Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
kwann watu wa ccm wanapenda kuja na hoja dhaifu,hata kama ni kanisa mbona huduma za jamii zinazo simamiwa na kanisa mnazitumia kama hosptal na shule? Lakini ccm ikifika wakati huu wa kusaka madaraka wanaanza kuwafitinisha wakristo na waislam
 
Haya mambo ya kuamuliwa vitu na "VITENGO" ama "MAJUKWAA" wakati mtu unayo "WILL OF CHOICE" ni upuuzi. Mimi sikwenda shule miaka yote hiyo halafu watu wachache waje kunipangia cha kuamua, never! Hakuna cha kitengo, jukwaa, tamko wala propaganda ya kuniambia mpigie kura huyu na mwache yule, nitaamua mwenyewe.

Kwani nilipokaa kwenye BVR masaa 12 mlinisaidia? Ndugu zangu waislamu na wakristo naomba tusiwe drawn kwenye mtego mdogo kiasi hichi wa kuturudisha nyuma ktk mabadiliko. Tunajua mwaka 2010, watu walifuata matamko ya majukwaa/vitengo na sasa hivi wanajutia uamuzi ule. Mwaka huu amua mwenyewe kwa utashi wako, na sio kuamuliwa na watu makajanja na
 
Kama kanisa linabadilisha watu kutoka kuwa waovu kuwa wema, kama vile shule inavyokusudiwa kubadilisha watu kutoka ujinga kuwa na maarifa, kuna ubaya gani Msigwa kutumia mifano hiyo iliyo dhahiri?

Wewe kwako kanisa ni chukizo?

Unataka aseme shetani ndiye anafanya wtu kuwa wema?

Kweli u.p.umbavu ni utumwa kama ilivyo dhambi.

Sasa amesema na Watanzania tumemwelewa. Wewe na bichwa loko lililojaa ushen.zy wa kishetani ndiye unajua unachokitafuta. Na umpu.m.b.avu wako utakuua, utake utistake.

it's called political correctness my friend, if you want to be a good politician then you have to play by its rules.
 
Hili gazeti la kufungia maandazi serikali inatakiwa kulifungia mara moja

Thubutuuu! Huenda Serikali na CCM wanahitaji kuwatumia tena kueneza propaganda zao kufanikisha ushindi wa kishindo unaotokana na goli la mkono, ndiyo sababu Mamlaka husika haiwezi kuchukua hatua japo kuwapa onyo tu kwakuwa huenda ni wao(CCM) ndiyo wanawatuma kama ilivyofanyika kule Igunga dhidi ya hijab ya kufoji ya Fatma Kimario!
 
Haya mambo ya kuamuliwa vitu na "VITENGO" ama "MAJUKWAA" wakati mtu unayo "WILL OF CHOICE" ni upuuzi. Mimi sikwenda shule miaka yote hiyo halafu watu wachache waje kunipangia cha kuamua, never! Hakuna cha kitengo, jukwaa, tamko wala propaganda ya kuniambia mpigie kura huyu na mwache yule, nitaamua mwenyewe.

Kwani nilipokaa kwenye BVR masaa 12 mlinisaidia? Ndugu zangu waislamu na wakristo naomba tusiwe drawn kwenye mtego mdogo kiasi hichi wa kuturudisha nyuma ktk mabadiliko. Tunajua mwaka 2010, watu walifuata matamko ya majukwaa/vitengo na sasa hivi wanajutia uamuzi ule. Mwaka huu amua mwenyewe kwa utashi wako, na sio kuamuliwa na watu makanjanja na wewe ukafuata tu km upepo.

Nakumbuka mwaka 2004, kuelekea uchaguzi wa 2005 nikiwa kijana mdogo wa sekondari, alikuja Mh. Ndesamburo wilyani kwetu. Nilipokuwa namsikiliza, nilivutiwa sn na sera zao & niliapa tangu mwaka huo siku nikianza kupiga kura nitapigia CDM. Ndivyo nilivyofanya 2005 & 2010.

