Mapenzi ni hiari, kama una mke mzinzi na huwezi vumilia mwache.
Kumbuka, katika sheria si kila halali ni haki. Hao walioua magoni wao na kuachiwa inawezekama walitumia kipnegele cha 'temporal Insanity', lakini je kuua mtu sababu ya K moja tu ni haki?
Malengo ya taasisi yeyote kama ni kutetea haki ya binadamu, basi ina wajibu wa kutetea haki ya binadamu huyo endapo itapokonywa hata kama ana tabia ya aina yeyote.
Kwa hiyo sababu tu mwanamke ni mzinzi apigwe hata akifa poa? Kisa? To feed men's ego?Absurdity of Weak Men!
Kongosho dada yangu, umesema vema hapa juu ya uwezekano wa amri ya mahakama, nanukuu,'temporal Insanity', hivyo kama nilivyosema kitendo cha mtu mzima tena ndani ya ndoa kumpiga mwenzake huwa sio planned hata kidogo, wengi wametenda hilo la kupiga, lakini inapofika jioni wanakuwa pamoja na mapenzi wanapeana na kuombana msamaha. Kumbe basi kuita kwamba ni mens Weak, hiyo hakika ni utetezi dhaifu sana.
Unasema huoni sababu eti kisa ni K tu, dada yangu, wewe mara zote japo sikufahamu, lakini kwa kukusoma tu natambua ya kuwa sio mtoto, hivyo basi katika mwili wa binadamu katika viungo mhimu na hatari pia ni viungo vya uzazi. Tukiwa kwa mfano DSM kwenye public transport (daladala, ndio usafiri wangu) huwa tunasukumana na kugusana almost sehemu zote za miili yetu, na katika hilo no body care, lakini linapokuja swala la kugusanisha vikojoleo tena mbaya zaidi aidha na mke wa mtu ama mume wa mtu, hilo halikubaliki hata kidogo.
Najua tunatofautiana sana, kimalezi, kimtazamo nk, katika kusema kwangu unaweza kusema hii ni ile mnaita mfumo dume, lakini mimi ninachokisema ndicho kilichopo moyoni mwangu.
Nakutakia weekend njema dada Kongosho
Last edited by a moderator: