Free talk: Mwanamke shtuka!

Free talk: Mwanamke shtuka!

Habari wana MMU.

Kuna hili jambo ningependa tujadiliane ama tushirikishane kidogo.

Hakuna asiejua kuwa kila mwanamke kabla hatujavurugwa na dunia huwa matamanio yetu ni siku moja kuolewa na kutengeneza familia na mwanaume fulani hivi amazing(fantancy vs reality).

Sasa tatizo linakuja kuwa huwa wanawake wengi wana mentality kuwa maandalizi ya familia ya baadae haswa kwa mambo yanayohusu assets na gharama zingine ni majukumu ya mwanaume na sio mwanamke.
Hivyo unaweza kukuta binti ana kazi nzuri tu ila hata kujiwekeza kununua hata kiwanja walaaa hawazi au hata kufungua biashara. Anawekeza kwenye mikoba,mawigi,simu za bei ghali,viatu nk. Vitu ambavyo ukivipigia mahesabu unakuta ana viwanja vitano vikubwa tu huku kijijini kwetu.

Hebu fikiria unaolewa ukiwa angalau umejiwekeza kiasi fulani hivyo mkiunganisha nguvu na mwenza wako angalau mnapiga hatua kadhaa kwa haraka kuliko kusubiria mwanaume afanye kila kitu.

Wakati mwingine unakuta binti anadate mwanaume mwenye expossure ya kutosha na mfanyabiashara mzuri, hata kuomba basi hata aelekezwe abc's za biashara, hata kuunganishwa kibiashara nehiiii.
Au unadate mwanaume mwenye uwezo mkubwa kifedha hivyo kazi yake ni kuomba kununuliwa simu ya milioni 2 nk, vitu vya anasa ambavyo kwa kiasi kikubwa havikuongezei lolote la maana zaidi ya sifa za kijinga. Ni kwanini usimuombe mtu wa aina hiyo hata business idea, au angalau uanze jambo lako ie biashara,ujenzi nk kisha umuombe akuongezee kiasi fulani cha pesa? Kwa mwanaume mwenye upeo atakuona una akili na anaweza kukusogeza mahali pazuri.

Mwingine unakuta ni mama kabisa ila hata haiwazii kesho ya mtoto wake ambae anamlea peke yake, yuko busy na starehe na kutumbua pesa za child support, kesho na keshokutwa baba hayupo mtu anaanza kuhaha wakati nafasi ilikuwepo akaichezea

Maisha yamebadilika sana jamani basi nasi wanawake tubadilike in a positive way, tuyaishi maisha halisi na sio ya kuigiza ili angalau tunapoingia kwenye maisha ya ndoa angalau tuwe na cha kuongeza sio ndio ukiolewa umtwishe mwanaume majukumu ya familia mnayoijenga,familia ya kwao na ya kwenu pia. No wonder wanakufa mapema hawa watu.

Tuzitumie fursa vizuri pale zinapopatikana kabla haijawa too late.
Jamani hapa simchagulii mtu maisha ila hakikisha hautokuwa na majuto baadae kuwa "laiti ningejua"!!! Maana hakuna anaependa kesho yake iwe ya kuunga unga.

Nawasilisha.
Tatizo hili huanzia wanapokuwa shule... UTAWASIKIA... mimi nasomewa... sijihangaishi wakati ntakuja kuolewa...
 
Shit happens though, hata wanawake unamsaidia boyfriend weeh afu akifanikiwa hakujui au mume anakwambia wewe sio wa hadhi yang
.
Mmh sex ni mutual benefits, ila nyie mkinyimwaga ndo wa mnaongoza kulia lia lol. Na laiti tungejua; hawa wapenzi ni bora tungewapa hela hata kama watatukimbia; kuliko kuwapa "raha za ndoa zetu" tunazoziacha kwenye vitanda tunavyolalia na watu wasio na ndoa na sisi

Wanatuacha kila siku, sisi tukiwaacha basi wanasusa kila kitu. Waliosomesha wakaachwa ni wachache kuliko ambao hawakuachwa, ila wamekomaa na kuachwa tu.
 
Shit happens though, hata wanawake unamsaidia boyfriend weeh afu akifanikiwa hakujui au mume anakwambia wewe sio wa hadhi yang
.
Mmh sex ni mutual benefits, ila nyie mkinyimwaga ndo wa mnaongoza kulia lia lol. Na laiti tungejua; hawa wapenzi ni bora tungewapa hela hata kama watatukimbia; kuliko kuwapa "raha za ndoa zetu" tunazoziacha kwenye vitanda tunavyolalia na watu wasio na ndoa na sisi
Hahaa..

Unataka kusema kwamba tusomeshe? Manake naona unazunguuuka sana..