NITAAMUA mwenyewe, si Kitengo,wala jukwaa, wala tamko, wala kanisa, wala msikiti watanitenga na CDM. I have the "Will & Power" to Choose.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Chadema.
 
hivi jamani ninyi mnaohangaika na hawa waislam uchwara, wa hako kagazeti, kuwafafanulia maana halisi ya kauli ya Msigwa, hivi kweli mnafikiri wao hawaielewi hiyo kauli??!! Hawa waislam uchwara wanaielewa vizuri sana kauli ya Msigwa lakini kinachofanyika hapo ni uzandiki wa kutumia hii midini ya kikoloni kuchonganisha waafrika. Kwa Mwislam kutoa tafsiri ya jinsi hii kwa waislam wenzake ni muendelezo ule ule wa kudharauliana kati ya waislam wenyewe, mintarafu maneno ya mwalimu Nyerere kuwa "Mtu akikudanganya, na yeye anajua kuwa unatambua kuwa anakudanganya, na wewe ukamkubalia, Anakudharau". Hapa hamna cha sana zaidi tu ya waislam wa hako kagazeti kuwadharau waislam wenzao. Badala ya kuwahimiza waislam wenzao wakazanie ilmu dunia kwa kwenda shule wao wanacapitalize kwenye ujinga wa waislam walio wengi kwa faida ya ccm iliyowadidimiza waislam hao kwa miaka nenda miaka rudi. Ni ujinga ulioje huu??!! Nakumbuka Nyerere alitumia maneno ambayo, baadaye, hawa wasomi uchwara, na wapumbavu, wakataka kuyapa hayo maneno mujarab ya Nyerere tafsir hizi hizi za kishenzi; mwalimu alitumia maneno kwamba "I cant let my country go to the dogs": tafsri ya moja kwa moja hapo (direct translation kama inayofanywa na haka kagazeti uchwara) itakuwa mwalimu alimaanisha "siwezi kukaa kimya niache nchi yangu itawaliwe na ma mbwa". Basi wasomi uchwara, na bila shaka walikuwepo hawa wa haka kagazeti, wakashadidia eti Nyerere kawatukana watanzania wasio wanaccm kuwa ni ma mbwa!!!!!

Ndiyo maana mimi huamini kuwa ni kweli kabisa watu wanaposema kuwa ccm imedumaza kabisa elimu ya nchi hii, kwa walio wengi, ili idumishe ujinga wa walio wengi kwa minajili ya kuiwezesha kuwapumbaza na hatimaye kutawala milele isivyo halali. Watanzania wengi, hasa waislam, wanaangamia si kwa kupenda bali kwa kukosa maarifa walionyimwa, na wanayoendelea kunyimwa, kwa miaka mingi, na serikal ya ccm. Ubaya zaidi ni pale waislam wenzao walioona mwanga kidogo wa ilmu, badala ya kuwatoa wenzao kwenye hayo maangamizi ya ccm, kwa kuwapa ilmu na kuwakazania waende shule, wao ndo kwaaaaaaaanza wanawasokomezea kabisa wenzao kwenye shimo la umauti wa ccm.

Na hili si jambo la kushangaza wala la bahkati mbaya. Dini hizi za kuja(dini za kikoloni) zimetumika sana kuchochea chuki, mapigano, vita na dhulma dhidi ya jamii mbalimbali duniani. Maisha mengi sana yameangamizwa kwa kuchochewa na dini hizi ambazo zilianzishwa huko mashariki ya kati na kuenezwa maeneo mengine duniani. wachochezi wa dini hizi za kuja, huku wakijifanya waaumini wa Mungu, wanajificha nyuma ya dini hizi wakijifanya kuubiri wema wa Mungu huku nia yao hasa ni kuubiri uzandiki, fitna na chuki wakiwa na kiu ya kuona mifarakano na kuchinjana kati ya ndugu na ndugu. Huwa napata shida sana napomuona mswahili wa kinyerezi anajinasibu sana na mwarabu, kajitwika vilemba na kanzu, kifimbo mkononi na kijastibikozi chake basi anajiona eti yeye naye ni mwaaaaaaarabu kweli kweli na anafikia hata hatua ya kuwadharau waafrika wenzie, ambao kihakika kabisa ni damu yake ya karibu kuliko hao waarabu. Ni ajabu kuwa Waafrika wanapendana zaidi kwa kujiita ndugu katika imani (za kuja/kuletewa) kuliko wanavopendana kwa kujiita ndugu wa/katika damu!!!!

