by a moderator:
Msigwa yeye ni mchungaji
na anajua tuhuma zipo za CHADEMA kuwa chama cha wakristo
hata kama hizo tuhuma si za kweli na za kutunga
hakupaswa kuwa reckless na kuanza kuita CHADEMA kanisa

Mifano ipo mingi ya kufikisha ujumbe

Kutumia mifano ya aina hiyo ni ama uzembe au kiburi na kutokujali kina nani hawatapendezwa

Kuna vitu vinashangaza sana, NYIE BAVICHA mtu tena mchungaji kashasema CDM ni kanisa, sasa nyie mnabisha nini? mambo ya kwamba hakumaanisha nyie mmejuaje?
 
Msigwa ni mkristo, ningeshangaa sana angetoa mfano wa Chadema ni kama msikiti..Tatizo kubwa la watu wengi huwa wanafiki sana kwenye imani zao, Msigwa yupo sahihi kabisa kwasababu katolea mfano wa kitu anachokijua na kukiamini. ni sawa na leo litoke gazeti la kikristo liseme wakristo kula nyama iliyochinjwa na muislamu ni kuudhalilisha Ukristo,kitu ambacho si kweli kuwa Ukristo unadhalilika. Kwahiyo hilo gazeti la Al huda ndiyo linafanya uchochezi kwasababu mtu aliyetamka hivyo ni wa imani ambayo yeye anaifahamu na ndiyo maana kaltolea mfano huo. Hata viongozi wetu ambao ni wakristo wanaoalikwa kwenye hafla ya Kiislamu halafu wanavaa kanzu ,ule ndiyo unafiki. Wanavaa kanzu huku wanafuga nguruwe,ule sasa ni kuudhalilisha uislamu. kwanini wasiende kama wanavyoenda kwa imani yao, kwasababu ule ni mwaliko tu.

Hapo kwenye maandishi mekundu inaonyesha wazi nyie watu ni wabaguzi sana! Msigwa amekosea alipaswa aisemee CHADEMA bila kuihusisha na dini yoyote!
 
hisia, mihemko, mahaba, na mgandamizo wa hisia za kidini ndio zinazowatawala waandishi na wahariri wa gazeti husika
 
Yaani Mchungaji Msigwa kuifananisha Chadema na Kanisa ni mfano tu lakini Al-Huda wao kuhoji wapo kibiashara daah!!

Double standard tu hiyo, hakuna lolote
 
Ni kweli gazeti walichosema unategemea kauli ya Mchugaji wa Chadema itakuwa na maana gani mkuu?

Kweli ndugu sijui mwalimu labda kutoka oxford au Harvard aje akuelimishe ndio utaelewa!
Ngoja nikufundishe kwa mifano kama Yesu(kama hautakuwa umekwazika na kauli hii basi umenielewa,kama kuna tatizo bado basi kuna tatizo zaidi ya kuelewa)
 
hisia, mihemko, mahaba, na mgandamizo wa hisia za kidini ndio zinazowatawala waandishi na wahariri wa gazeti husika

The same applied to Mchungaji Msigwa, hisia, mihemko, mahaba, na mgandamizo wa kidini ndio zilizomtawala msigwa na kusema CHADEMA ni kanisa.
 
Tatizo chadema hamtaki kukubali kuwa huyu mchungaji wenu amekosea...! Hivi kweli alio kuwa ana wahutubia wanajua maana ya tamathali za semi,falsafa na mambo mengine mnayo fikiri? Kwenye siasa hakuhitaji mafumbo hasa linapo kuja swala la dini...! Msigwa ni mjinga tuu kasema mwenyewe kuwa Chadema ni kama kanisa wana hubiri wokovu..mnategemea watu watafsiri nini tena wakati matamshi yako clear tuu hapo na watu wanatakiwa kuvuta picha ya kanisa?

Kinacho waponza Chadema wengi ni kujifanya wasomi na wajuaji ...oooh tamathali...!

Jengeni tabia ya kuambia ukweli huyu Msigwa amekosea ....?

Mkuu uvumilivu ulimshinda Msigwa ameona bora amwage mboga kama waislamu tukiamua kumwaga ugali kwa kutoichagua CHADEMA sawaa!! Mimi nafikiri Msingwa angetumia busara na uungwana kama angeisemea CHADEMA bila kuihusisha na dini yoyote!!
 
