Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,431
Gwiji la siasa za Mageuzi Nchini Tanzania Freeman Mbowe, ama Mtemi Isike, Laingwanan au Ustaadh Aboubakar Mbowe kama anavyofahamika huko Zanzibar, sasa anatajwa kama ndiye mpigania haki, demokrasia na uhuru anayeheshimika zaidi barani Africa, wachunguzi wa siasa za dunia wanamuweka Mbowe juu ya Mwl Nyerere, Mandela, Nkurumah na wapigania uhuru wengi wa zamani, kwa vile yeye anapambana na watawala makatili wa kiafrica ambao wamejitwisha udikteta kutokana na kulewa madaraka baada ya kuchukua madaraka kutoka kwa wazungu.
Tukumbuke kwamba kupambana na Mkoloni mweusi ni hatari zaidi kuliko mkoloni mweupe, hii ni kwa sababu wako tayari kukufanya chochote ili waendelee kufaidi utamu wa madaraka ya nchi yaliyojaa neema kibao za marupurupu walizojiwekea wao wenyewe kwa kutumia katiba mbovu walizoziandika wenyewe kwa matakwa yao.
Wapigania uhuru wa zamani waliungwa mkono na weusi wenzao kwa vile lengo lilikuwa kupata uhuru, lakini kwenye harakati za sasa za Mbowe na Chadema ni kuleta usawa kwenye nchi kwa kuleta katiba itakayowaondoa miungu watu, hii kazi si nyepesi na imejaa mamluki wengi mno, hapa ndipo Mbowe anapokuwa tofauti na wale wa zamani na ndio panapomuweka juu yao, ni hatari sana kufanya siasa kwenye nchi iliyojaa mamluki wanaotega mitego ya usaliti ili walipwe bakhshishi na watawala, hata hivyo Mbowe ameruka vihunzi vyote na kushinda na sasa anapambana na Polisi tu, wanasiasa walio madarakani wanamuogopa vibaya sana.