Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
Kuna watu walisema lowasa ni sawa na mtume muhamady lkn hiki kijarida kilikaa kimya.
 
Msigwa yeye ni mchungaji
na anajua tuhuma zipo za CHADEMA kuwa chama cha wakristo
hata kama hizo tuhuma si za kweli na za kutunga
hakupaswa kuwa reckless na kuanza kuita CHADEMA kanisa

Mifano ipo mingi ya kufikisha ujumbe

Kutumia mifano ya aina hiyo ni ama uzembe au kiburi na kutokujali kina nani hawatapendezwa

safi saana "The boss" uko sahihi kabisa na umeeleweka vizur
 
Kama nisuala la kutafsiri maneno haina shida. Maana kila mtu anatafsiri kwa kadri akili yake inavyo mtuma.
 
Gazeti limeripoti kama alivyosema Mchungaji wa Chadema Msigwa.

Kasema kweli Chadema ni kama Kanisa.

Sasa hapo unalishambulia gazeti kwa kosa gani, wewe umejuaje kama Mchungaji Msigwa alikuwa hana maana hiyo.

safar hii hamutuwezi hata muanzishe hoja za kidini...na kwa nn ailete mada hii hapa??...huu ni ujinga kushabikia udini
 
Kama huna cha kuandika nyamaza kimya,kama umekasirika jinyonge. sawasawa,umesahau lukuvi alivyozungumza kanisani?hukusema kwa vile yuko kanisani kwanini azungumzie siasa? Na msigwa hakuwepo kanisani lakini amezungumzia habari za kanisa,kinacho kukera nini sasa?usiwe mjinga wewe kuwa muelewa.
 
Kuna watu humu mnajifanya wasomi kumbe hakuna kitu. Tangu hii mada imeanzishwa nyie mnabishana dini dini alafu mpaka sasa sijaona nani bingwa. Msomi wa kweli hawezi bishana kitu ambacho hakina hitimisho lenye jibu sahihi. Debate ya dini huwa haina mshindi kila mtu atatetea upande wake kwa hiyo ni bora kubaki na imani yako bila kutetereka na sio kutoleana Maneno machafu humu ambayo yanapunguza thamani zenu kama wanadamu. Muogopeni mwenyezi mungu kwa Maneno yenu humu jf maana sisi mtaani tunaishi vizuri tu watu wa dini tofauti na kishirikiana katika mambo ya kijamii ila humu jf ndo kuna udini Sana tena Sana mpaka jukwaa linaboa .
 
Hakuna kitu kilokuwa low, and nothing has been blown out of proportion, it was bad judgement on his part kutumia maneno hayo, kama previous contributors walivosema, there were a lot of examples angeweza kutumia, without resorting to religion. Wakati huu is no time to add fuel to the fire.
bill of right is part of our constitution na ina guarantee freedom of expression na speech. acheni kuturudisha kwenye ukoloni wa waarabu na wazungu, no way!!
 
Mwandishi amesema "wanachama waislam matatani". Na hili sio mara ya kwanza kwa magazeti ya kiislam kuituhumu CDM. Some time haya magazeti yanatakiwa yachukuliwe hatua za kisheria maana kama anachodai Mwandishi si kweli basi mamlaka huska zinatakiwa zisiache mambo haya hivi hivi. Na kama kweli tuhuma hizo ni za kweli basi msajili wa vyama vya siasa aangalie hili. Naomba nisisitize kua tusipende sana kuingiza udini kwenye siasa maana ni hatari sana. Angalia makundi kama ISIS na boko haram yanavyoua maelfu ya watu. Hata kule Rwanda mauaji ya halaiki yalichochewa na vyombo vya habari visivyojali weredi wa uandishi wa habari.
 
Udini!! udini!! udini!! Huyu mwislam huyu mkristo. Lakini wote ni watanzania.
 
Alijuayuko kanisani kwake jaman msameheni..inawezekana alikuwa aanahubiri neno lakutoa sadaka ama kuchangia chama akapitiwa.
 
Nimefadhaishwa sana na gazeti la Al-Huda litokalo kila wiki toleo na.523 SHAWWAL1436 la tar23-29, Julai 2015 Uk wa mbele limepambwa na maneno.

Msigwa: CHADEMA kama kanisa
*Asema wanahubiri habari ya wokovu
*Wanachama waislamu sasa mashakani

Kimsingi kauli hizo ni za kichochezi dhidi ya waislam na wakristo! Ifahamike kuwa Mchungaji Msigwa(Mbunge wa Iringa) alitoa kauli hiyo kifalsafa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema! Msigwa alisema "...CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, unatubu unafanya kazi!"

Mimi siyo msemaji wa Msigwa, lakini nimekerwa na gazeti hilo kwa sababu kauli ya Msigwa haikulenga kutugawa Wanachama wa CHADEMA kwa misingi ya kidini! Ni kama kauli ya Tundu Lissu alipotamka kuwa "...John Pombe Magufuli na kabila lake la MaCCM..." hakulenga kuwa kuna kabila la MaCCM!