Tatizo chadema hamtaki kukubali kuwa huyu mchungaji wenu amekosea...! Hivi kweli alio kuwa ana wahutubia wanajua maana ya tamathali za semi,falsafa na mambo mengine mnayo fikiri? Kwenye siasa hakuhitaji mafumbo hasa linapo kuja swala la dini...! Msigwa ni mjinga tuu kasema mwenyewe kuwa Chadema ni kama kanisa wana hubiri wokovu..mnategemea watu watafsiri nini tena wakati matamshi yako clear tuu hapo na watu wanatakiwa kuvuta picha ya kanisa?

Kinacho waponza Chadema wengi ni kujifanya wasomi na wajuaji ...oooh tamathali...!

Jengeni tabia ya kuambia ukweli huyu Msigwa amekosea ....?

Vema,ndio maana nimeshangaa wasomi wahariri wa gazeti ndio wanakuwa wa kwanza kujifanya kutoelewa na kueneza uchochezi!Hayo maneno ya "waislam sasa mashakani" wameyatoa wapi na kwa utafiti UPI?Mbona hatukuona reaction ya waliokuwa mkutanoni?Kimsingi wao walimwelewa Msigwa,wakristu kwa waislamu!Sasa kama hao wananchi walielewa wahariri wameshindwaje kuelewa?Hakuna lolote zaidi ya chuki tu na kuweka weledi wa kazi pembeni
 
Viongozi wa Chadema yapasa wachunge ndimi zao kwani ni wengi hutumia misemo ya kikristo (kilokoe) majukwaani wakati wana wafuasi wa dini tofauti!
 
The same applied to Mchungaji Msigwa, hisia, mihemko, mahaba, na mgandamizo wa kidini ndio zilizomtawala msigwa na kusema CHADEMA ni kanisa.
kinacho ni shangaza ni wanachadema kuto mkemea Msigwa badala yake wana mtetea eti tamathali za semi Teh Teh...hivi Msigwa alikuwa ana wahutubia watu wanao jua kuwa ni tamathali za semi? Msigwa ni mjinga lakini hakemewi.....Unaposema Chadema ni kama kanisa umesha wagawa watu...hivi hakukuwa na mfano mwingine?
 
Vema,ndio maana nimeshangaa wasomi wahariri wa gazeti ndio wanakuwa wa kwanza kujifanya kutoelewa na kueneza uchochezi!Hayo maneno ya "waislam sasa mashakani" wameyatoa wapi na kwa utafiti UPI?Mbona hatukuona reaction ya waliokuwa mkutanoni?Kimsingi wao walimwelewa Msigwa,wakristu kwa waislamu!Sasa kama hao wananchi walielewa wahariri wameshindwaje kuelewa?Hakuna lolote zaidi ya chuki tu na kuweka weledi wa kazi pembeni
Sasa Kama Msigwa amesema Chadema ni kama kanisa na wana hubiri wokovu unategemea waislam wasiwe mashakani?,,,,Hivi mnatetea nini nyie?
 
kinacho ni shangaza ni wanachadema kuto mkemea Msigwa badala yake wana mtetea eti tamathali za semi Teh Teh...hivi Msigwa alikuwa ana wahutubia watu wanao jua kuwa ni tamathali za semi? Msigwa ni mjinga lakini hakemewi.....Unaposema Chadema ni kama kanisa umesha wagawa watu...hivi hakukuwa na mfano mwingine?

Cha ajabu wanalishambulia gazeti lilioandika alichokisema Msigwa, ila msigwa wanamfuga bila kujua wanafuga bomu, watu walisema kitambo CDM ni sawa na kanisa, wao wakabisha sasa mchungaji wa hilo kanisa(CDM) katangaza wazi, bao wanabisha
 
Pro-Chadema wamebakia kujivua nguo tu hapa na kuwapa wakati mgumu viongozi wao mbele ya jamii za Waislam.

Tunapenda sana kuwasoma mnavyopambana na Waislam.

Tutakutana October kwenye box la kura.

Teh teh teh
 
Nilitegemea Magazeti mengi maana taaluma ya uandishi ni moja, Basi na wao wangenukuu kama gazeti hili lilivyoandika ikaonekana wote wamekereka,
Magazeti ya Kikristo nayo yangekuwa yanaegemea Chadema kama msingi unaoangaliwa na kanisa.
Mawazo ya mtu mmoja yasilipoteze taifa,,uandishi wa Habari una adabu vile vile
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom