Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,840
hivi ungetajwa msikiti,kungekuwa na mada hii saa hizi hapa?why kanisa mkuu?njia ya kuwakata ngebe si kushauri watu waache kutaja mifano ya kanisa,bali waichukulie mifano hiyo katika usahihi wake sawa tu na kama ungetajwa msikiti.Likitajwa kanisa au msikiti halafu minung'uno ikaanza kama hivi,hatuko salama.Ni lazima kanisa na misikiti itajwe na watu wawe na amani bila kustuka.Ndio uhuru wenyewe.Msigwa ni mtanzania huru.Ila baadhi ya watz waliomsikia hawako huru,ndio maana manung'uniko.Tuwaweke huru,siku nyingine wakisikia kanisa waendelee na kazi zao bila shida.
Tupo kwenye uchaguzi na maadam hii kauli imekuwa divisive ni lazima tuwe kwenye crisis containment mode mkuu. Haya mengine jamii itaelimishwa baadaye. Sioni sense of urgency kwenye hoja yako utafikiri kuwa uchaguzi uko mwaka kesho. HAIJALISHI kama Msigwa ni Mtanzania huru ama la. HAIJALISHI kama ungetajwa msikiti kungetokea nini. HAIJALISHI kama Msigwa alimaanisha tamathali ama la. Hayo yatafafanuliwa baadaye polepole na jamii kuelimishwa. Kwa vile kauli hiyo imetafsriwa negatively Msigwa atoe ufafanuzi tu alichomaanisha. Is this difficult to do? Kwa mwanasiasa aliye makini na anayejali?
CHADEMA wanashtumiwa kuwa ni chama cha Wachagga, mara cha kibaguzi, mara SACCOS na sasa ni kanisa. Unaweza kudharau tuhuma hizi lakini in politics you don't take anything for granted mkuu hasa kwenye jamii yetu ambayo wapiga kura wetu wengi hasa huko vijijini wanaweza kuyumbishwa kirahisi sana na wapotoshaji hawa waliofilisika kisera.