Kwahiyo siyo kweli kuwa Msigwa alimaanisha CHADEMA ina wafuasi wa Kikristo pekee!

Naomba mamlaka husika iingilie kati! Mungu Ibariki Tanzania!
Wemwenyewe mamlaka bado ujiamini??nenda peleka malalamiko police ukiwa na vithibitisho na pia ujiandae kulipa garama zakesi kama utashindwa
 
hilo gazeti na mengine kama hayo mbona kawaida sana kuchochea sema serikali imetulia labda inasubiri wazidi...ila itikadioz ao ni kuchochea...utanielewa kama ni mtu makini na mchambuzi makini
 
Nilichokiona kwa gazeti ilo niangalizo tu...
Niiman yngu kua muandishi hakua na maana pana kama ulivyoidadavua kiuelewa wako..
Siungi mkono kauli ya msigwa kufananisha chama na dini anayoamin yeye hali ikiwa viongozi wajuu waliowngi ndan ya chama wametokana na dini hio...
Niiman yangu kua alichoongea alimaanisha A huku akiamin kua atapata majibu B...
Waislam hawampi m2 kura kwasababu ya mahakama ya kadhi kama nilipitia kwa mchangiaji flani ivi kumuhusisha Pinda na waislam..
Niimani yangu kua unataka kuniaminisha kua waislam wanatumika kwa matukio maalum haswa unapowaletea maswala yanayowahusu kimantiki hio basi itakua waislam haki yao yakura kikatiba itakua imeondoka...
Kauli kama za Msigwa hazipaswi kutumika ktk majukwaa hata kama ukiichukulia kimifano tu.
 
kama tunataka kuwa salama tunatakiwa kuwadhibiti wapumbavu wanaoweza kuangamiza taifa kwa fikra zao finyu za kutumia mambo ya hatari katika jamii kutafuta mafanikio kisiasa.

mtu yeyote anayetumia dini, kabila na mambo mengine ambayo kwa yeye anaona nikiwavuta watu wenye imani fulani au kabila fulani nitakuwa na mtaji mkubwa sana kisiasa bila kupima athari kwa jamii kwa njia yake ni mpumbavu ambaye tukimnyamazia tunakuwa wapumbavu sote.

wawe wana siasa, viwe vyombo vya habari, kiongozi au mtanzania yeyote iwe ni hatari kufanya propaganda zinazohatarisha jamii.
 
Aisee! mimi huwa napata shida sana linapokuja swala la dini. Waafrika hususani watanzania sidhani kama tunapaswa kuangaliana kwa misingi ya dini. Waafrika tuna matatizo yetu mengi sana kama umaskini, maradhi na ujinga. Hawa ndiyo maaadui wa kupambana nao, na sio kuanza kutoleana macho kwa misingi ya dini.

Inawezekana kweli Msigwa hakuwa sahihi lakini huyu mwandishi naona kama ameenda mbali sana. Hii inaweza kuibua hisia za kidini kati ya wakristo na waislamu. Ni hatari sana, God Bless Tanzania.
 
mwenye makosa ni mchungaji msigwa, sio gazeti hii iwe fundisho kwa wanasiasa kuangalia kauli zao hasa ktk wakati huu kuelekea uchaguzi mkuu, kila wanachosema kinarekodiwa na kuangalia kina maana gani anatakiwa mchungaji ajiangalie kwani ni vigumu kutumikia mabwana wawili hata hizi kauli za tunaanza na mungu tunamaliza na mungu bado zinaweza kuigharimu CDM.

ukiwa kwenye uwanja wa siasa ongea siasa hapo Mungu haingii siasa zenyewe hizi za kimagumashi watu wanaangalia maslahi yao Mungu ataingiaje hapo.
 
Mkuu wanakera sana! Wanatufanya tuchelewe kujadili mustakabali wa taifa letu wanatutumbukizia mambo ya kipuuzi, wanataka kutuchelewesha tujadili upuuzi wao huu wa udini!

Ni kweli Mkuu, huu upepo wa mashariki ya kati na nchi za magharibi unatuathiri sana waafrika. Sisi tuna shida zetu na kamwe hatutaweza kuzitatua kama tunaanza kuangaliana kwa misingi ya dini. Hao wanaopigana kwa maslahi ya dini huko wao walishaendelea tayari. Tupambane na maadui zetu wa tangu uhuru (Ujinga, Maradhi na umaskini).
 
gazeti limesema ukweli wa Msigwa alichoogea--sasa iweje hii iwe uchochezi.Msigwa alisema "CHADEMA ni kama Kanisa"
Kwa lugha ya kimahesabu, hii ni CHADEMA = KANISA--nani haelewi hii mpaka aulizwe Msigwa?
 
Kiujazacho moyo wa mtu ndicho kimtokacho kinywani mwake
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom