Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,915
- 30,259
- Thread starter
- #281
Chief...Fuma...
Mimi nisiyejua chochote nazungumza na mjuzi lakini huyu mjuzi anashindwa kutambua ukweli kuwa yapo malalamiko ya kweli.
Halafu time factor ni muhimu sana, jambo hili lilitokea lini na "mtuhumiwa" alifanya hayo akiwa kama nani, Mwenyekiti UWT au nani? Hapa time factor ni muhimu sana ili tuendane sawasawa na matukio yote na shutuma pia. Mwandishi au mleta uzi aeleze tu bila jazba kuhusu maswali yetu; kwa nia njema tu ya kuelimishana.
Kisa ni kirefu lakini nitakueleza kwa mukhtasari.
Uongozi wa Chuo ulitoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa msikiti na kanisa.
Waislam walitangulia katika kutaka kuanza ujenzi wa msikiti baada ya kupata vibali vyote.
Wakati shughuli inataka kuanza Mama Kabaka akawaambia Waislam kuwa hatambui vibali hivyo.
Askari wakaitwa kudhibiti eneo na mabanda yaliyokuwa yamejengwa yakavunjwa na hapo hapo Waislam 11 wakaondolewa UDOM.