Freeman Mbowe atoa magari ya wagonjwa Hai

Freeman Mbowe atoa magari ya wagonjwa Hai

Watu walitoa wakati hakuna uchaguzi:



Tena mpaka ma Land Cruiser, wacha vipanya:



Tena brand new siyo mtumba:



Kijana usicheze na chama dume.
haya ma cruiser ni ya serikali asilimia mia mbili! hilo tunajua wala msitake mifagio isiyowahusu magamba! ni kodi zetu hizo! hizo za kina filikunjombe, mbowe na kina ndesamburo tunjua jitihada zao wanazofanya! kuna tofauti kubwa sana ya hizo ambulance! kama unajiamini embu weka full pic ya hiyo landcruiser anayokabidhi bwana UPE hapo na uangalie za kina Mbowe na filikunjombe ambazo zimeandikwa mpaka mchangiaji
 
Freeman Mbowe amefanya jambo zuri sana na la kupigiwa mfano. Ila mimi kama shabiki wa cdm sifurahishwi sana na hali hii ya kutoa mambo ya maendeleo haswa mwaka wa uchaguzi. Kwa kiasi kikubwa hali hii tunaipigia kelele huko ccm kwani ikifika wakati wa uchaguzi ndio unawaona viongozi wao wakianza kurekebisha miundo mbinu kama ya maji, barabara, umeme nk. Lakini wakishapata kura huwaoni tena jimboni. Kama amewahi kutoa misaada mingine yenye tija katika jimbo lake kabla ya mwaka huu ni sawa lakini kama ni sasa naona tunaanza kutumia mbinu zilezile za kiccm.

Kwa mtu anayeangalia ukweli hapa anaweza kupata shida na dhamira ya mtoaji. Ni kweli kwamba ni muwajibikaji ama ndi walewale wanaotumia uelewa finyu wa wananchi kuwapiga bao? Nasema hivo huku nikizingatia wajibu mkubwa sana wa mbunge ni kuisimamia na kuiwajibisha serekali na wala sio mfadhili, lakini hazuiwi kutoa msaada kutoka kwenye mfuko wake au kuhamisisha watu waliokaribu naye kusaidia kutatua kero zilizo jimboni mwake na taifa kwa ujumla. Ila hali hii isisubiri tu mwaka wa kampeni maana kuna uwezekano wa kuwa ni walewale. Watanzania tuwe makini ili tusirudie kosa.

Hili gari aina ya Mercedece Benz aliulizia vipuri vyake kabla hajalikabidhi? hata madereva wake wanahitaji mafunzo maalum kama kuendesha Ferrali, je hai inamafundi wa kutengeneza hili gari likiharibika au ndo wataagizwa kutoka ujerumani? Pia ni sera ya serikali kutokutumia vifaa chakavu sasa hili gari la mtumba si ni kinyume cha sheria zetu za manunuzi?

Analikabidhi January wakati badget ilitengwa July mwaka jana sasa mafuta ya hili gari yatatoka budget ipi? Dereva wake atalipwa kutoka budget ipi? Halafu vifaa vyake ni kama vya flying doctors sasa hao manesi keshawafundisha namna ya kuvitumia. Vipuri vilivyoko bohari ya serikali ni vya landcruiser na madereva wa halmashauri wamefunishwa namna ya kuyamiliki haya magari, sasa hili la mtumba itakuwaje?

Gari kama hili liliwahi kutolewa na mawematatu kule misungwi lilipaki kwa kukosa shokapu tu, na watengenezaji walisema hawatengenezi tena vipuri vya hiyo model na madukani zikakosekana.
 
haya ma cruiser ni ya serikali asilimia mia mbili! hilo tunajua wala msitake mifagio isiyowahusu magamba! ni kodi zetu hizo! hizo za kina filikunjombe, mbowe na kina ndesamburo tunjua jitihada zao wanazofanya! kuna tofauti kubwa sana ya hizo ambulance! kama unajiamini embu weka full pic ya hiyo landcruiser anayokabidhi bwana UPE hapo na uangalie za kina Mbowe na filikunjombe ambazo zimeandikwa mpaka mchangiaji

Ahaaa, kwa uongo ni nona, Riz1 uliambiwa niwaziri wa afya? dogo kaguswa kajishika mfukoni katoa kitu cha ukweli sio hicho kipanya, KUB mzima unatoa kipanya? hata wajerumani watamshangaa sana. Mbona tulimwambia alipeleke hai lile shangingi likawe ambulance aligoma!
 