Mimi mwanamke wangu awe na viable bussiness idea ...namsupport in every means ...from earth to the moon and backwards..ila kusomesha binti yuko kwao never..
 
Nikiwa binti, mara nyingi ijumaa tulikuwa na mikesha ya vijana, sio tu kuombeana ila nakukumbushana vitu mbalimbali. Namshukuru Mungu kwa ajili ya Pastor wetu, kuna muda alikuwa anatupa makavu hadi kanisani unapaona pachungu, Ila alitutengeneza tukawa watu fulani amazing sana.

He used to tell us young ladies; muda ambao hujaolewa ndo muda wa kufulfil your dreams; making an identity of your own. Once ukiolewa mara nyingi sana utatimiza ndoto/kutembea na vision ya mumeo. Majority tunaua ndoto zetu tukiingia ndoani (sad). So alitutaka tufanye kazi kwa bidii, adding values to our lives, sio tuspend kwenye unnecessary starehe kujifanya slay queens; waiting to get married and chop our hubby's money. Kuna wakati anamsimamisha kijana mdogo yupo high school (inspiration) ila tu ni anachakarika akikutajia assets zake, mimi limama lizima naona aibu na kupata tabu sana. Hakutaka kusikia kitu "I'm doing nothing". Kuna maisha zaidi ya kuolewa, what if usipoolewa, ndo utaishi ukiinvest kwenye kujiremba milele?

Hujapanga, unakaa home, make sure una vitu/assets zako. Sio kusubiri zawadi na vyombo vya send off ndo ukaanzie maisha, wewe binafsi unabeba nguo na viatu na mapochi.
Na alikuwa anatuambia kabisa, tusiende tukawe mizigo kwa waume zetu, hata chumvi ikiisha unasubiri baba atoke kazini. Wengine wanalia mume wangu ananinyanyasa sana, Ila wakati mwingine ni kwa sababu huna mchango wowote financially nyumbani, anakuchokaa. Afu pamoja na kuzaa, bado tuna wajibu wa kutimiza ndoto za watoto wetu. Watoto wako wasishindwe kutimiza ndoto zao kisa baba amekataa kuwahudumia au hayupo au tukasema ni kazi ya baba yao tu. Though sio kama kila mtu atafanikiwa kuinvest as we wish, ila kuwa na ile spirit ya kuthubutu/ kutaka kufika mahala fulani ni jambo zuri sana. Kwa sababu hata usipofanikiwa leo, you won't rest till you make it happen.

Na maisha yana ups and downs, hata ukiolewa na bilionea possibly kuna siku maisha yatashake kidogo, sasa ukiwa slay queen, hicho kipindi cha mpito kitapita salama? Usije ukamuua kwa presha mumeo kwa kutaka aendelee kukuhudumia as it was before, au utakimbia nyumba? au utatafuta sponsors ili uendelee kumaintain status?. Make your own identity lady. Mwanamke ana nguvu ya kumultiply, chochote kidogo kitakachopandwa kwake/kufanywa na yeye, atakitunza hadi kiongeze na vingine. (I missed magazeti mweeh)

Na ni kweli umetoa gazeti

Ulipokuwa binti!!! Siku hizi umekuwa mmama?

Huwa napenda michango yako hujaa busara na hekima.
 
Ishu ni hawa wanawake wenye idea hii ni wachache..

Wazee baba ukikuta mwanamke wako ana akili za kujikwamua kiuchumi msaidie atimize ndoto yake..

Don' t let her down..


espy na Heaven Sent nawatakia usiku mwema.View attachment 805531
Unfortunately wanaume ndo wa kwanza kuua ndoto zetu. Mara sitaki msomi, sijui mfanyakazi sijui nani mweeh, eti mnaogopa mwanamke mwenye kipato huwezi kumcontrol tofauti na asiye na kipato ambaye utamtreat utakavyo na haondoki ng'oooo. An inferior, weak and abusive man, lazima ahofie mwanamke mwenye kipato kwa sababu wengi wakiwa abused; sio wa enzi za mama zetu za kuhofia nikiondoka ntaendaje kuanza maisha (sio kiburi ila kuna muda unaona kabisa hapa tulipofikia mmh). Utegemezi unanunua hadi utu wako sometimes, mtu anakuabuse weee ila upo tu unajivumilisha hadi yakupate makubwa. Respect and treat well your woman uone kama mwanamke mwenye akili ataondoka akuache
 
Unfortunately wanaume ndo wa kwanza kuua ndoto zetu. Mara sitaki msomi, sijui mfanyakazi sijui nani mweeh, eti mnaogopa mwanamke mwenye kipato huwezi kumcontrol tofauti na asiye na kipato ambaye utamtreat utakavyo na haondoki ng'oooo. An inferior, weak and abusive man, lazima ahofie mwanamke mwenye kipato kwa sababu wengi wakiwa abused; sio wa enzi za mama zetu za kuhofia nikiondoka ntaendaje kuanza maisha (sio kiburi ila kuna muda unaona kabisa hapa tulipofikia mmh). Utegemezi unanunua hadi utu wako sometimes, mtu anakuabuse weee ila upo tu unajivumilisha hadi yakupate makubwa. Respect and treat well your woman uone kama mwanamke mwenye akili ataondoka akuache
Kuna ujinga fulani huwa wanajazana hivyo wanajikuta badala ya kutengeneza wanaharibu.
 
Hahaa..

Unataka kusema kwamba tusomeshe? Manake naona unazunguuuka sana..

Mimi mwanamke wangu awe na viable bussiness idea ...namsupport in every means ...from earth to the moon and backwards..ila kusomesha binti yuko kwao never..
Financial support sio lazima kusomesha bana. . Kuna business ambazo unaweza ukamsupport baby ukajikuta umetoa kiasi kinachotosha kumsomesha mtu kabisa teh
 
Kuna ujinga fulani huwa wanajazana hivyo wanajikuta badala ya kutengeneza wanaharibu.
Teh tumewashtukia mbona, watapata tabu sana kama wataendelea kuona ni sawa kutomtreat vyema mkeo na yeye anatakiwa aendelee tu kujivumilisha
 
Unfortunately wanaume ndo wa kwanza kuua ndoto zetu. Mara sitaki msomi, sijui mfanyakazi sijui nani mweeh, eti mnaogopa mwanamke mwenye kipato huwezi kumcontrol tofauti na asiye na kipato ambaye utamtreat utakavyo na haondoki ng'oooo. An inferior, weak and abusive man, lazima ahofie mwanamke mwenye kipato kwa sababu wengi wakiwa abused; sio wa enzi za mama zetu za kuhofia nikiondoka ntaendaje kuanza maisha (sio kiburi ila kuna muda unaona kabisa hapa tulipofikia mmh). Utegemezi unanunua hadi utu wako sometimes, mtu anakuabuse weee ila upo tu unajivumilisha hadi yakupate makubwa. Respect and treat well your woman uone kama mwanamke mwenye akili ataondoka akuache
Ila ukipata mwanaume anayekuheshimu na akakupa support to the maximum mpe haki ya kuenjoy the superiority as a MAN.

Kosa ni pale dharau, ignoring nyingi zinapoanza...! Kuna wanawake hawajielewagi ...lazima tabu ziinuke.

Na shwatan alivyo mbaya..! Everything goes down in a friction of second.

Mtupe heshima pia pale tunapokuwa wa kwanza kuwasupport.
 
Umenena vyema Espy, kwa kweli ni wanawake wachache sana kwasasa wanaofikiria maendeleo kwa jitihada zao wenyewe pasipo kuwepo mkono wa mwanaume.

Unakuta dada kaajiriwa (binafsi/serikali) na ana muda hata wa zaidi ya miaka mitatu kazini lakini hana lolote alilowekeza zaidi ya kuhangaika na fashion kila siku... Wengi hatukumbuki kuwa nafasi na muda tulionao sasa baadaye tunaweza tusiupate, nyakati zinabadilika uchumi nao unakuwa sio rafiki.. Siku utakayoingiwa na akili ya kufanya kitu angalau kikaonekana cha manufaa kwako na kwa yeyote ajaye (mume/watoto) ndo utakapo ng'amua kuwa huna tena uwezo wa kufanya hivyo na ndipo itabaki tu simulizi kuwa yule dada enzi zake alikuwa yuko vizuri kiuchumi...Muda huo akili unayo lakini huna vitendea kazi.

Mambo mengine tuwe tunayaacha yanatupita, si lazima kuyumbishwa na dunia, kushoto upo, huku upo , kule upo yaani kila kinachokuja umo....

Tujaribu pia kuangalia na aina ya marafiki wa kuambatana nao, wao kila siku wazungumzia fashion mpya tu na kutambiana madanga, wafikiri lini utapata wazo la kusema uinvest kwenye kitu cha maana???

Nimewahi kuwa na rafiki, alinizidi kwa umri (miaka 6) lakini sioni alichokuwa akinifaidisha zaidi ya kunipa stori tu za kupelekana maduka ya mikoba + nguo + viatu + stori za madanga aliyonayo...

Nikimshauri mawazo mazuri utasikia maisha yenyewe hayaeleweki, tutumie....Nikaona hili BOX halinifai...

*Kama una uwezo na nafasi ya kufanya kitu fanya, huyo mume endapo utajaaliwa aje akute angalau una pa kuegemea...Mkiunganisha nguvu pamoja angalau mnakuwa mmejisogeza sogeza....
 
Back
Top Bottom