Dini inapofikia kiwango cha kutumika kueneza ubaya na uovu kwa kiwango hiki, tena uovu dhidi ya ndugu wa damu moja, basi dini hiyo inapoteza kabisa u maana wake na inabakia kuwa ushenzi tu sawa na uchawi na ushirikina.

Ni wajibu wa waislam wanaoijua vizuri dini yao kukataa dini yao kugeuzwa ushenzi kama wafanyavyo waandishi kama hawa wa gazeti hili la Al-Huda. Ni wajbu wa waislam waliobahatika kupata ilmu dunia kuhangaika kuona kuwa, jamii yao ya kiislam, ambao wengi wao hawajabahatika kupata ilmu kama wao, nayo inapata ilmu kwa kuweka miundombinu na kuwahimiza waislam kuitafuta ilmu. Mtume (saw) amesema “itafuteni elimu ijapokua iko ktk miji ya china, kwani kutafuta ilimu ni wajibu wa kila islamu” (Ibnu Abdul-Bar). Mtume (saw) akaongeza “sadaka iliyo bora ni islamu kujifunza ilimu, kisha akamfunza mwenzie”......sasa cha ajabu hawa kina ritz, aL-hUDA, faiza foxy na wenzao wengine wa kaliba yao, badala ya kuwafunza waislam wenzao ilmu wao wanawajaza ujinga na upumbavu mtupu, nia ikiwa ni kuisaidia ccm iendelee kuwatawala, kuwanyonya na kuwakandamiza waislam, na jamii nyingine za watanzania, daima.

Mwalimu alionya - Nanukuu;

“Wale wenye bahati ya kupata elimu, wanao wajibu wa kulipa jasho ambalo wengine wamejitolea. Ni sawa na mtu aliyepewa chakula chote katika kijiji chenye njaa, ili apate nguvu za kwenda kuhemea katika sehemu zilizo mbali. Mtu huyu akipokea chakula hicho na halafu asiwaletee ndugu zake, basi yeye ni msaliti…”.

Hapa, Mwalimu alikuwa akiwakumbusha vijana wasomi, tena wa dini zote wakiwemo waislam, wanaopata elimu kwa jasho la Watanzania kutumia elimu yao kwa maendeleo ya wananchi badala ya maendeleo binafsi, au kwa manufaa ya kikundi (chao) cha kitabaka nchini. Kufanya hivyo ni usaliti kwa umma. Waandishi uchwara wa kagazeti ka Al Huda wanausaliti na kuudhalilisha umma wa Kiislam, wanawadhihaki na kuwang'ong'a kuwa hawana ilmu kwa kuwapa tafsir za kidhalilishaji, kijinga na kipumbavu kesha wanakaa pembeni wakiwacheka kwa jino pembe, wakiwaangalia waislam wenzao wakivurugana kwenye tope la ujinga, huku wenzao wasio waislamu, na ni wakristo to be precise, wakichanja mbuga kujiwekea miundo mbinu ya ilmu kila kona, kukwea vidato na vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi. Matokeo ya muda mrefu ya haya ni waislam kuzidi kuachwa nyuma kielimu na kimaendeleo na mwishoni kuishia malalamishi yasiyoisha

Waislam wema kote nchini tunawakumbusha tena na tena, na ni kwa nia njema tu na kama hutaki unaacha....shtukeni sasa dhidi ya huu upumbavu mnaojazwa, Vuteni shuka sasa kabla hakujacha kabisa, la msivute shuka milele.

nafikiri nawewe ndio walewale. kama yeye ni mchungaji kwanini awe mwanasiasa? hii ndio sababu anaongea mambo yanayo leta utata. hata biblia inasema yakaisali mwachie kaisali. yeye achane na siasa ahubiri injiri. unataka niambia chadema hakuna mkosefu au mwenye dhambi? yy amesema ukiingia chadema unaombewa unakuwa msafi maana yake chadema hakuna rushwa uonevu wala ukiukwaji wa katiba. kama anaona siasa inalipa achane na uchungaji kama slaa
 
Haya mambo ya kuamuliwa vitu na "VITENGO" ama "MAJUKWAA" wakati mtu unayo "WILL OF CHOICE" ni upuuzi. Mimi sikwenda shule miaka yote hiyo halafu watu wachache waje kunipangia cha kuamua, never! Hakuna cha kitengo, jukwaa, tamko wala propaganda ya kuniambia mpigie kura huyu na mwache yule, nitaamua mwenyewe.