haya ma cruiser ni ya serikali asilimia mia mbili! hilo tunajua wala msitake mifagio isiyowahusu magamba! ni kodi zetu hizo! hizo za kina filikunjombe, mbowe na kina ndesamburo tunjua jitihada zao wanazofanya! kuna tofauti kubwa sana ya hizo ambulance! kama unajiamini embu weka full pic ya hiyo landcruiser anayokabidhi bwana UPE hapo na uangalie za kina Mbowe na filikunjombe ambazo zimeandikwa mpaka mchangiaji


Jumuisha na ile used ya Mh Nchimbi ambayo aliitoa kwa watu wa Manispaa ya Songea, hizi brand new L/C siyo siri zinaukakasi kama kweli zaweza tolewa mtu binafsi.
 
Hili gari aina ya Mercedece Benz aliulizia vipuri vyake kabla hajalikabidhi? hata madereva wake wanahitaji mafunzo maalum kama kuendesha Ferrali, je hai inamafundi wa kutengeneza hili gari likiharibika au ndo wataagizwa kutoka ujerumani? Pia ni sera ya serikali kutokutumia vifaa chakavu sasa hili gari la mtumba si ni kinyume cha sheria zetu za manunuzi?

Analikabidhi January wakati badget ilitengwa July mwaka jana sasa mafuta ya hili gari yatatoka budget ipi? Dereva wake atalipwa kutoka budget ipi? Halafu vifaa vyake ni kama vya flying doctors sasa hao manesi keshawafundisha namna ya kuvitumia. Vipuri vilivyoko bohari ya serikali ni vya landcruiser na madereva wa halmashauri wamefunishwa namna ya kuyamiliki haya magari, sasa hili la mtumba itakuwaje?

Gari kama hili liliwahi kutolewa na mawematatu kule misungwi lilipaki kwa kukosa shokapu tu, na watengenezaji walisema hawatengenezi tena vipuri vya hiyo model na madukani zikakosekana.

Siijui nia yako wewe mchangiaji kama umechangia kwa dhamira njema ama la. Lakini na mimi bila kupepesa macho kama mshabiki wa cdm, mengi ya maangalizo yako ni ya msingi haihitaji ucdm au uccm kuona ukweli huo. Na ukweli huu ni lazima tuutumie kote kote iwe ni kwa mwanacdm au kwa mwanaccm au awaye yote ila mradi tuwe na dhamira njema kwa taifa letu. Kwa kuwa nimekubaliana sana na wewe mleta hii post nitajaribu kufuatilia record zako hapa jukwaani huwa unachangia kwa utanzania wako ama kwa mtazamo wa vyama. Ila nakupa bigup sana kwa maangalizo hayo.
 
Siijui nia yako wewe mchangiaji kama umechangia kwa dhamira njema ama la. Lakini na mimi bila kupepesa macho kama mshabiki wa cdm, mengi ya maangalizo yako ni ya msingi haihitaji ucdm au uccm kuona ukweli huo. Na ukweli huu ni lazima tuutumie kote kote iwe ni kwa mwanacdm au kwa mwanaccm au awaye yote ila mradi tuwe na dhamira njema kwa taifa letu. Kwa kuwa nimekubaliana sana na wewe mleta hii post nitajaribu kufuatilia record zako hapa jukwaani huwa unachangia kwa utanzania wako ama kwa mtazamo wa vyama. Ila nakupa bigup sana kwa maangalizo hayo.

Tindo, nachangia hoja wala sina ushabiki wa kichama, sote tunahitaji tanzania yenye ustawi na kumkosoa mtu sio kuwa hatumpendi, ni sawa na kumchapa mwanao sio kuwa humpendi unataka awe mwana mwema. Gen Collin Powel alisema "askari wakiacha kukueleza matatizo yao basi ujue wameshapoteza imani na wewe"
 
Siijui nia yako wewe mchangiaji kama umechangia kwa dhamira njema ama la. Lakini na mimi bila kupepesa macho kama mshabiki wa cdm, mengi ya maangalizo yako ni ya msingi haihitaji ucdm au uccm kuona ukweli huo. Na ukweli huu ni lazima tuutumie kote kote iwe ni kwa mwanacdm au kwa mwanaccm au awaye yote ila mradi tuwe na dhamira njema kwa taifa letu. Kwa kuwa nimekubaliana sana na wewe mleta hii post nitajaribu kufuatilia record zako hapa jukwaani huwa unachangia kwa utanzania wako ama kwa mtazamo wa vyama. Ila nakupa bigup sana kwa maangalizo hayo.

Binafsi nilishakataa ambulance aina ya Landrover110 kwa madai kuwa hilo gari halina balance katika barabara za vumbi (off road) lakini management wakalazimisha lilifanya kazi miezi mitatu likapinduka wakati fundi akilifanyia majaribio (road test). tulimweleza mfadhili ambaye alikuwa mwingereza akatuomba samahani na kuleta ambulance nyingine aina ya Landcruiser.
 
Tindo, nachangia hoja wala sina ushabiki wa kichama, sote tunahitaji tanzania yenye ustawi na kumkosoa mtu sio kuwa hatumpendi, ni sawa na kumchapa mwanao sio kuwa humpendi unataka awe mwana mwema. Gen Collin Powel alisema "askari wakiacha kukueleza matatizo yao basi ujue wameshapoteza imani na wewe"

Nikupongeze sana kwani hapa jukwaani kumekuwa na tabia ya kuchangia kwa mtazamo wa kivyama. Unakuta kosa ama udhaifu unaofanywa na chama A, washabiki na wanachama wa chama B wanapiga sana kelele, lakini udhaifu ule ule unaofanywa na chama B washabiki na wanachama wake wanakaa kimya ama kujitoa ufahamu. Matokeo yake unakuta jamii au hata wakati mwingine taifa kwa ujumla tunaingia matatizoni. Na kwa kiasi kikubwa tabia hii ndiyo inayoligharimu taifa letu. Nadhani unaijua tabia ile ya kukuta mtu kavurunda akiangaliwa watu wanakaa kimya kwani ni mwenzetu.

Mimi ni mshabiki sana wa cdm lakini kwenye hili la gari nimepongeza lakini sikupata raha ya moja kwa moja toka huu uzi ulipoletwa hiyo jana. Simply dhamira yangu huwa inapata walakini kwenye mambo ya aina hii bila kujali ni nani aliyefanya. Na hata ukifuatilia post zangu kwenye huu uzi nimetoa maangalizo mengi ambayo si ya kishabiki na sehemu kubwa ni kwa ajili ya faida ya taifa.
 
Tatizo la Hai sio ambulance ni ukosefu wa madatari na madawa hospitalini.Sasa hiyo ambulance itakuwa inawakimbiza watu kuwapeleke mahali kusiko na madawa na madaktari?

Kwa hiyo ni wajibu wa mbunge kuajiri madaktari? Kama ndivyo,ni nini wajibu wa serikali inayokusanya kodi? Au kwenu nyie magamba ni kutumia kodi zetu kuzurula duniani,kulipana posho,kuhonga wapiga kura,kununua wapinzani na kupiga dili kama za epa na escrow
 
Hili gari aina ya Mercedece Benz aliulizia vipuri vyake kabla hajalikabidhi? hata madereva wake wanahitaji mafunzo maalum kama kuendesha Ferrali, je hai inamafundi wa kutengeneza hili gari likiharibika au ndo wataagizwa kutoka ujerumani? Pia ni sera ya serikali kutokutumia vifaa chakavu sasa hili gari la mtumba si ni kinyume cha sheria zetu za manunuzi?

Analikabidhi January wakati badget ilitengwa July mwaka jana sasa mafuta ya hili gari yatatoka budget ipi? Dereva wake atalipwa kutoka budget ipi? Halafu vifaa vyake ni kama vya flying doctors sasa hao manesi keshawafundisha namna ya kuvitumia. Vipuri vilivyoko bohari ya serikali ni vya landcruiser na madereva wa halmashauri wamefunishwa namna ya kuyamiliki haya magari, sasa hili la mtumba itakuwaje?

Gari kama hili liliwahi kutolewa na mawematatu kule misungwi lilipaki kwa kukosa shokapu tu, na watengenezaji walisema hawatengenezi tena vipuri vya hiyo model na madukani zikakosekana.

Katoe lako,serikali chakavu imeshindwa
 
Tatizo la Hai sio ambulance ni ukosefu wa madatari na madawa hospitalini.Sasa hiyo ambulance itakuwa inawakimbiza watu kuwapeleke mahali kusiko na madawa na madaktari?

Suala la madawa ni la Serikali hata hili la Ambulace ni la serikali pia kwa hiyo kama kasaidia hili moja ni muhimu na Serikali ikatekeleza hilo lingine lakini cha ajabu kwa kuwa tu Jimbo linaongozwa na upinzani Serikali ya CCM ipo tayari watu wote wafe kwa magonjwa eti wanapewa adhabu kwa kuchagua upinzani.
 
Back
Top Bottom