Mzee wa Vyombo
Member
- Sep 26, 2013
- 25
- 7
kongosho mia/mia..naamini hivyo pia...
Mwanamme anayepiga mkewe kwa sababu yeyote ni 'WEAK', period!
sikubali kipigo na sitaruhusu kufumaniwa wala kufumania
Una uhakika unaweza kuzuia kipigo kutoka kwa mwanaume mwenye hasira za kijinga kama hizi?Mie hata nifumaniwe, kipigo Nope!i
Namuunga mkono huyo jamaa kwa namna alivyoliona kosa
Lakini hakustahili kumpiga mkewe!
Ndg yangu Kongosho, kwani hao TGNP na TAMWA walimutuma huyo dada akafanye uzinzi asb yote hii. Mbona mnazibambikia hizi taasisi majukumu mengine ambayo yako nje ama mbali na majukumu yao. Siiungi mkono sana mwanandoa yeyote kumpiga mwenzake lakini lipokuja swala mahususi kama hilo lolote linaweza kutokea ikiwemo kupigwa na hata kufikia kupoteza maisha/uhai wa mhusika.
Wapo watu waliwaua wagoni wao, kisheria ni kosa kujichukulia sheria mkononi, lakini mahakama ziliwaachia huru kutokana na aina ya tukio lilivyotokea na huyo mhusika alivyorespond kwalo, hebu mara nyingi tujaribu kuuvaa uhusika, imagine kama ungekuwa wewe ungefanya nini.
Eti TGNP, TAMWA, nk, kumbe basi watu wanaweza kuamua kufanya upuuzi ndani ya ndoa zao kwa kujua ama kutambua kuwa hizo taasisi zipo kwa ajili ya yao na kutetea upuuzi wao. Nitazishangaa hizo taasisi za namna hiyo ambazo zitaacha mambo ya msingi kama ya mirathi ya wajane, utumikishwaji wa watoto wadogo nk, na kwenda kushughulikia mambo ya kujitakia kama hayo.
Una uhakika unaweza kuzuia kipigo kutoka kwa mwanaume mwenye hasira za kijinga kama hizi?
Huyo si mkewe tena kumbuka...
Kweli hii mbaya kabisa na imevuruga sana hekima ya mwanzo!niliona ni sawa....ila kumpiga hapana......
Sasa kuna haja gani ya kumpiga kwa kumfumania mtu na unamwacha? Kwa nini asimwache tu?
Ego?
Uzinzi ni A, kuchukua sheria mkononi ni B
Havichangamani! Kama ameumia sana, angempa talaka tu maana hata kisheria inaruhusiwa kumwacha kwa kuwa na mahusiano nje ya ndoa.
Mwanamme anayepiga mkewe kwa sababu yeyote ni 'WEAK', period!
Duh! Anaukika kama jamaa alikua hatambui huyo ke ni Mke wa watu?
Adabu na fundisho zuri lingepatikana kwa kuwahukumu wote!!
Sijui, but ikitokea nitajua la kufanya hapo hapo.
TGNP na TAMWA ndio walimtolea mahari huyo bwana?...acha mtu apewe mkong'oto kidogo maana hakuna taasisi inayoshughulikia mafumanizi
Kupiga ni kutoa adhabu...wala sio ego.
Sawa!!!!kutoa talaka nayo ni adhabu...
Wasiache kwakuwa kuna kupigwa......Hapa kitu cha muhimu ni kwa wanaume na wanawake waliopo kwenye ndoa waache zinaa basi..
Inawezekana!!!!!!!!!!!!Ukiacha zinaa haya mengine yote yatukuayo baada hayawezi pata nafasi...
Usikute njemba ilikuwa na viazi a.k.a baunsa. Kwa hiyo mume akafyata na kusingizia hana hatia.
mfumo dume, ampige ili iweje, unafikiri inasaidia?bora wakae chini waongee, je kama hamridhishi.
tena huyu lazima ashitakiwe,mbona wanaume wanafumaniwa na kusamehewa
Wewe unadhani huyo mwanaume alipanga kumpiga mkewe?
Hapo waongee nini sasa na kama ni maji ndio yashamwagika...
Huko kutoridhishwa ndio uamue kwenda kuzini? Kwa nini usingeliongea na mumeo?
Suala la wanaume wengine kufumaniwa na kusamehewa linahusiana vipi na hili tukio?