Kwani nilipokaa kwenye BVR masaa 12 mlinisaidia? Ndugu zangu waislamu na wakristo naomba tusiwe drawn kwenye mtego mdogo kiasi hichi wa kuturudisha nyuma ktk mabadiliko. Tunajua mwaka 2010, watu walifuata matamko ya majukwaa/vitengo na sasa hivi wanajutia uamuzi ule. Mwaka huu amua mwenyewe kwa utashi wako, na sio kuamuliwa na watu makajanja na

That means we have share our views here! Thanks bro - John Peter M
 
Mkuu kama wewe ni "msomi" nitashangaa sana. Huwa sielewi hili neno la kukwepesha maada.

Niwe msomi nisiwe msomi siyo ishu. Tunajadili kauli ya Msigwa na jinsi ilivyotafsriwa na hili gazeti la Kiislamu we unaleta kauli za J.K tena zisizohusiana na ishu ya udini inayolalamikiwa na wadau hapa. Kauli za J K si ukazianzishie thread yake huko?

Kama tabia hii ya kubambika mambo mahali pasipostahili ndo usomi basi potelea mbali kaa huko na usomi wako. Tena mimi darasa la saba nifikishie salamu zangu kwa msomi mwenzio Mh. Mulugo!
 
Credible Viewer

Wewe ndio mchochez,kwani ulijuaje kama Msigwa hakukusudia unacho kikataa wewe? Al huda "wame quote" direct kutoka kwa source,je wewe hio hoja yko kuwa Msigwa hajakusudia "uchochez" ume qoute kwa nani?

Msigwa amekanusha kauli yake au wewe ndo msemaji wake? Hio falsafa kwanini aitumie ya "symbol" ya kanisa?wakat tayar kuna vugu vugu la udini na mivutano ya kidin isio kwisha?

Tena tuhuma nyengine zinaelekezwa hko hko chadema?Kwani Msigwa hakuona falsafa nyengine ya kusema?

Mfano,kwanini msigwa asiseme "Chadema ni kama maji ya kunywa,kila mtu atayahitaji" n.k,Falsafa ya udini haikubaliki hata kama yeye ni mchungaji?

Msigwa ndio mchochozi pamoja na wewe.Al huda ni wasafi,wao wamefanya direct quote from the source.

Njia ni moja,mafikio tofauti.

Kama gazeti limefanya direct quote, je Msingwa alisema ""*Wanachama waislamu sasa watakuwa mashakani"*????
 
Sasa uchoche uko wapi hapo? aliyesema chadema ni kama kanisa ni Msigwa au gazeti? Maneno yamesemwa na msigwa kabisa mlitakiwa kutoa lawama kwa msigwa!
Hivi kama chadema ni kama kanisa hivi waislam wafate nini kanisani? Huu ndio ukweli ...!
Bora Msigwa kavunja ukimya kabisa kasema chadema ni kama kanisa!

Hapa ndio mtajua kuwa kuna umuhimu wa kuchunga ndimi zenu...Msigwa amezoea kuropoka bungeni sasa amekwenda kuendelea kuropoka mtaani! Hapo amebugi kabisa!

Kimsingi Msingi heading ya habari ilitakiwa kuwa Msigwa asema Chadema ni kama kanisa!

Sioni uchochezi wowote zaidi ya kuandika ukweli ulio semwa na Mnyika...hivi mlitaka waseme baada ya kauli hiyo Waislam watafurahi? Uwezi ukasema chadema ni kama kanisa halafu utegemee waislam kuja kanisani!

Msigwa anajua fika chama chake kimekuwa kikisakamwa na hili tatizo la kuwa ni chama cha kikristo sasa na yeye kaweka wazi kuwa Chadema ni kama kanisa....! Mfungeni speen gavernor ya mdomo!

