Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
Wakati mwingine wanasiasa huwa wanavigharimu sana vyama vyao pale wanapotoa kauli majukwaani bila kufikiri mara mbili, hali hii tumeshaiona mara nyingi tu katika majukwaa ya siasa za tanzania,na mbaya zaidi ni pale wanaposhindwa kujitokeza kuomba radhi au kutolea ufafanuzi kauli hizo
 
Narudia tena jamani eeeeeeh humu ndani, mukajiandikishe BVR kama mupo manzese mwenge mbagala mbezi kurasini temeke gongolamboto tabata kimara masaki oysterbay tegeta sinza ...yaaani namaanisha BONGOLAND tumia haki yako tumia fursa shauri yako huenda mwakani ukaenda kubeba maboksi na uchaguzi ujao usiwepo ...kwaherini
 
Sasa uchoche uko wapi hapo? aliyesema chadema ni kama kanisa ni Msigwa au gazeti? Maneno yamesemwa na msigwa kabisa mlitakiwa kutoa lawama kwa msigwa!
Hivi kama chadema ni kama kanisa hivi waislam wafate nini kanisani? Huu ndio ukweli ...!
Bora Msigwa kavunja ukimya kabisa kasema chadema ni kama kanisa!

Hapa ndio mtajua kuwa kuna umuhimu wa kuchunga ndimi zenu...Msigwa amezoea kuropoka bungeni sasa amekwenda kuendelea kuropoka mtaani! Hapo amebugi kabisa!

Kimsingi Msingi heading ya habari ilitakiwa kuwa Msigwa asema Chadema ni kama kanisa!

Sioni uchochezi wowote zaidi ya kuandika ukweli ulio semwa na Mnyika...hivi mlitaka waseme baada ya kauli hiyo Waislam watafurahi? Uwezi ukasema chadema ni kama kanisa halafu utegemee waislam kuja kanisani!

Msigwa anajua fika chama chake kimekuwa kikisakamwa na hili tatizo la kuwa ni chama cha kikristo sasa na yeye kaweka wazi kuwa Chadema ni kama kanisa....! Mfungeni speen gavernor ya mdomo!

" Chadema ni Kama Kanisa- Msigwa "

Mkuu acha kujiweka nyuma kiasi kikubwa hivyo! Hivi nikikwambia wewe ni msafi kama paka, utalalamika umeitwa paka?? Kwa nini usitumie hata akili yako kidogo tu! Hizi chuki unapandikiza kwa faida ya nani!? Na watu wasipokuelewa unavyojaribu kuharibu mantiki ya Msigwa utafanyaje?? Acha utoto mkuu, usikubali kukuwa mwili na nywele, ikuze pia akili yako.

C.C
Ritz.
Lizabon et al.
 
Wakati mwingine wanasiasa huwa wanavigharimu sana vyama vyao pale wanapotoa kauli majukwaani bila kufikiri mara mbili, hali hii tumeshaiona mara nyingi tu katika majukwaa ya siasa za tanzania,na mbaya zaidi ni pale wanaposhindwa kujitokeza kuomba radhi au kutolea ufafanuzi kauli hizo
Bora wewe umehamua kusema ukweli Msigwa kakosea lakini baadhi ya Bavicha wana mtetea...
 
Nakatishwa tamaa ya kuona Wapinzani wakitwaa dola ktk nchi hii.Viongozi na Makada wa chama hawako makini ktk kauli na matendo yao,wafuasi wao nao ndio kabisa lugha nzuri za kisiasa hawazielewi,ukisoma comments za baadhi ya watu hapa utabaki unajiuliza kama hawa watu wanaifahamu vizuri siasa au la.Watu wanaanza kuwalaumu Waislamu kwa yaliyoandikwa na gazeti la Al-Huda,binafsi sililaumu hilo gazeti kwasababu ndio Kazi ya kila chombo cha habari kutumika na vyama fulani vya kisiasa kama mdomo wao wa propaganda, hivyo limetimiza wajibu wake,ni juu ya wanasiasa wa vyama vya upinzani kuwa waangalifu ktk kauli zao,CCM ni wazoefu sana wa siasa za maji taka na hayo mnayoyaona ni rasha rasha tu,mvua kamili zinakuja.

CHADEMA mnapaswa kukumbuka kwamba sasa hivi tupo ktk makubaliano ya kupata wagombea wa nafaasi zote kwa tiketi ya UKAWA.Lazima tukubali kwamba kwa miaka mingi ya uchaguzi vyama vya upinzani vimeshindwa kuiondoa CCM madarakani vikiwa vinagombea kila chama kivyake.Muungano wa UKAWA ni matokeo ya vyama vya upinzani kugundua kwamba 'umoja ni nguvu' na 'utengano ni udhaifu',Ni ukweli kwamba vyama vikuu viwili vya CHADEMA na CUF ndivyo vyama vyenye wafuasi wengi zaidi na wafuasi wao wengi wanatoka kwenye dini kubwa mbili nchini za Kikristu na Kiislamu,Ukiangalia kwa jicho la tatu,lengo la kuanzishwa kwa UKAWA ni kuwaleta wafuasi wa imani hizi kubwa mbili hapa nchini pamoja kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ujao,hii baada ya kila chama kugundua kwamba uwezokano wa kuitoa CCM madarakani kwa kutegemea kura za wafuasi wa imani flani tu ni mdogo sana.

Sasa basi,ndugu zangu Wakristu mnaotoa kauli za namna hii zenye kuchochea kutokuaminiana na kubaguana hivi mnaiweka UKAWA ktk wakati mgumu sana,tukubali tu Msigwa alikosea,huo ndio uungwana.Tumsifanye Msigwa akaamini alikuwa sahihi kwa kauli yake hii,kiukweli hasa kauli yake hii inaweza kuiumiza CHADEMA kisiasa.
 
Hivi jamani mambo engine tunayakuza hivi inawezekana mwislamu anaweza akatolea mfano kanisa ataeleweka ndiyo maana Msigwa katolea sehemu anapoabudia
 
Waswahili hawaelewi wanataka nini...wapi na lini...

ndio maana CCM inawatumia itakavyo na hawana ujasiri wa kuiadhibu.....

uko sahihi sana mkuu. na huu ujuwaji wetu usiokuwa na maana ndio unaotumika na CCM kama mtaji wa kuendelea kuwanyonya watanzania. after all hizi dini zipo kwa ajili ya kutusaidia tuishi vizuri na kwa amani lakini nashangaa kuna watu haswa wanasiasa wanazitumia vibaya kuwadhulumu wengine. wenye dini zao (wanaojua machimbuko ya dini hizi ) wapo wanatuangalia na kutucheka tu kwa namna ambayo wamefanikiwa kutugawa kidini ili watutawale na kutuibia rasilimali zetu vizuri. huu ni ukichaa ambao kama hautapata tiba muafaka tutajikuta ni soko la silaha za viwanda vya wenzetu waliotuletea dini hizi .
 
Mkuu acha kujiweka nyuma kiasi kikubwa hivyo! Hivi nikikwambia wewe ni msafi kama paka, utalalamika umeitwa paka?? Kwa nini usitumie hata akili yako kidogo tu! Hizi chuki unapandikiza kwa faida ya nani!? Na watu wasipokuelewa unavyojaribu kuharibu mantiki ya Msigwa utafanyaje?? Acha utoto mkuu, usikubali kukuwa mwili na nywele, ikuze pia akili yako.

C.C
Ritz.
Lizabon et al.
Hivi wewe Bavicha kati ya Mimi na msigwa nani amesema haya? "Chadema ni kama kanisa tuna hubiri wokovu "

Hivi una hitaji kuwa na degree kujua Msigwa amekosea? Hivi kwanini mnapenda kuabudu watu? ina maana huoni kosa la Msigwa?
 
...
Kasema kweli Chadema ni kama Kanisa...

Kunatofauti kubwa ya maana ya sentensi hizi mbili:
1.Chadema ni kama Kanisa
2.Chadema ni Kanisa

Hata hivyo, nakubaliana na The Boss, Mch. Msigwa 'alikosea'.
 
Kunatofauti kubwa ya maana ya sentensi hizi mbili:
1.Chadema ni kama Kanisa
2.Chadema ni Kanisa

Hata hivyo, nakubaliana na The Boss, Mch. Msigwa 'alikosea'.
"Chadema ni kama kanisa tuna hubiri wokovu "

Chama cha siasa kama Chedema hizo ndiyo kazi zake?
 
Siku zote waislamu mnapenda kuishi pekeyenu japo siwote wenye mtazamo huo. Lakini majority wanatamani hivo. Jambo ambalo kwa nchi kama Tanzania ningumu na hitakuja tokea. Wakrsto wanawapenda sana nduguzao waislamu japo waislamu hasa wenye misimamo yakijinga heti swalatano hawapendi hata kulitamka jina la John. Upendo wa wakristo ndo unawafanya waishi kwa amani popote walipo. Take that can help you.
 
Hivi kwa nini waislam ni watu wa kulalamika sana na kuchokonoa chokonoa watu kwa hisia za kidini?Get some life for God's sake
 
Gazeti la alhuda linamilikiwa na BAKWATA ya CCM. kwa hiyo lazima wafanye uchochezi kwa manufaa ya maCCM.

CC: FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
"Chadema ni kama kanisa tuna hubiri wokovu "

Chama cha siasa kama Chedema hizo ndiyo kazi zake?
ndo matokeo haya ya akili kiduchu zitokanazo na elimu isiyo sahihi ya shule za kata za ccm.

ni heri mtu ambaye hajasoma kabisa kuliko mtu aliyesoma nusu nusu. mtu aliyesoma nusu nusu huwa anaishia kuwa jinga kubwa kabisa kuliko yule ambaye hakuliona kabisa darsa
 
Mkuu kauli ya Mchangaji Msigwa kufananisha Chadema kama Kanisa wewe huwezi kuiona kama tatizo sababu wewe ni mkirsto. Chadema ni chama cha siasa kuna watu wa dini tofuati tofuati unadhani watu wataelewa vipi kauli hii ya Mchangaji? ?


Unafikiri huo uchafu wa alihudaa unatupunguzia nini??

Mkae au msimame ukristo utawatawala milele hamna namna mnaweza kuukwepa!!!
 
Nyie viumbe wa ajabu sana uchochezi gani gazeti limefanya? Mbona karibia magazeti yote yaliandika hii habari.

Labda nikuulize wewe kweli au siyo kweli Mchungaji Mnyika akusema Chadema ni kama Kanisa?

Tuonyeshe uchochozi wa hilo gazeti.
Uchochezi ni hapo alipoongeza waislam kuwa mashakani. Hapo ndiyo kosa la mwandishi lilipo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom