Credible Viewer
JF-Expert Member
- May 22, 2015
- 444
- 118
Nimefadhaishwa sana na gazeti la Al-Huda litokalo kila wiki toleo na.523 SHAWWAL1436 la tar23-29, Julai 2015 Uk wa mbele limepambwa na maneno.
Msigwa: CHADEMA kama kanisa
*Asema wanahubiri habari ya wokovu
*Wanachama waislamu sasa mashakani
Kimsingi kauli hizo ni za kichochezi dhidi ya waislam na wakristo! Ifahamike kuwa Mchungaji Msigwa(Mbunge wa Iringa) alitoa kauli hiyo kifalsafa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema! Msigwa alisema "...CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, unatubu unafanya kazi!"
Mimi siyo msemaji wa Msigwa, lakini nimekerwa na gazeti hilo kwa sababu kauli ya Msigwa haikulenga kutugawa Wanachama wa CHADEMA kwa misingi ya kidini! Ni kama kauli ya Tundu Lissu alipotamka kuwa "...John Pombe Magufuli na kabila lake la MaCCM..." hakulenga kuwa kuna kabila la MaCCM!
Kwahiyo siyo kweli kuwa Msigwa alimaanisha CHADEMA ina wafuasi wa Kikristo pekee!
Naomba mamlaka husika iingilie kati! Mungu Ibariki Tanzania!
Msigwa: CHADEMA kama kanisa
*Asema wanahubiri habari ya wokovu
*Wanachama waislamu sasa mashakani
Kimsingi kauli hizo ni za kichochezi dhidi ya waislam na wakristo! Ifahamike kuwa Mchungaji Msigwa(Mbunge wa Iringa) alitoa kauli hiyo kifalsafa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema! Msigwa alisema "...CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, unatubu unafanya kazi!"
Mimi siyo msemaji wa Msigwa, lakini nimekerwa na gazeti hilo kwa sababu kauli ya Msigwa haikulenga kutugawa Wanachama wa CHADEMA kwa misingi ya kidini! Ni kama kauli ya Tundu Lissu alipotamka kuwa "...John Pombe Magufuli na kabila lake la MaCCM..." hakulenga kuwa kuna kabila la MaCCM!
Kwahiyo siyo kweli kuwa Msigwa alimaanisha CHADEMA ina wafuasi wa Kikristo pekee!
Naomba mamlaka husika iingilie kati! Mungu Ibariki Tanzania!