Jamani kuna rafiki yangu alichukua mkopo wa gari aina ya NOAH kutoka bank ya CRDB na aliweka nyumba yake kama dhamana, lakini kwa bahati mbaya gari lenyewe limeibiwa jana maeneo ya Kongowe na mbaya zaidi gari lenyewe lina muda wa miezi miwili tu tangu aanze kulitumia.
Yaani mshikaji kadata balaa hajui afanye nini? na bank kama kawaida wanataka chao tu. Wakuu tusaidiane kumshauri huyu mwenzetu.
Kwanza nataka kujua alikopa Noah kwa ajili ya biashara au kutanulia? Kwa vyovyote imeshakwenda, basi na nyumba hawezi kuuza manake ipo kama dhamana, hivyo akope tena kwa rafiki arudishe Noah ya watu kama anataka kusevu nyumba.
Asiumize kichwa kumkopa mtu mmoja milioni 10 ni vigumu, anapaswa kukopa watu hata 10 kila mmoja M1 au 2 na arudishe hela hizo polepole ndani ya miaka 2 hivi matatizo yatakuwa yamekwisha.
Akope hasa kwa marafiki wa kweli au kwa ndugu wajomba, shangazi, n.k. hawa hawa watamwonea aibu kuchukua nyumba yake.
Ningemkopesha lakini lazima aweke nyumba yake mikononi mwangu na nyumba hiyo tayari benki imeshaiweka kibindoni.