Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,921
- 30,266
- Thread starter
- #481
Mr...unataka kusema masheikh walihusishwa na uasi uliofanywa na Tanganyika rifles?
bado kuna vitu nahisi havijakaa sawa either hii haikuwa kweli au kuna story zaidi nyuma ya pazia, kwanini Mwalimu auchukie uislamu hivyo bila sababu za msingi!?
Taarifa zilizokuwa zimeenea ni kuwa kulikuwa na njama ya kupindua serikali na kumuua rais.
Hili lilimhangaisha sana baba yangu ikabidi amuulize Kheri Rashid Baghdelleh ukweli wa uvumi huu.
Baghdelleh alikuwa serikalini na rafiki ya baba yangu toka utoto wao na akimjua vyema babu yangu.
Baghdelleh alimwambia baba yangu viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamewekwa kizuizini kwa kuwa serikali inataka kuvunja vyama vyote vya wafanyakazi na kuunda chama kimoja chini ya TANU.
Hili likikamilika babu yangu na wenzake katika trade unions wataachiwa.
Kweli baada ya NUTA kuundwa wakaachiwa.
Walioshitakiwa kwa uhaini ni wanajeshi peke yao.
Ama kuhusu Uislam historia ndiyo kama hii tuliyonayo hivi sasa.
Historia ambayo mimi mimeusahihisha.
Nimetafiti na kuandika vitabu na paper kadhaa kuhusu Uislam na Siasa Tanzania ambazo nimeziwasilishwa kwenye vyuo vingi - University of Dar Salaam, Mzumbe University, University of Johannesburg, University of Ibadan, Kenyatta University, Zanzibar State University, University of Iowa, Northwestern University Marekani, Zentrum Moderner Orient, Ujerumani
na kwengineko.