" Chadema ni Kama Kanisa- Msigwa "
 
Thread kama hii zinapata wachangiaji wengi kuliko ukiweka mambo ya uchumi wa taifa!
 
Msigwa yeye ni mchungaji
na anajua tuhuma zipo za CHADEMA kuwa chama cha wakristo
hata kama hizo tuhuma si za kweli na za kutunga
hakupaswa kuwa reckless na kuanza kuita CHADEMA kanisa

Mifano ipo mingi ya kufikisha ujumbe

Kutumia mifano ya aina hiyo ni ama uzembe au kiburi na kutokujali kina nani hawatapendezwa

Msigwa ni mkristo, ningeshangaa sana angetoa mfano wa Chadema ni kama msikiti. Ni sawa na muislamu kutoa mfano wa chadema ni sawa na msikiti. Tatizo kubwa la watu wengi huwa wanafiki sana kwenye imani zao, Msigwa yupo sahihi kabisa kwasababu katolea mfano wa kitu anachokijua na kukiamini. ni sawa na leo litoke gazeti la kikristo liseme wakristo kula nyama iliyochinjwa na muislamu ni kuudhalilisha Ukristo,kitu ambacho si kweli kuwa Ukristo unadhalilika. Kwahiyo hilo gazeti la Al huda ndiyo linafanya uchochezi kwasababu mtu aliyetamka hivyo ni wa imani ambayo yeye anaifahamu na ndiyo maana kaltolea mfano huo. Hata viongozi wetu ambao ni wakristo wanaoalikwa kwenye hafla ya Kiislamu halafu wanavaa kanzu ,ule ndiyo unafiki. Wanavaa kanzu huku wanafuga nguruwe,ule sasa ni kuudhalilisha uislamu. kwanini wasiende kama wanavyoenda kwa imani yao, kwasababu ule ni mwaliko tu.
 
kwa mwanafunzi kuijua lugha, ikiwemo jinsi sahihi ya kuitafsiri, kama chombo muhimu, na sahihi, cha mawasiliano, ya kuandika na kuongea, ni moja ya silaha muhimu sana ya mwanafunzi kuyaelewa na kuyafaulu masomo mengine anayofundishwa. sasa kama tafsri za lugha wanazopeana wenzetu waislam ndo hizi, na ni wazi tafsiri za namna hii hutolewa sana humo misikitini, unategemea ufaulu wa aina gani kwa wanafunzi na shule za kiislam???

kesho na kesho kutwa shule za kikristo, na wanafunzi wa kikristo, zikipaa kwa ufaulu wakati shule za kiiislam, na wanafunzi wa kiislam, zikitaga mayai utaskia vizingizio vingi tu...oooh necta inatuhujumu waislam, mara ooo MoU, mara ooooo hiki mara oooo kile.

watu mnajazana uharo na mavi vichwani mnategemea mavuno yatoke wapi?!! mtavuna hayo hayo mnayojazana.
 
Mkuu naona leo umeibamba mada barabara, utajimwaga kwa uwezo wako wote!
Kabamba mimi au kabamba Mchugaji Msigwa kufananisha Kanisa na Chadema gazeti kuhoji mnaishia kuwatuna Waislam.
 
Nyie viumbe wa ajabu sana uchochezi gani gazeti limefanya? Mbona karibia magazeti yote yaliandika hii habari.

Labda nikuulize wewe kweli au siyo kweli Mchungaji Mnyika akusema Chadema ni kama Kanisa?

Tuonyeshe uchochozi wa hilo gazeti.

"Lowasa ni kama Mohammed"
Tueleze hapo shekhe alimaanisha mini?

Mbona magazeti hayakunukuu habari na kusema "wakristo sasa mashakani lowassa akiteuliwa"?
Ni kwamba waandishi ni wanataaluma na walielewa lipi lilikuwa lengo,sasa Leo imekuwa habari kwasababu ni mfano toka upinzani
 
Ndo gazeti la dini gani na mbona lina jina la ajabu hivyo? yanauzwa wapi na waaandishi wao elimu zao zipoje?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom